BODABODA WA MKE WANGU 2
Asubuhi na mapema nampigia Amoni rafiki yangu namwambia aende nyumbani kwangu haraka, kama alivyoniahidi kuwa nimruhusu apumzike na asubuhi na mapema wataamkia kwangu kuangalia usalama.
Alienda peke yake nyumbani kwangu
View attachment 2609139
Alienda na kufika nyumbani kwangu alimkuta mke wangu yupo pale nyumbani, akaongea naye kuhusu ilivyokuwa jana na jinsi ambavyo waligonga mlango hakuna aliyefungua wala anayejitingisha humo ndani, akamuuliza kuna usalama wowote na nini kinachoendelea?!
Sasa kabla hajafika na kumuuliza, mimi nilikuwa nimeshampigia tena mke wangu kabla. Yaani baada ya kumpigia Amoni akaenda nyumbani kuona usalama ukoje, nilimpigia tena mke wangu ambaye tangu jana alikuwa hapatikani baada ya kumpigia mara ya kwanza asipokee, safari hii akapokea
nilishtuka kuona kapokea, atleast naweza kujua kinachoendelea.
Nikamuuliza kuna nini huko mbona tangu jana sikupati na wala simu yangu hupokei?
Akaniambia jana alichoka sanaa hivyo alilala mapema sanaa na simu yake haikuwa na chaji hivyo ilikaa on na baada ya muda ikajizima kwa
chaji kuisha.
Sasa binafsi mwanzo sikuwaza kama kunaweza kuwa na kitu cha yeye kunificha, nilikuwa nikimuamini sanaa, na hata hili la kutokumuambia kuwa nilipigiwa na dada wa kazi akaniambia kuna vurugu huku sio kwamba nilikuwa nimepanga kumficha, ila nilianza tu taratibu
kuwa mbona jana ulikuwa hupokei simu na baadaye kutokupatikana ili anielezee yeye mwenyewe tatizo, maana mimi nilichokifikiria ni kutakuwa na tatizo, japo niliwaza sana bila kupata majibu kuwa ni matatizo gani huyo jamaa anaweza kuyaleta hapo nyumbani maana ni mtu tunayemuamini
vizuri tu.
Basi aliponiambia vile halafu akawa hajanieleza chochote, ilibidi ninyamaze kwanza nisimuelezee kuwa dada wa kazi alinipigia halafu akawa hajanielezea vizuri akakata simu.
Nilimwambia sawa haina shida, tukazungumza mazungumzo mengine, ila sikuwa sawa hata kidogo
moyoni mwangu nikawa nikijiuliza ni kitu gani huyu mke wangu ananificha hapaa.
Na sasa rafiki yangu Amoni anafika kwangu na kuanza kumuelezea mke wangu kilichotokea jana, anataka afahamu shida ni nini ili akanieleze.
Mke wangu alishtushwa sanaa na kile ambacho alikiskia kutoka
kwa Amoni, akakumbuka jinsi alivyonidanganya kwenye simu kuwa hakuna shida yoyote ni simu tu haikuwa na chaji na yeye alikuwa ameshalala.
Sasa huo mshtuko Amoni ndiye aliyeuona vizuri na kunisimulia kuwa mke wako baada ya kumuelezea kuhusu kilichotuleta jana usiku na akashindwa
kufungua mlango, ameonekana kushtuka mnoo ndo mimi nikaelewa sababu ya kushtuka kwake ambayo ni kama nilivyowaeleza.
Mke wangu alimwambia Amoni kuwa yeye alikuwa amelala na alikuwa na usingizi sana, sauti aliziskia lakini hakujua ni za akina nani hivyo hakutaka kufungua kabisaa
hivyo ikabidi akae kimya.
Sasa Amoni akamuuliza kwani dada huyu (dada wa kazi) hakutufahamu kuwa ni sisi akafungua au na yeye alikuwa anausingizi kama wewe? Alimjibu kuwa, alishagamzuia kufungua mlango kwa mgeni yoyote usiku wakiwa wameshalala tayari.
Basi, akamwambia kuwa
usalama upo wala asiwe na wasiwasi, na kuhusiana na suala hilo la vurugu za yeye na Prince (yule Dereva bodaboda) asijali yeye ataongea na mume wake ila sio issue kubwa.
Na hivyo ndivyo alivyonieleza Amoni baada ya kutoka kwa mke wangu
Sasa Amoni pamoja na na kunielezea yote hayo ila ilibidi pia anielezee mtazamo wake binafsi,
Aliniambia mke wangu kwanza alishtuka nilivyoelezea kilichotuleza nyumbani usiku huo tukigonga na asifungue, jambo ambalo linatia wasiwasi, lakini pia anadanganya kusema alikuwa na
usingizi na kuwa hakujua sisi ni akina nani, kwa sababu mlango tuliugonga kwa nguvu zote lakini hakuna mtu anaitikia, na kwa sababu tulikuwa na wasiwasi kuwa kunaweza kuwa na shida ndani kama ulivyotueleza, tulitaka hadi kuuvunja huo mlango ndo baadaye tukaona tuache kwanza
tukusikilize, ndo ukatuambia twende kwa prince mwenyewe. Huyo mtu anausingizi gani huo? Hata Samaki hawalali hivo. Lakini pia anasema hakujua sisi ni akina nani, hiyo ni uongo kwa sababu tulikuwa tunaita kabisaa “shemeji, ni mimi Amoni” fungua mlango, fungua, kuna usalama huko?”
kiufupi majina yetu tuliyataja hata kama alikuwa hajui sauti kwa sababu ya usingizi basi hata majina yetu angeyaskia.
Akaniambia, mchunguze mke wako, kaka nahisi umepigwaa
Nilichokaa, na muda huo nilipaswa niwe kwenye kikao kwa ajili ya mambo ya kikazi hayo yaliyonipeleka mkoani
Nilichelewa kikao kwa muda mrefu kweli, na pia hata baada ya kuingia, akili yangu haikuwa sawa, nikiwaza mke wangu anakitu gani ananificha.
Kila nikijaribu kuwaza may be kuna cheating ananifanyia kwa huyo bodaboda, naishiwa nguvu, najilazimisha kukataa kuwa haiwezekani Kabisaa
Nilimaliza hicho kikao kwa mbinde na nilirudi hotelini nikiwaza nifanye nini, simu za mke wangu zikawa zinaingia sipokei maana nina hasira sana, kwanini anidanganye au kunificha kitu mimi mume wake, au ananicheat hapaa
Niliwaza na ndipo nilipoamua kumpigia tena dada wa kazi.
Dada alipokea nikaongea naye kitaratibu ili asiogope aweze kunielezea.
Nilimuuliza jana hizo vurugu ulizokuwa unazisema hapo nyumbani uliponipigia ni zipi? Kuna nini kinaendelea?!
Nieleze wala usiogope
Akaogopa kabisa kusema, akaniambia kaka mimi naogopa nikiongea chochote dada atanitoa roho mimi naomba tu wewe mwenyewe umpigie umuulize, ni mke wako yule, akuelezee au wewe mwenyewe fuatilia tu mwenyewe kujua kinachoendelea,
Maana mimi hapa hata sina amani, dada amejua kuwa
nilikupigia simu kukwambia kuna vurugu ndani za yeye na Prince amenigombeza tangu asubuhi ni kunisema na amesema nitarudi nyumbani kwa sababu ya huu mdomo wangu, amenipiga na kunipiga, amenikasirikia sanaa hataki hata kuniona. Naogopa sana na yeye ndo alinileta hapa kufanya kazi
Ilinibidi nikate simu.
Nikajikaza kiume kuhudhuria kikao cha kesho yake ambacho kilikuwa ni cha mwisho
Ambacho kiliisha jioni kabisaa, na hivyo kesho yake asubuhi na mapema nikaanza safari ya kurudi nyumbani, nikiwa na hasara nyingi mnooo
Ukweli unaenda kugundulika katika sehemu inayofuata.
Na tutajua hasa nini kilichokuwa kina endelea huko
Baki na mimi hapa hapa
Kwa ajili ya sehemu ya mwisho
BODABODA WA MKE WANGU 3
( THE LAST EPISODE )
Kutokana na ukaribu wa mara kwa mara ambao mke wangu alikuwa nao na huyo Dereva wake wa bodaboda, zilianza kujengeka hisia katikati yao, zilianza kama utani, wakitaniana mambo ya kimapenzi lakini sasa ikafika
hatua hisia zao zikawa more serious, marafiki zake Prince (huyo dereva wa bodaboda) walikuwa kila siku ni kumcheka jinsi ambavyo mtoto anaonekana kumuelewa lakini yeye anakuwa muoga. Bodaboda wenzake walimuona zuzu sana kwa sababu amekuwa na ukaribu mnoo na mke wangu mpaka wote
wanaonyeshana hisia za kupendana lakini yeye anakuwa muoga kisa mimi mume wake huyo mwanamke, walimwambia unapaswa kuhit and run, huyo ni mke wa mtu lakini anajilengesha kwako kila siku halafu wewe umezubaa.
kibaya zaidi ni kuwa huyo mke wangu alikuwa ni mzuri sanaaa, sasa na
hiyo marafiki zake wakasimama nayo kama point kumshangaa huyo Prince anavumilia vipi, na Wakamwambia hizo chance ni mara moja kwa life time, huwezi pata tena, japo pia wapo wengine ambao walimuonya asiwasikilize hao.
Kitu nilichojifunza hapa ni kuwa, hakuna jambo baya kama mke wa
mtu kuruhusu mazoea na mwanaume mwingine, hilo jambo ni hatarii mnoo japo sio mara zote litakuwa hatari, maana mke wangu na Prince walianza na uteja kama kawaida, yaani mke wangu alikuwa mteja mzuri wa Prince, safari zake anamuita Prince ampeleke, lakini ile kuwa na free time
mara kwa mara, akitaka kwenda huku yuko naye kule yuko naye, hakuna bodaboda yeyote tofauti anayemtumia mpaka sasa ikafika hatua jamaa akawa family friend anaweza kuja nyumbani muda wowote na akaondoka muda wowote, binafsi mm hata mara moja sikuwahi kuhisi kama kuna kitu kitakuja
kutokea, nilikuwa nikimuamini sana Prince na mke wangu nilimuamini pia. Kumbe mazoea yao yalikuja kuzaa mapenzi. Maana sasa prince aliona anachoshauriwa na marafiki zake ni kweli, na kwanza isitoshe yeye mwenyewe kwa muda mrefu sana amekuwa akitamani ni vile tu aliniogopa mimi
Yote hayo nilisimuliwa na rafiki yangu Amoni ile siku nimekuja kutoka safarini huko mkoani.
Wakati nipo njiani nilimpigia na kumueleza kila kitu kuhusu mazungumzo yangu na yule dada wa kazi, nikamwambia jinsi ambavyo nimegundua mke wangu kuna kitu kikubwa sanaa ananificha
Nina hasira sanaa na ninaenda kujua ni kitu gani hicho japo ninasuspect cheating hapo. Na kwa kweli moyo unaniuma mnoo, mke wangu nilimuamini sanaa. Amoni akaniambia, kabla hujafika kwako njoo upitie kwanza kwangu kuna file la mke wako ninalo.
Nilishtuka sanaa, nikamuuliza file
gani? Akaniambia straight, file la mke wako na huyo Prince.
Nilihisi kuchanganyikiwa yaani, niliendesha gari kama kichaa, mpaka ikanipelekea kusumbuana na traffic police huko njiani, lakini ni kwa sababu stress zilikuwa ni nyingi kichwani.
Nilifika kwa Amoni, Akaanza kunieleza
Kuwa baada ya kuondoka kuongea na mke wangu na akaona jinsi ambavyo kuna kitu mke wangu anaficha (kama tulivyoona sehemu iliyopita) plus na zile doubt alizokuwa nazo
Aliwaza, akaamua kumtafuta mshikaji wake ambaye alikuwa ni bodaboda wa kile kile kituo cha Prince, lakini pia na
yeye alikuwa na ukaribu na Prince, alimpigia simu akamuomba wakutane, ile wamekutana kwanza akampiga castle lite tatu, jamaa alikuwa ni mpenzi sanaa wa castle lite
Halafu ndo akamuuliza sasa anafahamu vipi kuhusu Prince na mke wangu
Inshort alimtengenezea mazingira mazuri ya yeye
kuropoka kila kitu. Ndo jamaa akamsimulia kila kitu kama nilivyozungumza hapo awali, kumbe jamaa alikuwa anawasimulia yote yanayoendelea ili kuwaonyesha yeye sio mnyonge.
Na kumbe hata ule usiku wamekuja kugonga nje mlangoni, Prince alikuwepo ndani.
Sasa ndugu msomaji
kuhusu zile vurugu zilikuwa zinahusu nini ambazo hadi dada alinipigia simu, hilo nitakuachia mwenyewe kutafsiri.
Ila ukweli ni kuwa usiku huo Prince alilala humo ndani na asubuhi na mapema akarudi kwake, akaenda kuwasimulia washikaji zake baadaye pale kijiweni
Baada ya rafiki yangu Amoni kunisimulia hayo yote. Jasho lilikuwa likinitoka na imagine sipati picha, Speed ya kwanza nilifikia kwa Prince kabla ya kwenda kwangu baada ya kutoka kwa Amoni.
Nilifika nikaambiwa Prince amehama, jana usiku kaondoka na vitu vyake.
Kumbe mke wangu alipomueleza kuwa nimejua aliona hiki ni kifo, alihama usiku huo, sijui alihamia wapi kwa haraka kiasi hicho.
Nilijaribu kuwauliza kama wanafahamu alikohamia majirani wote hakuna anayefahamu.
Ndipo Amoni akaniambia, huyo hajahamia sehemu bado ila atakuwa
kwa washikaji zake, issue ni kujua yupo kwa nani. Ilibidi tuachane naye nikadeal na mke wangu anieleze vizuri hili.
Nilienda mpaka nyumbani namkuta dada wa kazi peke yake, mke wangu hayupo.
Akaniambia dada ameondoka,
Sijui kaenda wapi, ila hakuwa sawa kabisaa Na amekataa
Kuniambia anapoenda
Wazo lililoniijia haraka haraka ni kuwa ametoroka na Prince.
Hakya Mungu nilitamani njiripue.
Nilienda kwa kila niliyemjua ni mtu wa karibu wa Prince anieleze Prince yuko wapi na mke wangu lakini wote hakuna aliyenipa jibu la Prince alipo, japo nina uhakika
Katika wote wale niliowapitia yupo mmoja ambaye alikuwa akijua Prince alipo, ni vile tu huwezi jua ni nani.
Niliamua kupiga simu nyumbani kwao mke wangu, wakasema hayupo huko, ikabidi niwaeleze kwa ufupi kinachoendelea, na wao wakaanza kuhaha huko, nikajua kabisaa huyu kaenda na
Prince kweli, kama hata kwao hawajui alipo. Baadaye kidogo nikapokea simu ya dada yangu ananiambia mke wangu yupo kwake analia tangu amekuja, ananiomba mimi msamaha na anasema nimtafute mume wake,
Ikabidi niende kwa dada nimeenda nikamkuta kumbe yupo huko, na kumbe kashamueleza
dada kila kitu, akikiri makosa yake na kuomba msamaha
Nikamueleza dada aibu hii yeye angekuwa ndio mimi angeivumilia vipi?!
Nikamwambia dada, hii aibu mimi siwezi ivumilia na huu ukatili niliotendewa na huyu mwanamke ni kama mauti.
Wakati tunaendelea kuongea, ndugu zake mke
wangu walinitafuta kujua nimefikia wapi kumpata mtoto wao, na walinipigia wakiwa kwangu kumbe na wao walikuwa wanahangaika kumtafuta tangu pale nilipowapigia kuwaeleza kupotea kwa mke wangu.
Nikawaambia njooni huku kwa dada ndio yupo huku, niliwaelekeza kwa dada ni wapi wakafika
Niliwaambia kila kitu from A to Z. Hadi wao walijiskia aibu sana kwa kile alichokifanya mtoto wao, wakamuombea msamaha maana alikuwa akilia tangu wamekuja anaomba tu msamaha.
Mimi niliwaambia ni ngumu kuuforce moyo ambao umevunjika namna hii eti uanze kumpenda mtu tena, naomba
Mchukueni mwende naye, siku nikiwa tayari kurudiana naye nitakuja kumchukua.
Na hiyo ndo ilikuwa my final say baada ya mazungumzo yote.
Waliondoka naye, hakutaka kuchukua kitu chochote nyumbani aliondoka hivo hivo, akisubiria hasira zangu ziishe.
Mpaka sasa bado nasubiria moyo
Wangu ukiwa tayari kuwa naye, ndipo nitaenda kumchukua.
Ila kwa alichonitendea, itachukua muda mrefu sana kumsamehe arudi nyumbani.
Eeh bhana sina la ziada. Mwisho wa story yetu