Simulizi: Basi la shetani

Simulizi: Basi la shetani

BASI LA SHETANI: SEHEMU YA-12

Mazengo aliinua uso na kumtazama aliyekua anahesabu, aligeuka upande wa pili na kuwaangalia waandishi wa habari waliokua wamejipanga pale,
“Moja, mbili,tatuu” baada ya maneno hayo kilio kilitanda kwa watu wote waliokua wanaangalia tukio lile, mkewe ndiye hakuamini alijikuta akipoteza fahamu baada ya kuona mmewe amesukumwa na kudumbukia shimoni, tena shimo ambalo ingekua vigumu kwa mtu kupona kutokana na miamba iliyokua chini.
Winny ndiye hakuamini kilichotokea, Martin alizidi kumbembeleza bila mafanikio,
“Mpenzi wangu hata kama baba amekufa amini bado nipo na wewe” Martin aliongea maneno ambayo yalimpa Winny hasira,
“Kwani wewe ni nani kwangu, mimi nipo na wewe kukuchuna tu huna maana zaidi ya baba yangu”Winny alitamka baada ya kutolewa gundi mdomoni, Martin alipoona Winny hataki kutulia aliamua kumchoma sindano ya usingizi.
***
Katika eneo hilo la Hong Kong mita chache kutoka eneo yalipokua makao makuu ya tume ya kuthibiti madawa ya kulevya palikua na msitu mnene, msitu huo ulikua na wanyama wakali kitu kilichopelekea serikali ya China kupiga marufuku watu kuingia msituni hapo, pia katika ardhi ya msitu huo kulidaiwa kuwa na madini ya dhahabu, hivyo kukawa na kikundi kimoja kilichoamua kuingia msituni hapo kisirisiri na kuanza kuchimba, kilikua kikundi cha vijana zaidi ya mia moja, walijipanga msituni hapo wakichimba kwa kupokezana, walikua na mitungi ya hewa, walijipanga kuanzia mwanzo wa shimo hivyo walipokezana kutoa udongo kwa mtindo wa kumsogezea mwenzako ndoo hadi nje, na chakula kilitoka nje kwa mtindo wa kumsogezea mwenzako hadi shimo lilipokua limefikia, vijana hao walitoka sehemu mbalimbali kama Wuhan, Shanghai, Quanzhou, na hadi wengine walitoka katika kisiwa cha Taiwan, na Taipei,baada ya miaka mitatu wakiwa wanachimba bila mafanikio siku moja aliyekua ameshika jembe kwa mbele alishtuka kukutana na shimo, alipotazama juu alishtuka kuona mwanga kwa mbali haraka alitoa taarifa kwa mwenzake aliyekua nyuma yake hivyo hivyo hadi kwa kiongozi wao aliyekua nje kabisa,baada ya taarifa kufika kwa kiongozi kiongozi alitoa amri ya kazi kuendelea, hivyo kijana huyo akalazimika kuendelea kuchimba, miamba iliyochongoka mwisho wa shimo hilo ilimpasa afanye kazi pale kwa umakini aweze kufukia miamba hivyo kusudi isimkate mtu, Kwa hali isiyo ya kawaida walishtuka kishindo cha mzigo uliodondoka kutoka juu, wote walishtuka, hawakujua lile shimo lilikua na kazi gani, walitetemeka kwa hofu na ndipo mmoja aliposogea karibu na kuona binadamu aliyewekwa ndani ya kiroba huku kichwa kikiwa nje, taarifa ilienda moja kwa moja kwa kiongozi wao na kiongozi akaamuru mtu huyo atolewe nje, hivyo kwa kupokezana walianza kumtoa nje huku akiwa hana fahamu, walimtoa nje ya kiroba, baada ya mita kumi tokea alipodondokea alirudiwa na fahamu na kuanza kupige kelele, hakujua mahali alipo, aliamini pale ndipo anabebwa aidha na malaika kwenda mbinguni au au mashetani kwenda motoni, hakuamini kama angekua hai tena,
“Ni mimi kweli nimesukumiwa ndani ya shimo, na niko hai hadi sahivi? siamini” alijisemea Mazengo, mikwaruzo aliyoipata kichwani hakuisikia zaidi alishindwa kujua ameokokaje, pia alishindwa kujua hao wanaombeba wametoka wapi na ni akina nani na nini kitatokea akifika huko anakopelekwa, ghafla wazo likamjia kichwani, akawa mbishi kubebwa, alikataa katu katu, alipiga kelele hadi vijana wa kichina wakaamua kuchimba shimo pembeni ili wamfiche na waweze kuendelea na kazi, walichimba shimo kwa haraka lakini bila kutarajia walishtuka kuona vitu vinavyongaa, kuangalai vizuri walikuta ni dhahabu zenye zaidi ya kilogramu kumi, hawakuamini macho yao taarifa ilifika kwa kiongozi wao huku wakieleza jinsi walivyokua wanachimba shimo kwa ajili ya kumhifadhi huyo mtu aliyedondoka na ndipo wakapata dhahabu, huku wakiendelea kushangilia walishtuka moto ukishuka kutoka juu na kutua sehemu ambayo mwili wa Mazengo ulipodondokea, hapo moja kwa moja wakagundua Mazengo ilibidi auwawe wakamuokoa.
Hawakupoteza muda walitoka na mazengo hadi msituni, walikua wakiongea kwa matendo, kutokana na njaa Mazengo aliyokua nayo alijikuta akila nyoka aliyechomwa. Lakini hakutaka kabisa kutoka msoituni hapo kwani alimini atauwawa pale atakapogundulika na maadui zake.
***
Kilio kilizidi baada ya mkaa kushushwa shimoni, watu walivuta picha na kuona jinsi mwili wa mazengo unavyoungua, Martin ndiye alikua na furaha kupita kiasi kuona kesi yake imefutika, mke wa Mazengo alikua akizinduka na kupoteza fahamu mara kwa mara, bado tukio hilo la kuchomwa moto lilikua likiendelea kurushwa katika vituo vya televisheni, askari wa kichina walionekana kuongeza mkaa kwa wingi shimoni kisha kulifunika kwa juu ili aungue na kuteketea moja kwa moja, ingekua vigumu kwa mtu yeyote aliyekua anaona tukio hilo kuamini kama Mazengo bado yupo hai.
***
Haraka kiongozi wa waliokuya wakichimba madini, aliwaacha vijana wake msituni na kusafiri hadi New Delh nchini India kwa ajili ya kuuza madini, vijana wake walibaki na Mazengo msituni wakimwabudu kama Mungu aliyewapa utajiri, kwani bila yeye wasingepata madini kirahisi,kila asubuhi wote walikua wakimsalimia kwa heshima japo hawakuweza kuwasiliana kwa lugha zaidi ya matendo.
“Ama kweli ukimtumaini Mungu hakuna linaloshindikana, sipati picha dunia nzima itakaponiona nikiwa hai tena” alijisemea Mazengo huku akiwaza kwa jinsi gani angeonana na mkewe tena.
***
Baada ya Martin kuamini amekamilisha zoezi la kumuua Mazengo haraka alipanga mbinu za kumuua mkewe kisha aweze kumuua Winny, ili siri isiweze kugundulika. Alifanya mawasilino na daktari mmoja wa Muhimbili na kumhonga kiasi kikubwa cha pesa kusudi aweze kumuweka mke wa Mazengo chumba cha pekee cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu, Mainda ndiye alikua anamuuguza, alisitisha masomo yake akawa anashinda nae hospital. Haraka mipango ya kumhamishia katika chumba maalumu ilifanyika, alipewa chumba cha peke yake ambacho hata Mainda hakuruhusiwa kuingia katika chumba hicho hivyo alilazimika kukaa mlangoni mda wote, daktari mmoja tu ndiye alikua akimhudumia mama Winny siku zote, presha ilimpanda kwa kiasi kikubwa , yote kutokana kushuhudia tukio la kuuwawa kwa mumewe.
Katika hali ya kawaida ambayo ilikua ikitokea katika nyingi ya hospital pale anapotokea mgonjwa mwenye hela basi mara nyingi huweza kuhamisha mgonjwa asiye na pesa ili kupisha mwenye hela atibiwe kwanza, kwa bahati mbaya au nzuri asubuhi moja ya siku ya jumamosi kuliletwa mgonjwa mmoja mwanamke aliyekua katika hali mbaya, hivyo alilazimika kuwekwa katika chumba maalumu, na hapo ndipo mme wake aliweza kuhonga pesa nyingi na kumuondoa mke wa Mazengo katika chumba hicho, mke wa mazengo alihamishiwa katika chumba cha wagonjwa wa kawaida, bila Mainda kujua hivyo Mainda aliendelea kukaa mlangoni akiamini mama Winny ndiye yupo ndani, akiwa ameinamisha kichwa chini aliona daktari mmoja aliyevaa gauni lakini hakutembea kama mwanamke, kitendo hicho kilimpa wasiwasi hasa baada ya daktari huyo kufungua mlango ambao Mainda aliamini mama Winny ndiye aliye ndani.

Itaendelea

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI: SEHEMU YA-13

Shunie hearly kisukari dumejeuri Born2xhine bright platnumz Flozzg

Mainda aliingiwa na wasiwasi na kunyanyuka alipokua ameketi, alitembea kwa kunyata hadi mlangoni, lakini kabla hajafungua alisikia kishindo cha mtu kuanguka chini, alitaka kupiga kelele lakini aliogopa sana zaidi akaamua kufungua mlango ili kuhakikisha usalama wa mama Winny,
“Mamaaaa” Mainda aliongea kwa sauti kubwa baada ya kushuhudia mwili wa muuguzi aliyekua anamuuguza mama Winny ukiwa chini huku utumbo ukiwa nje, kisu kikubwa kiliinuliwa na kumkata mgonja aliyekua kitandani, mgonjwa huyo ambaye Mainda aliamini ni mama Winny hakuwa na nguvu ya kuongea ingawa alionekana kupata maumivu makali,
“Sijatumwa kuja kukuuwa wewe, bado una siku za kuishi lakini ili usinitie matatizoni lazima ukae kimya” yalikua maneno kutoka kwa muuaji huyo kisha Mainda akapigwa ngumi nzito katika paji la uso, ngumi hiyo ilimfanya aanguke chini na kupoteza fahamu, muuaji alikipanguza kisu chake damu kwa kutumia nguo ya Mainda na kutoka.
Martin alipokea taarifa ya kazi kukamilika, hivyo aliamini kazi yake inaendelea kupungua, muuaji alimhakikishia kwa kuchukua mkanda wa moja kwa moja kuwa tayari ameshafanya mauaji ya mtu aliyekua katika chumba maalumu, Martin aliridhika na mkanda huo kumbe ukweli ni kwamba bado mama Winny alikua hai, ingawa alikua katika hali mbaya kiafya,
***
Winny alichomwa sindano za usingizi kila alipozinduka, Martin hakutaka kumuuulia pale hotelin, zaidi alimuweka ndani ya kiroba akiwa hajitambui na kuita vijana wake waliokua wakiishi nchini Zambia ka lengo la kuenda kumtupa porini,
Ndani ya kiroba kuliwekwa bomu lenye madini ya nyuklia, aliamuru Winny akatupwe katika msitu wowote ndani ya masaa 12 ili bomu liweze kulipuka,
“usiku wa leo nataka mkamtupe kwa umakini, naomba mfanye kazi kwa uangalifu mkubwa, huyu ni binti kama akipona anaweza nisababishia mimi matatizo, hivyo naomba muwe makini, mkifika msituni chimbeni shimo kisha mfukieni” Martin alimaliza kisha kuukabidhi mwili wa Winny ndani ya buti la gari aina ya Toyota surf.
Ilikua majira ya saa moja usiku saa za Zambia, vijana watano waliokua wawindaji haramu katika hifadhi ya taifa ya Lusaka, walikua wamejificha juu ya mti ili kusubiri giza liingie vizuri ili shughuli yao ya uwindaji haramu ianze waliendelea kujadili jinsi maisha yanavyoenda, waliongea lugha ya Kinyiha, ilipotimu saa mbili kamili walijipanga kushuka, walibeba silaha zao za jadi kama mishale, manati, na rungu, lakini kabla ya kuteremka, waliona mwanga wa gari, haraka walipanda juu zaidi na kujificha vizuri, hofu iliwaingia wakidhani ni askari wa msituni, kwa macho yao walishuhudia vijana waliwili waliburuza kiroba hadi sehemu moja, kijana mwingine alishika jembe na kuanza kuchimba chini, na baada ya hapo alifukia kiroba hicho chini, bado vijana hao juu ya mti hawakuelewa kitu kilichokua kikiendelea lakini wote waliwaza labda ni kitu kinachofichwa,
“Itakua ni pembe za ndovu au madini” walijisemea kwa lugha ya Kinyiha, baada ya vijana hao kukamilisha zoezi hilo waliwasha gari na kutokomea, wawindaji hao walipohakikisha kuwa gari imeshatokomea nao walishuka mtini kwa lengo la kuenda kufukua kilichofukiwa ardhini, walifukua kwa kutumia viganja walitoka na kiroba kilichokua na uzito kati ya kilo 30-45, haraka walikifungua,
“Binadamu, mbona hawana huruma”, alisema kijana mmoja kwa lugha ya Kinyiha, hawakuona sababu ya kukaa eneo hilo hasa baada ya kukuta bomu ndani ya kiroba hicho hiyo ikimaanisha patalipuka mda wowote, ingawa waliamini mtu huyo ameshakufa,
“Tena msichana mzuri hivi ?” alijisemea kijana mwingine huku wakiendelea kutembea kwa haraka, walimbeba begani kwa kupokezana hadi katika nyumba yao waliyoijenga pembeni kidogo ya msitu.
Uzuri wa Winny, uliwachanganya vijana hao hasa baada ya kufika nae ndani na kummulika vizui ingawa waliamini ameaga dunia lakini walijikuta wakimtamani na kufanya nae mapenzi,
“Cha kufanya hapa ni kumwingilia kimwili hadi asubuhi alafu tumzike huku ndani na sisi tuhame eneo hili” wote walikubaliana na kuanza kazi hiyo mara moja, walimbaka kwa zamu, alipakwa mafuta ya kumlainisha na pamoja na kumuosha kila baada ya mmoja kumbaka, waliamini ni kitu kibaya kufanya mapenzi na maiti lakini hawakuweza kujizuia kwa uzuri wa Winny,
“Alafu atakua amekufa mda sio mrefu maana bado ni wa mto kabisa” walijisemea vijana hao baada ya kuona jinsi joto lilivyotawala mwili wa Winny bila kujua kwamba Winny alikua amechomwa sindano ya usingizi hivyo mwiili wake ulikua na joto kama kawaida. Shimo refu liliendelea kuchimbwa ndani hapo, mmoja akiwa kifuani mwingine alikua ameshika jembe ili waweze kuificha siri hiyo. Hadi kufika saa kumi kamili asubuhi shimo lenye futi zadi ya 15 lilikua likiusubiri mwili wa Winny ambao bado vijana waliendelea kuufaidi.
***
Mainda alizinduka na kuanza kupiga kelele, wauguzi walijazana kumsikilia na ndipo alipoanza kutoa maelezo jinsi muuaji alivyoingia wodini, na jinsi alivyomfuata na kupigwa ngumi ya uso, lakini hali yake ilibadilika na kuwa ya furaha baada ya kuambiwa kuwa mama Winny hajauwawa aliyeuwawa ni mgonjwa mwingine,
“Asante Mungu, lakini kuna kitu kinatesa hii familia maana huyu mtu alikua na lengo la kumuua mama wawatu, na huyu mtu yawezekana ndiye aliuwa wazazi wangu”Mainda aliongea huku akitokwa na machozi, kutoka wakati huo mama Winny alikua chini ya uangalizi mkali tena kisirisiri,Mainda alihangaika sana kutafuta angalau pesa za kundelelea kumtibu ikiwezekana hata mdhamini wa kumpeleka nje ya nchi.
Alijaribu kuongea na viongozi mbalimbali, ili aweze kusaidiwa lakini wengi wao waliishia kumwambia wakutane hotelini, kamwe Mainda alijiheshimu, hakufikiria kamwe kumvulia mwanaume nguo ili aweze kupata msaada wa kitu chochote.
***
Taarifa ya habari ya saa kumi na moja nchini Zambia iliongoza kwa habari juu ya mlipuko mkubwa uliotokea katika hifadhi ya taifa, ulikua mlipuko mkubwa kuliko yote iliyowahi kutokea nchini humo, taarifa hiyo ilimpa sana Martin furaha, aliamini kazi yake imekamilika, kichwani alimuwaza sana Kemmy,
“Sasa acha nikale maisha na rafiki yako” alijisemea Martin kimoyomoyo.
***
Mwendo wa saa kumi na moja asubuhi, wawindaji waliokua wakimbaka Winny, walikua wametosheka, walimuogesha kwa maji ya baridi, kisha wakamfunika kwa shuka jeupe, walitaka kumzika kwa heshima za marehemu,
walimuweka pembeni ya shimo na kuanza kumuombea, kabla ya kumshusha shimoni, wakati wakiendelea na hayo Winny alianza kurudiwa na fahamu zake, kwa mbali alisikia watu wakiongea lugha isiyoeleweka,bado hakuwa na nguvu ya kufumbua macho, hakuwa na uwezo wa kufanya chochote zaidi ya kusikia kwa mballi, alisikia watu hao wakizidi kuongea na hatimaye alihisi akibebwa na kushushwa shimoni, yote hayo alikua akisikia lakini hakuwa na uwezo wa kufanya chochote, alihisi kama anaota alijikuta akitaka kujaribu kusema
“Shindwa kwa jina la yesu” lakini sauti haikutoka kwa kutumia kamba walimzomfiringishia alifikishwa mwisho wa shimo, kisha kufanyikwa maombi mengine kabla ya kufukiwa…

INAENDELEA

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI: SEHEMU YA-13

Shunie hearly kisukari dumejeuri Born2xhine bright platnumz Flozzg

Mainda aliingiwa na wasiwasi na kunyanyuka alipokua ameketi, alitembea kwa kunyata hadi mlangoni, lakini kabla hajafungua alisikia kishindo cha mtu kuanguka chini, alitaka kupiga kelele lakini aliogopa sana zaidi akaamua kufungua mlango ili kuhakikisha usalama wa mama Winny,
“Mamaaaa” Mainda aliongea kwa sauti kubwa baada ya kushuhudia mwili wa muuguzi aliyekua anamuuguza mama Winny ukiwa chini huku utumbo ukiwa nje, kisu kikubwa kiliinuliwa na kumkata mgonja aliyekua kitandani, mgonjwa huyo ambaye Mainda aliamini ni mama Winny hakuwa na nguvu ya kuongea ingawa alionekana kupata maumivu makali,
“Sijatumwa kuja kukuuwa wewe, bado una siku za kuishi lakini ili usinitie matatizoni lazima ukae kimya” yalikua maneno kutoka kwa muuaji huyo kisha Mainda akapigwa ngumi nzito katika paji la uso, ngumi hiyo ilimfanya aanguke chini na kupoteza fahamu, muuaji alikipanguza kisu chake damu kwa kutumia nguo ya Mainda na kutoka.
Martin alipokea taarifa ya kazi kukamilika, hivyo aliamini kazi yake inaendelea kupungua, muuaji alimhakikishia kwa kuchukua mkanda wa moja kwa moja kuwa tayari ameshafanya mauaji ya mtu aliyekua katika chumba maalumu, Martin aliridhika na mkanda huo kumbe ukweli ni kwamba bado mama Winny alikua hai, ingawa alikua katika hali mbaya kiafya,
***
Winny alichomwa sindano za usingizi kila alipozinduka, Martin hakutaka kumuuulia pale hotelin, zaidi alimuweka ndani ya kiroba akiwa hajitambui na kuita vijana wake waliokua wakiishi nchini Zambia ka lengo la kuenda kumtupa porini,
Ndani ya kiroba kuliwekwa bomu lenye madini ya nyuklia, aliamuru Winny akatupwe katika msitu wowote ndani ya masaa 12 ili bomu liweze kulipuka,
“usiku wa leo nataka mkamtupe kwa umakini, naomba mfanye kazi kwa uangalifu mkubwa, huyu ni binti kama akipona anaweza nisababishia mimi matatizo, hivyo naomba muwe makini, mkifika msituni chimbeni shimo kisha mfukieni” Martin alimaliza kisha kuukabidhi mwili wa Winny ndani ya buti la gari aina ya Toyota surf.
Ilikua majira ya saa moja usiku saa za Zambia, vijana watano waliokua wawindaji haramu katika hifadhi ya taifa ya Lusaka, walikua wamejificha juu ya mti ili kusubiri giza liingie vizuri ili shughuli yao ya uwindaji haramu ianze waliendelea kujadili jinsi maisha yanavyoenda, waliongea lugha ya Kinyiha, ilipotimu saa mbili kamili walijipanga kushuka, walibeba silaha zao za jadi kama mishale, manati, na rungu, lakini kabla ya kuteremka, waliona mwanga wa gari, haraka walipanda juu zaidi na kujificha vizuri, hofu iliwaingia wakidhani ni askari wa msituni, kwa macho yao walishuhudia vijana waliwili waliburuza kiroba hadi sehemu moja, kijana mwingine alishika jembe na kuanza kuchimba chini, na baada ya hapo alifukia kiroba hicho chini, bado vijana hao juu ya mti hawakuelewa kitu kilichokua kikiendelea lakini wote waliwaza labda ni kitu kinachofichwa,
“Itakua ni pembe za ndovu au madini” walijisemea kwa lugha ya Kinyiha, baada ya vijana hao kukamilisha zoezi hilo waliwasha gari na kutokomea, wawindaji hao walipohakikisha kuwa gari imeshatokomea nao walishuka mtini kwa lengo la kuenda kufukua kilichofukiwa ardhini, walifukua kwa kutumia viganja walitoka na kiroba kilichokua na uzito kati ya kilo 30-45, haraka walikifungua,
“Binadamu, mbona hawana huruma”, alisema kijana mmoja kwa lugha ya Kinyiha, hawakuona sababu ya kukaa eneo hilo hasa baada ya kukuta bomu ndani ya kiroba hicho hiyo ikimaanisha patalipuka mda wowote, ingawa waliamini mtu huyo ameshakufa,
“Tena msichana mzuri hivi ?” alijisemea kijana mwingine huku wakiendelea kutembea kwa haraka, walimbeba begani kwa kupokezana hadi katika nyumba yao waliyoijenga pembeni kidogo ya msitu.
Uzuri wa Winny, uliwachanganya vijana hao hasa baada ya kufika nae ndani na kummulika vizui ingawa waliamini ameaga dunia lakini walijikuta wakimtamani na kufanya nae mapenzi,
“Cha kufanya hapa ni kumwingilia kimwili hadi asubuhi alafu tumzike huku ndani na sisi tuhame eneo hili” wote walikubaliana na kuanza kazi hiyo mara moja, walimbaka kwa zamu, alipakwa mafuta ya kumlainisha na pamoja na kumuosha kila baada ya mmoja kumbaka, waliamini ni kitu kibaya kufanya mapenzi na maiti lakini hawakuweza kujizuia kwa uzuri wa Winny,
“Alafu atakua amekufa mda sio mrefu maana bado ni wa mto kabisa” walijisemea vijana hao baada ya kuona jinsi joto lilivyotawala mwili wa Winny bila kujua kwamba Winny alikua amechomwa sindano ya usingizi hivyo mwiili wake ulikua na joto kama kawaida. Shimo refu liliendelea kuchimbwa ndani hapo, mmoja akiwa kifuani mwingine alikua ameshika jembe ili waweze kuificha siri hiyo. Hadi kufika saa kumi kamili asubuhi shimo lenye futi zadi ya 15 lilikua likiusubiri mwili wa Winny ambao bado vijana waliendelea kuufaidi.
***
Mainda alizinduka na kuanza kupiga kelele, wauguzi walijazana kumsikilia na ndipo alipoanza kutoa maelezo jinsi muuaji alivyoingia wodini, na jinsi alivyomfuata na kupigwa ngumi ya uso, lakini hali yake ilibadilika na kuwa ya furaha baada ya kuambiwa kuwa mama Winny hajauwawa aliyeuwawa ni mgonjwa mwingine,
“Asante Mungu, lakini kuna kitu kinatesa hii familia maana huyu mtu alikua na lengo la kumuua mama wawatu, na huyu mtu yawezekana ndiye aliuwa wazazi wangu”Mainda aliongea huku akitokwa na machozi, kutoka wakati huo mama Winny alikua chini ya uangalizi mkali tena kisirisiri,Mainda alihangaika sana kutafuta angalau pesa za kundelelea kumtibu ikiwezekana hata mdhamini wa kumpeleka nje ya nchi.
Alijaribu kuongea na viongozi mbalimbali, ili aweze kusaidiwa lakini wengi wao waliishia kumwambia wakutane hotelini, kamwe Mainda alijiheshimu, hakufikiria kamwe kumvulia mwanaume nguo ili aweze kupata msaada wa kitu chochote.
***
Taarifa ya habari ya saa kumi na moja nchini Zambia iliongoza kwa habari juu ya mlipuko mkubwa uliotokea katika hifadhi ya taifa, ulikua mlipuko mkubwa kuliko yote iliyowahi kutokea nchini humo, taarifa hiyo ilimpa sana Martin furaha, aliamini kazi yake imekamilika, kichwani alimuwaza sana Kemmy,
“Sasa acha nikale maisha na rafiki yako” alijisemea Martin kimoyomoyo.
***
Mwendo wa saa kumi na moja asubuhi, wawindaji waliokua wakimbaka Winny, walikua wametosheka, walimuogesha kwa maji ya baridi, kisha wakamfunika kwa shuka jeupe, walitaka kumzika kwa heshima za marehemu,
walimuweka pembeni ya shimo na kuanza kumuombea, kabla ya kumshusha shimoni, wakati wakiendelea na hayo Winny alianza kurudiwa na fahamu zake, kwa mbali alisikia watu wakiongea lugha isiyoeleweka,bado hakuwa na nguvu ya kufumbua macho, hakuwa na uwezo wa kufanya chochote zaidi ya kusikia kwa mballi, alisikia watu hao wakizidi kuongea na hatimaye alihisi akibebwa na kushushwa shimoni, yote hayo alikua akisikia lakini hakuwa na uwezo wa kufanya chochote, alihisi kama anaota alijikuta akitaka kujaribu kusema
“Shindwa kwa jina la yesu” lakini sauti haikutoka kwa kutumia kamba walimzomfiringishia alifikishwa mwisho wa shimo, kisha kufanyikwa maombi mengine kabla ya kufukiwa…

INAENDELEA

the Legend☆
Muendelezo vipi leo
 
BASI LA SHETANI: SEHEMU YA-14

Winny alirejewa na fahamu zake zote ingawa hakuwa na nguvu kutokana na njaa aliyokua nayo, alijaribu kuongea lakini mdomo wake ulizibwa na udongo uliokua unamshukia ndani ya shimo hakujua nini kinachoendelea kwa mda huo,
“Mungu mimi ni mwenye dhambi lakini naomba nisaidie, niepushe na kifo hiki” Winny alijisemea moyoni huku akijaribu kwa nguvu zote kuinua mikono juu,
“Washa taa tuone kama udongo umemfukia vizuri” alisema kijana mmoja kwa lugha ya Kinyiha na bila kupoteza mda walimmulika Winny, hawakuamini macho yao baada ya kuona mkono wa Winny ukiwa umenyooshwa juu kama ishara ya kuomba msaada, walitupa majembe pembeni na kukimbilia porini kwa hofu kubwa, walimini mwanamke huyo atakua ni jini,
“ Haiwezekani mtu tangu jana hajaongea halafu leo anaongea, ni mzimu wa mtu aliyekufa” waliendelea kujisemea huku wakiendelea kukimbia.
Winny alijitahidi kusimama, na baada ya muda aliweza kusimama alijiegesha pembeni ya shimo hakujua amefikaje ndani yashimo hilo na hakujua sababu ya yeye kufika pale, huku akiwa anaendelea kujaribu kutoka shimoni alikumbuka jinsi baba yake alivyosukumwa shimoni,
“Baba kweli, uliuwawa kifo cha kikatili na ninajua dhahiri huna hatia yoyote? Kwanini hata wasiniuwe mimi baba akabaki? Winny alilia moyoni huku machozi yakitiririkia mdomoni, hakujali asili ya chumvi iliyopo katika machozi, aliyalamba bila kujali, yote hiyo kupunguza kiu na njaa iliyokua inamuandama.
Hakujua ni kwa jinsi gani ambayo angeweza kufanikiwa kutoka sehemu ile, alijuta sana kumjua Martin, aliamini mipango yote imesababishwa na Martin,
“Martin popote ulipo Mungu akulaani, wewe ndio chanzo cha kuharibika kwa maisha yangu” alijisema Winny baada ya kukata tama kabisa ya kutoka shimoni hapo, aliketi chini na kusali sala za mwisho hasa baada ya kuona giza likiingia bila ya mtu yoyote kufika katika nyumba ile, alijua ni dhahiri kama asingepata chochote cha kuliwa basi lazima angekufa kwa njaa,
“Mungu wewe wajua sababu ya nini niyapitie haya, naamini bado una kitu cha kunifunza katika haya maisha,naomba kama unaweza niepushe na kikombe hiki lakini si kwa mapenzi yangu ila ni kwa mapenzi yako” baada ya kusema maneno hayo Winny alianguka chini, na kutulia akisubiri miujiza itokee aweze kushiba.
***
Baada ya Martin kuamini kwamba ameiteketeza familia ya Mazengo alipanda ndege ya shirika la Ethiopia hadi jijini Nairobi Kenya, alipanga kukaa hapo siku tano, kabla ya kurejea nchini Tanzania kwa ajili ya kuendelea na shughuli zake, utajiri wake ulimuwezesha kuzunguka majiji hata zaidi ya kumi na tano pasipo kuyumba kifedha,
Kemmy, alipokea tiketi ya ndege ambayo ilimtaka asafiri hadi nchini Kenya ili aweze kuenda kukaa na Martin kwa mda wa siku tano, ilikua furaha zaidi kwa Kemmy, alizidi kujiona mwanamke wa kipekee duniani, aliona ameshayapatia maisha kwa kupata kila kitu anachotaka na kwa mda anaotaka, hakuamini kama angeweza kufika mahali ashinde njaa kama alivyokua anaskia baadhi ya watu wakilalamika maisha magumu mtaani.
Daraja la kati katika ndege ya Air Tanzania Company Limited, ATCL (Shirika la ndege la Tanzania) lilipakia abiria ishirini huku Kemmy akiwa mmojawapo, ilikua safari ya moja kwa moja kutoka uwanja wa Mwalimu nyerere hadi uwanja wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi,ambapo alisubiriwa na gari ambayo ingempeleka moja kwa moja hadi mtaa wa Muindi Mbingu, sehemu iliyopo hotel ya Big Knife, Martin alikua amekodi chumba kwa ajili ya kujinafasi kwa siku tano. Kemmy alitamani sana kufika jijini Nairobi.
***
Baada ya Mazengo kuchunguzwa na wachina waliokua wanachimba madini na kugundulika kuwa amezingiziwa kesi, wote walimuonea huruma, alikua akipewa sehemu ya kuandika kwa Kiswahili kisha maneno hayo yalihamishwa sehemu maalumu kwa ajili ya kutafsiriwa, wote walimuonea huruma kwa jinsi aliyostahili kufa kifo kibaya, japo aliomba iwe siri ili asigundulike kuwa yupo hai. Kiongozi wa vijana hao alirejea kutoka nchini India alikopelekea madini kwa ajili ya kuyauza, alifanikiwa kupata fedha nyingi sana, alihakikisha vijana wote wanapata kiasi kikubwa cha fedha, huku Mazengo akipewa nusu nzima ya kaisi cha pesa kwani ndiye alikua chanzo cha kupatikana kwa madini hayo kirahisi,
“Hapa nilipo sioni thamani ya pesa yoyote mtakayonipa, hapa nahitaji tu mnilinde ili nisiuwawe, mkinipa hii pesa na kurudi Tanzania basi lazima nitauwawa na nitaacha hizi pesa, naombeni ulinzi kwa namna yoyote, mke wangu sijui alipo pamoja na mtoto wangu sijui alipo, cha kwanza naomba watafutwe waletwe karibu na mimi ili niweze kufurahi pamoja na wao” yalikua maandishi Mazengo aliyoandika, maandishi hayo yaliwapa wakati mgumu wachina hao kuwa ni kwa jinsi gani wangemlinda kwa siku zote, lakini mchina mmoja alitoa wazo la Mazengo kupelekwa kwa mwalimu hodari wa kufunza ngumi,mateke,kungfuu,judo,karate,taekwondo , mieleka,dragon stail,snake stail,sarakasi,power kick,monkey stail wazo kutoka kwa kijana huyo liliafikiwa na wachina wote kwani waliamini baada ya mazengo kufundishwa vyote hivyo basi angeweza kujilinda mwenyewe na ingekua vigumu kwa mtu yoyote kumuua, hivyo moja kwa moja alitafutwa mwalimu mwenye uwezo mkubwa wa kutoa elimu hiyo na alipatikana mwalimu mmoja kwa jina la Vajiralong kutoka nchini Thailand, Vajiralong aliishi ndani ya maji katika ziwa la Phayao, huko huko Thailand. Mazengo hakuamini kama ataweza mazoezi ambayo angeenda kufanya lakini ili kujilinda maisha yake aliamini lazima apambane kusudi Mungu amsaidie baada ya hapo aliomba wachunguzi watumwe nchini Tanzania ili kumchunguza mkewe na mtoto wake ikiwezekana wasafirishwe hadi nchini Thailand kwa ajili ya kupewa mafunzo.
Haraka kikosi cha uchunguzi cha kimataifa FBI (Federal Bureau of Infestigation) kilichoaminika kufanya uchunguzi kwa weledi kilipokea kazi ya kumfuata mke wa Mazengo pamoja na mtoto wake aitwaye Winny, Mazengo aliwapa taafira zote na wote wakaahidi kuifanya kazi hiyo kwa siri kubwa.
“Taarifa za kwanza za uchunguzi zitakuja baada ya wiki moja, hivyo uwe tayari kuzipokea” lilikua jibu kutoka kwa FBI na mara moja wakaanza safari ya kulekeea Tanzania huku Mazengo akisafirishwa hadi nchini Thailand kuanza mazoezi makali.
***
Nchini Zambia hali ya hewa ilibadilika ghafla, manyunyu yalianza kunyesha, Winny alikua akihema kwa kasi ya ajabu, giza lilitawala kila kona, aliamini siku yake ya kufa imefika mara baada ya mvua iliyoandamana na ngurumo za radi, bila kutarajia alishtuka kuona maji yanaanza kupenya ndani na haraka kuanza kupenya ndani ya shimo, sauti ya vyura ilitawala pande zote, alijibanza pembeni huku hofu ikizidi kumtawala,
“Mungu kwa nini unaruhusu nife maji, eh Mungu kifo cha maji ni kibaya niokoe” Winny alijisemea lakini hali haikubadilika kwani wakati huo maji yalikua yamemfikia kifuani, kila alipojaribu kujikoa alishindwa lakini chanzo cha kushindwa huko kikiwa ni njaa,
“Hivi hapa njaa ndio inanifanya nife na sio maji kwa nini nisinywe haya maji pamoja na kula hawa vyura nikapata nguvu?” Winny alijiuliza sawali hilo na bila kupoteza mda alikinga maji kwa kutumia viganja na kuyanywa, alikamata chura,
“Kuja na hapa pumbavu” alitamka kwa hasira huku akitafuna miguu ya chura aliyekua ndani ya shimo hilo, hakujali kelele za chura huyo zaidi aliukata mdomo mwake kwa na kuutafuna pamoja na mifupa yote, hakuona kinyaa kutafuna utumbo wa chura lakini kikubwa kilikua kujiokoa maisha yake, katika hali ya kushangaza alijikuta akipata nguvu za kujitoa ndani ya shimo licha ya utelezi alifanikiwa kufika juu, alipata furaha ya ajabu hasa baada ya kuona mvua ikipungua, hakutembea kwenda sehemu yoyote kutokana na giza, alikaa mahali na kutulia, jina Martin halikutoka kichwani mwake,alishindwa kumuelewa nia yake hasa.
***
Wapelelezi kutoka FBI waliingia nchini Tanzania na kuanza upelelezi wao mara moja, na tayari ndani ya wiki moja walipata taarifa za mwanzo kuwa mke wa Mazengo na mtoto wake walishaaga dunia,kilichokua kikifuata ni kujua wamekufaje na baada ya hapo maiti zao ziko wapi, hivyo uchunguzi wa kwanza ulitumwa nchini Thailand,
Mazengo aliangus kilio cha machungu, alipatwa na hasira za ajabu,
“No, no,no”(hapana ,hapana hapana) wataona cha moto” alijisemea Mazengo huku akiendelea na mazoezi yake, walimpa msisitizo wa kuhakikisha maiti zinapatikana na kama maiti hazitapatikana basi itakau hawajafa,Mazengo alifarijika na taarifa ya kusikia maiti zitapatikana, hapo aliongeza hasira ya kufanya mazoezi kwa hasira zaidi ya mara kumi ya alivyoenda, mwalimu wa Mazengo Vajiralong alimfundisha Mazengo namna ya kuishi kwenye maji hata kwa miezi sita bila kumeza hata tone la maji, pia alimfundisha kujigandisha ili asiweze kuumwa wala kuhisi njaa, mazoezi yote yalikua ni ndani ya maji..

Je nini kitatokea ?!

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI: SEHEMU YA-15

Licha ya mvua kuendelea kunyesha Winny alikua akitokwa na jasho kutokana na mbu waliomfanya ajipige pige mara kwa mara kuwafukuza, kwa kupitia upenyo nyumba hiyo alifanikiwa kuona wanyama wakali pale radi ilipomulika, alitetemeka kwa hofu hasa pale aliposikia mingurumo ya simba na chui.
Alimuomba Mungu aweze kumsaidia pakuche salama ili aweze kutafuta msaada wa kutoka mahali pale,
“Kwanza huku ni wapi?” ni swali Winny alilojiuliza bila kupata jibu, hakujua kama bado yupo Zambia au yupo wapi, ingawa alijua dhahiri hayupo Tanzania kutokana na lugha aliyosikia vijana wale wakiongea wakati akifukiwa shimoni.
***
Pamoja na kufundishwa kupigana pia Mazengo alifundishwa kumsoma mtu saikolojia , alifundishwa kusoma hisia za mtu, umri wa miaka arobaini haukumfanya mwalimu wake Vajiralong kushindwa kumpasua msamba, japo ilikua shida kwa Mazengo lakini kutokana na hasira ya kupewa taarifa ya mkewe kuuwawa ilimfanya ajitoe ufahamu na kuapa kujifunza kwa bidii ili siku moja aweze kulipa kisasi kwa wauwaji wote.
***
Baada ya Winny kuvumilia usiku mrefu aliweza kuona jua likichomoza kwa mbali, kichwani mwake hakuwaza kitu zaidi ya kutoka mahali pale, hakujua angeelekea wapi kwani alishaamini Martin sio mtu mzuri kwake,
“Kama Martin ndiye ametuma watu waje kunizika nikiwa mzima basi ana nia ya kuniuwa” alijisema Winny huku akijifunga shuka lililokua ndani hapo, alitoka na kusimama nje, hakujua njia ilipo, hakujua aelekee wapi ,
“Ngoja nichukue kisu hapa ndani”, alijisemea Winny na kurudi ndani, alichukua kisu kilichokua ndani hapo na kutoka nacho kama silaha, baada ya kuwaza kwa dakika tatu aliamua kuelekea upande wa kulia ambao aliamini ndio upande wa kuume tena wenye nguvu,alitembea kwenye tope, lililomsababishia kuanguka mara kwa mara, hakujua kama yupo eneo la hifadhi ya taifa, na katika upande wa kulia aliokua akielekea ulikua ndio upande wa kuingiza zaidi ndani ya hifadhi.
“Mungu nisaidie” alijisemea Winny baada ya kuona gari aina ya Land Rover, ambazo mara nyingi zilitumiwa na walinzi wa hifadhi za wanyama, gari hilo iliendeshwa taratibu kutokana na hali ya hewa, walikua ni askari wa msitu waliokua wakifanaya doria katika msitu huo, Winny akajiwa na wazo la kulala chini, hapo alipolala alikipachika chini kisu alichokua ameshikilia, alizidi kuingiwa na hofu hasa baada ya kuona gari ikielekea mahali alipolala,
“Najifanya nimekufa” alijisemea Winny moyoni baada ya kuona askari mmoja akishuka garini na kumsogelea, alimpekua Winny kwa haraka na kumuita mwenzake aliyekua ndani ya gari, walizungumza kingereza wakijiuliza kuhusu mwanamke huyo,
Winny hakuzungumza chochote, zaidi alizidi kujibana pumzi yake, walimgeuza geuza pale chini, hadi shuka alilokua amejifunika nalo likamtoka mwilini,
“Maaskari wote walipagawa baada ya kuona mwili wa Winny, hakika wote walijikuta wakimeza mate, askari mmoja alijikuta akipenyeza kidole cha kati ndani ya uke wa Winny, huku akisema ,
“Ooooh yeaaaaahs” Winny alijitahidi kuvumilia, alijiua ni dhahiri kuwa kuna uwezekano wa kubakwa,katika yale mazingira, baaada ya dakika tano, walichukua shuka lake na kumfunika, hapo bila askari hao kuona alikichomoa kile kisu ardhini na kukishikilia kwapani, alijikuta akiomba Mungu asishikwe vibaya kusudi kisimchome. Baada ya hapo alibebwa na kutupwa ndani ya gari, kisha gari kuanza safari.
Maamuzi ya kumbeba na kuondoka naye yalikua ni kumpeleka mochwari, kwani askari hao waliona kama ameshakufa napengine waliamini amekufa kwa maji usiku wa kuamkia siku hiyo.
Winny alipoachwa mwenyewe nyuma ya gari aliendelea kupumua kama kawaida, kila alipowaza kuruka alijikuta akitamani kuruka pale atakapoona amefika sehemu zenye watu wengi ili aweze kupata msaada wa kufika nchini Tanzania kumkwepa Martin ambaye aliamini kama atamuona ataweza kumuuwa.
***
Mainda akiwa na mama Winny walihifadhiwa katika chumba cha siri nyumbani kwa mchungaji mmoja, jijini Dar es salam, alifanyiwa matibabu kwa siri hasa baada ya kutokea vifo vya mara kwa mara, Mainda alikua akiomba Mungu usiku na mchana, kusudi mama Winny aweze kuwa mzima wa afya kwani kitendo cha kumshuhudia mumewe akiuwawa kilizidi kumtia machungu, Mainda alifanya kazi ya ziada kumbembeleza na kuzidi kumpa matumaini kwamba siku moja wangekutana mbinguni.
***
Baada ya dakika arobaini na tano gari iliyombeba Winny ilifunga breki nje ya geti la Lusaka Trust Hospital (LTH) ,Winny aliona huo ndio wakati muafaka wa kutoka ndani ya gari, alichungulia pande zote na hapo aliona gari la takataka likipakia taka eneo hilo, bila kupoteza mda alipoona askari wameshuka na kuingia katika mapokezi ya hospital hiyo naye alitoka na kukikamata kichochoro cha kulekea barabara kuu ya Independence Ave, alipiga kama hatua mia mbili ndipo alipoweza kukutana na barabara kubwa iliyo katikati ya mji, kila mtu alikuwa akihangaika na shughuli zake, hali ya hewa ya manyunyu ilimfanya kila mtu awe busy na kazi yake,
“Nitaanzia wapi Mungu wangu” alijisemea maneno hayo baada ya kubanwa na mkojo hakuwa na lakufanya zaidi ya kuachilia kidogo kidogo, kila alipofika mahali palipotwama maji basi aliachilia kidogo kwani alimini hakuna atakayemgundua.
Madaktari wakiwa na machela walifika ilikoegeshwa Land Rover ya askari, walishangaa sana baada ya kutoona mwili uliotakiwa kwenda kufanyiwa uchunguzi,wote walishangaa hasa baada ya watu waliokuja karibu kusema wameona msichana akishuka garini, waliona kama maaajabu, huku wakihisi wamebeba mzimu.
***
“Winny alitembea kama kilomita tatu, ndipo alikutana na wanafunzi wa chuo cha David Kaunda Technical , walikua wamevaa sare nzuri, Winny alijaribu kuwasalimi kwa kingereza cha kuungaunga, moja kwa moja wakajua ni mtu anayehitaji msaada, walimwamuru kuongozana nao hadi walipokua wakiishi.
“Kweli hawa wanafunzi wa Zambia ni waelewa na wenye upendo wa dhati, ingekua ni wa pale chuo cha IFM ningeshakula misonyo ya maana” alijisemea Winny wakiendelea kupiga hatua za haraka haraka, alimshukuru Mungu kwani aliamini kuwa atakua salama na ataweza kufika Tanzania bila matatizo yoyote.
Wanafunzi hao waliokubali kumsaidia Winny walikua wakimwangalia Winny kutoka juu hadi chini kila mmoja alipendezwa naye, kila mmoja aliamini Winny atafaa sana katika kazi yao ambayo waliifanya kwa siri.
***
Edson alianza kwa kujaribu kuuza madawa ya kulevya katika mitaa ya magomeni, Mwananyamala na Kinondoni, yote hayo ili kujifunza biashara hiyo kabla ya kuwekeza mtaji mkubwa, alitamani sana kukutana na msambazaji mkubwa wa madawa hayo ili aweze kuzungumza naye na kumpa mfululizo mzima wa namna ya kusafiri na namna ya kujua madawa yenye ubora na madawa bandia.
“Kuna mtu anaitwa Martin, ukiweza kumpata huyo ndio atakupa utaratibu mzima” maneno hayo kutoka kwa muuzaji mdogo yalimfanya Edson kumtafuta huyo Martin usiku na mchana,
“Sio rahisi kukutana na Martin ovyo ovyo, na ukae makini maana akijua unamfuatilia unauwawa mara moja” yalikua maneno yaliyozidi kumkatisha Edson tamaa ya kukutana na Martin,
“Kama kweli unataka mfanye biashara basi namba zake hizo mpigie simu” kijana aitwaye Shedrack alimkabidhi Edson namba za Martin na ilikua baada ya Martin kupokea ujumbe wa kazi , Edson alitoa simu yake ya mkononi na kuipiga namba ya Martin.,

INAENDELEA

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI: SEHEMU YA-16

Wanafunzi waliompa Winny msaada wa malazi, walikua wakiusubiri usiku wa siku hiyo kwa hamu, lengo lao likiwa kumnadi Winny kwa wanaume, Winny hakujua kitu kilichokua kichwani kwa wale wasichana zaidi alizidi kumshukuru Mungu kwa kumpa msaada huo, saa zilienda taratibu, alijilaza ndani cha chumba kidogo kilichoonekana kutumiwa na wanafunzi wale wote,
“Hata hawajisomei mchana wanalala tu” Winny alijisemea moyoni kwani aliamini wanafunzi wa chuoi huwa na tabia ya kujisomea lakini kwa hao hali ilikua tofauti, walipofika chumbani kwao wote walilala hali hiyo ilimfanya na Winny aweze kulala baada ya kupewa chakula.
Usiku wa saa mbili kamili kwa masaa ya Zambia timu ya wanawake hao iliamka kitandani, waliingia bafuni na kuoga, kisha kujiremba ipasavyo, Winny alianza kuhisi kitu ambacho kilikua kinaenda kutokea, wasichana hao walivaa nusu uchi, kila aliyewaona hakuweza kuamini kama walikua ni wanafunzi, Winny hakutaka kuachwa mahali hapo, zaidi aliomba kwa kutumua kingereza cha kuunga unga, alikubali kuwapa kampani lakini alidai hana nguo za kuvaa, na mara moja alitafutiwa nguo inayomwenea, wote walipendeza sana, Winny alirembwa vilivyo, kigauni kifupi cha rangi nyekundu kiliendana na rangi yake nyeupe pamoja na rangi nyekundu ya mdomoni pamoja na miwani nyeusi ilizidi kumfanya avutie zaidi.
Baada ya dakika tano Uber iliegesha nje ya chumba chao, wote walitoka na kuingia ndani ya gari, na safari ikaanza, ilikua kawaida ya dereva huyo kuwachukua kila siku hadi Monte Carlo Casino hapo palikua ni sehemu maarufu jijini Lusaka palipofanyika starehe zote, kuanzia ukahaba, kamari, uuzaji wa madawa ya kulevya, na mauaji ya kulipizana visasi, kilichoipa jina zaidi sehemu hiyo ni sababu ya kuwa karibu na majengo ya Bunge la Zambia.
“WELL COME MONTE CARLO CASINO” yalikua maandishi makubwa yaliyowakawaka angani, nje jumba hilo lililokua limejengwa chini ya ardhi, kila aliyeingia ndani ya jumba hilo lazima angejikuta akifanya uhuni kwani kinadada walikua nusu uchi na sigara mdomoni, walicheza mziki huku wengine wakinyonyana ndimi, waliozidiwa walijikuta wakifanya mapenzi bila aibu, waliokua wakivuta shisha na bangi walirukwa na akili, kwa ujumla ilikua ni sehemu isiyo salama kwa binadamu anayetarajia kuuona ufalme wa mbinguni.
Winny alishangazwa na mazingira yale, hakuwahi kuyaona mambo kama hayo kabla, alijikuta akiogopa,
“Don’t wory Winny, you are in safe place (ondoa wasiwasi Winny uko sehemu salama)” yalikua maneno ya mmoja wa wasichana walioingia na Winny sehemu ile, Winny alielewa maneno hayo na kujitoa ufahamu na kuanza kucheza, moja kwa moja aliona wenzake wakifanya mapenzi ukutani na kupokea pesa, naye hakutaka kuzubaa, alinyanyuka taratibu na glass yake iliyojaa Wyne aina ya Saint Anna, alicheza taratibu huku akizungusha kiuno chake kwa maringo, taa za kuwaka waka za kila aina ya rangi zilikua zikipamba ukumbi huo pamoja na kuficha maovu yaliyokua yakifanywa hadharani, kwa ukaribu Winny alimuona mmoja wa marafiki zake waliokuja nae pale, alimkonyeza kwa jicho la kulia huku akimpungia mkono, Winny alijibu kwa kupunga mkono kwa mbali, huku Winny akizidi kucheza taratibu hasa pombe ilipoanza kumkolea alibadili aina ya kucheza na kuanza kuinama inama ovyo, wanaume waliokua wakisoma mchezo na ambao walikua wahudhuriaji wa pale walijua moja kwa moja Winny ni mgeni wa pale, hivyo kila mmoja alikua macho kusubiri alewe ili ampate kirahisi.
***
Edson alipiga namba za simu alizopewa,
“Halo mkuu, mimi naitwa Edson natumai naongea na bwana mkubwa Martin” Edson alijitambulisha kwa furaha,
“Wewe nani sijakusikia” ilikua sauti nzito iliyomwogopesha Edson,
“Mimi naitwa Edson, nakupigia simu kutoka Dar es salam, hizi namba nimepewa na bwana mmoja akaniambia wewe ndiye Martin” Edson alijaribu kumwelewesha zaidi lakini katu Martin hakuwa mtu wa kukubali mara moja juu ya mtu anayemtafuta, alijitahidi kufanya uchunguzi kabla ya kufanya mazungumzo na mtu kusudi kujilinda na kuwa salama.
Baada ya hapo alifanya mawasiliano na vijana wake, aliwapa kazi ya kumchunguza Edson, ili ahakikishe sio mtu mbaya aweze kufanya naye biashara,
“Hakikisheni hana tatizo na pia usikute ni mpelelezi kwa namna yoyote, nataka nikitoka Nairobi, nifanye nae kazi hela nilizotumia kuteketeza hii familia zirudi”, alijisemea Martin kwa hasira huku bado akiamini kwa asilimia zote kuwa Mazengo, mkewe na Winny ni marehemu. Vijana wake walimhakikishia usalama wa Edson baada ya kuchunguza namba zake za simu kwa kutumia mitambo ya tarakilishi (computer) , simu za Edson hazikuonekana kuwa za kipelelezi, alionekana ni mfanyabiashara mdogo wa madawa ya kulevya,
“Wiki ijayo nakuja, naomba tukutane Serena Hotel tuweze kuongea” sauti nzito ilipenya masikioni mwa Edson, alipata furaha ya ajabu, alizidi kuamini kuwa ndoto yake ya kuwa tajiri mkubwa itatimia, hasa baada ya kukutana na Martin.
Martin hakuwa mtu wa kukurupuka bado, licha ya kupewa uhakika kutoka kwa vijana wake bado alipata wasiwasi hivyo ilipofika siku ya jumamosi siku ambayo alipanga kukutana na Martin, aliagizwa mtu mwingine Hotel ya Serena ,yote hayo ilikua kuhakikisha usalama wa Martin.
Edson alieleza shida yake, alieleza kiasi cha pesa alichokua nacho, waliongea mengi lakini hakujua kama aliyekua anaongea naye sio Martin, bali alikua ni mtu aliyekua amevaa kofia kubwa iliyomfunika machoni, alikua na kifaa maalumu cha kurekodi ili aweze kumsikilizisha Martin,
“Tutafanya kazi lakini kabla yua kuanza, lazima utembelee masoko, hivyo itakupasa usafiri katika majiji makubwa ya afrika, ili uweze kupata masoko makubwa, cha kufanya anzia Zambia na hakikisha unaitembelea Casino moja inayoitwa MONTE CARLO, hapo nenda onana na meneja wa casino hiyo jitambulishe na umwambie umeagizwa na Martin Tanzania, atakuelewa na ili uweze kujificha ukiwa pale unaweza ukatafuta msichana wa kukaa nae, ili uweze kumtumia kupata wateja wa kike, na ili aweze kukusambazia ndani ya casino hiyo, siuanajua tena bhana biashara ikifanywa na mdada mambo huwa mazuri kidogo ?” ulikua mfululizo wa maneno kutoka kwa Martin bandia, maneno hayo yalimfanya Edson azidi kufarijika,
“Ehe nikishatoka Zambia nitatembelea wapi?” Edson alimuuliza Martin bandia ambaye hakutaka kuangalia mtu machoni, alitazama pembeni huku akivuta sigara aina ya Malboro,
“Anzia hapo alafu utapata maelekezo zaidi huko huko” alijibiwa na maongezi yakaishia hapo, kila mmoja akatawanyika,Edson alikamata mtaa wa Ohio, huku Martin bandia akipenya na Matkaba Stret huko huko Upanga..
***
Baada ya wiki moja Winny alikua ameshazoea biashara ya kujiuza huko Zambia, kila siku alihudhuria katika Casino ya Monte Carlo, Siku moja akiwa anaendelea kucheza huku akirembulia wanaume alimsikia mwananume mmoja akiongea na simu kwa kutumia lugha ya Kiswahili, alishtuka sana kwani ilikua mara ya kwanza kuskia lugha hiyo ndani ya casino hiyo, alipenya katikati ya watu hadi kumfikia, alikaa karibu yake, macho yao yakagongana na kujikuta anamsogelea kijana huyo, alikua kijana mdogo lakini alivaa vito vya thamani, kabla ya kusemeshana walijikuta wameduwaa, kila mmoja akisubiri kumsemesha mwenzake.

INAENDELEA

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI: Sehemu ya-17

Winny aliinamisha kichwa chini na kuendelea kucheza taratibu, wimbo wa msanii Akon kutoka Senegal unaojulikana kama Be with you ulikua ukipamba ukumbi wa Monte Carlo, watu waliokua wamelewa walikua wakifanya dhambi za hadharani huku Winny akiendelea kumsogelea mwanaume aliyekua mbele yake,
“Let’s dance together (Tucheze pamoja)” Winny aliongea kwa sauti ya chini huku akiiunua mkono wake wa kushoto na kuupandisha mabegani kwa mwanaume huyo. Bila kuchelewa mwanaume huyo nae alijibu mashambulizi kwa kushusha mkono wake wa kulia kiunoni kwa Winny, kilikua kiuno chembamba kilichopambwa kwa shanga laini,
“Please may ask you a question ?(samahani naweza kukuuliza swali ?”) Mwanaume huyo alianzisha maongezi
“Worry out, you can do it (ondoa shaka waweza fanya hivyo)” Winny alijibu huku mziki ukiwa umekolea,
“What’s your name, and where you come from,”(unaitwa nani na unatokea wapi)”swali hilo kutoka kwa mwanaume lilimshtua Winny, hakutaka kujulikana kirahisi kabla ya kujua nia ya mwanaume huyo
“Let me ask first, who a you? (acha mimi nainze kukuuliza wewe ni nani)? Winny alibadilika na kutaka kumjua mwanaume huyo kwanza,
“Edson, from Tanzania, ( Edson natokea Tanzania)” alijibu mwanaume huyo huku bado wakiendelea kucheza pamoja,
“Realy, from Tanzania ?me to am from Tanzania, I called Winny,( kweli, kutoka Tanzania? Mimi pia natokea Tanzania naitwa Winny,)”.
Baada ya kufahamiana walibadilisha lugha na kuanza kuongea Kiswahili, huku wakiendelea kupata pombe. Ilikua vigumu kwa mwanaume yeyote kucheza mziki na Winny kisha amuache bila kulala nae, kwa jinsi Winny alivyojua kumteka mwanaume kwa mwili wake mzuri, huku wakiendelea kucheza Winny alikua akinywa mafundo kadhaa ya pombe na kunza kumnywesha Edson kwa mdomo, mikono yao ilikua ikichezeana sehemu za siri bila aibu, msisimko mwa hali ya juu uliwatawala.
“Huyu huyu atanifaa kwa kuzunguka naye kama Martin alivyoniagiza” Edson aliwaza kichwani mwake, alifurahi kukutana na msichana wa kitanzania ambvaye aliamini atamsaidia kazi zake kwa urahisi, hapo moja kwa moja alimuomba msichana huyo wachukue chumba kwa ajili ya kupumzika pamoja hadi siku ambayo ingefuata ili waweze kupanga mipango yote kwa utaratibu,
“Usijali Winny, nitakurudisha kwenu Tanzania na kama ulivyosema kuwa baba yako aliaga dunia basi nitakujengea nyumba na mama yako nitahakikisha mnaishi maisha mazuri lakini kuna kazi moja nitataka tushirikiane kuifanya”
“Kazi gani hiyo, nitakua tayari”,
“Kazi rahisi tu ambayo inahitaji umakini na siri ya hali ya juu”
“Viungo vya binadamu ama nini”
“No, Winny sio viungo vya binaamu bali ni madawa ya kulevywa, mimi nitakuelekeza kila kitu namna ambavyo tutafanya tuweze kupata pesa nyingi kwa mda mfupi”
“Sawa tutakua pamoja, mradi pesa ipatikane”.
Yalikua maongezi kati ya Edson na Winny, maongezi hgayo yalifanyika katika chumba cha wageni baada ya kucheza mziki na kufurahia mapenzi usiku kucha, kuanzia asubuhi hiyo hadi jioni walikua chumbani wakipanga namna ya kutafuta wateja, meneja wa Monte Carlo alimpa Edson bahasha yenye mija sita ya kutembelea kutafuta masoko, hapo Zambia alikaa kwa siku tatu kisha aliweza kusafiri na Winny hadi katika jiji la Maputo nchini Msumbiji (Mozambique) kisha walipita katika nchi zote za kusini mwa jangwa la sahara .
***
Mazengo aliendelea kupata mafunzo, huku mwili wake ukizidi kuwa na nguvu kupita kiasi, aliweza kubeba mizigo mizito kadri siku zilivyozidi kusonga. Baada ya miezi mitatu alitoka ndani ya maji na kuingia nchi kavu kwa ajili ya mazoezi ya kuimarisha mifupa ya mikono, mchanga wenye moto mkali uliwekwa ndani ya ndoo kisha kazi yake ilikua kuchomeka mkono ndani hadi mchanga upoe, mwanzo alikua akipata shida lakini kila alipokumbuka machungu ya kuambiwa mkewe ameaga dunia alipatwa na hasira na kujikuta anafanya mazoezi makali kumzidi kitu kilichomshangaza hadi mwalimu wake,
“Aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa,” aliitoa sauti hiyo pale alipokua akimwagiwa maji ya moto mgongoni, yote hayo ilikua kufundishwa namna ya kupenya katikati ya moto bila kuungua, kila siku machungu yaliongezeka kutokana na wana FBI kutofanikiwa kuleta mifupa ya wanafamilia wake.
***
Kiongozi wa wachina waliokua wakichimba madini alifungua account na kuijaza kiasi kikubwa cha fedha, fedha hizo zilikua kwa ajili ya kumpa Mazengo siku ya kuagana pale atakapomaliza mafunzo, walipanga kumpa kiasi hicho cha pesa kwa kumshtukiza, ili waweze kukumbukana.
***
Siku moja ya jumapili, ikiwa ni miezi minne tangu Mainda na mama Winny wapewe msaada wa malazi na matibabu nyumbani kwa mchungaji Agrey Emanuel, huku hali ya mama Winny bado ikiwa ni ya kutisha, walipata taarifa mbaya ya ajali ya gari,iliypotokea maeneo ya TAZARA, taarifa hiyo ilimfanya Mainda alie mfululilzo huku mama Winny akiwa hajitambui kitandani.
ijali hiyo ilisababishwa na gari kupoteza mwelekeo na kugongana uso kwa uso na lori la mizigo, mwili wa mchungaji Agrey na mkewe uliharibika vibaya.
“Eh Mungu kwa nini unayaruhusu haya majaribu, mwenyewe waona ni siku mbili zilikua zimesali kabla ya mtumishi wako Agrey kumhamishia mama Winny India kwa ajili ya matibabu zaidi lakini ona mama huyu nae anakufa kabla hajapata matibabu hayo baba, eh Mungu nayekuabudu na kukutukuza fanya njia pasipo na njia,” Mainda alitamka maneno hayo kisha akapiga magoti na kusali sala ya BABA YETU mara mbili.
Mipango ya mazishi ilianza mara moja, wachungaji wengi walikusanyika nyumbani kwa mchungaji huyo, lakini hakuna aliyeelewa juu ya uwepo wa Mainda na mama Winny pale nyumbani zaidi ya ndugu wa marehemu ambao nao waliifanya kama siri.
***
Licha ya Edson na Winny kufanya kazi pamoja, tayari walianza kupendana, mapenzi yao yalikua moto moto, walitembea pamoja kila mahali,Winny alijikuta akisahau mapenzi matamu aliyoanza kupewa na Martin kabla ya kukoswa koswa kuuwawa, hata siku moja hakumueleza Edson juu ya mahusiano yake ya nyuma.
“Huyu ndiye mwanaume, angalau anakupenda na kukufundisha njia za kutafuta pesa”, Winny alijisemea huku akimfurahia zaidi Edson kwani licha ya kumpenda kimapenzi alimfundisha pia biashara ingawa ilikua haramu yeye hakujali, aliamini kazi ni kazi.
“Wiki tatu zijazo tutakua Tanzania kuna sherehe nataka kuwa na wewe mpenzi, niwaringishie wenzangu” Edson alimpa Winny taarifa ya sherehe iliyoandaliwa na mkubwa wao wa kazi ambaye ni Martin, ilikua ni sherehe kubwa ambayo ilijumuisha wafanya biashara wote wakubwa wa madawa ya kulevya katika majiji ya Arusha, Mwanza, na Dar es salam. Winny alisita kidogo lakini baada ya kubembelezwa alikubali kuhudhuria sherehe hiyo huku ikiwa ni mara ya kwanza kurudi Tanzania tangu aondoke na Martin zaidi ya miezi minne iliyopita.
***
“Sasa hapa mnatakiwa kuhama, mtu aliyekua anawagharamia hapa amekwishakufa, bajeti yenu nayo imekufa” yalikua maneno makali mithili ya msumari wa moto kupenya ndani ya moyo wa Mainda,
“Tafadhali mama yangu tuhurumie tu, mimi ni mwanao na huyu ni mama mwenzako tena mjane, mwonee huruma” Mainda aliongea kwa huruma huku akiwa amepiga magoti mbele ya dada wa marehemu Agrey, alikua dada wa umri wa makamo, ilikua ngumu kwa Mainda kuamini maneno hayo lakini dada huyo alimaanisha ukweli kuwa hawakustahili kuonekana tena nyumbani hapo,
“Nawapa wiki mbili muangalie ustaarabu mwingine” aliongea dada huyo kisha kuondoka huku akitingisha makalio, Mainda aliinamna na kumbusu mama Winny, hakutaka kumuacha afe mwenyewe kitandani zaidi alianza kuwaza maisha baada ya kutoka mahali pale,
“Acha ufie mkononi mwangu mama, siwezi kukuacha”, Mainda alijisemea maneno hayo na alipanga kesho yake kuenda kwa mchungaji mmoja aliyekua rafiki na marehemu Agrey, aliitwa mchungaji Paschal Mwalugaja,
“Huyu alikua rafiki wa Agrey lazima atanisaidia nikimuelezea tatizo langu”, alijisemea Winny akiwa bafuni kujiandaa kwa safari ya kuelekea Tabata shule kwa mchungaji Paschal, ambaye aliamini ndiye atakayekua msaada wake.

INAENDELEA

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI: SEHEMU YA-18

Saa nne kamili asubuhi, mchungaji Paschal Mwalugaja akiwa amekati katika kochi sebuleni kwake alisikia sauti ya mtu akibisha hodi mlangoni,
“Karibu ingia” aliongea mchungaji baada ya kutoka nje mlango wa geti ulisukumwa , aliingia binti mdogo ambaye sura haikua geni machoni kwake, alijaribu kukumbuka mahali alipomwona kumbukumbu hazikumjia kwa haraka,
“Shikamoo baba, ah samahani bwana Yesu asifiwe mchungaji” Mainda alisalimia kwa heshima,
“Amina binti hujambo” mchungaji Paschal aliongea huku akipokea mkono wa salamu kutoka kwa Mainda
“Sijambo mchungaji, sijui kama unanikumbuka mimi ni mtoto niliyekua naishi na marehemu mchungaji Agrey”, Mainda alijitambulisha huku akiketi katika kochi barazani,
“Ahaaaa, nimekukumbuka, maana hapa nilikua najaribu kufikiria nilipokuona kumbukumbu zikawa haziji kwa haraka sasa nimekukumbuka, vipi za utokako hawajambo?” aliongea Paschal huku akiweka biblia yake pembeni tayari kumsikiliza Mainda,bila kuchelewa Mainda alianza kuelezea kila kitu juu ya dada wa marehemu Agrey kutaka kuwafukuza,
“Yaani naomba tu utusaidie tuweze kukaa hapa kwako, kama ulivyokua unapendana na marehemu Agrey basi naomba uzidi kumuenzi kwa kutulea maana kikubwa tupate mahali tu pakukaa, hata kama ni chakula mimi nitakua naondoka kwenda kutafuta lakini mahali pa kukaa penye usalama nimeona ni wewe unaweza kunisaidia, sitaki mama Winny auwawe na watu wabaya kama waliomuua mumewe kwa kesi ya uwongo” Mainda aliongea mengi, hadi akaanza kutokwa na machozi kitu ambacho kilimfanya mchungaji asimame na kumsogelea kumbembeleza,
“Usilie binti nitakusaidia, naomba nyamaza tafadhali” mchungaji Paschal aliongea hayo huku akimfuta kwa kitambaa chake.
Kwa kuwa Mainda alikua katika kipindi cha kubalehe basi alivutia machoni kwa kila mwanaume,alikua na ngozi nzuri laini inayomeremeta, maziwa madogo yaliyokaa vizuri ndani ya blauzi yake, aliposimama makalio yake yalibinuka kwa mbali,hakika hata mchungaji Paschal alishindwa kuvumilia,
“simuachi huyu mtoto ni mrembo sana” alijisemea moyoni huku akimtazama kifuani.
“Basi acha kulia binti yangu, vipi umekula ?” Paschal aliongea hayo kusudi apate kisingizio cha kuingia nae ndani, na kwa kuwa alikua hana mke basi hakuogopa chochote,
“Sijala mchungaji lakini kama unanipa chakula naomba nipe katika mfuko nikale na mama Winny kwani hata yeye hajala” Mainda alisema kwa sauti ya furaha, kwani alimini tayari ameshapata msaada wa kumuokoa mama Winny kutoka katika mikono ya watu wabaya,
“Usijali ingia ndani ule kisha nitakupa kingine utaondoka nacho mkale pia kesho nitawafanyia mpango mje hapa nyumbani rasmi” baada ya mchungaji kusema maneno hayo Mainda alkinyanyuka na kumpa mkono wa shukrani kisha wakaingia ndani, kaa hapo ule acha mimi nikaoge maana nataka kutoka ili nikupe lifti,
“Sawa mchungaji hakuna tatizo” alijibu Mainda huku akijipakulia chakula mezani. Mchungaji Paschal aliingia chumbani kwake na kujifunga taulo kisha kuingia bafuni.
“Dakika kumi na tano tayari Mainda alikua ameshashiba nae Mchungaji alikua ameshatoka bafuni,
“Sasa njoo angalia chumba ambacho utakaa na huyo mama,” maneno hayo yalipenya masikioni mwa Mainda, na haraka alinyanyuka na kumfauta nyuma, hadi katika chumba kilichokua na kila kitu, jiko, chumba sebule na choo, kilikamilisha chumba maarufu kama (MASTER ROOM) nashukuru sana mchungaji hakika wewe ulikua rafiki wa kweli wamarehemu mchungaji Agrey,
“Asante sana binti yule ni rafiki yangu siku nyingi sana, Mungu amlaze mahali pema peponi”, aliongea mchungaji Paschal
“Amina” aliitikia Mainda lakini bila kutarajia alishtuka kidogo pale mchungaji alipomgusa kifuani,
“Ah mchungaji” Mainda aliongea huku akiangalia chini kwa aibu kutokana na kuguswa mahali hapo,
“Usijali binti mkono umeteleza, lakini naomba uingie uoge ngoja mimi nikavae nguo chumbani kwangu ili tuondoke” mchungaji Paschal aliongea maneno hayo, Mainda aliingiwa na wasiwasi lakini kutokana na imani yake juu ya mchungaji kutokua na mambo kama hayo alijipa moyo na kukubali kupokea kanga aliyopewa na mchungaji kwa ajili ya kuingia bafuni,
“Mainda aliingia bafuni na kuonga, huku mlango wa chumbani ukiwa wazi, alihakikisha mlango wa bafuni umefungwa , alioga kwa haraka kusudi asimcheleweshe mchungaji.
Mchungaji alinyata na kurudi katika chumba kilichokua na bafu ambayo Mainda alikua akiogea, kimya kimya aliijilaza mvunguni akimsubiri Mainda kwa hamu.
***
THE LIFE PARK, Mwenge ulikua ukumbi uliotarajiwa kufanyiwa sherehe iliyoandaliwa na Martin,kulijengwa sehemu maalumu kwa ajili ya sherehe hiyo, ulinzi wa kutosha uliwekwa mahali hapo kwani waliotakiwa kuja mahali pale ni mamilionea na mabilionea wa biashara haramu kutoka katika miji yote,ambayo waliongozwa na Martin, pia Martin alitoa ruhusa ya kila mmoja kuhudhuria na mwanamke wake ili sherehe iweze kupendeza zaidi, hivyo wake wa matajiiri pia walitarajiwa kuupamba ukumbi ule.
Siku tatu kabla ya sherehe kila kitu kilikua kimeshawekwa sawa, pombe za bei ghali zilijazwa mahali hapo, wageni wengine walioalikwa kutoka Lagos nchini Nigeria, na wengine kutoka Jakarta, Indonesia walikua tayari wamewasili nchini Tanzani kwa ajili ya sherehe hiyo.
***
“Hili gauni litakupendeza sana mpenzi, na mimi nikivaa suti yangu hakika watatuonea wivu”
“Kweli kabisa ila hiki kiatu mimi sijakipenda, nikilewa ninaweza kuanguka” Yalikua mazungumzo kati ya Edson na Winny ndani ya NAIROBI CLOTHING STORE, lilikua duka maarufu san jijini Nairobi Kenya, sehemu hiyo palikana nguo kutoka kutoka katika mataifa mbalimbali ikiwemo, Uturuki, Italia, Australia, Japan na China. Walifanya manunuzi ya kila kitu walichohitaji, na kusafiri hadi jijini Kampala, ambapo walipanga kukaa huko hadi siku ya sherehe ifike ili waweze kutua katika uwanja wa LIFE PARK kwa helkopta ya kukodisha,
“Nataka kila mtu akuonee wivu” Edson alimwambai Winny.
Hadi wakati huo bado Winny hakujua kama anayeandaa sherehe ni Martin.
***
Martin na Kemmy walikua jijini London, Uingereza kwa ajili ya kufanya manunuzi yao ya nguo, Kemmy aliona maisha yake kama ndoto isiyokatika, hakutaka kitu akakosa au kusema kitu asisisikilizwe,
“Nitakuvalisha pete siku ya sherehe” Martin alimwambia Kemmy huku akiwa amemkumbatia huku wakiendelea kuchagua nguo katika duka la nguo la LONDON DESIGNER, lilikua duka kubwa la nguo katika mji wa LIVERPOOL, hakika Kemmy aliiisubiri siku hiyo kwa hamu.
***
Mainda alimaliza kuoga na kutoka bafuni huku kanga ikiwa kifuani, alinyooka moja kwa moja na kufunga mlango wa chumba kisha akarudi na kujiangalia katika kioo, aliitumia kanga yake kujifuta taratibu kuanzia kichwani hadi miguuni.
Kwa kupenyeza jicho mchungaji Paschal alijikuta akimeza mate mfululizo, hakuamini kama msichana yule alikua mrembo kiasi hicho hasa alipoanza kujipaka mafuta kwa maringo,Mainda alifanya hivyo akiamini hakuna mtu anayemuona hivyo alijikuta akijipapasa sehemu za siri huku akijishika maziwa huku akijiangalia katika kioo, alitabasamu mwenyewe.
Paschal alizidi kuchanganyikiwa ,
“Eh Mungu nisamehe kwa hili kosa ninaloenda kulifanya, Eh Mungu baba naomba tu maana mimi ni mchungaji ila naona naanza kuwala kondoo wangu mwenyewe” alijisemea Paschal kimoyomoyo na kuanza kujitoa mvunguni, Mainda alishtuka kusikia kishindo mvunguni alihisi labda ni nyoka, lakini kishindo cha nyoka kisingeweza kuwa kikubwa vile,
“Mchungajiiiiiiiiiiiiii” aliita lakini alishangaa kumuona mchungaji akitoka mvunguni,
“Usiogope binti yangu” alitamka mchungaji huku akiwa uchi wa mnyama, alimsogelea Mainda nae Mainda akawa anajitahidi kujifunika kwa viganya vya mkono sehemu za siri,
“Mungu nisaidie nilishinde jaribu hili” alijisemea Mainda kwa sauti huku akiuondoa mkono wa mchungaji ulioshika begani..

Itaendelea

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI: SEHEMU YA-19

Ilikua mara ya kwanza kwa Mainda kuona maumbile ya mwanaume katika mazingira yale, alijua ni dhahiri pale asingeweza kutoka salama,
“Kweli niliwahi kusikia mapenzi ni matamu lakini sio kwa maumbile haya Mungu nisaidie tu” alizidi kujisemea Mainda moyoni huku akizidi kusogea ukutani ambapo mchungaji Paschal alimfuata,
“Wewe ni binti mzuri sana, nilipokuona hisia zangu zimekushukia, nahitaji penzi lako kwa gharama yoyote, nakuahiddi kukutunza maisha yako yote, nakuomba kubali tulale pamoja kisha ukamchukue mgonjwa wako mje hapa nyumbani, nakuomba tufanye kwa siri kubwa”aliongea mchungaji kwa sauti ya chini huku akimpapasa Mainda aliyekua akitetemeka kwa hofu,
“Sihitaji msaada wako, acha nikafie sehemu nyingine lakini mimi sio wa kutumikia ngono, nilikuheshimu kama baba yangu lakini unanifanyia hivi,? niache au nipige kelele”alifoka Mainda lakini ghafla alijikuta akikaa kimya baada ya mchungaji kusogea pembeni katika begi lililokua ukutani na kutoa bastola yake ndogo,alipapasa shingo ya Mainda kwa kutumia mdomo wa bastola hiyo, kitu kiichompelekea Mainda kutulia kama aliyemwagiwa maji, alikiogopa sana kifo, hakutaka kufa amuache mama Winny akiteseka,
“Unataka au hutaki, nikumalizie hapa hapa” alitamka mchungaji Paschal kwa sauti ya kutisha ,
“Naogopa nitaumia”, alijibu Mainda kwa sauti ya upole, hakuwa na lakufanya kusudi kuokoa maisha yake alijikuta akikubali kuelekea kitandani kwa ajili ya kufanya mapenzi na mchungaji, alivuta taswira ya hadithi walizokua wakipiga shuleni kuhusu mwanamke kuanza kufanya mapenzi kwa mara ya kwanza huumia sana hasa anapokutana na mwanaume mwenye maumbile makubwa,
“Mungu nisaidie, najua ni kosa naenda kufanya lakini ili niweze kuokoa maisha yangu yanipasa nifanye hili, naomba niepushe kwa lolote baya, eh Mungu uwe na mimi” Mainda alisema maneno hayo kisha akashtukia kubebwa na kutupwa kitandani, kisha mchungaji akamlalia kifuani.
Yalikua maumivu yasiyoelezeka, sauti ya Mainda iliishia ndani ya chumba, mziki mkubwa ulimeza kilio cha Mainda, kutokana na Mainda kutotaka kwa ridhaa yake kitendo kile uume wa mchungaji ulipata shida kupenya katika uke wa Mainda, hatua hiyo ilizidisha maumivu makubwa na baada ya dakika saba hivi mchungaji alifanikiwa kuvunja bikra ya Mainda, damu ilimtoka lakini mchungaji hakujali, aliendelea kumlazimisha kufanya kitendo hicho.
Hadi kufikia saa saba ya mchana ndipo mchungaji alitoka na Mainda huku wote wakikubaliana kuifanya siri,
“Leo tu ndio umeumia siku nyingine hutaumia tena Mainda usijali” mchungaji alikua akimbembeleza Mainda aliyeonekena kutokwa na machozi wakati wote wa safari.
“Naomba nikae kwenye gari hadi usiku ili niende nyumbani, siwezi kutembe nikiwa hivi” Mainda alimwomba mchungaji aweze kumuhifadhi hadi usiku ili kuificha hali aliyokua nayo.
***
Kitendo Mainda alichofanyiwa alikiona kama ni kitendo cha udhalilishaji, hakutaka mtu yeyote ajue, aliamua kuifanya siri yake, hakutaka hata mama Winny ajue,
“Mungu nisamehe kwa yote haya ni katika harakati za kumuokoa mama Winny” alijisemea Mainda huku akitembea kwa shida kuelekea nyumbani majira ya saa moja usiku, alifika na moja kwa moja alipitiliza hadi bafuni, alioga kisha kuingia chumbani alipo mama Winny, mapigo ya moyo yaliongezeka kasi hasa baada ya kukuta nguo zake na za mama Winny zipo ndani ya kiroba kikubwa,
“SIKU ZIMEBAKI MBILI MSIONEKANE HAPA” yalikua maandishishi machache kwenye kikaratasi juu ya meza, maandishi hayo yalimchanganya sana Mainda, hakujua angekimbilia wapi suala la kuenda kuishi kwa mchungaji Paschal lilimtoka kichwani, aliona kama kuenda kuishi nyumbani kwa mchungaji ni sawa na kusaini mkataba wa kuteswa kingono, siku zote alitamani kuwa na mpenzi mwenye umri sawa na wake, Wakati akitafakjari hayo dada wa marehemu aliingia chumbani,
“Shkamoo dada” Mainda alisamilia kwa unyenyekevu wa hali ya juu huku akikificha kikaratasi alichokua akikisoma,
“Sihitaji shikamoo yako, nahitaji muondoke hapa, huyo mgonjwa wako atafia hapa ndani hadi ashaanza kunuka, naomba kesho kutwa msiwe hapa, yaani kesho ni mda wenu kuhama, mfyuuuuuuuuuuuu”, maneno hayo yaliyoandamana na msonyo wa maana yaliumuacha Mainda katika wimbi la mawazo, aliona giza nene mbele yake, alipiga magoti na kuamua kumshirikisha Mungu katika kufanya maamuzi,
“Mungu nisaidie kuamua juu ya hili jambo zito mbele yangu, niende kwa mchungaji Paschal au nikawe ombaomba mtaani?” baada ya Mainda kutamka maneno hayo alijikuta akichukua maamuzi magumu ya kuhama na mama Winny, akakae nae pambeni ya barabara, aliona maisha yakigeuka na kuwa ya tabu kupita kiasi.
Hali ya mama Winny iliendelea kuwa mbaya, hasa baada ya kukosa dawa alizokua akitumia, kidonda kilimtokea shingoni kikawa kinaoza siku baada ya siku.
***
Siku ya ijumaa jioni tayari Edson na Winny walikua wamewasili nchini Tanzania, bila kupoteza mda waliamua kununua nyumba ya kifahari siku hiyo hiyo ili waweze kukaa kwa siku moja wakisubiri sherehe iliyaondaliwa na Martin,
“Kuna nyumba moja ipo karibu na chuo cha ustawi wa jamii, ilikua inauzwa milioni mia tisa” yalikua maneno ya dalali maarufu kwa jina la BWANA MANYUMBA, alikua dalali maarufu katika mitaa ya Mwenge
“Pesa sio tatizo” Edson alitamka huku akiendesha gari kwa haraka ili aweze kuenda kuangalia nyumba yenyewe, baada ya dakika kumi na tano tayari gari iliegeshwa nje ya nyumba, Winny alikua amejilaza katika gari, hakujua kitu chochote kilichokua kikiendelea kutokana na uchovu aliokua nao, hivyo Edson alishuka na BWANA MANYUMBA huku Winny akibaki ndani ya gari akiwa amelala usingizi.
Ilikua nyumba nzuri yenye kila kitu cha muhimu, ilikua na ukuta mkubwa na ndani ya ukuta kulkikua na mazao mengi yaliyopandwa, hakika Edson hakuleta ubishi katika kutoa pesa, watu wanaohusika katika kuuza nyumba walitafutwa kwa haraka, na nyumba ikafanyiwa malipo siku hiyo hiyo bila Winny kujua chochote.
Baada ya kuifanyia malipo walikabidhiana funguo na kila mtu akatawanyika , Edson alipanga kuondoka na Winny kwa ajili ya kuenda kupata chakula cha usiku katika mgahawa wa KFC uliopo Mliman City, hivyo aliondoa gari kwa kasi lakini akiwa katika foleni za mataa ya Bamaga, aliingiwa na huruma baada ya kumuona mtoto wa kike akimburuza mtu kwa kutumia kipande kikubwa cha pipa lililokatwa na kufungwa kwa kamba,
“Wewe binti nini tatizo?” Edson aliuliza baada ya kuegesha gari pembeni ,
“Ni stori ndefu kaka, ila kiufupi tumefukuzwa mahali tunapokaa na huyu mama yangu anaumwa sana” mtoto huyo alijibu kwa uoga,
“Sasa kwa mfano nikikuambia uniombe msaada utaniomba msaada gani?” Edson aliuliza swali,
“Nitaomba mahali pa kuishi tu penye usalama ili mama yangu apone”, mtoto huyo alijibu lakini alipokumbuka mchezo aliofanyiwa na mchungaji alijikuta akiingiwa na wasiwasi,
“Sawa omba watu wampakie huyu mama ndani ya gari nikawahifadhi mahali hadi kesho ili tujue cha kufanya” Edson alitamka hayo na haraka mama mgonjwa alipakizwa kwenye gari na safari ya kurudi katika nyumba aliyonunua ikaanza,
“Jina lako ni nani?” Edson aliuliza wakati akigeuza gari,
“Mimi naitwa Mainda” msichana huyo alijibu
“Je huyu mama yako kabisa au vipi?”
“Hapana huyu sio mama yangu kabisa huyu ni jirani yangu anaitwa mama W….” kabla hajamalizia sentenesi hiyo alikatishwa na mlio wa simu ya Edson kuita,
“Naamu mkuu, mimi tayari nipo Tanzania, ndio nataka niende nikapate dinner hapo Mliman City” baada ya Edson kupokea simu hiyo alimsitisha Mainda kuendelea na maongezi,
“Tutaongea zaidi kesho” alitamka Edson baada ya kukata simu. Mainda alipogeuka kiti cha nyuma alimuona msichana aliyelala usingizi, hakuweza kuona sura yake kwani alijifunika na kitambaa usoni.
Baada ya dakika saba tayari Edson aliegesha gari nje ya nyumba aliyonunua, alisaidiana na Mainda kumuingiza mama Winny ndani, hadi wakati huo bado Winny hakujua kitu chochote kilichokua kikiendelea. Na baada ya Edson kumkabidhi Mainda chumba alitoka na kumuacha pale,
“Kesho asubuhi nitakuja basi tuangalie namna ya kufanya”,
“Sawa nashukuru sana na sana”, Mainda aliona ameanza maisha mapya, alimuona Edson kuwa kijana mwenye roho ya ubinadamu, aliingia na kumwogesha mama Winny vizuri kisha wakapumzika kwa ajili ya kuisubiri siku ambayo ingefuata ambayo ilikua jumamosi.
“Martin na Kemmy waliingia Tanzania siku hiyo ya ijumaa wakitokea London, wote wakawa wanasubiri siku inayofuata kwa hamu ili waweze kufurahia sherehe iliyoandaliwa kwa gharama kubwa..

Inaendelea

the Legend☆
 
Mleta uzi mbona humpi credit mwandishi aisee
Hata jina tu inatosha imagine ungekuwa ww ndie mwandishi
Pleased heshimu jasho la mtu kwani ada ya mja hunena muungwana ni kitendo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom