Simulizi: Basi la shetani

Simulizi: Basi la shetani

Mleta uzi mbona humpi credit mwandishi aisee
Hata jina tu inatosha imagine ungekuwa ww ndie mwandishi
Pleased heshimu jasho la mtu kwani ada ya mja hunena muungwana ni kitendo.
Mkuu ukiona hivyo ujue sijamjua mtunzi ni nani, hii simulizi ilitumwa kwenye moja ya whatsapp group exactly kama nnavyoiwasilisha hapa. Nothing more, nothing less

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI: SEHEMU YA-20

Usiku wa kuamkia siku ya jumamosi, ulikua usiku mrefu hasa kwa waliokua wakisubiri sherehe iliyoandaliwa na Martin, kila mmoja aliona saa zikienda taratibu,Kemmy alikua na furaha zaidi, hakuamini kama kweli alikua mbioni kuvishwa pete ya uchumba na mwanaume tajiri tena tishio kwa watu.
“Eh Mungu nashukuru kujuana na Winny kwani ndiye chanzo cha mimi kukutana na huyu tajiri” alijisemea Kemmy ikiwa imetimia saa kumi na moja kamili alfajiri.
Siku ilikua na hali ya hewa nzuri, jua lilichomoza na hakukuwa na dalili yoyote ya mawingu, shamrashamra zilianza mara moja katika ukumbi wa LIFE PARK majiko ya mkaa yalikua yakipaliwa mkaa wa uhakika, mbuzi na kuku zilikua zikichinjwa na wachomaji nyama mahari waliokodishwa kutoka Arusha walikua kazini kuchanganya viungo,
“Nataka wageni wangu waanze kula na kunywa saa nne kamili ya asubuhi hadi kesho saa nne kamili ya asubuhi” Martin alikua akiongea na mpishi mkuu kwa njia ya simu, hivyo kila kitu kiliandaliwa kwa wingi ilikua sherehe ya masaa ishirini na nne.
***
“Mpenzi ni mda wa salon sasa nikajiandae siunajua nataka kuwafunika wanawake wote hapo ukumbini?”
“Sio kitu cha kuuliza mpenzi, jiandae twende salon mara moja nataka upambwe zaidi ya bibi harusi”
“Waaaoh, asante sana mpenzi” yalikua maongezi kati ya Edson na Winny, waliamka na kukabidhi chumba walichokodi na haraka waliingia ndani ya gari na kuondoka kuelekea CONNEXION THE HOUSE OF BEAUTY , ilikua sehemu ya kisasa katika upambambaji mitaa ya Bamaga, saa moja kamili tayari Winny alikua akipambwa na wanawake zaidi ya watano, kila mmoja alipamba sehemu yake wakati mwingine akitengeneza nywele mwingine alikua akimsafisha meno ili yaweze kung’aa ipasavyo.
“Mpenzi mimi nikuache hapa, nitakuja kukuchukua mda ukifika”
“Sawa dear, uwe makini barabarani”
“Usijali mpenzi mwaah”, Edson na Winny walioneshana mapenzi ya hadharani, hawakuona aibu kupigana mabusu mbele ya wadada waliokua salon hapo,
“Na nyie mnapendana hadi kero” alitamka dada mmoja wa salon
“Ohooooooooo na wewe ushaona wivu, ole wako nikukute hapo” Winny alijibu huku akicheka,
“Ah wapi akiingia kwangu nakuambia unapigwa chini”, aliongea dada mwingine
“Hakuna anayeweza kumpa vitu navyompa mimi” Winny alizidi kujitetea, waliendelea kupiga stori nyingi zinazohusiana na mapenzi pamoja na madhaifu ya wanaume katika mapenzi.
Edson aliendesha gari hadi katika nyumba mpya aliyonunua siku iliyopita, lengo lake likiwa kuficha zaidi ya million mia tano alizokua nazo katika box ndani ya gari,alipofika alifurahi kumkuta Mainda akifanya usafi,
“Shkamoo kaka”
“Marahaba , umeamkaje na mama yako”
“Nimeamka salama kaka, sijui wewe”
“Hata mimi nimeamka salama, naona unafanyafanya usafi”,
“Ndio kaka siunajua tena ni mazoezi pia?”
“Kweli nashukuru, ngoja mimi kuna mzigo nimeleta mara moja hapa, nataka kuondoka nadhani kesho saa kama hizi ndio nitarudi, kuna shughuli naenda kuifanya”aliongea Edson huku Mainda akipokea vitafunio kutoka kwa Edson, baada ya hapo Edson alianza kubeba mabox kutoka kwenye gari na kuyaingiza katika chumba kimoja na kukifunga.
Mainda alikua na shauku ya kumueleza Edson kitu lakini alikua akisita sita, lakini alipoona Edson anakaribia kuondoka alijikaza na kumuita,
“Lakini kaka samahani, unaweza kunisikiliza kwa dakika chache?” aliongea Mainda huku akitizama chini,
“Usijali waweza kuongea nakusikiliza”, alijibu Edson huku akitega sikio kwa makini,
“Usichukie lakini jana niliota kitu kibaya kuhusu wewe, yaani iko hivi niliota eti umekuja kama ulivyokuja sahivi lakini nikakuambia baki nyumbani huko unaenda kuuwawa, lakini hukunikubalia licha ya kukuhimiza ubaki uliktaa katu katu na ukaamua kwenda hukurudi tena, hakika hii ndoto ilinisikitisha sana hasa baada ya kutojua sehemu uliyoenda”, Mainda alikatiza maelezo yake baada ya kuona Edson akipuuzia kwa kucheka,
“Usijali mdogo wangu nitakua salama, hiyo ni ndoto tu haina ukweli wowote,” Edson aliongea kwa kujiamini
“Lakini kaka naomba tu uwe makini na kama haina ulazima wa kuenda huko unakoenda basi tubaki nyumbani tufunge kwa maombi ili kukemea pepo la ndoto hiyo” Mainda aliongea kitu ambacho kilimpa hasira Edson suala la kubaki nyumbani kwa ajili ya ndoto lilimtia hasira
“Wewe mtoto umeomba hifadhi kwangu, nimekupa sasa unaingilia maisha yangui kiasi hiki, yaani nibaki nyumbani,? Unajua gharama nilizotumia kwa ajili ya siku hii ya leo, umeniudhi nakuomba nikirudi nisikukute hapa, itakua una tabia za kipumbavu ndio maana umefukuzwa ulipokua unakaa, nikirudi nisikukute hapa, full stop.”, maneno hayo yalimwagika mdomoni kwa Edson huku akiondoa gari kwa kasi ya jabu.
“Mungu wangu kwani nimekukosea nini mimi, mbona mateso yanazidi, kila napoona mwanga giza linakuja, je nitaenda wapi mimi?” Mainda alijisemea huku akirudi ndani alifika na kupiga magoti pembeni ya kitanda alicholala mama Winny, akafanya maombi kwa mda wa nusu saa.
***
Majira ya saa tatu kamili mziki wa taratibu kutoka kwa DJ manywele ulianza kurindima taratibu katika ukumbi wa LIFE PARK, wahudumu waliokodiwa kwa mda kutoka katika kumbi za jirani zikiwemo Lukan Pub, KS pub , Ground Pub, Mwenge City Pub walikua tayari wamewasili, walipanga meza vizuri, tayari magari ya kifahari yalikua yameanza kutinga katika sehemu ya maegesho bila ya mtu kushuka, kwani walingoja hadi saa nne kamili ifike ili waweze kushuka kwa pamoja na sherehe iweze kuanza.
Macho ya watu watu wote yalikua yakiangalia gari aina ya BMW X6, ilikua ikiingia taratibu ndani ya geti la Life park, kila mtu alitamani kumuona ambaye angeshuka garini hapo, mda sio mrefu tena iliingia Marcedence Benz nyeusi ambayo ndani alikua Edson na Winny na hadi wakati huo Edson alikua hajamtaarifu Winny kitu chochote kuhusu kununua nyumba, magari yote yalikua yakifahari, wahudumu wote walikua wamejiandaa ipasavyo kwa kazi ambayo waliahidiwa ujira mkubwa,
“Leo hapa tutapata madanga ya uhakika”, aliongea mhudumu mmoja anayeitwa Neema ambaye nae alikodiwa kutoka KS Pub,
“Kweli hapa ukipata danga unaachiwa mshiko wa maana”, alijibu Glory kutoka Ground Pub.
***

Nchini Thailand ambako Mazengo alipokua akipewa mafunzo ya kivita alizidi kuwa kisu, siku zilivyozidi kusonga ndivyo alizidi kupata ujuzi, hadi mwalimu wake Vajiralong alianza kuhofia kuzidiwa ujuzi, Mazengo alikua na uwezo wa kupambana na papa ndani ya maji hadi kumuua.
Acount ya benk aliyofunguliwa ilizidi kujazwa pesa kama ishara ya shukrani kwa ajili ya kufanikisha madini kupatikana kirahisi.
***
Saa nne kasoro dakika mbili milango ya magari ilianza kufunguliwa na moja kwa moja wageni walipokelewa na kusindikizwa na mwamvuli hadi sehemu husika Martin na Kemmy walitajwa kuwa wageni wa mwisho kuingia ndani ya ukumbi huo.
“Hadi wakati huu bado wewe ndiye unaongoza kwa kupendeza” Edson alimnong’oneza Winny walipoketi, ukumbi ulikua kimya kumsubiri mgeni rasmi aingie, bado Winny hakujua chochote hukusu sherehe hiyo hakujua kama Martin ndiye mgeni rasmi.
“Haya sasa mgeni rasmi ndio anaingia mda sio mrefu , naomba wageni waalikwa wote tusimame ili kumkaribisha mgeni rasmi wetu na sherehe iweze kuanza mara moja” Sauti kupitia kipasa sauti ilisikika kutoka kwa MC (Master of Ceremony) na bila kupoteza mda wote walisimam lakini kabla ya kuingia kwa mgeni rasmi waliingia wanaume nane waliovaa suruali za jeans na makoti makubwa pamoja na miwani nyeusi, walikua walinzi wa Martin na kwa haraka walifanya ukaguzi kwa kutumia vifaa maalumu na kuhakikisha usalama upo, yaani hapakua na mtu mwenye silaha yoyote, baada ya hapo wanne walirudi na kuenda kumleta Martin wanne walibaki ukumbini,
“Baada ya dakika mbili mwanaume mmoja akiambatana na mwanamke aliyeonekana mdogo na mrembo walikua wakipiga hatua huku wameshikana mikono kuingia ukumbini hapo, mwanaume huyo alivaa suti nyeusi, huku mwanamke huyo akivaa gauni la kijivu, hakika ndiye mwanamke pekee aliyemzidi Winny kwa kupendeza pale ukumbini,
“Vipi mpenzi mbona unashtuka “ Edson aliongea kwa sauti ya chini hukua kimshika Winny aliyetaka kukimbia baada ya Martin na Kemmy kuingia ukumbini,
“Mpenzi umeamua kuja kuniua?” Winny alitamka maneno hayo yaliyompa Edson hali ya sintofahamu kwani Winny alimtambua Martin aliyeambatana na Kemmy, Winny aliingiwa na hofu zaidi baada ya macho yake kugongana na ya Martin,
“Mpenzi mbona uliniambia Winny aliliwa na simba porini ?” Kemmy alimnong’oneza Martin baada ya kumshuhudia Winny.
Hali ya Martin ilibadilika ghafla, alipandwa na hasira ya ajabu, alipigiza simu yake ya mkononi ukutani,
“Vipi mpenzi sikuelewi ujue au una mwanaume wako hapa sasa lazima kilka mtu ajue mimi ni mumeo leo” Edson alimwambia Winny huku akimshikilia na kumkumbatia kwa nguvu ili kuwaonesha wanaume waliokua mahali pale kuwa ni mpenzi wake.
Martin hakuamini kuona kitendo kile, hakuamini kama kuna mtu ambaye angethubutu kufanya masihara mbele yake kama alivyofanya Edson,
Safari ya kuelekea katika kiti chake ilibadilika na akanza kuelekea alipokua Edson na Winny.

INAENDELEA

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI: SEHEMU YA-21

Watu wote waliingiwa na mshangao, wahudumu waliingiwa na uoga wa ghafla, sura ya upole aliyokua nayo Martin ilibadilika na kuwa mkali kama simba,
“Give a gun (naomba bunduki)” Martin alisema huku akinyoosha mkono kwa mmojawapo wa walinzi wake na bila kuchelewa mlinzi huyo alitoa bunduki aina ya SMG iliyofichwa ndani ya koti kubwa na kumkabidhi, wahudumu pekee ndio walioingiwa na hofu lakini wageni wengine kwa kuwa walikua ni watu waliozoea biashara haramu zingine za kumwaga damu waliona ni kitendo cha kawaida,
“Hii itasababisha kelele, nipe kisu” Martin aliongea na haraka alikabidhiwa kisu kikubwa maarufu kama SIME alikishika na kumsogelea Edson aliyekua anatetemeka kwa hofu,Winny alikua amekaribia mlangoni ili aweze kukimbia ,
“Haa kazi gani hii tena” alijisemea mhudumu mmoja aitwaye Grace kutoka katika pub ya MWENGE CITY huku akitoa simu yake mfukoni aweze kupiga picha, Martin alipogeuka na kumkuta msichana huyo akichukua video, alimsogelea na kumchoma kisu cha tumboni kilichotokeza mgongoni,
“Pumbavu zako, fanya kilichokuleta hapa, kama umekuja kuhudumia hudumia achana na yasiyokuhusu” alitamka Martin kwa sauti kubwa huku akikichomoa kisu tumboni kwa Grace, damu nyingi iliruka na kuchafua ukumbi, wahudumu wote waliingiwa na hofu huku wakitaka kukimbia,
“Haya ni ya hapa hapa ndani ole wake atakayetoa nje ya hapa, mnaskia nyie makahaba?”Martin aliendelea kufoka huku akinyoosha mkono kwa wahudumu waliokusanyika sehemu moja wakitetemeka kwa hofu, Grace alianguka chini damu zilimtoka mdomoni na masikioni kisha akageuza macho na kukata roho, Edson alikua akitetemeka asijue la kufanya, maneno ya Mainda yalimjia kichwani, aliamini kuwa Mainda alikua malaika aliyetaka kumuokoa katika kifo ila ubishi wake ukamfanya shetani ashinde,
“Wewe uliniomba uanachama katika biashara zangu, nikakupa, hivyo basi kukupa uanachama haimaainishi ucheze na mwanamke wangu” Martin alitamka maneno hayo huku kisu kilichokua na damu kikitakenya shingo ya Edson, mkojo ulitiririka kwa kasi, hakuweza kuongea lolote zaidi alishusha pumzi na kutizama chini,
“Martin wewe ni muuaji mkubwa, ulitaka hadi kuniua mimi” Winny alitamka kwa hasira, maneno hayo yalimzidishia Martin hasira, alinyanyua kisu juu na kukishusha shingoni kwa Edson, wahudumu wote walibaki mdomo wazi, hawakuamini kama muuaji kama huyo ndiye alitakiwa kuwalipa mshahara,Winny alitoka nje kwa kasi , bila kufungua mdomo alitoka hadi nje ya lango la LIFE PARK,
“Kumbe ndio tabia yako, sikutaki” Kemmy alitamka maneno hayo akiwa anataka kutoka lakini Martin alimsogelea na kumkata shingo, ndani ya dakika tano pale ukumbini kukatokea vifo vya watu wanne,
“Huyo aliyekimbia namuomba akiwa hai alafu kimya kimya bila mtu yoyote kujua, namuhitaji akiwa hana hata kovu”, Martin aliongea kwa hasira na mara moja kundi la vijana watano wakiongozwa na Terry walitoka na kuanza kumfuata Winny nyuma,wapishi waliokua wakichoma nyama waliitwa ndani ya ukumbi na kukabidhiwa maiti zile,
“Kazi ya ziada imejitokeza hapa, hii miili ichomwe moto kimya kimya na mtu yeyote asijue, kama ikitokea mmoja wenu akavujisha basi wote nitawauwa hivi,
“Shaaaaaaaaaaaaa” ulikua mlio wa panga likipenya tumboni kwa mchoma nyama mmoja kusudi kuwaogopesha na wote kuona mwenzao ameuwawa walilazimika kuikata kata vizuri na kuenda kuibanika jikoni, mlinzi mmoja aliwalinda kimya kimya hivyo ingekua vigumu watu kugundua kilichokua kikiendelea.
Sherehe iliendelea kama kawaida,watu walianza kunywa na kula, harufu ya damu zilizomwagika hazikuzuia chochote, mziki ulipigwa na watu kuburudika kwa sana.
Winny alitoka na kukunja kushoto, alitembea huku akigeuka nyuma kama mtu anayekwepa kitu fulani baada ya kama hatua hamsini alisimama katika kituo cha daladala cha ITV,
“Mia mia tatu, Makumbusho, panda twende” ilikua sauti ya konda wa daladala akitafuta abiria, Winny hakuona sababu ya kupoteza mda, haraka alipanda na gari likaendelea na safari.
“Huyu haistahili aende mbali, lazima apatikane kabla hajapanda gari atatuletea usumbufu” Terry aliongea kama kiongozi aliyeongoza kundi la kumsaka Winny aweze kurudishwa kwa Martin tena akiwa hai, Kutokana mafunzo waliyokua nayo ilikua rahisi kujua upande Winny alioelekea kwani waliamini lazima angekimbilia sehemu yenye msongamano wa watu na haraka na wao walikunja kusoto, walitembea kwa kasi, Terry aliwaongoza wenzake na mara moja walianza kuipata harufu ya manukato aliyojipaka Winny siku hiyo,
“Hii harufu imeishia hapa, basi kapanda gari hapa”, Terry alisema baada ya wote kusimama katika kituo cha daladala cha ITV, kwa haraka walichunguza gari ambayo ilitoka hapo mda huo wakagundua gari inayoelekea Makumbusho ndiyo itakua imembeba,
“Wewe Matiko panda daladala acha sisi tukodi taksi” Terry aliamrisha na mara moja taksi iliyokua karibu iliitwa huku Matiko akipanda daladala.
Baada ya dakika kumi tayari Winny alikua katika kituo cha daladala cha Makumbusho, mapigo ya moyo yalimwenda kwa kasi hakujua aelekee wapi, kwa haraka aliona gari ambalo lilikua linatoka,
“Ngoja nikimbilie hili linaloondoka” alitamka Winny na haraka akakimbia na kupanda gari hilo bila hata kujua linakoelekea, alipita na kusimama nyuma kabisa, gari hilo lilikua likielekea Mabibo kupitia Mwananyamala, Magomeni, Manzese kisha Mabibo, Mapigo ya moyo ya Winny yalienda kasi, hakumaini kuona biandamu wa kawaida akifanya mauaji bila huruma kiasi kile, alivuta kumbukumbu na picha yake siku ya kwanza kuonana , jinsi alivyoonekana kuwa mwanaume mwenye upendo na heshima, hakuamini kama tabasamu alilooneshwa ndiye mtu huyo angeweza kuchinja mtu tena mbele za watu bila woga,
“Eh Mungu naomba tu niokoe nisiingie mikononi mwa huyu mtu sio mwema”, Winny alijikuta akitamka maneno hayo kwa sauti, kila mtu aligeuka kumtazama walihisi ni mwanamke aliyechanganyikiwa na maisha.
***
TIP TOP,Manzese.
Kulikua na magari mengi yaliyokua yamejipanga pembeni ya barabara, magari hayo yalifungwa vitambaa kuashiia yalikua yakisafiri kuelekea kwenye msiba, kinamama wengi waliovaa doti za kanga walikua wakiashiria hilo, ulikua msafara wa magari yasiyopungua ishirini, na kweli alikua ni mtoto wa mkuu wa majeshi ya Tanzania, hivyo wanajeshi waliokua wakihudhuria maziko hayo walikua wengi, pia gari za kijeshi zilikua zaidi ya tano,
Winny aliamua kushuka hapo ili ajifiche na msiba huo,
“Shkamoo mama”
“Marahaba mwanangu hujambo”
“Sijambo mama, samahani nikuulize huu msiba ni wawapi ?”
“Huu ni msafara wa msiba kuna mtoto wa mkuu wa majeshi amekufa sasa ni jirani yetu ndio tunataka kusafirisha, kwao ni sehemu moja inaitwa Mashati mkoani Kilimanjaro” Mama huyo alimuelezea Winny bila kujua lengo lake,
“Asante mama maana mimi nilikua na mama yangu sema amenipotea ghafla hapa na tulikua tunaenda katika huu msiba, sasa sijui nitawezaje kupata nafasi katika gari maana sijui nitampataje mama yangu kwa hapa”
“Unaweza kupata nafasi maana bado magari hayajajaa na ndio wanakaribia kuondoka, hivyo wahi kwa yule kaka pale uandikishe jina”, Haraka Winny alifanya hivyo, alindika jina kama mmojawapo ya watu waliotakiwa kwenda kuzika, na baada ya dakika kumi msafara ulianza kuondoka taratibu ikiwa ni saa tano asubuhi,gari yenye king’ora ilikaa mbele ili msafara uweze kupita bila foleni.
“Boss sasa hapa kazi inataka kuwa ngumu, huyu mtoto kapanda gari inayoenda msibani, na msiba wenyewe wanajeshi kibao, sijui tutamtekaje bila kusababisha vurugu” Terry alitoa taarifa kwa Martin baada ya Winny kuonekana akipanda gari lililokua katika msafara,
“Tumieni akili, hapo itabidi mtafute coster moja haraka muende nayo hadi msibani ili mumchukue kimya kimya nataka kumchunguza vizuri huyo “ Martin aliongea kwa msisitizo,
“Sawa mkuu, vipi sasa tutapataje watu wa kuandamana nao, siunajua msiba lazima na sisi coster yetu ipate abiria”,
“Terry ndugu yangu ina maana unazeka au vipi yaani operesheni ndogo kama hiyo inakusumbua kichwa ?? yaani watu wamejaa huku Dar es salaam unashindwa kuteka gari moja tu, au niambie huo msafara unapita barabara gani” Martin alifoka,
“Huu unapita barabara ya Shekilango kisha wakamate Bagamoyo Road,” baada ya Terry kutoa maelezo hayo simu ilikatwa na haraka Martin aliagiza kikosi kingine cha watu kumi kikiongozwa na James, kilikua kikosi namba moja kwa matukio ya hatari, kikosi hicho hakijawahi kushindwa kwa lolote, haraka kilipewa data zote kuhusu Winny, nguo alizovaa hadi gari aliyopanda.Kitu cha kwanza waliandaa gari yao waliandaa pia doti zaidi ya sitini za kanga, kisha walitengeneza kibali bandia cha kusafirisha msiba, gari iliwekwa lebo ya kuwa private kwa siku hiyo.
James na kundi lake waliendesha gari hadi pembeni ya jengo la KIBO COMPLEX lililopo Tegeta, waliegesha gari lao wakisubiri msafara wa msiba ambao Winny alikua mmojawapo wa waombolezaji.
King’ora cha gari la kijeshi kilisikika kwa mbali, magari yalikua yakienda kasi, mengine yakiegesha pembeni,
“James aliwasiliana na wenzake kuwa kazi ianze mara moja na bila kuchelewa walitupa chuma chenye ncha barabarani kikatoboa gurudumu la gari moja ambalo hufanya safari zake kutoka Tegeta Nyuki hadi Bagamoyo mjini, gari hilo lilipasuka gurudumu la nyuma na moja kwa moja liliegesha pembeni ya barabara,
“Mjomba vipi unataka kuuwa watu ili iweje” alitamka kondakta wa gari lililopasuka gurudumu, abiria wote walishuka kwa hasira wakitaka kumpiga lakini aliomba akidai ni bahati mbaya chuma hicho kumponyoka,
“Kwani kutengeneza gurudumu ni shi ngapi, tukulipeni na hawa abiria tuwapeleke hadi wanakoenda, maana nyie binadamu mmekosa utu kabisa”, aliongea James huku wenzanke wakitoa sapoti ya kusaidia kufikisha abiria walipokua wakienda na baada ya dakika tatu tayari abiria walikua wamepanda gari nyingine huku wakimshukuru Mungu kwa kuwaokoa na ajali ambayo ingetokea,
James na wenzake walifurahi kupata watu kirahisi, walishangilia moyoni,
“Ngoja huu msafara upite” alitamka dereva wa coster hiyo wakati msafara wa msiba ulipowafikia” msafara ulipokatika dereva wa magaidi hao aliwahi kuingiza gari barabarani na kuwa nyuma yao,
“Wote mko chini ya ulinzi atakayefungua mdomo tunammaliza bila utani, wote nyoosheni mikono juu, hapa safari imebadilika tunaelekea msibani huko Moshi na kwa haraka tuanze kuimba nyimbo za maombolezo” James aliongea maneno ambayo yalimfanya kila mmoja kubaki mdomo wazi,
“Unasemajeee” aliongea mmama mmoja alitekua kiti cha nyuma akiwa amepakata mtoto mapajani,
“Shit kimya” James alitamka kisha kumfauta huyo mama na kumnyonga hadi kufa, kitendo hicho kiliwafanya watu wote kuingiwa na hofu, kikosi cha watu kumi kilikua makini ndani ya gari hilo, vioo vilifungwa na ili kuhakikisha hawatoi taarifa popote walikusanya simu zao za mkononi na zote zikawashwa na kuachwa barabarani, ili ndugu watakaotafuta wenzao kwa kutrack simu isiwe rahisi kupatikana.

INAENDELEA

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI: SEHEMU YA-22

Abiria walilazimishwa kuimba nyimbo za msiba, ili kuzidi kuwaogopesha waliweka bomu ndani ya gari ile,
“Yeyote atakayeongea pindi askari wa usalama barabarani anakagua gari basi tutawalipua wote, hivyo mkitaka kuwa salama hakikisheni mnafuata masharti yetu, tunajua wengi wenu mna familia zinazowategemea, mtaacha familia zenu, msipokua makini” James alitamka kisha kuketi na kumuamuru dereva aendeshe kwa makini. Mateka hao walipoona askari wa usalama barabarani akilisimamisha gari hilo, walijawa na furaha lakini furaha yao ilikua ikiyeyuka baada ya mtekaji mmoja kutoa kiasi cha pesa na kumkabidhi kila askari wa usalama ili asiingie ndani ya gari, mdomoni waliimba nyimbo za msiba lakini moyoni walikua wakifanya maombi.
***
Katika ukumbi wa LIFE PARK seherehe iliendelea kama kawaida watu waliendelea kula na kunywa, Martin alionekana mwenye hasira kupita kawaida, alikunywa pombe bila kulewa, alionekana akikuna kichwa mara kwa mara, wahudumu walijawa na hofu, walifanya kazi huku wakitetemeka kwa hofu, “Kweli nimeamini hakuna kazi ndogo inayompa mtu pesa nyingi kama nilivyokua nafikiria” alijisemea mpishi mmoja huku akikumbuka jinsi alivyopewa hiyo kazi kwa haraka tena kwa kutaja msharaha anaoutaka, alijuta kwani aliamini siku hiyo angekua tajiri kwa kazi ndogo,
“Kumbe ilikua kazi ya kishetani, sitokaa nipapatikie kazi, acha nifanye ndogo zenye amani” alizidi kulalamika wakati akivipasua vichwa vya watu waliouwawa pale ukumbini. ***
Mainda , alizidi kumuomba Mungu amlinde Edson, pia aweze kumbadilisha wazo la kumfukuza, aliona maisha yakiwa magumu tena pindi atakapofukuzwa katika nyumba waliyohifadhiwa,
“Mungu nakuomba mateso haya yapungue, naomba tu huyu kaka msaidie na umpe huruma atuhifadhi” alijisemea Mainda katika maombi, hakujua kama Edson kwa wakati huo alikua marehemu.Mainda alivyotazama mandhari ya nyumba ile alifurahi kuona bustani nyingi zilizojaa matunda, mboga na mazao ya nafaka hivyo kazi yake ilikua ni kupalilia tu.
***
Kutokana na mwendo kasi wa gari za msiba majira ya saa kumi kamili alasiri, gari zilikua katika maegesho sehemu moja maarufu kama Mamsera, iliyopo wilayani Marangu mkoani Kilimajaro, msafara huo ulipumzika kwa mda ili waweze kunywa na kula, Winny alichungulia nje kabla ya kushuka,
“Mungu wangu nitakimbilia wapi?” alijisemea Winny baada ya kuona sura ya mwanaume mmoja aliyewahi kumuona na Martin siku za nyuma,
“Huyu mwanaume namjua ni mmoja wa walinzi wa Martin, na hapa itakua amenifuata kunikamata na kuniua” alijisemea moyoni na haraka aliwaza njia ya kumkwepa, alichukua doti za kanga alizopewa ndani ya gari na kujifunga, kisha alimuita msichana mmoja mwenye umbo kama lake,
“Shost nataka tuongee kitu, utakubali nikupe kiasi kikubwa cha pesa?” Winny aliongea huku akiwa anatembea nae, kuelekea sehemu ya kujisaidia,
“Usijali , nambie”? alijibu msichana huyo aliyeonekana kuwa na shauku ya kujua nini kinachotakiwa,
“Nataka uvae hizi nguo zangu ukirudi kwenye gari na mimi nivae zako, hivyo kama utaweza tukabadilishe chooni”, moja kwa moja msichana huyo bila hata kuuliza alikubali kufanya kama Winny alivyotaka. Zoezi la kula lilichukua dakika ishirini,kisha watu walianza kurejea katika magari yao ili safari iweze kuendelea, gari iliyobeba mateka iliendelelea na safari hadi katika Tarafa ya Mashati, kisha kuegeshwa pembeni ya soko dogo la Mrere lililopo karibu na kanisa katoliki la Mashati, hali ya hewa ilikua nzuri, mateka wote waliendelea kuimba nyimbo za kuomboleza, Gaidi mmoja aliyekua ameshuka Mamsera kwa ajili ya kuhakikisha Winny yupo katika msafara alihakikisha Winny amerudi kwenye gari, alimtambua kwa mavazi aliyovaa lakini hakujua kama aliyerudi sio Winny bali ni mtu aliyevaa nguo za Winny.
“Tayari ameshapanda gari sasa nyie cha kufanya subirni hapo hapo msafara ukipita na nyie muunge nyuma, lakini msifike nyumbani, ili tukishamteka iwe kazi rahisi kuondoka”, yalikua mawasiliano kutoka Mamsera na Mashati. Winny alibaki chooni, lakini ghafla alianza kusikitika kwani alijua yule msichana hana nguo ambazo angebadilishia, alimuonea huruma lakini yote alimuachia Mungu. Saa kumi na moja kamili jioni msafara ulikua unaingia nyumbani kwa mkuu wa majeshi Tanzania, hali ya majonzi ilkikua imetanda, waombolezaji waliokua nyumbani hapo walikua wakilia kwa huzuni , wengine walikua wakigaragara ardhini, waombolezaji kutoka Dar es salaam walipofika wengi wao walishindwa kuvumilia na kuanza kulia, msichana aliyekau amevalia nguo za Winny alishuka kwenye gari na kuanza kulia, huku akiendelea kulia alishtuka baada ya kusukumwa na mbaba mmoja aliyeonekana kuwa na nguvu , msichana huyo alianguka chini na mara ,moja walitokea wanaume wawili ambao walivalia mavazi ya huduma ya kwanza na kumbeba haraka haraka, msichana huyo alirusha miguu kuashiria kuwa hajaumia lakini ghafla alitulia baada ya kuchomwa sindano ya kumpoteza fahamu kwa mda, wanaume hao waliovaa nguo maalumu kwa ajili ya kutoa huduma ya kwanza walibeba tena wanaume wawili waliozimia kutokana na majonzi, Bila kupoteza mda James aliita gari la kubeba wagonjwa,(AMBULANCE) haraka gari iliyokuya ikitumika kutoa huduma katika wilaya ya Rombo na kuhamishia Wilaya ya Moshi mjini hasa katika hospital ya Kilimanjaro Christian Medical Centre (KCMC) ilifika kwa haraka na miili hiyo ilipakizwa huku ikifunikwa kwa kanga.James alikua mmoja ya wanaume waliovalia mavazi ya kutoa huduma ya kwanza, na baada ya dereva wa gari hilo kuona watu waliovalia mavazi hayo hakuuliza swali zaidi aligeuza gari na kuondoka bila kuhoji lolote,
“Moja kwa moja hadi Hospital ya Huruma” alitamka James na haraka dereva akaaza kukanyaga mafuta huku kingora kikilia magari yalikaa pembeni, ghafla kabla ya kukunja kushoto ili kuikamata barabara ya kuelekea hospital ya Huruma, dereva alishuka baada ya kutekenywa shingoni na kitu kama chupa, alipunguza mwendo na kugeuka, hakuamini macho yake baada ya kukutana na midomo ya bunduki, “Kimya hivyo hivyo, tunataka utufikishe Dar es salam, hapa hakuna mtu anayehitaji huduma ya hospital” James aliongea na haraka wale wanaume wawili waliokua wamepakiwa kwenye gari kwa kusudi la kupelekewa katika matibabu waliamka. Dereva alipigwa na butwaa, alianza kutetemeka kwa hofu aliona kama siku za kifo chake zimekaribia, James aliona hali ya dereva ikibadilika, aliona akianza kushindwa kumiliki usukani, hapo walimuamuru afunge breki, ili waweze kuendesha wenyewe, na mara moja dereva hakuleta ubishi alikubali kuachia usukani
“Sasa kama hatusaiidii chochote tunakaa naye ya kazi gani?” aliuliza mwanaume mmoja, hapo alichomwa sindano ya kumpoteza . James alikamata usukani, alikua akiendesha kwa mwendo wa kilomita 230 kwa lisaa, lengo lake likiwa kufika Dar es salam usiku huo huo,
“Tayari tumeshamuweka mkononi, tunakuja naye usiku huu huu utamuona hapo”, James alimpa Martin taarifa,
“Ndio maana nawakubali, muwahisheni nataka nimuue kesho saa nne nikifunga hii sherehe”, Martin alijibu na kukata simu. Kwa asilimia mia moja James na kundi lake waliamini msichana waliye nae ni Winny. Mateka waliendelea kukaa ndani ya gari waliletewa chakula ndani ya gari bila watu kujua. Taarifa kutoka kwa James ikaamuru mateka wote wauwawe ili siri isije ikagundulika,
“Tegeni mabomu ndani ya gari kisha mlipue, nyie rudini Dar es salam haraka sisi tupo huku Same” James aliwasiliaani na wenzake waliobaki na wale waliotekwa, na bila kuchelewa walifanya kama walivyoagizwa, waliendesha gari hadi sehemu inayoitwa Olele, gari ikaegeshwa,
“Tunaomba wote mlale chini,” ilikua ni amri kutoka kwa mtekaji mmoja na bila kupoteza mda walilala ndani ya gari licha ya wingi wao lakini wengine waliingia chini ya viti, “Atakayeinua macho tutampiga risasi au kumkata kichwa” sauti hiyo iliwatetemesha mateka wote, hivyo walilala na kutulia. Kumbe baada ya wale mateka kulala watekaji walitoka wote na kuwaacha pale, bila huruma waliminya rimoti, mlipuko mkubwa ukatokea na hakuna hata mmoja aliyepona, waliuwa zaidi ya watu hamsini wasio na hatia, kisha kwa kutumia gari iliyokua imeandaliwa walirudi Dar es salaam, ili kumkabidhi Martin kazi yake, wote walifurahi kutekeleza kazi hiyo kirahisi, bila hata mmoja wao kufa.

INAENDELEA

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI: SEHEMU YA-23

Hakuna askari wa usalama barabarani aliyesimamisha gari la kubebea wagonjwa hivyo ilikua rahisi kwa James kuweza kumfikisha mwanamke waliyeamini ni Winny jijini Dar es salam majira ya saa tisa usiku, sindano alizochomwa bado zilikua na nguvu mwilini hivyo mwanamke huyo hakujua chochote kilichokua kikiendelea.
Bado katika ukumbi wa LIFE PARK sherehe iliendelea, uchafu wa hali ya juu ulifanyika, mapenzi yalifanyika hadharani kutokana na ulevi kuwakamata watu sawasawa, Martin hakua na mtu wa kumliwaza zaidi alikua akikumbatia na kuwanyanyasa wahudumu kingono, aliita kila aliyemvutia na kumfanya kila alichotaka, hakuna mhudumu yeyote aliyethubutu kugoma au kubisha.
“Tayari tumeshafika mkuu, vipi tumlete ukumbini ?”
“Vipi yupo katika hali gani?”
“Bado hajarudiwa na fahamu vizuri maana sinilikuambia tumemchoma sindano za kumzimisha?”
“Basi muhifadhini hadi kesho saa tatu na nusu mumlete hapa ukumbini nataka kumua akiwa na fahamu zake, nataka ayasikie maumivu ya kifo”
“Sawa mkuu, hakuna kitakachoharika”. Yalikua maongezi kati ya James na Martin, wote walifurahi kuona kazi imekamilika salama,
“Hapa tutajipatia hela za kutosha, hii kitu mzee wetu kaifanya kwa hasira sana laziama atatoa ujira mzuri” James aliwaambia wenzake, wote waligongeshana mikono kwa furaha.
Usiku huo huo James na mwenzake mmoja waliondoka na gari hiyo ya kubebea wagonjwa na kwenda kuitelekeza katika daraja la Sarenda.
Msichana aliyedhaniwa ni Winny alihifadhiwa ndani ya nyumba ya James iliyoko Mikocheni wakisubiri siku inayofuata ili waweze kumpeleka kwa Martin akiwa ameshazinduka.
***
Winny alitembea umbali mrefu kutoka barabara kuu ya Himo- Tarakea, aliingia ndani ndani na kutafuta mahali penye kichaka na kujilaza, alijua ni vigumu kuukwepa mkono wa Martin lakini alijipa moyo kuwa atashinda, usiku mzima aliumia juu ya msichana aliyembadilishia nguo zake, aliamini ni vigumu kwa mwanamke huyo kupona,
“Mungu mlinde dada wawatu maana hana hatia” Winny alisema maneno hayo mara kwa mara, akiwa katikati ya kichaka.
***
Mainda hakulala usiku, kichwa chake kilitawaliwa na sauti ya Edson akiwa anawafukuza,
“Itakua ni hasira tu anaweza akaniacha hapa” alijisemea Mainda huku akimpuliza mama Winny aliyekua anaguna kwa maumivu yaliyotoka katika kidonda shingoni, kidonda hicho, kilikua kikichimba kwenda ndani na kilitoa harufu kali, kutokana na kidonda hicho hakuweza kuongea wala kumeza chakula kigumu hivyo Mainda alikua akichukua jukumu la kumtafunia na kumlisha kama mtoto, hata nguvu za kumeza zilikua shida hapo Mainda alikuaa akilazimika kukisukuma kwa ulimi, harufu kali haikumzuia Mainda kufanya hayo, bali aliamua kusimama nae hadi pale atakapoona mwisho,
“Sitakuacha, nitasimama na wewe hata kama utakufa basi utafia mikononi mwangu” Mainda alitamka akiwa anamsafisha haja kubwa.
***
Saa kumi na moja alfajiri Winny alitoka kichakani watu waliomuoa katika maeno aliyopita walimshangaa,
“Mndu mkachu nafuma mrin (huyu mwanamke ametoka mjini)” yalikau maneno ya wamarangu waliokua wakiwahi shambani kwa ajili ya palizi.
Watoto walipomuona akizunguka walikimbia na kujificha hawakutaka kuonana na mtu aliyetoka mjini, Winny hakujali macho ya watu, ingawa hakujua anaelekea wapi alitembea tembea hatimaye alifika katika shule ya sekondari Mwika,ikiwa imetimia saa mbili asubuhi, wanafunzi walikua katika gwaride la asubuhi kabla ya kuingia darasani.
“Hapa inabidi nijiokoe mwenyewe” alijisemea Winny na moja kwa moja alinyoosha hadi jikoni, ambapo alimuona mpishi ambaye alikua akiandaa chai,
“Shkamoo mama” Winny alimwamkia
“Marahaba mwanangu, karibu” mama huyo aliitikia.
“Mama mimi naitwa Winny, nimekuja huku jana kuna mmama alinichukua kutoka Morogoro, akaniambia kuna kazi nije kufanya nae huku sasa tumefika huku amenitelekeza, sina pakuenda na hata sijui nitafanyaje” Winny aliongea uongo ili aweze kupata msaada wa kuhifadhiwa,
“Yesu wangu, mwanangu pole sana, sasa hapa nikusaidie nini, au tuite askari ili huyo mtu atafutwe?” mama huyo aliongea huku akiweka sufuria chini,
“Haina haja ya kumshtaki , namuachia Mungu, lakini mimi kikubwa nipate kazi tu kama kuna mtu anahitaji msaidizi basi nimsaidie kazi yoyote nafanya”, Winny alitaka kupata kazi yoyote ili asionekane mzururaji mtaani hapo, ingawa alikua na zaidi ya dola elfu mbili lakini alitaka kufanya kazi ili aweze kupanga mipango ya kujificha zaidi, kwa bahati nzuri pale pale alipata kazi,
“Basi kama unaweza kunisaiidia sawa, utakua unakaa kwangu, asubuhi utakuja hapa kazini hadi saa tisa” mama huyo aliongea,
“Asante mama, nashukuru kwa kunisaidia” Winny aliongea huku akimpa mkono,
“Sawa mwanangu karibu sana mimi jina langu ni Njau, lakini wanafunzi wa hapa wananiita Mama mpishi, chukua hii eproni uvae” maongezi yaliishia pale na mara moja Winny aliingia jikoni.
***
Saa tatu kamili ndani ya gari aijna ya Lexus James akiwa na wenzake wanne walikua njiani kuelekea LIFE PARK, nyuso zao zilitawaliwa na furaha, mwili wa msichana waliedhania ni Winny ulikua umefungwa vizuri,
“Kwani nimefanya nini na mnanipeleka wapi?”aliuliza mwanamke huyo lakini hakujibiwa kitu zaidi aliambiwa
“Tulia tu utajua unakoenda” gari ilitembea mwendo mkali ili saa tatu kamili wakamkabidhi kwa Martin.
“Mkuu tupo getini vipi tumwingize ama vipi”
“Tulieni nae kwenye gari kwanza maana huyo nataka nimuue alafu nimuweke ndani ya kiroba niondoke nae” Ilikua amri kutoka kwa Martin. Ilipofika saa tatu na nusu Martin alijiwa na wazo la kuuwa wahudumu wote, haraka alimwita James na kumkabidhi kazi hiyo,
“Nataka hawa wahudumu wote wafe maana wanaweza kuniletea usiku” Martin alimnong’oneza James na mara moja James alipanga namna ya kuwauwa, kwa kutumia ishara za kigaidi James na Martin waliwasiliana,
“Sasa ndugu zangu mlioshirikiana na sisi katika sherehe hii, nashukuruni sana,tumefanya kazi ngumu, sasa naomba mnisamehe kwa mabaya yote mliyoyaona humu ndani naomba yaishie humu ndani,sisi ni binadamu tunakosea hivyo naomba mniwie radhi, kifuatacho mtaandamana na huyu ili muende kuchukua malipo yenu,kila mmoja atakua na mkatanba wake mkifika sehemu husika mtakabidhiwa kila mmoja kiasi alichosaini na katika kila mmoja namuongezea Laki moja moja kama Bonasi” yalikua maneno ya Martin mbele ya wahudumu, wahudumu wote walishangaa kumuona Martin akitabasamu, wote waliondoa wasiwasi na walifurahi kusikia ongezeko la mshahara, wote waliapa kutovujisha siri hiyo.
Baada ya wote kuafiki waliandamana na James kutoka ukumbini hadi katika gari aina Canter, wote walipanda na kuondoka na James, mioyo yao ilijawa na furaha kutoka salama eneo lile.
Vijana wawili walibaki ndani ya gari na msichana aliyedhaniwa ni Winny.
Baada ya dakika ishirini, James aliegesha gari nje ya Jengo kubwa karibu na majengo ya ubalozi wa Yemen, barabara ya Ali Haasan Mwinyi, alifungua lango na wote wakaingia ndani ya jengo kubwa, wahudumu hao hawakua na hata chembe chembe ya wasiwasi, zaidi mioyo yao ilitawaliwa na furaha, huku tabasamu pana likipamba nyuso zao.
James alitembea mbele huku kikundi hicho cha wahudumu pamoja na wapishi kilichokua cha zaidi ya watu 45 wakimfuata nyuma , walipita katika Kordo moja, hapakua na kelele za aina yoyote.
Ndani ya nyumba hiyo kulikua na chumba kimoja kilichokua kimejengwa maalumu kwa ajili ya kuulia watu kimya kimya, kilitengenezwa kwa sakafu maalumu ambayo ilikua ikitolewa kwa nguvu za umeme na kuacha shimo kubwa ambalo lilikua na asidi, hivyo walikitumia kwa ajili ya kufanyia mauaji ya kisiri.
Ilikua ngumu sana kwa mtu kushtuka mtego huo,
“Ingieni huko, kila mmoja ashikilie mkataba wake” James alitamka na kufungua mlango wote waliingia chumbani na hapo James akatoka kama mtu aliyesahau kitu, alifunga mlango na moja kwa moja alibonnyeza rimoti iliyokua ikiondoa sakafu kwa mda, hakuna aliyejua kitu kilichofanyika zaidi walijikuta wakiogelea ndani ya dimbwi lenye maji ya kuwasha, maji hayo yalipowaingia machoni waliwashwa sana, hakuna aliyeweza kupiga kelele kwani waliona sakafu ikijifunga na giza kutawala, hapo walikufa mmoja mmoja na kuyeyuka.
James alitoka na kuendesha gari hadi katika ukumbi wa LIFE PARK ili sherehe ikakamilishwe kwa kumkabidhi Winny kwa Martin.
Martin alikua amepanga kumuua Winny kikatili, alipanga kufanya nae mapenzi akiwa anamkata kiungo kimoja kimoja ili afe akiwa anapata raha na maumivu.

INAENDELEA

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI: SEHEMU YA-24

Saa nne kasoro dakika kumi, ukumbi wote ulitulia, ulikua wakati wa Martin kufunga sherehe kwa kutoa hotuba fupi,
“Ndugu zangu, natumai tumefurahia sherehe hii, naamini kila kitu kimeenda sawa na kama kuna mahali nilipokosea natumai wakati ujao nitarekebisha, wageni wangu kutoka Nigeria, na Zambia nawatakia safari njema mkakute kama mlivyoacha, lakini kabla ya kumalizia kabisa sherehe nataka niimalize kwa kuonesha roho ya kinyama mbele yenu, Mr James naomba aingizwe ndani” Martin aliongea hayo na mara moja msichana aliyefunikwa uso kwa kitambaa cheusi aliingizwa ndani, alikua akitetemeka kwa hofu, wanaume wawili wenye nguvu walimshika vizuri kiasi cha kutoweza kujigusa pale alipolazwa chali (KULALA KWA MGONGO) Martin alimtazama kwa makini kisha akaanza kuingiwa na mshangao, aligeuza uso na kumtizama James,
“Ni huyu ?”
“Ndio mkuu ni huyo, kwani huamini?”, james alijibu huku akiinama na kumfungua kitambaa kilichoufunika uso wake, Martin alichanganyikiwa na kuwafyetulia wale vijana risasi, ovyo, James alifanikiwa kutoka ukumbini na kupige kelele, watu pale ukumbini hawakuelewa kitu kilichosababisha Martin kuwa katika hali ile,
“ Hadi nyie wafanyakazi wangu mnaniletea mtu ambaye sijamuhitaji kwa sababu gani” Martin aliongea kwa hasira huku akitupa bunduki yake iliyoishiwa risasi,
“Je wewe ni nani ?” aliongea Martin huku akimsogelea mwanamke huyo aliyeletwa lakini kabla hajamfikia askari zaidi ya kumi waliingia na kumkamata Martin kwani kelele za James pamoja nna milio ya bunduki ziliwafanya askari wafike mapema,
“Chini ya ulinzi” ilikua sauti ya askari mmoja huku bunduki aina ya AK 47 ikimwelekea Martin, alinyoosha mikono juu pamoja na kupiga magoti, haraka alibebwa na kupakizwa ndani ya gari ya polisi pamoja na mwanamke aliyedhaniwa ni Winny,
miili ya waliouwawa ilipakiwa ndani ya gari lingine na kupelekwa hospitali ya Muhimbili kuchunguzwa na kuhifadhiwa.
“Hata kama nikifungwa gerezani lazima James nitakuuwa “, aliongea Martin gari likiwa linaondoka taratibu.
***
Baada ya Wiki tatu, kesi ya Martin ya kuuwa kwa kukusudia ilianza kusikilizwa katika mahakama ya kisutu akishtakiwa na Jamhuri, kwani hapakua na mtu yeyote aliyemshtaki Martin alitumia pesa kujaribu kuhonga lakini kulikua na vikwazo,
“We mzee sikia, mimi nakuhukumu miaka mitano lakini ukikaa mbili nakurudisha uraiani wewe ondoa shaka” yalikua maneno ya hakimu mkuu aliyetakiwa kutoa hukumu kwa Martin baada ya kupokea rushwa, Martin alikubali kufungwa miaka mitano lakini kabla ya kusafirishwa kwenda gereza la Segerea, aliomba kufanya kikao na baadhi ya wafanyabiashara waliokua wakisambaza dawa alizokua akiuza, kilikua kikao cha siri, ambapo alipata uhakika wa kutengeneza pesa akiwa bado gerezani .
“Bsi ndio kama hivyo vijana wangu, pigeni kazi kwa bidii nikitoka nawapa bonasi, nawaachia huyu Adeleka, kila kitu atakisimamia” alimaliza kwa kumkabidhi madaraka raia wa Nigeria aliyeitwa Adeleka, alimpa kazi ya kusafiri kila nchi ili kutafuta masoko, na baada ya hapo alipelekwa rasmi kutumikia kifungo huku kichwani kwake akimuweka James pamoja na Winny kiporo.
***
BAADA YA MWAKA MMOJA.
Hali ya mama Winny ilizidi kuwa mbaya , Mainda alichanganywa na mambo mawili,cha kwanza ni kuhusu hali ya ugonjwa uliomkabili mama Winny na kingine ni kuhusu kijana aliyewapa sehemu ya kuishi kwani ilikua imetimia mwaka mmoja tangu aondoke bila kurejea
“Kwani ina maana kasahau hapa au vipi, alisema atarudi lakini hadi sasa bado” Mainda aliwaza hilo mara kwa mara na hakupata majibu kuhusu Edson, kila siku alilala akijua atakuja kesho lakini hakutokea, kila siku aliendelea kulima mazao mbalimbali ndani ya geti, na mara nyingi alikua pembeni ya kitanda cha mama Winny akisali, harufu kali kutoka ka mama Winny ilizoeleka, hakuna hata mgeni mmoja aliyeingia ndani ya nyumba ile na hakuna mtu aliyejua ni watu wa aina gani wanaoishi humo.
Siku moja aliamua kuvunja chumba ambacho Edson aliingiza mabox, alitumia nyundo kuvunja kitasa, hakuamini macho yake, pesa nyingi zilizo ndani ya mabox yale zilimfanya afurahi kupita kiasi aliruka ruka kwa furaha lakini ghafla alitulia na kujiuliza swali,
“Hivi nafurahi kwani ni zangu?” alijiuliza swali hilo na kuanza kuzihesabu taratibu.
***
Winny alipata wakati mgumu sana kufanya kazi ya upishi kadri siku zilivyokua zinasonga alizidi kupata ujuzi lakini baada ya mezi sita tangu aanze kazi ile alianza kuumwa mara kwa mara, mwili wake ulikua ukichoka sana, huku mafua yasiyopona yakimuandama, alipoona hali hiyo alilazimika kuenda hospital ya Mwika Health Centre, hapo ndipo maisha yake yalibadilika ghafla baada ya kupokea majibu ya kuwa na virusi vya UKIMWI, alikiona kifo kikiwa mbele yake, mwili wake uliporomoka kwa kasi, hakupata hamu ya kula tena, alizitumia pesa zake kununua eneo na kujenga nyumba yake karibu na shule ya sekondari hapo mwika,
“Mungu kwa nini umeyaruhusu haya yatokee?’ Winny alikua akijisemea mara kwa mara.
***
Ilimchukua siku thelathini Mainda kukamilisha zoezi la kuhesabu pesa zile, lakini hakujua afanye nini, nafsi ilimsuta kuzitumia kwa kuwa hakujua aliyeziweka hapo alikua na malengo gani,
“Hivi mtu amenipa hifadhi alafu nije kutumia na pesa zilizo ndani kwake ?” haiwezekani hapa inabidi nikatangaze kanisani ili atafutwe na kama hayupo duniani basi tuzitumie” alijisemea Mainda huku akiikumbuka ndoto aliyoota siku moja kabla ya Edson kuondoka.
Baada ya siku tatu alisikia tangazo la mkutano wa injili, ulikua mkutano ambao ungedumu kwa siku tatu mfululizo,
“Hawa hawa wachungaji naenda kuwaomba ushauri wa nini cha kufanya na hizi pesa pia njia za kumpata Edson” alijisemea Mainda, japo ilikua vigumu kumuamini mchungaji yeyote kutokana na kitendo alichofanyiwa na mchungaji Paschal mwaka mmoja uliopita alijitahidi kuondoa imani mbaya juu ya wachungaji,
“Huyu hataweza kunifanyia vile vitu” alijisemea Mainda huku akielekea katika mkutano huo uliokua ukifanyika katika kiwanja kidogo cha chuo cha ustawi wa jamii.
Hakika mchungaji alitoa mahubiri mazuri, kila aliyesikiliza alirejewa na matumaini aliyokwisha poteza, pia kulikua na wachungaji wawili kutoka Nigeria,
“Mkutano utaendelea tena kesho, tukutane katika viwanja hivi hivi,mimi mchungaji Christian” yalikua maneno aliyofunga nayo mkutano na mara moja Mainda alianza kupenya katikati ya watu ili aweze kuomba kuonana na mchungaji huyo akiamini kuwa ndiye atakayemsaidia na kumshauri kuhusu pesa zilizoachwa na mtu aliyeondoka na kutorudi kwa mda mrefu.
***
Mazengo alikua imara zaidi ya simba, mwalimu wake aliona kuwa Mazengo hawezi kupigwa na mtu yeyote duniani, hivyo alitoa taarifa kwa wachina waliompeleka, baada ya majadiliano na ili wachina kweli waamini kuwa mazengo amekua imara, ilimpasa afanyiwe mtihani, ulikua mtihani mgumu sana, alipaswa kusafiri hadi katikati ya msitu wa Amazon, aweze kuishi huko kwa miezi sita, bila silaha yoyote,
“Wewe kule nenda silaha utazikuta huko huko maana kuna watu wanaenda huko na silaha na wanakufa na kuziacha huko hivyo wewe nenda utakuta silaha zote huko”, yalikua maneno kutoka kwa mwalimu wake na bila ubishi haraka safari ilipangwa, alipanda ndege ya wachina hadi anga ya Brazil ambapo ni mojawapo ya nchi zilizopakana na msitu huo mnene na hatari kuliko msitu wowote duniani , wakiwa anga ya msitu Mazengo alikabidhiwa parachuti pekee, kisha akafunguyliwa mlango maalumu wa kurukia, hakuwa na hofu hata kidogo, ingawa aliamini msituni hapo kuna wanyama wakali na nyoka wa kila aina lakini aliamini ataushinda mtihani huo.
“All the best maaaaaaaaaaaaan, (Kila la heri mbaba)” lilikua neno la rubani wakati Mazengo akiwa anajirusha, aliteremka taratibu akisaidiwa na upepo, kwa mbali alishuhudia nyoka wakubwa wakitambaa msituni hapo.
“Mungu uwe na mimi, katika hii safari” alijisemea Mazengo huku hasira ikiwa ni kwa aliyeangamiza familia yake.
***
“Mainda na mchungaji Christian waliongea mengi, Mainda alimueleza kila kitu hadi kiasi cha pesa alichokua nacho,
“Unatania au ni kweli binti” mchungaji aliuliza kwa mshangao, hakika hakuamini kama kuna mtu anayeweza kuweka hela kiasi kile ndani kisha aondoke na akae zaidi ya mwaka mmoja bila kurudi nyumbani.
Binti naomba kaa nalo na iwe siri yako, hakika wewe ni binadamu wa kipekee sana kama angekua mtu mwingine asingetoa taarifa kama hii, sasa wewe cha kufanya ni kuitunza siri hii, yaani usimwambie mtu yeyote, hadi huu mkutano ukiisha basi tutapanga namna ya kumpata mwenye mali zake na najua hawezi kukuacha hivyo lazima atakutibia huyo mgonjwa wako hadi apone, nakusihi nenda kapumzike hadi kesho uje tena hapa”, mchungaji Christian aliongea huku akiwa haamini vitu alivyosikia kutoka kwa Mainda, baada ya hapo Mainda alimuelekeza mchungaji sehemu anayoishi.
“Jasiri haachi asili”lilikua neno la kwanza kutoka kwa mchungaji baada ya Mainda kuondoka,
“Kweli ni mimi Christian nimepata hii taarifa ??” alijiuliza Christian na kutabasamu,
***
Christian kabla ya kuokoaka na kufungua kanisa alikua jambazi mkubwa, ambaye alianza kufanya matukio ya wizi tangu akiwa shule ya msingi, kitu kilichopelekekea kutosoma sekondari, alijiunga na magenge ya wizi katika mitaa ya Ungalimited Arusha, alifanya matukio makubwa sana ya wizi wa kutumia silaha, alikua anauwa watu bila huruma, baadaye akahamia Dar es salam ambapo siku moja walifanya tukio la wizi katika Hotel ya Serena kwa bahati mbaya wenzake watano waliuwawa akapona peke yake, hapo alimua kuokoka lakini sio kwa ajili ya kuhubiri neno la Mungu bali ni kuiba kwa neno la Mungu, hapo alilazimika kusafiri hadi nchini Nigeria na kupewa mafunzo ya uchungaji, hapo kila mtu alitokea kumuamini, lakini kiuhalisia alijikusanyia sadaka kwa lengo la kunufaika yeye mwenyewe.
Hivyo siku aliyopewa taarifa kutoka kwa Mainda alikumbuka mambo yake ya zamani na moja kwa moja alitoa simu yake na kumpigia mmojawapo ea viongozi wa magenge ya ujambazi aliyeitwa Fork,
“Fork fanya tuonene leo leo kwa haraka,
“Mzee nipo Tarakea katika mpaka wa Tanzania na Kenya kuna mission tunaenda kufanya Nairobi” alijibu Fork
“Wewe nakuambia geuza msafara wako, usiku huu huu mfike Dar es salam kuna donge nono liko mahali” mchungaji Christian aliongea na mara moja safari ya Fork na kundi lake iligeuka.

INAENDELEA...

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI: SEHEMU YA-25

Katika magonjwa yaliyokua yanasumbua watu wengi duniani mojawapo ilikua ni saratani aina zote, wagonjwa wengi waliougua saratani mwisho wao ulikua kuaga dunia kwa mateso makali, mama yake Winny ane alikua mmojawapo ya wagonjwa walioteseka kwa saratani, watalamu wengi wa afya kutoka kote duniani walikua wakikesha usiku kucha ili waweze kupata tiba lakini hawakufanikiwa, nchi za Afrika ndizo zilikumbwa zaidi na tatizo hilo.
Lakini kwa bahati nzuri baada ya kuhangaika kwa miaka mingi wataamu kutoka katika chuo kikuu cha Lebanon, Beirut Arab University (BAU) walifanikiwa kugundua dawa ambayo iliweza kutibu ugonjwa wa saratani, dawa hiyo iliweza kumtibu panya waliyemuambukiza wadudu wa saratani, mda wa kuifanyia majaribio kwa binaamu pia ilifanikiwa kutibu binadamu.
Taarifa za kupatikana kwa dawa hiyo ilisambaa kote duniani, kila nchi ilitamani kusaidia wananchi wake wanaoishi na saratani watibiwe, katika nchi zilizotamani wananchi wake watibiwe Tanzania ilikuwepo, ilikua tayari kugharamia nusu ya matibabu hayo pamoja na usafiri.
Matangazo na vipeperushi vikaanza kutolewa kuwa wenye wagonjwa wajitokeze kuandikisha majina yao.
Mainda akiwa njiani kutoka kwa mchungaji pia alipata taarifa hiyo, uso wake ulijawa na furaha, aliamini mama Winny atapona kulingana na pesa zilizokua ndani, aliamini mchungaji Christian atamsaidia kwa kila kitu.
“ Kwa wenye wagonjwa mnatakiwa kuwasilisha vielelezo vyenu kwa ofisi ya serikali iliyo katibu na wewe na ili kuenda lazima uhakikishe unalipia robo ya gharama huku serikali ikilipia robo tatu” ndivyo tangazo lilivyoeleleza, Mainda alililala kwa furaha na kulipopambazuka haraka alijajiandaaa kwenda kwa mchungaji juu ya kumueleza kuhusu kutibiwa kwa mama Winny.
***
Fork na vijana wake watano waliingia jijini Dar es salam na kukutana na mchunngaji Christian, usiku huo huo walikaa kikao cha kujadili namna watakavyochukua pesa na nyuymba kutoka kwa Mainda,
“Wazee hii ishu ifanyike kimya kimya, huyo binti na huyo kilema wake anayelala kitandani nataka hata wafe lakini pesa ni zangu nyie mtachukua nyumba na ile nyumba iko sehemu nzuri mkiuza hata billion mnapata” mchungaji Christian aliongea kwa msisitizo, wote walikubaliana na mara moja mpango huo ukanza lakini kichwani kwa Fork aliingiwa na huruma, hakutaka kufanya kifo cha kinyama kama walivyokua wamepanga, bali alitaka kumuua Mainda na mama Winny bila kuwaona wakifa. Kikao kikadumu hadi asubuhi majira ya saa kumi na mbili, Mchungaji Christian alitoka na kama kawaida alielekea eneo la mkutano wa injili, alishangaa kumuona Mainda akiwa na tabasamu pana mdomoni, aliamini kuna habari mpya,
“Karibu sana binti, unaendeleaje ?
“Naendelea vizuri kabisa namshukuru Mungu”
“ Mbona asubuhi asubuhi?”
“Kuna habari nimeipata katika vyombo vya habari kuhusu dawa ya saratani iliyopatikana huko Beirut, Lebanon, na watu wengi wanasafiri kufuata matibabu, nikaona na mimi nije kukushirikisha ili tuweze kumsafirisha yule mgonjwa wangu hata ikibidi kwa pesa ambazo zipo kule ndani kwa hiyo tusisitangaze tena kwanza naomba kwanza tumsaidiie huyu mama”, Mainda aliongea kwa huruma, hakujua moyoni kwa mchungaji kulikua na mambo gani,
“Sawa basi acha niangalie namna ya kufanya , kesho ndio siku ya mwisho wa mkutano nitakusaidia kupata na wewe barua ya kuenda “ Mchungaji alijibu kisha kujipongeza kimoyomoyo alimiani hiyo ndiyo njia pekee ya kumdhululumu mali zote kirahisi.
Mainda alirudi nyumbani na kuendelea na kazi zake taratibu huku akiwa amerejewa na matumaini .
Mchungaji Christian alikaa tena kikao na Fork, usiku na wakajadiliana mambo ya kufanya,
“Kazi imekua rahisi, hapa tunachukua kilaini kabisa” alitamka Fork.
Baada ya siku tano Mainda alikua katika maandalizi ya safari, japo ilikua vigumu kupata kibali cha kusafiri kuelekea Lebanon mchungaji Christian alihakikisha amekipata kwa kuhonga, hakuna mtu wa hali ya chini aliyefanikiwa kupata kibali, matajiri wengi walitumia rushwa kupata kibali.
Muunganiko wa nchi za Afrika Mashariki chini ya wizara ya afya walikubaliana wagonjwa wote kutoka katika nchi zao wakutane nchini Uganda, ndege kubwa yenye kubeba abiria mia nane ilikua katika kiwanja cha Entebe Intenation Airport (ENA).
“Mainda wewe nenda kwa amani kabisa, muombe Mungu akusimamie katika safari yako natumai tutaonana, chukua hii simu tuwe tunawasiliana ukiwa njiani, nikutakie kila la heri” mchungaji Christian alikua akiagana na Mainda kabla ya kupanda basi ambalo lilitakiwa kusafirisha wagonjwa kutoka Dar es salam hadi jiji Kampala, Uganda.
Christian ndiye alikabidhiwa kila kitu katika nyumba ile, kilichobaki kilikua njia ya kutengeneza mazingira ya kumuaminisha Mainda kuwa mchungaji hakuwa mtu mbaya, hivyo haraka Christian alitengeneza mchezo na akina Fork,
“Hapa inatakiwa gari ndogo ya hata million mbili, tuende Mochwari ya Muhimbili tununue maiti kisha tuje tuichome ndani ya gari alafu simu yangu itumike kumtumia Mainda ujumbe wa kuwa mchungaji Christian amekufa na kila mahali taarifa hiyo isambae, hapo naamini atajua asilimia zote mimi ni mtu mzuri” alimaliza Christian na haraka mpango huo ulifanyika.
***
Maisha ya Mazengo yalikua hatarini ndani ya msitu wa Amazon, kila alipokanyaga alikoswakoswa na mnyama aina tofauti, silaha nyingi pamoja bidhaa za aina tofauti zilijaa ndani ya msitu, aliona mijusi wakubwa na nyoka wanaoweza kumeza hadi ngombe wawili, mara nyingi alitembea akiwa ameshika wanyama kama vile sungura, kicheche, nguchiro na wengine kusudi pale anapokutana na mnyama mkali aweze kumrushia mnyama mojawapo aliemshika ili kumchanganya,nyoka aina ya Koboko walikua wakirusha mate ambayo aliyakwepa kwa ustadi mkubwa, alikua akiumwa na nyuki mara nyingi alipoingia katika mapango ya miti.
***
Winny alianza kuona aibu kwa mwili wake jinsi ulivyoisha, uzuri ake ulipotea, hapo alianza kuamini maneno ya watalamu wa afya waliompa majibu ya kuwa ni muathirika wa VVU hapo aliamua rasmi kutumia vidonge vya kupunguza makali ya vizuri hao ARV baada ya kuanza kutumia mwili wake ulianza kurudi taratibu, licha ya kuishi maisha ya kawaia tena akiwa kijijini bado umbo lake lilizidi kuwatamanisha wanaume wengi, kila aliyemuona jinsi alivyonenenpa alihishi kuwa alipatwa na matatizo mengine lakini sio UKIMWI kama ilivyosemekena, kichwani mwake aliwaza kwa jinsi gani ambavyo angerudi Dar es salam angalau akakutane na rafiki yake Kemmy, hakujua kama kwa mda huo ni marehemu, kuhusu familia aliamini hadi wakati huo hata akirudi hawatamtambua tena,
“Nitafia hapa hapa Mwika” alijisemea Wnny mara kwa mara.
***
Usiku wa saa nne kamili ulikua usiku wa furaha zaidi kwa Mainda, walikua wamebakiza mita mia moja kabla ya kuingia nchini Uganda, mda wote ndani ya gari alikua akisali na kuimba, lakini furaha yake iliyeyuka baada ya kuongea na mtu asiyemfahamu , mtu huyo alitumia simu ya mchungaji Christian,
“Amekufa ?” aliuliza kwa sauti kubwa huku akiangua kilio
“Ndio amepata ajali mda mfupi uliopita na tulipotaka kumuokoa tulifanikiwa kuokota simu ndani ya gari lakini kabla ya kumtoa yeye gari ililipuka na kumuunguza hadi kuwa majivu” maneno hayo yalimfanya Mainda aishiwe nguvu, alilia kama mtoto mdogo hakuamini kama kweli mtu aliyempa msaada mkubwa kiasi kile alikua amekufa kifo kibaya tena ghafla,
“Eh Mungu nilikua nimepata mtetezi lakini ona tena shetani amemchukua, nitajificha wapi mimi,? Ngoja tu mama Winny apone kisha nikachukue pesa zilizobaki pale ndani niweze kuzipeleka bank” alijisemea Mainda kwa huzuni.
***
Bila kupoteza muda Fork alitengeneza hatimiliki bandia ya nyumba aliyoishi Mainda, huku mchungaji akitoweka na pesa kwenda nchini Nigeria.
Hatimilikia ilikamilika na haraka nyumba ile ikauzwa kwa wazungu kutoka Ujeruman Mainda akiwa Uganda kabla hata hajasafiri kwenda Lebanon.

INAENDELEA

the Legend☆
 
Mkuu ukiona hivyo ujue sijamjua mtunzi ni nani, hii simulizi ilitumwa kwenye moja ya whatsapp group exactly kama nnavyoiwasilisha hapa. Nothing more, nothing less

the Legend☆
Sawa mkuu ila watu wanaiba kazi za waandishi na kama ni hivyo si kosa lako ila sina hakika na huyo aliye share kama alikuwa na ruksa toka kwa mwandishi, hii kazi bado inachangamoto kubwa hasa usawa huu wa maendeleo ya sayansi na teknolojia.
 
BASI LA SHETANI: SEHEMU YA-24

Saa nne kasoro dakika kumi, ukumbi wote ulitulia, ulikua wakati wa Martin kufunga sherehe kwa kutoa hotuba fupi,
“Ndugu zangu, natumai tumefurahia sherehe hii, naamini kila kitu kimeenda sawa na kama kuna mahali nilipokosea natumai wakati ujao nitarekebisha, wageni wangu kutoka Nigeria, na Zambia nawatakia safari njema mkakute kama mlivyoacha, lakini kabla ya kumalizia kabisa sherehe nataka niimalize kwa kuonesha roho ya kinyama mbele yenu, Mr James naomba aingizwe ndani” Martin aliongea hayo na mara moja msichana aliyefunikwa uso kwa kitambaa cheusi aliingizwa ndani, alikua akitetemeka kwa hofu, wanaume wawili wenye nguvu walimshika vizuri kiasi cha kutoweza kujigusa pale alipolazwa chali (KULALA KWA MGONGO) Martin alimtazama kwa makini kisha akaanza kuingiwa na mshangao, aligeuza uso na kumtizama James,
“Ni huyu ?”
“Ndio mkuu ni huyo, kwani huamini?”, james alijibu huku akiinama na kumfungua kitambaa kilichoufunika uso wake, Martin alichanganyikiwa na kuwafyetulia wale vijana risasi, ovyo, James alifanikiwa kutoka ukumbini na kupige kelele, watu pale ukumbini hawakuelewa kitu kilichosababisha Martin kuwa katika hali ile,
“ Hadi nyie wafanyakazi wangu mnaniletea mtu ambaye sijamuhitaji kwa sababu gani” Martin aliongea kwa hasira huku akitupa bunduki yake iliyoishiwa risasi,
“Je wewe ni nani ?” aliongea Martin huku akimsogelea mwanamke huyo aliyeletwa lakini kabla hajamfikia askari zaidi ya kumi waliingia na kumkamata Martin kwani kelele za James pamoja nna milio ya bunduki ziliwafanya askari wafike mapema,
“Chini ya ulinzi” ilikua sauti ya askari mmoja huku bunduki aina ya AK 47 ikimwelekea Martin, alinyoosha mikono juu pamoja na kupiga magoti, haraka alibebwa na kupakizwa ndani ya gari ya polisi pamoja na mwanamke aliyedhaniwa ni Winny,
miili ya waliouwawa ilipakiwa ndani ya gari lingine na kupelekwa hospitali ya Muhimbili kuchunguzwa na kuhifadhiwa.
“Hata kama nikifungwa gerezani lazima James nitakuuwa “, aliongea Martin gari likiwa linaondoka taratibu.
***
Baada ya Wiki tatu, kesi ya Martin ya kuuwa kwa kukusudia ilianza kusikilizwa katika mahakama ya kisutu akishtakiwa na Jamhuri, kwani hapakua na mtu yeyote aliyemshtaki Martin alitumia pesa kujaribu kuhonga lakini kulikua na vikwazo,
“We mzee sikia, mimi nakuhukumu miaka mitano lakini ukikaa mbili nakurudisha uraiani wewe ondoa shaka” yalikua maneno ya hakimu mkuu aliyetakiwa kutoa hukumu kwa Martin baada ya kupokea rushwa, Martin alikubali kufungwa miaka mitano lakini kabla ya kusafirishwa kwenda gereza la Segerea, aliomba kufanya kikao na baadhi ya wafanyabiashara waliokua wakisambaza dawa alizokua akiuza, kilikua kikao cha siri, ambapo alipata uhakika wa kutengeneza pesa akiwa bado gerezani .
“Bsi ndio kama hivyo vijana wangu, pigeni kazi kwa bidii nikitoka nawapa bonasi, nawaachia huyu Adeleka, kila kitu atakisimamia” alimaliza kwa kumkabidhi madaraka raia wa Nigeria aliyeitwa Adeleka, alimpa kazi ya kusafiri kila nchi ili kutafuta masoko, na baada ya hapo alipelekwa rasmi kutumikia kifungo huku kichwani kwake akimuweka James pamoja na Winny kiporo.
***
BAADA YA MWAKA MMOJA.
Hali ya mama Winny ilizidi kuwa mbaya , Mainda alichanganywa na mambo mawili,cha kwanza ni kuhusu hali ya ugonjwa uliomkabili mama Winny na kingine ni kuhusu kijana aliyewapa sehemu ya kuishi kwani ilikua imetimia mwaka mmoja tangu aondoke bila kurejea
“Kwani ina maana kasahau hapa au vipi, alisema atarudi lakini hadi sasa bado” Mainda aliwaza hilo mara kwa mara na hakupata majibu kuhusu Edson, kila siku alilala akijua atakuja kesho lakini hakutokea, kila siku aliendelea kulima mazao mbalimbali ndani ya geti, na mara nyingi alikua pembeni ya kitanda cha mama Winny akisali, harufu kali kutoka ka mama Winny ilizoeleka, hakuna hata mgeni mmoja aliyeingia ndani ya nyumba ile na hakuna mtu aliyejua ni watu wa aina gani wanaoishi humo.
Siku moja aliamua kuvunja chumba ambacho Edson aliingiza mabox, alitumia nyundo kuvunja kitasa, hakuamini macho yake, pesa nyingi zilizo ndani ya mabox yale zilimfanya afurahi kupita kiasi aliruka ruka kwa furaha lakini ghafla alitulia na kujiuliza swali,
“Hivi nafurahi kwani ni zangu?” alijiuliza swali hilo na kuanza kuzihesabu taratibu.
***
Winny alipata wakati mgumu sana kufanya kazi ya upishi kadri siku zilivyokua zinasonga alizidi kupata ujuzi lakini baada ya mezi sita tangu aanze kazi ile alianza kuumwa mara kwa mara, mwili wake ulikua ukichoka sana, huku mafua yasiyopona yakimuandama, alipoona hali hiyo alilazimika kuenda hospital ya Mwika Health Centre, hapo ndipo maisha yake yalibadilika ghafla baada ya kupokea majibu ya kuwa na virusi vya UKIMWI, alikiona kifo kikiwa mbele yake, mwili wake uliporomoka kwa kasi, hakupata hamu ya kula tena, alizitumia pesa zake kununua eneo na kujenga nyumba yake karibu na shule ya sekondari hapo mwika,
“Mungu kwa nini umeyaruhusu haya yatokee?’ Winny alikua akijisemea mara kwa mara.
***
Ilimchukua siku thelathini Mainda kukamilisha zoezi la kuhesabu pesa zile, lakini hakujua afanye nini, nafsi ilimsuta kuzitumia kwa kuwa hakujua aliyeziweka hapo alikua na malengo gani,
“Hivi mtu amenipa hifadhi alafu nije kutumia na pesa zilizo ndani kwake ?” haiwezekani hapa inabidi nikatangaze kanisani ili atafutwe na kama hayupo duniani basi tuzitumie” alijisemea Mainda huku akiikumbuka ndoto aliyoota siku moja kabla ya Edson kuondoka.
Baada ya siku tatu alisikia tangazo la mkutano wa injili, ulikua mkutano ambao ungedumu kwa siku tatu mfululizo,
“Hawa hawa wachungaji naenda kuwaomba ushauri wa nini cha kufanya na hizi pesa pia njia za kumpata Edson” alijisemea Mainda, japo ilikua vigumu kumuamini mchungaji yeyote kutokana na kitendo alichofanyiwa na mchungaji Paschal mwaka mmoja uliopita alijitahidi kuondoa imani mbaya juu ya wachungaji,
“Huyu hataweza kunifanyia vile vitu” alijisemea Mainda huku akielekea katika mkutano huo uliokua ukifanyika katika kiwanja kidogo cha chuo cha ustawi wa jamii.
Hakika mchungaji alitoa mahubiri mazuri, kila aliyesikiliza alirejewa na matumaini aliyokwisha poteza, pia kulikua na wachungaji wawili kutoka Nigeria,
“Mkutano utaendelea tena kesho, tukutane katika viwanja hivi hivi,mimi mchungaji Christian” yalikua maneno aliyofunga nayo mkutano na mara moja Mainda alianza kupenya katikati ya watu ili aweze kuomba kuonana na mchungaji huyo akiamini kuwa ndiye atakayemsaidia na kumshauri kuhusu pesa zilizoachwa na mtu aliyeondoka na kutorudi kwa mda mrefu.
***
Mazengo alikua imara zaidi ya simba, mwalimu wake aliona kuwa Mazengo hawezi kupigwa na mtu yeyote duniani, hivyo alitoa taarifa kwa wachina waliompeleka, baada ya majadiliano na ili wachina kweli waamini kuwa mazengo amekua imara, ilimpasa afanyiwe mtihani, ulikua mtihani mgumu sana, alipaswa kusafiri hadi katikati ya msitu wa Amazon, aweze kuishi huko kwa miezi sita, bila silaha yoyote,
“Wewe kule nenda silaha utazikuta huko huko maana kuna watu wanaenda huko na silaha na wanakufa na kuziacha huko hivyo wewe nenda utakuta silaha zote huko”, yalikua maneno kutoka kwa mwalimu wake na bila ubishi haraka safari ilipangwa, alipanda ndege ya wachina hadi anga ya Brazil ambapo ni mojawapo ya nchi zilizopakana na msitu huo mnene na hatari kuliko msitu wowote duniani , wakiwa anga ya msitu Mazengo alikabidhiwa parachuti pekee, kisha akafunguyliwa mlango maalumu wa kurukia, hakuwa na hofu hata kidogo, ingawa aliamini msituni hapo kuna wanyama wakali na nyoka wa kila aina lakini aliamini ataushinda mtihani huo.
“All the best maaaaaaaaaaaaan, (Kila la heri mbaba)” lilikua neno la rubani wakati Mazengo akiwa anajirusha, aliteremka taratibu akisaidiwa na upepo, kwa mbali alishuhudia nyoka wakubwa wakitambaa msituni hapo.
“Mungu uwe na mimi, katika hii safari” alijisemea Mazengo huku hasira ikiwa ni kwa aliyeangamiza familia yake.
***
“Mainda na mchungaji Christian waliongea mengi, Mainda alimueleza kila kitu hadi kiasi cha pesa alichokua nacho,
“Unatania au ni kweli binti” mchungaji aliuliza kwa mshangao, hakika hakuamini kama kuna mtu anayeweza kuweka hela kiasi kile ndani kisha aondoke na akae zaidi ya mwaka mmoja bila kurudi nyumbani.
Binti naomba kaa nalo na iwe siri yako, hakika wewe ni binadamu wa kipekee sana kama angekua mtu mwingine asingetoa taarifa kama hii, sasa wewe cha kufanya ni kuitunza siri hii, yaani usimwambie mtu yeyote, hadi huu mkutano ukiisha basi tutapanga namna ya kumpata mwenye mali zake na najua hawezi kukuacha hivyo lazima atakutibia huyo mgonjwa wako hadi apone, nakusihi nenda kapumzike hadi kesho uje tena hapa”, mchungaji Christian aliongea huku akiwa haamini vitu alivyosikia kutoka kwa Mainda, baada ya hapo Mainda alimuelekeza mchungaji sehemu anayoishi.
“Jasiri haachi asili”lilikua neno la kwanza kutoka kwa mchungaji baada ya Mainda kuondoka,
“Kweli ni mimi Christian nimepata hii taarifa ??” alijiuliza Christian na kutabasamu,
***
Christian kabla ya kuokoaka na kufungua kanisa alikua jambazi mkubwa, ambaye alianza kufanya matukio ya wizi tangu akiwa shule ya msingi, kitu kilichopelekekea kutosoma sekondari, alijiunga na magenge ya wizi katika mitaa ya Ungalimited Arusha, alifanya matukio makubwa sana ya wizi wa kutumia silaha, alikua anauwa watu bila huruma, baadaye akahamia Dar es salam ambapo siku moja walifanya tukio la wizi katika Hotel ya Serena kwa bahati mbaya wenzake watano waliuwawa akapona peke yake, hapo alimua kuokoka lakini sio kwa ajili ya kuhubiri neno la Mungu bali ni kuiba kwa neno la Mungu, hapo alilazimika kusafiri hadi nchini Nigeria na kupewa mafunzo ya uchungaji, hapo kila mtu alitokea kumuamini, lakini kiuhalisia alijikusanyia sadaka kwa lengo la kunufaika yeye mwenyewe.
Hivyo siku aliyopewa taarifa kutoka kwa Mainda alikumbuka mambo yake ya zamani na moja kwa moja alitoa simu yake na kumpigia mmojawapo ea viongozi wa magenge ya ujambazi aliyeitwa Fork,
“Fork fanya tuonene leo leo kwa haraka,
“Mzee nipo Tarakea katika mpaka wa Tanzania na Kenya kuna mission tunaenda kufanya Nairobi” alijibu Fork
“Wewe nakuambia geuza msafara wako, usiku huu huu mfike Dar es salam kuna donge nono liko mahali” mchungaji Christian aliongea na mara moja safari ya Fork na kundi lake iligeuka.

INAENDELEA...

the Legend☆
Mainda jinga hili bora liibiwe tu
 
Aisee nmeanza kuisoma jana leo nim kwamia kwenye sehemu ya 13... Hadithi nzuri sana yenye mafunzo mengi japo vitu vingi ni vya nadharia mfano namna ya ilivyopangwa Mazengo kuuwawa na kuokoka kwake huko kwenye shimo la dhahabu ila ukweli unabaki kama ulivo kwamba inafunza sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sawa mkuu ila watu wanaiba kazi za waandishi na kama ni hivyo si kosa lako ila sina hakika na huyo aliye share kama alikuwa na ruksa toka kwa mwandishi, hii kazi bado inachangamoto kubwa hasa usawa huu wa maendeleo ya sayansi na teknolojia.
Uko sahihi mkuu. So far bado najaribu kufuatilia mtunzi hasa wa hii simulizi ni nani, ili apate credit anayostahili. kwa taarifa nlizopata so far inasemekana anaitwa Deo Massawe (to be confirmed)

the Legend☆
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom