Simulizi: Basi la shetani

Simulizi: Basi la shetani

BASI LA SHETANI: SEHEMU YA-26

Mtunzi: DEO MASSAWE

Idadi ya wagonjwa ilitakiwa kuwa mia nane lakini hadi kufikia siku ya ijumaa wagonjwa zaidi ya elfu moja walikua uwanja wa ndege, matajiri kwa maskini walitapakaa kila kona katika uwanja wa ndege wa kimataifa jijini Kampala kwani safari ilikua ni siku inayofuata yaani jumamosi, matajiri waliokua na wagonjwa wao ambao hawajapata vibali walikua wakiuwa wagonjwa wa maskini kisirisiri ili waweze kuchukua vibali vyao, hivyo katika hifadhi wagonjwa waliyohifadhiwa kulitokea vifo vya ajabu ajabu.Vijana wengi walipata jaira ya kuiba vibali pamoja na kuuwa wagonjwa.
Mainda hakumuacha mama Winny hata kwa sekunde moja licha ya kuonekana mtoto mdogo kuliko watu wote waliokua na wagonjwa pale.
Tajiri mmoja kutoka nchini Kenya alikua anamvizia Winny kuliko maelezo, aliagiza vijana tofauti tofauti watano waweze kuiba kibali cha Mainda, kila mmoaja alikua akimtega Mainda bila mafanikio hadi kufika usiku wa ijumaa bado tajiri huo hakuamini kama mtoto wake aliyekua anaumwa saratani ya damu asingeweza kusafiri kwa ajili ya kukosa kibali,hapo aliwatafuta vijana aliowapa kazi na kuwaongezea dau mara kumi zaidi,
“Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu” walijisemea vijana hao na kuanza kupanga mbinu ya kumuibia Mainda vibali vyake,walikaa kikao cha nusu saa, baada ya hapo wakawa wamepata njia rahisi ambayo walipanga kuitumia siku ya jumamosi kabla ya safari ambayo ilipangwa kuwa saa tano kamili.
***
Fork hata baada ya kuuza nyumba alitaka kabisa kumuondoa Mainda pamoja na mama Winny duniani, hakutaka hata siku moja aje kuingizwa katika matatizo,
“Kweli mchungaji kasema tuuze lakini je kama mchungaji akija kunigeuka?” alijiuliza Fork na kujijibu mwenyewe
“Hapana huyu lazima afe” moja kwa moja aliwasialia kwa barua pepe (E-mail) na majambazi mwenzake wa nchini Uganda ili waweze kummaliza Mainda kabla ya safari, picha ya Mainda ilitumwa na mara moja majambazi wawili walifika katika sehemu waliyohifadhiwa, walimuona na wote wakaanza kupanga namna ya kuwauwa .
***
Mainda alikua na furaha pamoja na huzuni,furaha yake ilikua juu ya mama Winny ambaye alikaua anaenda kupata matibabu na huzuni ilikua juu ya mchungaji Christian, alilia mfululizo lakini licha ya hayo hakujua kama kuna zaidi ya watu saba wanaomuwinda, alikua na matumaini hasa baada ya sauti kusikika kupitia kipasa sauti kuwa wagonjwa wote wawekwe tayari kwani ilibaki nusu saa ndege iweze kuruka kila mgonjwa alikua na mwangalizi wake.
Hali ya hewa ilianza kubadilika taratibu, upepo ulivuma kutoka kusini kwenda kaskazini kwa Kampala,wingu zito lilitanda angani kuashiria mvua ingenyesha mda wowote, kama ilivyo kawaida watu walianza kukimbia kimbia maeneo ya uwanjani hapo.
Mainda alibanwa na mkojo aliouvumilia kwa mda mrefu, alikua katika mstari mrefu wa kukagua vibali lakini ghafla aliingiwa na huruma baada ya kumuona mmama aliyetembea akiwa anagongana na watu, mmama huyo alijifunga kanga nyingi na alivaa miwani, hapo Mainda aliamini ni kipofu, mmama huyo alizidi kutembea na safari hii alitembea na kusimama karibu na Mainda, alikua akipapasa kwa mkono kana kwamba kuna mtu alikua amemshika mkono, Mainda alimuacha mama Winny na kumsogelea mama huyo aliyeonekana akihangaika sana,
“Kuna nini mama?”
“Nimebanwa na haja mwanangu, naomba nisaidie tu, nisije kujidhalilisha hapa” maneno hayo yalimfanya Mainda kuvuta picha pia kwa upande wake jinsi alivyobanwa na mkojo, uliokua unaanza kupenya taratibu, hapo alipata nafasi ya yeye pia kwenda kukojoa, haraka alirudi katika mstari na kumuomba aliyekua nyuma yake amuangalie mgonjwa wake kwa mda , bila ubishi aliyekua nyuma yake alikubali, Mainda alishikilia mkoba wake na kumshika mama huyo mkono hadi msalani, walingia wote lakini bila kutarajia mama huyo alibadilika na kuvua kanga alizokua amejifunga, alitoa chupa mfano wa marashi na kumpulizia Mainda usoni, haikupita dakika tatu Mainda likua amepoteza fahamu, mmama aliyejifanya kipofu alipozitoa kanga mwilini kumbe alikua ni kijana wa kiume aliyepewa kazi na tajiri kutoka Kenya, aliupekua mkoba wa Mainda na kutoa huko kibali cha kusafiria mabacho ndio kilikua kinahitajika, Mainda aliachwa pale chooni akiwa hajitambui.
Kwa bahati mbaya zaidi hata kijana ambaye Mainda alimkabidhi mama Winny naye alikua mmojawapo ya vijana waliokua wamepewa kazi na tajiri kutoka Kenya, hivyo alipoona mwenzake amekamilisha zoezi alijitoa katika mstari na kukaa pembeni.
***
Vijana wawili walioagizwa na Fork kwa ajili ya kuhakikisha Mainda na mama Winny wamekufa walichanganyikiwa baada ya kutomuona Mainda.
***
Mvua kubwa ilianza kunyesha huku dakika zikiwa zimebaki tano kabla ya ndege kuruka watu wote walienda kujificha huku wengine waliokosa namna ya kusafiri walipakiza wagonjwa wao katika magari tayari kwa safari za kuwarudisha makwao.
Mwaili wa mama Winny ukiwa juu ya kitoroli maalumu cha kubebea wagonjwa ulikua ukinyeshewa na mvua, hakuna mtu aliyehangaika nao, watu waliomuona kwa mbali waliamini ameshaaga dunia na wanaohusika nao wamemtelekeza,ndege ilianza taratibu kuiacha ardhi, huku Mainda akiwa chooni bila kujitambua, mlango wa chumba alichokua ulitiwa kufuli hivyo hakuna mtu aliyeweza kuingia humo na hakuna mtu aliyehisi kama kuna mtu ndani.
Majambazi walioagizwa na Fork waliusogelea mwili wa mama Winny huku wakiwa na miamvuli waliburuza toroli lililombeba hadi sehemu ya maegesho walipoegesha gari lao kwani baada ya kutoa taarifa kwa Fork kuwa Mainda haonekani walipewa amri ya kuuchukua mwili wa mama Winny waende kuutupa msituni au katika sehemu yoyote ambayo hatapona. Kitendo cha kutoka naye hakikuwashtua watu kwani kila aliyeona alijua ni mgonjwa aliyekosa nafasi ndani ya ndege.
Gari aina ya Vits ilikamata barabara ya kutoka uwanja wa ndege (KAMPALA ROAD) lengo lao likiwa ni kuenda kumuhifadhi ndani hadi usiku ili waweze kwenda kumtupa sehemu moja iitwayo Speena Beach Entebbe, gari ilitembea kwa kasi mwili wa Mama Winny ukiwa umelazwa viti vya nyuma.
TUNNED ROAD ilikua ni barabara inayotokea upande wa ziwa Victoria ambayo barabara hiyo ilipita malori makubwa yaliyobeba samaki kupeleka uwanja wa ndege, kutokana na hali ya mvua ya siku hiyo lori moja likashindwa kukunja kona ili kuikamata barabara ya Kampala ajali kubwa ikawa imetokea na kuzuia magari kupita, foleni ikaazia kutoka Uwanja wa ndege, hakuna gari iliyoweza kuenda wala kurudi.wakati huo Majambazi wa Fork walikua karibu na CAVE AVIATO BAR & RESTAURENT palikau ni mahali tulivu kwa kujipatia chakula na vinywaji lakini palikua na sifa mbaya ya wizi wa magari mara kwa mara,
“Tuingie hapa tunywe supu” aliogea jambazi mmoja na mara dereva alikunja kushoto na kuegesha gari nje ya mgahawa huo, moja kwa moja bila kujua kama kuna wezi waliokua wanawasomea ramani walikamata viti na kuketi .
Kwa haraka majambazi waliokua wanafanya wizi katika mgahawa huo waliwasiana na wapishi na mara moja supu waliyoagiza ikawekwa madawa ya kulevya, haikupita dakika kumi, wote walisinzia na kulala fofofo,bila kupoteza mda funguo za gari walizoweka mezani zilichukuliwa na wezi wawili na moja kwa moja wakaenda na kuondoa gari kwa kasi ya ajabu, foleni iliyokua barabarani kutokana na ajali ya lori ilikatika baada ya lori lililoangauka kusogezwa pembeni, magari yalikua yakienda kasi kufidia mda waliosimama, hakuna askari wa usalama barabarani aliyesimamisha gari kwani walijua kila mmoja ana haraka kutokana na kukaa kwenye foleni kwa mda mrefu.
“Baada ya kutembea kwa kilomita kumi na tano ndipo mmoja kati ya hao majambazi wawili alipogeuka katika viti vya nyuma na kushangaa kukuta mtu aliyelazwa.
Waliamini mtu huyo amekufa kwani walivyomtikisa hakuwa anaongea kitu wala hakusikia akihema.
“Itakua ni hawa waliotakiwa kuenda kutibiwa nje sasa amekufa akachwa, huyu tutatafuta watu wampeleke mochwari, sio vizuri tumtupe” alitamka dereva huku gari ikiwa inaenda kasi ya ajabu.
***
Siku hiyo mochwari zilikua zinapokea maiti kwa wingi sana hiyo ni baada ya wagonjwa wengi kutolewa hospitalini na kushindikana kusafirishwa hivyo wengine walikufa kwa kutikiswa wengine waliuwawa kutokana na familia kuhofia gharama, hivyo katika sehemu za kuhifadhia maiti zilizo karibu na uwanja wa ndege zilikua zikipokea maiti mfululizo , ilifika mahali hata ikawa maiti ikiletwa haipimwi, ili kuokoa mda ilikua inapelekwa katika majokofu moja kwa moja bila kuthibitisha kama mtu ameaga dunia au la…

INAENDELEA

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI: SEHEMU YA-27

Mtunzi: DEO MASSAWE

Serikali ya Uganda kupitia wizara ya mambo ya ndani ilitangaza hali ya hatari kwa maafa ya wagonjwa wa saratani hasa katika jiji la Kampala, wageni wengi waliopeleka wagonjwa kutoka sehemu tofauti tofauti walitelekeza wagonjwa katika vyumba vya kulala wageni, wengine barabarani, hivyo serikali ikatoa kikosi maalumu cha kuhakikisha maiti yoyote itakayopatikana ipelekwe sehemu husika kuhifadhiwa.
***
Wezi walioiba gari iliyokua na mwili wa mama Winny waliendesha gari hadi karibu na hospital ya Entebbe General Hospital (EGH) bila kupoteza mda walichukua karatasi kuandika jina Ester Wangari kutoka Kenya,kisha waliegesha gari na kuita vijana fulani waliokua pembeni ya barabara,waliwapa kazi ya kuutoa mwili mwa mama Winny ili waweze kuupeleka hospitalini hapo,kutokana na hali iliyokua ikiendelea huko Uganda haikushangaza watu kuona mwili wa mtu ukibebwa na kupelekwa mochwari kwa mda huo, ilikua ni majonzi kwa taifa zima.
Kama ilivyo kawaida ya kutokea fursa katika matatizo basi kwa waliohusika na kuhifadhi mwili walikua wakitaka rushwa kwa kisingizio cha majokofu kujaa,
“Masanduku yamejaa, hivyo maiti yenu haitapata sehemu ya kuihifadhi labda tusubiri nyinginme zitoke” lilikua jibu kutoka kwa wahusika wa mochwari, lakini kila mtu alipotoa kitu kidogo basi alipewa nafasi ya kuhifadhi maiti yake,
“Huyu atakua mkenya tumemuokota barabarani nae” alitamka mmojawapo ya kijana aliyeupokea mwili wa mama Winny, kwa bahati nzuri mama Winny hakuwekekwa kipao mbele kwakuwa hakuletwa na watu wanaoleweka, mwili wake ulilazwa sakafuni,
“Ngoja kwanza tuhifadhi za wenye pesa” alijisemea mkuu wa mochwari hiyo ya (EGH).
***
Msimamizi wa vyoo , alishangaa kuona mlango mmoja wa chumba ukiwa umefungwa kwa kufuli tofauti na zinazotumika mahali pale ikiwa imepita masaa manne, alikisogelea na kuikagua kufuli vizuri hakujua ina maana gani hapo alimuita mfanya usafi wa choo hicho, hapo ndipo waliamua kukivunja, walipigwa na butwaa baada ya kumkuta msichana mdogo akiwa amelala, walipiga kelele na watu wakajaa eneo lile kushuhudia kile kitendo,hakuna mtu aliyejua kilichosababisha hadi yule msichana kuwa mahali pale, walimsachi katika mkoba wake uliokua chooni hapo na wakatambua ametokea Tanzania ,
“Awahishwe hospital bado anahema” alitamka mmoja wa watu waliokua wamemzunguka baada ya kumshika kifuani na kukuta mapigo ya moyo yakidunda, haraka gari la kubebea wagonjwa lilifika na haraka safari ikaanza ya kuelekea Entebbe General Hospital, hakika hospital hiyo ndiyo iliongoza kwa kupokea wagonjwa pamoja na maiti kwa siku hiyo, haraka alitundikiwa chupa za maji huku akipewa msaada wa kupumua kwa mashine.
Baada ya nusu saa Mainda alizinduka,
“Mama, mama, wanataka kuniua, Mungu tusaidie, Mungu mlinde mama Winny” Mainda alipiga kelele huku akichomoa sindano za mipira zilizokua zinamuongezea maji pamoja na kuondoa mashine iliyokua inamsaidia kupumua, wauguzi walifika na kumtuliza,
“Mama Winny yupo wapi, naomba mnisaidie kumuwahisha kwenye ndege akatibiwe anaumwa sana, naomba fanyeni haraka wameshatangaza kuwa zimebaki dakika tano nisaidieni tafadhali”maneno ya Winny yaliwafanya wauguzi kuchanganyikiwa wasijue la kufanya,
“Ndege ilishaondoka zaidi ya masaa matatu” alijibu muuguzi mmoja, Mainda hakuamini maneno hayo, alijikuta akishiwa nguvu hasa baada ya kuambiwa kuwa amekutwa chooni akiwa hajitambui, machozi yalimtoka mfululizo,
“Mama Winny yupo wapi sasa”, aliuliza Mainda huku akitoa maelezo ya jinsi alivyosafiri kutoka Tanzania na mgonjwa wake hadi pale alipoombwa na kipofu aliyeenda kumgeuka chooni, wauguzi wote walimuonea huruma,
“Naombeni basi mumtafute mama yangu” alisisitiza Mainda lakini hakuna mtu aliyemwelewa kwani ilikua vigumu kumtafuta mtu ambaye alikua mgonjwa kiasi kile,
Kwa asilimia zote Mainda aliamini kuwa mama Winny ameshaaga dunia,
“Kama hajafanikiwa kusafiri basi atakua ameaga dunia” alijisema Mainda huku akijiwa na wazo la kutembelea sehemu za kuhifadhia maiti,bila kupoteza mda alinza katika hospital aliyopelekwa, alitoka nje huku akiacha mkoba wake wodini, mita mia moja na hamsini ndipo mochwari za hospitali hiyo zilikua, Mainda alionekana kama mtu aliyerukwa na akili.
***
Serikali ya Uganda pia ilimwaga wakaguzi kila kona huku wengine wakitembelea mahospitalini ili kuhakikisha huduma za dharura zinatolewa, kwa ubora, wanaohusika na kupokea maiti walizibeba maiti zilkizokua sakafuni kwa kutolipiwa kitu kidogo na kuzihifadhi ili kukwepa mkono wa sheria, kitendo hicho kilipelekea mwili wa mama Winny kuwekwa ndani ya jokofu,palikua ni sehemu yenye ubaridi uliotengeneza barafu, pia kulikua na harufu kali.
Mainda aliingia katika chumba hicho, akiamini kama mama Winny atakua ameaga dunia basi lazima angekua amehifadhiwa sehemu hiyo, hakuwa na hofu kuingia sehemu hiyo,
“Jamani kuna mama mmoja ameletwa hapa anaitwa Lusia au mama Winny, ni mimi nilikuja nae nahisi kama atakua ameaga dunia atakua amehifadhiwa hapa” Mainda alijieleza mapokezi na moja kaa moja alipewa ruhusa na kuingia ndani, hakuchelewa alinyooka moja kwa moja hadi katika jokofu ambalo walikua wakifunga,
“Samahani masisita, kuna mgonjwa wangu anaitwa mama Winny au Lusia, alikua na kidonda shingoni, sijui yupo hapa”, Mainda aliuliza,
“Mwenye kidonda ni huyu hapa kwenye jokofu lakinia nanitwa Ester Wangari” alijibu muuguzi mmoja na huku akifungua mlango wa jokofu hilo,
Mainda alidondoka chini baada ya kuuona mwili wa mama Winny ukiwa ndani ya jokofu,
“Kwa nini umeamua kunitoka mapema hivi, nitaishi na nani ? amka mama amka tafadhali”, Mainda alilia kwa uchungu lakini wauguzi walipofungua jokofu lile walishangaa kuona mmama huyo akijaribu kurusha mikono kwa shida,
“Itakua hajafa, lakani tukimtoa ni aibu kwetu na pia tunaweza kuchukuliwa hatua” alisema muuguzi mkuu,
“Hapana kama hajafa tumtoe tu uhai wa mtu ni wa muhimu zaidi ya kazi zetu” aliongea sista mmoja na bila kutarajia Mainda alishuhudia mwili wa mama Winny ukitolewa na moja kwa moja ulipelekwa wodini, chupa za damu na maji zilitundikwa haraka pamoja na mashine ya kumsaidia kupumua,
“Ndio alitaka kukata roho mda sio mrefu” wauguzi walinong’onezana huku matibabu yakiendelea.
Baada ya siku kumi na tano mama Winny alikua amepata nafuu kidogo, aliweza kuongea japo ka shida, aliumwa sana kichwa na mishipa ya shingo Mainda alikua naye karibu alisali usiku na mchana kumuomba Mungu amnusuru.
***
Siku ya Ishirini ilikua mwisho wa huduma za bure katika hospital hiyo ambayo ilikua ikitoa huduma kwa siku 20 za mwanzo kwa mgonjwa yeyote. Hapo Mainda hakua na lakufanya zaidi ya kuondoka na mama Winny aliyeweza kutembea kwa tabu, alitumia lisaa lizima kutembea mita mia moja, afya yake ilidhoofika sana, waligeuka kuwa omba omba katika jiji la Kampala,
“Hapa nakusanya tu nauli ya kurudia Dar es salam nikawe tajiri”, alijisemea Mainda kila alipowaza kuhusu hela nyingi alizoacha ndani ya nyumba aliyoachiwa na Edson. Alipoomba msaada na nauli kutoka kwa matajiri huko Uganda alionekana kama mtu aliyerukwa na akili,
“Wewe umevaa matambara alafu unasema una hela nyingi nyumbani, ? toka ofisini kwangu haraka” yalikua majibu aliyopewa baada ya kuingia katika ofisi za watu binafsi, na kweli alionekana mchafu kupita kiasi, alioga kwa kunyeshewa mvua yeye na Mama Mainda,
“Mwanangu wewe niache tu nife peke yangu, umesimama na mimi vya kutosha Mungu atakulipa” mama Winny alimwambia Mainda baada ya kuelezewa mapito yote aliyopita nayeye,
“Kama kweli unataka nikusaidie, kubali masharti yangu, mimi nitakupeleka hadi nyumbani kwako lakini nitafanya na wewe mapenzi maana nimekupenda, kisha nikikufikisha kwako utanilipa pesa zangu je umekubali?” ni jibu ambalo lilimchanganya Mainda baada ya kuomba msaada kwa kijana mmoja wa kiganda, hakika lilikua swali gumu Mainda aliwaza mengi lakini kila alipovuta picha ya maisha anayoishi pale Uganda alipachukia,
“Nitakujibu kesho” Mainda aliagana na kijana huyo akimwahidi kumjibu kesho,
“Sawa ni wewe tu ukiamua kukaa hapa uteseke au nikupeleke nyumabni kisha nifanye na wewe mapenzi”. Alimaliza kijana huyo.

INAENDELEA

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI: Sehemu YA-28

Mtunzi: DEO MASSAWE

Ulikua usiku uliojaa mawazo katika kichwa cha Mainda,
“Mama kuna mtu anataka kuniingilia kimwili ili aweze kunipa msaada wa mimi na wewe kufika Dar es salam” Mainda alimwambia mama Winny lakini hakupewa jibu zaidi ya kumuona mama Winny akiinama na kulia kwa uchungu, alijiona mzigo kwa Mainda, manyunyu yaliyowanyeshea nje ya duka la wahindi yalilizidi kufanya hali ya ubaridi izidi kuwakamata, walijilaza sakafuni wakiwa wamekumbatiana,
“Potelea mbali, sitoi mwili wangu heri tufie hapa” alijisemea Mainda huku akilifuta wazo la kuenda kutoa rushwa ya ngono, alibaki akiombaomba hapo jijini Kampala kidogo alichopata alikitumia kumnunulia mama Winny dawa za kumkausha kidonda.
***
Licha ya msitu wa Amazon kuwa na wanyama wa kila aina pia kulikua na aina nyingi za miti, baadhi ya miti hizo kulikua na zenye uwezo wa kutengenezea dawa za kutibu magonjwa mbalimbali, pia kulikua na miti yenye sumu pamoja na miti ya maajabu, aina zote hizo za miti Mazengo alizijua, kwa mda alioshi msituni hapo aligundua dawa nyingi sana, siku baada ya siku alizidi kuzoeana na wanyama wakali, kitu kilichompa nafasi nzuri ya kukusanya mizizi ya dawa kwa ajili ya kuja kusaidia watu waliokua na magonjwa mbalimbali,
“Nataka nikasaidie watu wenye matatizo kama marehemu mke wangu,” Mazengo alijisemea huku akitokwa na machozi, kila alipomkumbuka mkewe aliinamisha kichwa chini na kumuombea kwani alimini kwa asilimia zote alikua marehemu.
***
Baada ya mwaka mmoja tangu Martin anze kutumikia kifungo gerezani, serikali ya Tanzania iliamua kufanya mabadiliko katika muundo wa mahakama, hivyo kila kitu kuhusiana na mahakama kikawa kimebadilishwa,
“Ah hapo sawa sahivi nitakua huru, mkuu wa magereza ni rafiki yangu,waziri wa mambo ya ndani ni rafiki yangu, mkuu wa jeshi la polisi Tanzania ni rafiki yangu, sasa mimi nitaishi gerezani kwa sababu gani?” Martin alijisemea pale alipopata taarifa juu ya mageuzi yaliyofanyika , asilimia kubwa ya watu waliopata nyadhifa za juu walikua marafiki zake wakubwa.
BAADA YA WIKI MOJA.
Tayari Martin aliachiwa huyu baada ya mkuu wamagereza kutembelea gereza la Segerea na kumuona rafiki yake,
“Lakini bwana Martin unatakiwa usafiri nje ya nchi, ukakae huko kwa kipindi chote ambacho ulitakiwa kukaa hapa gerezani”
“Hilo halina tatizo, nataka nikafanye kidogo mazoezi ya mwili, nataka kuenda kujifunza mbinu mbalimbli za kupigana , naskia Thailand ndio wako vizuri kuhusu hili” aliongea Martin na haraka alianza kupeleleza kuhusu waalimu wa Kung fuu, hapo ndipo alipata jina la VAJIRALONG kutoka BANGKOK, THAILAND, alifanya nae mawasilino kupitia Website (tovuti) walielewana na Vajiralong alikubali kumpa mafunzo . Safari ya kuelekea kisiwa cha Phayao iliandaliwa mara moja.
***
Wachina waliomuokoa Mazengo waliandaa sherehe kubwa ya kumuaga baada ya kuhitimu mafunzo, kila mmoja alikua tajiri kutokana na biashara walizobuni kutokana na mitaji ya kuuza madini, zawadi za kila aina zilinunuliwa magari zaidi ya mia moja yalinunuliwa kwa ajili ya mazengo, pamoja kiasi kikubwa cha pesa tofauti na ambazo aliwekewa katika account yake, Siku zilisogea taratibu Mazengo akiwa na Vajiralong,
“Kuna mwenzako anakuja kujifunza mafunzo kama ya kwako, anatarajia kuingia hapa kesho hivyo wakati kesho ukifanyiwa sherehe ya kuagana mimi nitakua napokea mwanafunzi mwingine, mimi nakubariki kwa mikono miwili, ukakae salama, umuamini Mungu ndiye anaweza kila kitu, usipigane bila sababu ya msingi, haya mafunzo niliyokupa ni yako ya kujilinda na sio kuanzisha vita au kuonea watu labda unaweza kumfundisha mtu wako wa karibu pia naamini katika msitu niliokupeleka kule Amazon umejifunza mambo mengi ikiwa ni pamoja na dawa za magonjwa mbali mbali, hapo ukizidisha ujuzi katika hayo madawa utapata hadi dawa za kutibu UKIMWI pamoja na dawa moja inayopatikana katika hiyo miti ya maajabu ambayo inaweza kurudisha umri wako nyuma au ukampa mtu yeyote na umri wake ukarudi nyuma lakini kama hujui hiyo dawa inaweza rudisha maisha ya watu watano pekee, sasa ni wewe utaangalia nani wa kumrudisha,” ulikua wosia wa Vajiralong kwa Mazengo.
***
Siku ya jumamosi asubuhi uwanja mkubwa ulio nje kidogo ya kisiwa cha Phayao kilitawaliwa na shamrashamra, matajiri wengi walifurika mahali pale, ulinzi uliiimariswa huku Mazengo akiwa ndiye mgeni rasmi wa sherehe hiyo, mda wote alionekana mwenye mawazo, kila alipofikiria jinsi maisha yake yanavyoelekea kuwa mazuri bila mkewe kuwepo aliona mali atakazopata hazina thamani, wala hatafurahia maisha yake. Saa nne kamili sherehe zilianza rasmi watu wengi walihutubia ikiwa ni pamoja na Mazengo kuonesha mafunzo aliyopata, wachina wote walifurahi kumuona mtu aliyewasababishia utajiri akiwa amepata mafunzo ya kutosha.
Kutokana na sababu zilizokua nje ya uwezo wa marubani ndege ambayo ilitakiwa kumfikisha Martin katika kisiwa cha Phayao ilichelewa hadi sherehe kuisha , hivyo wakati Mazego akiaga ndipo ndege iliyombeba Martin ilitua uwanjani hapo. Martin alipokelewa na Vajiralong huku kwa mbali Mazengo akiwa katika gari maalumu kwenye msafara wa kuelekeaa katika meli iliyokua imebeba zawadi zake, Meli hiyo ilikodiwa maalumu kuhakikisha Mazengo anafika nyumbani Tanzania.
***
GSG (Germany Security Group) kilikua kikundi maalumu kilichokua kinatoa huduma ya ulinzi nchini Tanzania huku makao makuu ya kikundi hicho yakiwa jiji Dar es salam nchini Tanzania, wajerumani hao walikua wakitoa huduma bora ya ulinzi, walikua na silaha za kutosha, mbwa wakali na wenye mafunzo ya hali ya juu, hakika kilikua kikundi namba moja cha ulinzi nchini Tanzania, kila kampuni au mtu binafsi aliyekodisha ulinzi kutoka katika kampuni hiyo alipewa mbwa mwenye mafunzo ya hali ya juu, pamoja na hayo makao makuu ya kikundi hicho ilikua nyumba ambayo Mainda aliachiwa na Edson.Siku moja katika hali ya kushangaza magaidi kutoka katika kikundi cha Al Queda waliweza kuvamia makao hayo makuu na kuiba silaha nyingi pia katika uvamizi huo waliweza kusababisha vifo vya walinzi kadhaa, pamoja na mbwa watano waliokua muhimu zaidi, kitendo hicho kiliwatia hasira wajerumani na kuamua kuagiza walinzi wenye mafunzo makubwa zaidi kutoka katika nchi za Urusi na Israel, ulinzi uliimarishwa katika jengo hilo, mbwa wakali na wenye mafunzo waliagizwa kutoka Marekani na China.
“Ilikua marufuku kwa mtu yeyote kuingia katika jengo hilo, matangazo yaliwekwa mtu kutosogelea nyumba hiyo kwa mita hamsini bila idhini.
***
Mazengo aliwasili nchini Tanzania baada ya wiki tatu, hakutaka kujulikana na watu moja kwa moja alienda hadi Kibaha huku magari yake pamoja na vitu vyote vikihifadhiwa katika ghala ya magari maeneo ya Posta, hakuona sababu ya kupoteza muda zaidi ya kuanza kutoa dawa kwa watu waliokua na matatizo mbalimbali,
“NABII ANAYEPONYA MAGONJWA MBALIMBALI AMETOKEA HUKO KIBAHA” zilikua habari zilizogonga vichwa vya habari kote duniani, Mazengo alitoa huduma pasipo malipo yoyote, mizizi aliyotoka nayo katika msitu wa Amazon ilichemshwa na kuwa dawa, watu walipeleka wagonjwa waliokua wamezidiwa na wote walipona, watu wengi kutoka kote duniani waliifuata tiba hiyo, foleni ilikua kubwa lakini hakuna hata mtu mmoja aliyejua kama ni mazengo kwani alivaa sura ya bandia, waandishi wa habari walipomfuata kumhoji alitishia kutokutoa dawa endapo atafuatiliwa,
“Mimi ni binadamu wa kawaida na nipo kuwasaidia binadamu wenzangu” lilikua jibu kutoka kwa Mazengo kila alipoulizwa na waandishi wa habari.
Pamoja na watu waliopata taarifa hiyo ya kuponywa magonjwa ni Mainda , alitamani sana kuona mama Winny akipata huduma hiyo, lakini kilichomsumbua ni juu ya kufika Tanzania kutokana na kuomba msaada pasipo kupewa.
Mainda akiwa anaendelea kuzurura katika jiji la Kampala alifanikiwa kupewa msaada wa dola mia, alilia kwa furaha, alimshukuru mama wa kizungu kwa kumpa kiasi hichgo cha pesa lakini yote hayo ilikua baada ya kuokota mkoba uliodondoshwa na mzungu huyo na kumrudishia ndipo alipopewa kiasi hicho cha pesa.
“Asante Mungu sahivi nitarudi nyumbani na moja kwa moja mama Winny ataenda kupata tiba” alijisemea Mainda kwa furaha huku akiuangalia ufunguo wa nyumba aliyachiwa na Edson.
“Asante Mungu kwa haya yote unayotenda juu ya maisha yangu, naomba unifikishe nyumbani salama na mama Winny akapone tuendelee na maisha kama zamani” alijisemea moyoni huku akijiandaa na safari.
Winny nae hakua nyuma pale alipopata taarifa ya nabii aliyetokea huko Kibaha, alifurahi kusikia kuwa anaponya hadi ukimwi, mara moja alipanga safari baada ya kuamaini atapona aliamua kuuza nyumba yake aliyojenga huko Mwika ili aweze kurudi jijini Dar es kuanza maisha mapya, hivyo haraka alifanya mawasiliano na madalali.
***
Kwa kutumia basi lililokua linafanya safari zake kutoka katika jiji la Kampala hadi Dar es salam lijulikanalo kama Kampala Express Mainda na mama Winny walikaa siti za nyuma huku wote wakiwa na matumaini ya kuanza maisha mapya, furaha ilizidi baada ya kuona wakiingia katika jiji la Dar es salam majira ya saa tano usiku katika kituo cha mabasi Ubungo,
Kwa kuwa mama Winny alipoondoka nyumbani alikua hajitambui basi hakujua kitu chochote kuhusu nyumba aliyokua anakaa kabla ya kusafiri kwenda Kampala.
“Mama hakuna haja ya kulala hapa kituoni maana nyumba ambayo tulikua tunakaa ipo karibu tu hapo tunaweza chukua hata usafiri wa bajaji”
“Sawa mwanangu kama kuna usalama na una uhakika na tunapoenda basi sawa twende mwanangu, Mungu atatusaidia “baada ya kusema hayo walikodi bajaji lakini dereva aliwapa sharti la kuwaacha katika chuo cha Ustawi wa jamii mita chache kutoka nyumba ilipokuwa.
Baada ya dakika kumi tayari walikua wameshashuka katika bajaji, walitembea taratibu, Mainda aliikumbuka njia iliyoelekea katika nyumba hiyo lakini alishangaa jinsi kulivyokua na utulivu wa hali ya juu,Mita hamsini za mraba kuzunguka nyumba hiyo hakukuwashwa taa yoyote hivyo giza lilitawala.
Mbwa kiongozi wa kikundi hicho cha walinzi alikua na mafunzo ya kukariri harufu za watu katika nyumba ile, katika harufu alizokua amekariri ni pamoja na ya mama Winny pamoja na Mainda na hiyo ilitokana na kule ndani kubaki na baadhi ya nguo walizokua wakivaa hivyo Mainda na mama Winny walifanikiwa kufika hadi katika lango la nyumba hiyo bila mbwa kubweka. Walinzi zaidi ya watano walikua ndani ya geti, walikaa tayari kwa hali yoyote ya hatari na kikubwa walitegemea mbwa kubweka kwa hali yoyote ya hatari.
“Mainda alitoa funguo wa mlango mdogo wa geti, akaweka mkoba chini na kuupenyeza katika tundu, mlango ulifunguka lakini kutokana na giza bado hakuona kitu chochote.
Walinzi walishtuka sana mlango kufunguka pasipo mbwa kubweka, hivyo moja kwa moja midomo ya bunduki ilielekezwa mlangoni, pengine walihisi labda mbwa wao wameshalishwa sumu,
“Ingia mama ngoja nichukue huu mkoba”, Mainda alimpisha mama Winny apite ili yeye abaki nyuma kwa ajili ya kuingiza mizigo, lakini katika hali ya kushtukiza Mainda alishtuka kusikia milio mitano ya risasi pale mlangoni, alichanganyikwa na kupiga kelele, alisikia kishindo cha mtu kuanguka chini na moja kwa moja alijua ni mama Winny, taa ziliwashwa haraka uvumilivu ulimshinda na kuamua kuingia ndani na geti, kwa macho yake aliuona mwili wa mama Winny ukiwa ardhini huku ukivuja damu,mama Winny alikua akirusha mikono kuomba msaada, lakini Mainda alipojaribu kuinama kwa ajili ya kumsaidia nayeye alipigwa risasi ya mkono iliyompelekea kupoteza fahamu..

the Legend☆
 
BASI L A SHTEANI: SEHEMU YA-29

Mtunzi: DEO MASSAWE

Ulinzi uliimarishwa maradufu, walinzi wote walijiandaa kwa silaha, huku mwili wa mama Winny na Mainda ukichukuliwa hadi stoo,' taarifa ilitumwa kwa mkuu wa kampuni hiyo ya ulinzi aliyekua nchini Korea kaskazini kwa shughuli za utafutaji wa silaha, na mara moja alitoa amri ya kuwaweka wanawake hao chini ya ulinzi mkali, alitoa pia amri ya kuwapa matibabu ili waweze kuja kuchunguzwa vizuri, hivyo aliamrisha kuwakuta wakiwa wazima, hapo mara moja daktari wa kikundi hicho aliitwa na kuanza kutoa matibabu mara moja katika chumba cha matatibabu, mama Winny alikua amepigwa risasi katika miguu yote miwili,huku marina akipigwa risasi ya mkono, chupa za damu na maji zilitundikwa kwa haraka kutokana na damu nyingi iliyopotea, zoezi la kutoa risasi zilizoingia mwilini lilianza huku wote wakiwa hawajitambui.
Bado walinzi walishangaa hadi wakati huo mbwa kutobweka, zaidi mbwa walikua wakiongeza ulinzi,
“Itakua kuna kitu hapa maana sio kawaida watu wageni kuingia na mbwa kutobweka” waliongea walinzi lakini bado mbwa walikaa pembeni ya vitanda ambavyo Mainda na mama Winny walilazwa.
Baada ya nusu saa daktari alikamilisha zoezi la kuwashona vidonda na wakawa chini ya ulinzi mkali.
Kwa mtu aliyekua na uelewa juu ya mbwa alijua dhahiri kuwa mbwa wote walikua na huzuni juu ya tukio la Mainda na mama Winny, mbwa walikua wamekaa kwa huzuni huku ndimi zao zikiwa nje.
Baada masaa matatu Mainda alizinduka na kujikuta katikati ya walinzi waliokua na bunduki, mapigo ya moyo yalienda kasi,
“Mungu nisaidie” lilikua neno la kwanza kutamka baada ya kuzinduka, mkono wake ulikua umetundikwa juu, huku akijihisi maumivu, tukio la milio ya risasi lilimjia kichwani na hapo ndipo alikumbuka juu ya kishindo cha mama Winny kuanguka chini kwa asilimia kubwa aliamini kuwa mama Winny ameshaaga dunia,
“Hapa ni wapi?” aliuliza Mainda lakini hakujibiwa kitu chochote zaidi ya sauti yake kurekodiwa, walinzi waliokua pembeni yake hawakuruhusiwa kuzungumza nae kitu chochote.
Mainda alipojichunguza alikua amefungwa kwa pingu miguu yote pamoja na mkono wa kushoto, alitupa jicho pembeni na kumuona mama Mainda, kumbukumbu za kitu kilichokua mbele yake kilikua ni hitaji la dawa, kwa mama Winny, hakujua kama angeweza tena kufikia zile dawa.
BAADA YA WIKI MBILI.
Kiongozi huyo wa GSG alirejea huku akiwa na hasira, aliamini Mainda na Mama Winny walikua na mpango waliiotaka kuufanya lakini ikashindikana,
Kiongozi huyo aliitwa Mackon ambaye akiwa nchini Tanzania aliambatana na mkalimani wake kwa jina la Jackson,
“Dada!, huyu anaakuuliza kuwa wewe ni nani na kwa nini ulitaka kuvamia tena hili jengo kama mlivyovamia mara ya kwanza na kundi la Al queda kwani huwa unalipwa kiasi gani cha pesa?” swali hilo ambalo Jackson alilifafanua kutoka kwa Mackon likimuendea Mainda na kumshtua sana, aliinamisha kichwa chini na kuanza kuelezea jinsi alivyoachiwa nyumba ile na Edson, alitoa maelezo ambayo yalichukua dakika kumi na tano lakini Mackon aliona kama binti huyo anacheza na akili zake, mara moja aliamuru Mainda apelekwe katika chumba kidogo kilichojenga pembeni kidogo,
“Sema ukweli” Jackson alizidi kumsisitiza Mainda aseme ukweli lakini hakuweza kuongea zaidi na happo ndipo Mackon aliamua kumning’iniza juu na moto kuwashwa chini, kuni mbichi zilikwekwa chini moshi mkubwa ukavuka na kumwingia Mainda kisawasawa, mbwa bado walikua wakihuzunika kwa kitendo kile, mbwa waliamini watu wale ni watu walioshi katika makazi yale lakini kwa kuwa hawakuweza kusema lolote waliishia kuhuzunika.
Mainda alilia kwa uchungu hasa alipowaza kuhusu mama Winny, ndoto za kupata dawa iliyokua ikitolewa na nabii huko Kibaha ilipotea.
Baada ya mateso makali Mainda alirudishwa ndani na kufungwa pingu, walinzi hawakujali juu ya mkono wake ulioumia, zaidi walikua wakimsubiri mama Mainda apate nafuu ili nayeye aweze kuteswa ili waweze kupata uhakika kama wao ndio walihusika na hadi magaidi wa kikundi cha Al quide kupenya katika jengo hilo bila kuonekana.
***
Huduma ya Mazengo ilianza kuingia dosari kote duniani, makampuni ya kutengeneza madawa yalianza kupata hasara kwa watuamiaji kupungua, wagonjwa wa UKIMWI waliotumia dawa kutoka kwa Mazengo walipona na kuachana na dawa za ARVs walizokua wakitumia, pia mahospital mengi ya kibinafsi yalianza kupata hasara baada ya kushindwa kujiendesha, wagonjwa wengi walitolewa hospitalini na kupelekwa kwa Mazengo, hivyo vikao vya siri vilianza mara moja baina ya watu wenye makampuni ya kutengeneza dawa pampja na mahospital binafsi, kilikua kikao cha kuhakikisha Mazengo anatokomezwa na utoaji wake wa dawa unasitishwa.
kikao kilikamilika baada ya wiki moja, pesa nyingi zilichangwa kwa ajili ya magaidi watano wakubwa walioandaliwa kwa ajili ya kusafiri kutoka Marekani hadi nchini Tanzania kwa lengo la kuja kumwangamiza Mazengo, kikundi hicho kiliongozwa na gaidi kwa jina la Crowl ambaye aliwahi kushiriki katika matukio makubwa ya kihalifu nchini Marekani na hakuwahi kushindwa katika kazi yoyote aliyopewa, hakuwa tayari kuikosa shilingi Bilion mia moja aliyoahidiwa endapo angemteketeza Mazengo, hivyo alihakikisha timu yake inakua imara kwa kazi iliyokua mbele yao pia wakati wakisubiri Crowl aje kumuangamiza Mazengo waliendelea na kazi ya kubuni aina mbalimbali za magonjwa ili waweze kuusambaza na kuanza kuuza dawa kufidia hasara waliyopata.
***
Martin alichanganyikiwa baada ya kupata taarifa ya UKIMWI kutibiwa nchini Tanzania, aliwaza ni kwa jinsi gani angeweza kutoka katika mazoezi aliyoyafuata nchini Thailand,
“Lazima nipate hii tiba kutoka kwa nabii” alijisemea Martin huku akipanga mipango ya kumtoroka mwalimu wake, alifanya mawasiliano kisiri siri na matajiri ambao waliagiza ndege hadi jijini Bangkok,
“Naona unataka kusafiri kwa kuenda kupata huduma huko nyumbani kwako, nakupa siku kumi uweze kusafiri na kurudi” yalikua maandishi kutoka kwa Vajiralong kutokana na uwezo wake wa kujua hisia za mtu juu ya kitu anachowaza .Martin alipewa ruhusa na mwalimu wake na haraka alianza safari , alitakiwa kusafiri kisirisiri, hakutaka kujulikana kabisa, aliandaa walinzi wake ambao walitakiwa kumlinda afikapo nchini Tanzania.
***
Winny alifanikiwa kuuza nyumba na kusafiri hadi Kibaha, katika uwanja ambao Mazengo alitolea huduma kulijaa watu, wagonjwa waliozidiwa walipewa kipaombele cha kuwahi huduma hiyo, kazi ilikua usiku na mchana, watu kutoka nchi zote walikua eneo hilo, jeshi la polisi liliamini kila alieykua maeneo hayo alikua akihitaji dawa hivyo hawakuzingatia sana ukaguzi wa watu waliotoka nchi za nje kuja pale, ndege zenye uwezo wa kutua katika viwanja vya kawaida zilitua mahali pale, bila kukaguliwa kitendo hicho kilimsaidia Crowl na kundi lake kufika pale bila tatizo.
***
Mainda na mama Winny walionewa huruma na mmojawapo wa walinzi waliokua wakiwalinda,
“Dada nataka kukuokoa maana hapa mtakufa”
“Nitakushukuru sana, naomba nisaidie tu niokoke nataka kuenda kupata dawa huko Kibaha, huyu mama anaumwa sana, mimi sitakuja tena hapa”
“Upo tayari nifanye na wewe mapenzi alafu usiku wa leo nikutoroshe ?”
“Ndio nipo tayari”, Mainda hakuona thamani ya mwili wake lengo lake lilikua kuokoka mikononi mwa Macknon, afya ya mama Winny iliyokua inazidi kudhoofika ilimfanya kukubali kutoa mapenzi kwa mlinzi wa zamu ili aweze kutoroshwa usiku huo.
Mainda alisali kumuomba Mungu, juu ya kitendo ambacho alitakiwa kukifanya,
“Mungu sio kupenda kwangu, nahitaji kujiokoa mahali hapa, nimeamua kusimama na mama Winny hadi apone naomba nisamehe kwa hii dhambi nayoenda kuitenda sahivi” Baada ya kutamka maneno hayo alifunguliwa pingu na kwa sababu alilalazwa chumba kimoja na mama Winny basi alisogea kitandani kwake na kumfunika macho kwa kitambaa cheusi,
“Mama Winny natoa mapenzi ili kujiokoa mimi na wewe, hivyo nakufunika macho ili usione kitu mwanao nachofanyiwa na kama utasikia nikiwa nalalamika basi unisamehe, lengo langu ni kujiokoa na wewe”, alisema Mainda na haraka alirudi na kuvua nguo mbele ya mlinzi aliyetaka kupewa mapenzi, alisimama mbele yake na kumuangalia kwa huruma, huku akianza kuvua blauzi yake, mlinzi alipagawa kuona jinsi kifua cha Mainda kilivyoumbika, maziwa yalikua madogo ya kuchongoka, Mainda aliendelea kuvua nguo safari hii machozi yakimtoka, woga ulimzidi baada ya mlizni huyo kumsogelea, alivuta picha ya maumivu ambayo angeyapata dakika chache zijazo.
***
Wazungu watano walishuka katika ndege, na moja kwa moja wakajiandikisha majina na kukaa kusubiri huduma, vyakula vya kila aina viliuzwa katika viwanja ambayo Mazengo alikua akitolea huduma,
“Simple work (kazi rahisi) alijisemea Crowl baada ya kuangalia Mazingira ya mahali ambapo Mazengo alikua akitolea huduma, moja kwa moja aliwapanga vijana wake.
Mazengo alikua ndani ya chumba kidogo ambacho aliingia mtu mmoja mmoja,
“Mimi nitakua wa kwanza kuingia na nikiingia nitamuua na nyie mtaingia mmoja mmoja na kila mtu akitoka anaingia moja kwa moja kwenye ndege atakaeingia wa mwisho ataingia na kabla ya kutoka ili wasitushtukie tutalipua bomu moja huku upande mwingine watu lazima watashtuka na wataanza kukimbia ovyo hapo wa mwisho atakuaja na kuingia ndani ya ndege na itapaa, hapo tutakua tumemaliza kazi” maneno hayo yalizungumzwa kwa kingereza na wakaanza kufanya mazoezi kimawazo, huku wakisubiri siku ifuatayo ambayo ndio kazi ilikua inatakiwa kufanyika.

INAENDELEA

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI: SEHEMU-30

Mtunzi: DEO MASSAWE

Kutokana na watu wengi maarufu kuenda kupata dawa kwa Mazengo au nabii kama alivyoitwa na watu basi mashirika mbalimbali ya kijasusi yalikua yameweka kambi pale kisirisiri,Viongozi wakubwa dunaini walikua wanaenda pale kisirisiri walihakikisha ulinzi wa kutosha unakuwepo mahali pale,
Kila kiongozi wa nchi yoyote alipotaka kuenda kupata huduma hiyo alihakikisha usalama unatumwa kwanza kuja kufanya uchunguzi,
MOSSAD, (National Intelligence Agency of Israel) , hili lilikua shirika la kijajsusi kutoka nchini Israel, pia lilikua shirika namba moja duniani kwa utendaji kazi wake, hawa walikua wasomi wa hali ya juu, hawakuwahi kushindwa katika upelelezi au kuzuia mapigano yoyote, kikosi hiki pia kilikua katika uwanja ambao huduma ilitolewa kwa ajili ya kuchunguza usalama kabla ya waziri wao mkuu pamoja na viongozi wengine kutoka nchini kwao kuja kupata dawa kwani kila mmoja aliamini ana maradhi ambayo huenda hayajaonekana.
SIS, (Secret Intelligence Service) lilikua shirika la kijasusi kutoka nchini Uingereza, nalo lilikua nchini Tanzania kisirisiri kwani malkia wa Uingereza naye alitarajia kuwasili kupata huduma kwa Mazengo, hivyo walihakikisha kuna usalama wa hali ya juu.
CIA, (Central Intelligence Agency) shirika hili kutoka nchini Marekani liliwasili nchini kwani hadi raisi wa Marekani alikua akiwasili nchini Tanzania, viongozi hawa pamoja na makundi yao ya usalama yalikuja kwa siri kubwa, hivyo pamoja na kuhakikisha usalama wa viongozi wao pia walihakikisha usalama wa Mazengo ili viongozi wao pamoja na wao wapate dawa. Camera nyingi zilitegwa eneo hilo na kurusha matukio nchi husika.
***
Mainda alitokwa na machozi mfululizo, mapigo ya moyo yalidunda kwa kasi ya mara 130 kwa dakika baada ya kuona akishikwa kifua chake na mlinzi aliyejitolea kumsaidia,
“Binti nimesikitika sana kukusaidia ukiwa katika hali hii, mimi pia ni mzazi na wewe ni kama mwanangu naomba unisamehe kwa kitendo ambacho nilitaka kukifanya kwako, naomba nikwambie tu ni shetani alitaka kunipitia, nimeamini kweli una upendo wa dhati, sio kawaida kumuona binadamu kujitolea utu wake ili kuokoa maisha ya mtu mwingine, naomba nisamehe sana mwanangu kwa kuwa umeonesha moyo wa upendo kwa mama huyu hadi ukafika kiasi cha kutaka kunivulia nguo ukiwa unalia basi wewe ni binadamu wa kipekee sana, sio kwamba nilikua nakutania kukuomba mapenzi ili nikutoe bali nilikua namaansiha ukweli lakini kwa jinsi ulivyoonesha moyo wa upendo basi vaa nguo zako, tusubiri usiku wa leo nitakutoa maeneo haya”, maneno hayo yaliyopenya katika masikio ya Mainda yalimuacha mdomo wazi, hakutarajia kusikia hayo,alijikuta akimkumbatia mlinzi huyo kwa furaha, alimrukia na kumbusu mlinzi huyo mdomoni, na ili kumdhihirishia amefurahi basi alipenyeza ulimi wake katikati ya mdomo wa mlinzi huyo kitendo hicho kilimfanya mlinzi huyo apatwe na msisimko wa hali ya juu, hapo walinyonyana ndimi kwa mda, kisha wakatulia, Mainda alipiga magoti na kumshukuru Mungu, matumaini ya kutoka mahali pale yalianza kuonekana .
***
Saa tano na nusu ya usiku zoezi la kutoroshwa kwa Mainda na mama Winny mahali hapo lilianza, mlinzi alivaa mavazi yake na kujifunga mikanda ambayo angeitumia kuwafungia mwilini mwake na kutoka nao kwani baada ya tukio la akina Mainda kuingia katika nyumba hiyo ulinzi ulikua umeimarishwa maradufu,
“Sasa hapa nyie inabidi niwafungie katika mwili wangu, ili aonekanane ni mtu mmoja anatembea, nakuomba Mainda tuweni makini hapa nikigundulika kusaliti kampuni yangu nitauwawa” yalikua maneno ya mlinzi huku akimuelekeza Mainda namna ya kutoka.
Baada ya dakika kumi Mainda na mama Winny walikua wamejifunga mwilini kwa mlinzi, Mainda alijifunga kwa nyuma huku mama Winnya akifungwa kwa mbele, walitembea kwa kunyata, kwa kupitia mlango mdogo walifanikiwa kutoka nje, giza liliwasaidia pamoja na mbwa kutobweka. Kwa bahati mbaya hata kabla ya kutembea kwa mita kumi simu ya mlinzi iliita, kwa shida aliangalia katika screen, alishtuka kuona ni boss wake na alivyopokea alipewa amri ya kuwapokea wageni waliokua wakiwasili eneo hilo kwa wakati huo,
“Inanipasa nirudi haraka kazini” maneno hayo ya mlinzi yalimfanya Mainda atetemeke kwa hofu,
“Mungu wangu” aliongea Mainda,
“Hapa maisha yangu yapo hatarini, asilimia kubwa nitauwawa” aliongea mlinzi huyo huku akiwafungua Mainda na mama yake,
“Tutoroke basi kama ukirudi utauwawa” aliongea Mainda kwa huruma,
“Mimi nikitoroka hapa nitawatia ninyi matatizoni, hili kundi lina nguvu kubwa sana ni ngumu mtu kulikwepa, hadi hapa nilipofika sina msaada zaidi, heri mimi au ninyi mfe kuliko kukaa pamoja kisha tuuwawe wote, kwaherini yakuonana” baada ya kutamka maneno hayo mlinzi aliwaacha katikati ya giza na kurudi kazini, Mainda hakujua la kufanya alisimama na kumuomba Mungu afanye miujiza, huku akiwa anaendelea kusali alishtushwa na milio ya risasi,
“Mungu wangu kama ni mlinzi yule kauwawa basi nimekua chanzo cha kifo chake, Mungu nisaidie” baada ya kutamka hayo aliinama na kumburuza mama Winny, ili waweze kutoka mahali hapo, alimburuza kama mita kumi, ghafla akaona kitu kama macho yanayong’aa, alishtuka na kuanguka chini, aliamini ni macho ya mizimu kwani hapakua na binadamu mwenye macho ya kung’aa kiasi hicho, alijilaza kifudifudi, hakutaka kuona kilichokua kinakuja huko gizani aliamua kama ni kufa afe akiwa amelala kifudifudi.
***
Mawazo ya mlinzi kuhusu kuuwawa yalikua ukweli kwani aliporudi alikuta hali isiyo ya kawaida, kulikua na mbwa koko aliyeingia katika lango hilo akiwa na mfuko uliokua na nyama, hivyo kitendo hicho kiliwafanya waweze kuwasha taa na ndipo mlinzi mkuu wazamu hakuonekana pamoja na mbwa wa kikundi hicho, wakiwa wanashangaa kuhusu mlinzi huyo kutoonekana ndipo walishtuka ghafla akiingia huku akiwa hana hata bunduki, hakuna mlinzi aliyejiuliza zaidi ya kummiminia risasi hadi kumuua, wote waliogopa kusalitiana, mlinzi huyo aliaga dunia hapo hapo na haraka walinzi wengine walienda kukagua chumba alicholazwa Mainda na mama Wnny,
“No anyone(hakuna hata mmoja)” lilikua jibu kutoka kwa mlinzi mwingine na haraka mbwa waliitwa lakini hakuna hata mmoja aliyejitokeza,walinzi hao waliamini kuwa mbwa wao wameuwawa,haikua kawaida ya mbwa kutoonekena ndani ya geti.
***
Hali ya hewa ilibadilika ghafla katika jiji la Dar es salam, upepo mkali pamoja na ngurumo za radi kuashiria mvua,hali hiyo ilimzidishia Mainda hofu, alishtuka sana pale mwanga mkali wa radi ulipowaka na kuwaona mbwa walili wakubwa wakiwa pembeni yake,
“Kumbe yalikua macho ya mbwa, hawa” alijisemea Mainda kisha kwa kujikaza alisimama taratibu, na kujaribu kumgusa mama Winny ambaye alikua akivuja damu miguuni kwa kujitonesha vidonda, hakuwa na uwezo wa kutembea hivyo Mainda alivyokua anamburuza alimvunjavunja upya miguu yake,alimpima mapigo ya moyo na kuyakuta yanadunda,
“Mungu atatusadia tu” alijisemea Mainda baada ya kuhakikisha mama Winny ni mzima.
Hakutaka kupoteza mda kwani hakujua wale mbwa walikua na sababu gani pale, alisimama na kuanza kumburuza mama Winny lakini katika hali isiyo ya kawaida alishuka baada ya mbwa kumzuia kitu alichokua akifanya , walimzuia kumburuza kuhu wakilala chini, kwa uwezo wa Roho Mtakatifu Mainda alijiwa na wazo la kumbeba mama Winny na kumlaza bapa juu ya migongo ya mbwa hao, kisha safari ikaaza, Mainda alikaa katikati akiushikilia mwili huo, damu ilizidi kumchuruzika miguuni na kuacha matone mengi katika njia waliyopita.
***
Baada walinzi kushauriana kwa dakika mbili waliamua kufuata matone ya damu waliyoona nje ya mlango mdogo, matone hayo yaliashiria kuwa Mainda na mama Winny wamepitia hapo,moja kwa moja kwa kutumia kurunzi yenye mwanga mkali na bunduki mkononi walikua makini kuyafuatilia huku dalili za mvua zikizidi kuongezeka, kwa manyunyu kuanza kudondoka taratibu.

INAENDELEA

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI: SEHEMU YA-31

Mtunzi: DEO MASSAWE

Mainda alizidi kumuomba Mungu huku akipiga hatua kubwa kubwa, lengo lake likiwa kufika barabarani na kuomba msaada, machungu juu ya milio ya risasi alizosikia alizidi kuamini kuwa ni mlinzi aliyemtoa mahali pale ameuwawa, alijikwaa mara kwa mara kutokana na giza.
Walinzi waliokua wanawafuata walizidisha mwendo baada ya kuona matone ya damu ambayo hayajakauka vizuri,
“Wamepita hapa sahivi, huoni damu inaonesha kabisa sio mda mrefu wamepita hapa” alitamka mlinzi mmoja huku wakizidisha mwendo,
“Hawa wana mchezo fulani wanaochezo haiwezekani watukimbie lazima wafe” aliongea mlinzi mwingine aliyeonekana kuwa na hasira zaidi.
Mvua iliongezeka kiasi cha kuzuia matone ya damu kuonekana, walinzi walichanganyikiwa zaidi baada ya mvua kuongezeka zaidi, kwani waliamini ingekua vigumu kupatikana kwa Mainda na mama Winny.
Mbwa walimfikisha mama Winny Victoria pembeni kidogo ya barabara ya Bagamoyo, walimtupa chini wakarudi, Mainda aliwashukuru mbwa hao kimoyomoyo, huku machozi yakimtoka kwani alitamani aendelee kubaki nao.
***
Kutokana na hali ilivyokua kwa watu waliokua wanaenda kupata dawa huko Kibaha haikua ajabu kumuona mtu kama mama Winny akiwa katika hali ile, Mainda alijitahidi kusimamisha gari yoyote ili aombe msaada, lakini hakuna dereva aliyesimamisha, hapo ndipo alipata wazo la kupanga majani njiani, kitendo hicho kilipelekea magari yanayopita kupunguza mwendo,
“Una tatizo gani binti” aliuliza baba mmoja aliyekua ndani ya gari aina ya Toyota Lexus pembeni alikaa mwanamke aliyeonekana mlevi,
“Nomba msaada wako, nimetelekezwa hapa, nahitaji kufika kwa huyo nabii anayetoa dawa” Mainda aliongea uongo ili aweze kupata msaada, alimaini kama angeongea ukweli lazima angeogopwa,
“Mimi naelekea Mbezi mwisho, hivyo twende nikusogeze” kijana huyo aliongea huku akimfungulia mlango wanyuma,
“Nipo na mama yangu na hawezi kutembea amelala pale” aliongea Mainda huku akigeuka kwa ajili ya kumchukua mama Winny aliyekua amelazwa pembeni,
“Ah huyo ni binadamu kweli?” aliuliza kijana huyo huku akiondoa gari kwa kasi, alishangaa sana kuona biandamu akiburuzwa kwa namna ile, mvua ilizidi kuwa kubwa, Mainda na mama Winny waliloa sana lakini hakuna aliyejali na baada ya mda walipata usafiri ulioweza kuwafikisha hadi eneo ambalo Mazengo alikua akitolea huduma ikiwa ni saa tisa usiku.
Watu walikua wengi, wagonjwa waliozidiwa walipewa kipaombele cha kutibiwa mapema,Mainda alipofika hakuwa na mda wa kupoteza, haraka alitafuta mahali na kupumzika baada ya kujiandikisha katika orodha ya watu waliokua na wagonjwa waliozidiwa, kwa jinsi huduma ilvyokua inatolewa Mainda alikua ni mtu wa kupata huduma baada ya masaa manane,
“Mungu mkubwa sasa mama Winny atapona na tutaanza maisha mapya” alijisemea Mainda na kupumzika .
***
Martin hakutaka kujulikana, alivaa sura bandia pamoja na watu wengi maarufu ambao hawakutaka kujulikana walikua wamevalia sura bandia.
Winny alikua njiani lakini watu waliokuwa wamemuwekea Martin ulinzi walimuona,
“Huyu si ndie Winny, Yule aliyemuingiza boss wetu katika matatizo ?” aliongea kijana mmoja,
“Ndie huyo kunguni mkubwa amemsababishia boss wetu kuteseka gerzani” alijibu kijana mwingine huku wakiegesha gari pembeni na haraka walimpigia Martin simu na kumpa taarifa ya kuonekana kwa Winny,
“Mkamateni haraka mpelekeni kwenye nyumba yangu kule Goba” alijibu Martin na haraka Winny alichukuliwa na kupulizwa dawa ya usingizi, safari ya kuelekea Mbezi Goba ilianza.
Baada ya lisaa limoja Winny aliingizwa ndani ya jumba kubwa waliloishi wasambazaji wa madawa ya kulevya, jumba hilo lilikuwa na uzio mkubwa ambao hakuna mtu yeyote aliyejua kinachofanyika ndani ya jumba hilo,
“Huyo mteseni lakini msimuue hadi siku nitakaporudi” Martin alitoa amri hiyo na moja kwa moja Winny alianza kuteswa huku wakimtumia katika kujaribu madawa ya kulevya.
***
Kikundi cha MOSSAD tayari kilikua kimeweka mashaka juu ya Crowl na kundi lake, bila kuchelewa walipigwa picha na piicha hizo zilichunguzwa na ndipo walibainika ni magaidi, haraka walijipanga kumlinda Mazengo, risasi moja ilipigwa juu ili kushtua watu, kitendo cha kupiga risasi juu watu wote uwanjani walishangaa sana, hali ya amani kutoweka, watu walianza kukimbia ovyo, Martin alitoa amri kundi lale pia liweke ulinzi kwa nabii ili aweze kupata dawa, Mazengo alijikuta akiwekewa ulinzi na watu zaidi ya mia mbili bila kujijua.
Mainda alishtuka sana kusikia mlio wa risasi aliamini amekua na mkosi, alijua ni lazima mama Winny angekufa siku za karibu kwa kukosa huduma hiyo.
Ndege aliyoitumia Crowl na kundi lake ilizingirwa na wana FBI (Federal Bureal Investigation) ilipekuliwa na kukutwa na silaha ambazo waliamini zilikua ni kuvuruga amani ya eneo hilo.Crowl na wenzake wote waliwekwa chini ya ulinzi mkali huku huduma ikiendelea kutolewa.
Mazengo alipata wakati mgumu hasa pale alipowaona polisi ambao aliwajua dhahiri siku alizokua akizingiziwa kukamatwa na dawa za kulevya, alikua akilengwa lengwa na machozi hasa walipoingia majaji waliomhukumu kuchomwa kule nchini China,
“Haya yote ni mambo ya duniani nimekwishawasamehe kwani kama sio wao nisingefika hapa nilipo, lazima nijue kumshukuru mtu aliyenipa changamoto ya kufika hapa nilipo” alijisemea Martin huku akijifuta machozi.Ilifika zamu ya Mainda kumuingiza mgonjwa wake ndani, huku akisaidiwa na wamama wawili walifanikiwa kumfikisha mama Winny na kumlaza chini mbele ya Mazengo, hakika ilikua kama ndoto, Mazengo alisimama na kuruka juu, alionekana kama aliyerukwa na akili, kisha alirudi na kumkumbatia ,
“Mke wangu ni wewe au naota, na wewe ni Mainda?” Maneno hayo yalimchanganya Mainda,
“Tafadhali naomba msaidie mama yangu anauwa sana” alitamka Mainda baada ya kuonesha mshangao mkubwa juu ya maneno yaliyotamkwa na Mazengo,
Mazengo alijua ni dhahiri Mainda asingeweza kumjua pasipo kuvua sura ya bandia aliyokua ameivaa hapo alimvuta Mainda pembeni na kuivuya sura aliyokua ameivaa,
“Waoooooooooooooooooooooooooooooooooooooooh” Baba Winny shhamoo, simaini macho yangu ni wewe ama naota?” aliongea Mainda huku akitetemeka kwa hofu kwani kila mtu aliamini Mazengo alikwisha aga dunia siku nyingi. Wamama waliokua wamemsaidia Mainda kumbeba mgonjwa wake walitoka nje wakipiga kelele kutokana na kile walichokiona, askari wa kizungu waliingiwa na hofu juu ya kurudi kwa Mazengo, sura ya bandia aliyokua amevaa aliivua na kuiweka pembeni, bila kutarajia mashambulizi yalianza, makundi mawili yaligawanyika, kundi la kwanza likitaka auwawe kwani hawakuamini katika mzimu kuwapa dawa pamoja na askari waliowahi kumtesa kwa ajili ya kesi Martin aliyomuuzia wengi waliona aibu.
Martin alimbeba mkewe begani na kuanza kutoka naye nje watu walishangaa na kuanza kukimbia ovyo, kila aliyeshuhudia tukio lakusukumiwa shimoni na moto kushushwa hakuamini kumuona tena akiwa hai, wengi waliamini ni mzimu na wengine wakiamini lile tukio lilikiua la kutengeneza video.
Martin ndiye hakuamini, aliamini Mazengo kuwa hai kutamletea matatizo zaidi hivyo aliungana na watu waliotaka auwawe lakini akiwa tayari amepata dawa.
Mazengo alitangaza kusitishwa kutoa dawa, watu walilia kwa uchungu,
“Baba kama umeamua kusaidia watu basi saidia tu, najua ni jinsi gani nimeteseka na mama Winny hadi leo hii nakuja hapa nakutana na wewe, nakuomba saidia watu wagonjwa” Mainda alitamka huku akiwa amepiga magoti, Mazengo alikua akitoa machozi ya furaha, na hapo aliendelea zoezi la kutoa pembeni yake alilazwa mke wake, waandishi wa habari kutoka katika vituo vyote nchini walifika eneo hilo.
Watu waliotaka Mazengo auwawe walipatwa na hasira kwa jinsi vikosi vyenye nguvu vlivyoweka ulinzi mkali,
“Lazima tutamuua tu” alisema mmoajwapo wa wapiganaji wa Martin.

INAENDELEA

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI: SEHEMU YA-32

Mtunzi: DEO MASSAWE

Mpiganaji wa Martin aliykua amevaa gauni alichomoa bunguki aina ya SMG, aliinyoosha kwa Mazengo na kufyatua lakini watu wote walishangaa kumuona Mazengo akiidaka risasi. Kelele zilitawala kwa kitendo kile mashambulizi yalianza vikosi vyote vilivyotaka Mazengo auwawe vilikua vikimshambulia kwa risasi ambazo zilikua zikidunda mwilini mwake, alimshikilia mkewe kwa uangalifu huku Mainda akipiga kelele, watu wote waliamini ni ndoto, lakini ukweli ulikua huo, kuwa Mazengo alikua amerudi katika uso wa dunia akiwa mtu mwingine akiwa na nguvu zingine.
Baada ya mapigano kudumu kwa dakika ishirini pasipo kumuweza vikosi vyote vilipigwa na butwaa, taarifa zilisambaa dunia nzima. Zoezi la kutoa dawa likawa linaendelea.
Mataifa makubwa kama China, Finland, Singapore,Russia walianza kumsaka Mazengo ili akapewe uraia katika nchi hizo lakini katu hakutaka kutoka Tanzania, alitengeneza Hospital kuba kila tarafa nchini Tanzania, pamoja na kuanzisha shule za watoto wanaoishi katika mazingira magumu kote duniani. Mke wake alirudiwa na afya yake baada ya kupata dawa, maisha yakawa mapya wakiwa na Mainda,
Mazengo alikua anafanya safari za mara kwa mara kuenda katika msitu wa Amazon kwa ajili ya kuchukua mizizi ya kutengenezea dawa, dunia nzima ilimjua kwani pia alikua anasafiri katika nchi mbalimbali kufundisha wanajeshi na makomando.
***
Baada ya mwezi mmoja Mazengo aliongoza jeshi la polisi kuwakamata wauzaji na wasambazaji wote wa dawa za kulevya na kuwaweka ndani akiwemo Martin, huku watumiaji wote waliokua wamethirika na madawa hayo wakiwekwa sehemu maalumu kwa ajili ya matibabu
Pamoja na kuwa na furaha juu ya kukutana na mkewe bado mtoto wake wa pekee Winny alimnyima usingizi, hakujua ni mzima au amekufa lakini siku moja katika hali ya kushangaza alisikia taarifa za kuokotwa kwa msichana aliyedhoofika kupita kiasi, hapo alienda hadi hospital kuu ya Lugalo na ndipo alimkuta Winny, hakika alipata furaha ya ajabu, alimchukua na kumtibu.
“Baba, mama, Mainda naombeni mnisamahe kwa yote niliyowahi kukosea, hakika nilikua katika hatua za mwisho kufa, nilikua katika mateso makali, nilitumika vibaya kwa ujinga wangu, namshukuru Mungu alinipigania, Baba nakushukuru sana hakika anilikua siamini kama ni wewe umeniponya na jinsi nilivyokudharau hadi nikawa sikusikilizi, nakupenda sana baba yangu,Mama nakuomba nisamehe, najua ni jinsi gani ulikua unanipenda lakini nikaamua kukusaliti mama please nisamehe bure nina furaha sana kukutana na nyie tena, Mainda mdogo wangu nisamehe kwa haya yote yaliyotokea” Winny alikua akitamka hayo huku akitokwa na machozi aliinama na kuwalamba miguu wazazi wake kama ishara ya kuomba msamaha na kutubu.Wote walisimama na kushikana mikono.
“Tumeanza maisha mapya hakika tulikua tumepanda BASI LA SHETANI LAKINI TUMEFANIKIWA KUSHUKA KWA UWEZO WA MUNGU” alitamka Mazengo kwa uchungu huku akitoa dawa ambayo aliamini ni ya kurudisha umri nyuma wote waliinywa na kuamka asubuhi wakajikuta wamebadilika, Winny na Mainda walirudi na kuwa na miaka 3 huku mazengo na mkewe wakiwa na miaka 25, hakika ilikua dawa ya maajabu iliyoishangaza dunia nzima. Mainda na Winny walianza shule huku Mazengo na mkewe wakisimamia miradi yao, dunia nzima jina la Mazengo lilitawala.
***

MWISHO..

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI: SEHEMU YA-32

Mtunzi: DEO MASSAWE

Mpiganaji wa Martin aliykua amevaa gauni alichomoa bunguki aina ya SMG, aliinyoosha kwa Mazengo na kufyatua lakini watu wote walishangaa kumuona Mazengo akiidaka risasi. Kelele zilitawala kwa kitendo kile mashambulizi yalianza vikosi vyote vilivyotaka Mazengo auwawe vilikua vikimshambulia kwa risasi ambazo zilikua zikidunda mwilini mwake, alimshikilia mkewe kwa uangalifu huku Mainda akipiga kelele, watu wote waliamini ni ndoto, lakini ukweli ulikua huo, kuwa Mazengo alikua amerudi katika uso wa dunia akiwa mtu mwingine akiwa na nguvu zingine.
Baada ya mapigano kudumu kwa dakika ishirini pasipo kumuweza vikosi vyote vilipigwa na butwaa, taarifa zilisambaa dunia nzima. Zoezi la kutoa dawa likawa linaendelea.
Mataifa makubwa kama China, Finland, Singapore,Russia walianza kumsaka Mazengo ili akapewe uraia katika nchi hizo lakini katu hakutaka kutoka Tanzania, alitengeneza Hospital kuba kila tarafa nchini Tanzania, pamoja na kuanzisha shule za watoto wanaoishi katika mazingira magumu kote duniani. Mke wake alirudiwa na afya yake baada ya kupata dawa, maisha yakawa mapya wakiwa na Mainda,
Mazengo alikua anafanya safari za mara kwa mara kuenda katika msitu wa Amazon kwa ajili ya kuchukua mizizi ya kutengenezea dawa, dunia nzima ilimjua kwani pia alikua anasafiri katika nchi mbalimbali kufundisha wanajeshi na makomando.
***
Baada ya mwezi mmoja Mazengo aliongoza jeshi la polisi kuwakamata wauzaji na wasambazaji wote wa dawa za kulevya na kuwaweka ndani akiwemo Martin, huku watumiaji wote waliokua wamethirika na madawa hayo wakiwekwa sehemu maalumu kwa ajili ya matibabu
Pamoja na kuwa na furaha juu ya kukutana na mkewe bado mtoto wake wa pekee Winny alimnyima usingizi, hakujua ni mzima au amekufa lakini siku moja katika hali ya kushangaza alisikia taarifa za kuokotwa kwa msichana aliyedhoofika kupita kiasi, hapo alienda hadi hospital kuu ya Lugalo na ndipo alimkuta Winny, hakika alipata furaha ya ajabu, alimchukua na kumtibu.
“Baba, mama, Mainda naombeni mnisamahe kwa yote niliyowahi kukosea, hakika nilikua katika hatua za mwisho kufa, nilikua katika mateso makali, nilitumika vibaya kwa ujinga wangu, namshukuru Mungu alinipigania, Baba nakushukuru sana hakika anilikua siamini kama ni wewe umeniponya na jinsi nilivyokudharau hadi nikawa sikusikilizi, nakupenda sana baba yangu,Mama nakuomba nisamehe, najua ni jinsi gani ulikua unanipenda lakini nikaamua kukusaliti mama please nisamehe bure nina furaha sana kukutana na nyie tena, Mainda mdogo wangu nisamehe kwa haya yote yaliyotokea” Winny alikua akitamka hayo huku akitokwa na machozi aliinama na kuwalamba miguu wazazi wake kama ishara ya kuomba msamaha na kutubu.Wote walisimama na kushikana mikono.
“Tumeanza maisha mapya hakika tulikua tumepanda BASI LA SHETANI LAKINI TUMEFANIKIWA KUSHUKA KWA UWEZO WA MUNGU” alitamka Mazengo kwa uchungu huku akitoa dawa ambayo aliamini ni ya kurudisha umri nyuma wote waliinywa na kuamka asubuhi wakajikuta wamebadilika, Winny na Mainda walirudi na kuwa na miaka 3 huku mazengo na mkewe wakiwa na miaka 25, hakika ilikua dawa ya maajabu iliyoishangaza dunia nzima. Mainda na Winny walianza shule huku Mazengo na mkewe wakisimamia miradi yao, dunia nzima jina la Mazengo lilitawala.
***

MWISHO..

the Legend☆
Hiyo dawa na mm naitaka ya kurudisha umri nyuma
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom