Simkumbuki Wakili mnafiki kuliko Marando

Simkumbuki Wakili mnafiki kuliko Marando

Nape acha na wewe unafiki pamoja na ccm yako mmewaacha mafisadi papa waliozikwapua hizo pesa za EPA mnakimbilia kuwakamata akina Patel. Wakamateni akina meremeta na kagoda ndio tutawaona wa maana
 
Nape uongozi ulio2kuka ni pa1 n uwezo wa kutawala hisia zako.Acha ma2si unajishusha sn
 
kifupi ni kwamba marando ameeleweka vizur tu..sasa nape kama una uwezo wa kuwaeleza watz na ueleweke vizur zaid ya marando kaz n kwako!!!!
 
DSN,
Swala la Mzee wanguMarando kuwa mtetezi wa watuhumiwa wa EPA Mahakamani
na huku jukwaani akiwaita mafisadi LINAHITAJI USHAHIDI?
Uwakili ni taaluma isiyo na mipaka. Kila mtu anastahili haki ya utetezi mbele ya sheria, hata wenye kesi za mauaji hupewa mawakili na serikali.
 
Povu la nini weka hayo mawasiliano yasiyoacha shaka kwamba yametoka kwa Marando. Na kama hivyo ndivyo kwanini usimpeleke mahakamani kwa kusema uwongo na kukuchafulia jina badala ya kujificha nyuma ya keyboard na kulalamika?

Ha! ha! ha!... we ndio naona unatoa povu....... MTU UKIWA SHABIKI BWANA, HUWEZI KUKUBALI MAPUNGUFU YA UNACHO SHABIKIA...... We si unajua Kazi ya Marando na wateja wake wa EPA , halafu analyo tuambia jukwaani juu ya epa......! ILA ZITO Kuongozana na JK anakua MSALITI..... haya sasa msaliti mwingine huyu
 
Ama kweli nyani haoni kundule!Nape yani unataka kusema wewe si mnafiki hadi umwanzishie mwingine thread?CCJ wewe na kina Sitta hadi Mzee wetu Mwanakijiji hamkuwapa wananchi matumaini na humu JF ukipewa misifa kuwa ni mpinga fisadi na wewe tena baadaye ukaja na mambo ya siku 90 kuvuana magamba?

Nape unafiki wako humu unapimika bila hata shida yoyote,hadi ulipobanwa kipindi fulani ukaikana hii id,sasa umeirudia na unatu treat humu JF kama vile tunasahau mapema sana,ni kweli kama taifa tuna hiyo shida ya kusahau mapema,lakini humu ndani mambo siyo hivyo.Tunasahau lakini si mara zote,na pia si wote.

Unadai hukula pesa za EPA,unajuwaje kama unazopewa sasahivi si zile za EPA?Ama ni kwasababu hukupewa kipindi kile?Na si uliwapa watu siku 90?Nini kimekugeuza mawazo?
 
Nape kumbuka kuwa ili kukuziba mdomo na kashfa ya Jengo la umoja wa Vijana dhidi ya el ulipewa ukuu wa wilaya na kuhakikisha huhamii CCJ wewe na Sitta ukapewa kuwa mkuu wa propaganda na wewe umesomea propaganda hivyo endelea kuijenga CCM kwa kuibomoa PP lakini yana mwisho na kumbuka MKUKI kwa...................(Mwisho kabisa wewe ndio bingwa wa kutunga mambo zaidi na kukimbilia ushahidi,Mambo ya kutaka ushahidi ndio yanaliangamiza taifa,watu wanafanya utumbo halafu wanasema lete ushahidi)Marando anatetea watuhumiwa sababu anajua wao walikuwa wanatumiwa na CCM na unalijua hila ndio maana wameonewa Dagaa akina Faljara na papa na nyangumi wa EPA mnazidi kuwapa tenda na uraji zaidi.
 
Watu wangu wanaangamia kwa kukosa Maarifa!
 
Nimeshangazwa sana na shutuma za Marando juu yangu binafsi, Mwakyembe na Mzee Samweli Sitta.. Shutuma hizi zimenukuliwa kwenye baadhi ya vyombo vya habari likiwemo gazeti la TanzaniaDaima..alidai kabla ya kusema kuwa wengine wana kadi zaidi ya moja ya vyama tujiangalie. Sitawajibia kina Mwakyembe na Mzee Sitta lakini nitasema kidogo ninavyomfahamu Mzee wangu sana Marando. HILI LA MIEKUMILIKI KADI YA CHAMA ZAIDI YA KIMOJA SI WIMBO MPYA NI LA SIKU NYINGI, LAKINI NI LA KIPUUZI MAANA HATA NILIPOWAAMBIA WATOE USHAHIDI HATA WA KUSHIRIKI TU VIKAO VYA CCJ NITAJIUZULU HAWAKUWEZA MPAKA LEO WAKAISHIA KIGA KELELE BARABARANI BILA USHAHIDI..KWAHIYO HILI NI LA KIPUUZI.

NI MARANDO HUYU ANAYEWATETEA WATUHUMIWA WA KESI ZA EPA, MAHAKAMANI ANAWATETEA, JUKWAANI ANADAI NI MAFISADI NI MPAKA ALIPOTAKIWA KUJIELEZA NA BABAANGU JEETU PATEL, NI KWA KIASI GANI AENDELEE KUAMINIWA KUWA WAKILI WAKE WAKATI AMESHAMUHUKUMU KWENYE MAJUKWAA YA KISIASA KUWA YEYE NI FISADI, MASIKINI MARANDO KWA UNYENYEKEVU NA UANAFIKI WA HALI YA JUU KABISA AKAAANDIKA KWA MKONO WAKE KUWA, MANENO ALIYOYASEMA KUWA MIMI NAPE NIMEKULA PESA ZA EPA KUTOKA KWA JEETU YALIKUWA YAKISIASA NA KWAMBA ALISHINIKIZWA NA CHAMA CHAKE KUYASEMA..KWAMBA ETI ALIKUTA WAMESHAANDIKA ILE STORI YA KUTUNGA NA YEYE AKATAKIWA KUISOMA KAMA ILIVYO...HATA ALIPOWAKATALIA ALILAZIMISHWA KUYASEMA YALE... NAYE KWA UNAFIKI MKUBWA AKAKAA MBELE YA WAANDISHI WA HABARI NA KUROPOKA KUWA ETI Nape alikula pesa za EPA!!! Mtu mzima huyu!!!

Namheshimu sana sana Marando lakini anapofanya unafiki ni bora tuseme ili asije akawa mfano mbaya kwa vijana wasiomjua nao wakafuata unafiki wake...akibisha nitakuja na scan ya mawasiliano yake na Jeetu Patel hapa.. Tunaweza kumwamini huyu?

Mbali ya unafiki,hiyo ni njaa
 
Ndugu Nape

Nilishawahi kusikia kwamba Nape una masters.
Ni vigum kuamini kwa elimu na nafasi yako kwamba hujui kazi ya uwakili nini. Kwetu sisi wanasheria uwakili ni kuisaidia mahakama kufikia na kutoa uamuzi sahihi na sio kuwatetea km unavomaanisha.
 
Marando ana makosa mengi, na watu wa aina hii wanatuvurugia sana nchi yetu wamekuwa wanatuma vibaya fursa hii ya kidemokrasia kutaka kujinufaisha, wamekuwa si wa kweli kwa Taifa hili,wamewajaza vijana ujinga, wanatumia waandishi njaa kuandika uozo wao hii mbaya sana.....Marando elimu yako itumie kujenga nchi usiitumie kwa kujitazama mwenyewe madhara yake ni makubwa sana....Chunga kuchafuka kisiasa hakutokusaidia bali kutkupoteza ....
 
Nimeshangazwa sana na shutuma za Marando juu yangu binafsi, Mwakyembe na Mzee Samweli Sitta.. Shutuma hizi zimenukuliwa kwenye baadhi ya vyombo vya habari likiwemo gazeti la TanzaniaDaima..alidai kabla ya kusema kuwa wengine wana kadi zaidi ya moja ya vyama tujiangalie. Sitawajibia kina Mwakyembe na Mzee Sitta lakini nitasema kidogo ninavyomfahamu Mzee wangu sana Marando. HILI LA MIEKUMILIKI KADI YA CHAMA ZAIDI YA KIMOJA SI WIMBO MPYA NI LA SIKU NYINGI, LAKINI NI LA KIPUUZI MAANA HATA NILIPOWAAMBIA WATOE USHAHIDI HATA WA KUSHIRIKI TU VIKAO VYA CCJ NITAJIUZULU HAWAKUWEZA MPAKA LEO WAKAISHIA KIGA KELELE BARABARANI BILA USHAHIDI..KWAHIYO HILI NI LA KIPUUZI.

NI MARANDO HUYU ANAYEWATETEA WATUHUMIWA WA KESI ZA EPA, MAHAKAMANI ANAWATETEA, JUKWAANI ANADAI NI MAFISADI NI MPAKA ALIPOTAKIWA KUJIELEZA NA BABAANGU JEETU PATEL, NI KWA KIASI GANI AENDELEE KUAMINIWA KUWA WAKILI WAKE WAKATI AMESHAMUHUKUMU KWENYE MAJUKWAA YA KISIASA KUWA YEYE NI FISADI, MASIKINI MARANDO KWA UNYENYEKEVU NA UANAFIKI WA HALI YA JUU KABISA AKAAANDIKA KWA MKONO WAKE KUWA, MANENO ALIYOYASEMA KUWA MIMI NAPE NIMEKULA PESA ZA EPA KUTOKA KWA JEETU YALIKUWA YAKISIASA NA KWAMBA ALISHINIKIZWA NA CHAMA CHAKE KUYASEMA..KWAMBA ETI ALIKUTA WAMESHAANDIKA ILE STORI YA KUTUNGA NA YEYE AKATAKIWA KUISOMA KAMA ILIVYO...HATA ALIPOWAKATALIA ALILAZIMISHWA KUYASEMA YALE... NAYE KWA UNAFIKI MKUBWA AKAKAA MBELE YA WAANDISHI WA HABARI NA KUROPOKA KUWA ETI Nape alikula pesa za EPA!!! Mtu mzima huyu!!!

Namheshimu sana sana Marando lakini anapofanya unafiki ni bora tuseme ili asije akawa mfano mbaya kwa vijana wasiomjua nao wakafuata unafiki wake...akibisha nitakuja na scan ya mawasiliano yake na Jeetu Patel hapa.. Tunaweza kumwamini huyu?

shida kubwa ya viongozi wa ccm hamnazo!sasa hapa ndio umeandika nini??unachanganya changanya mambo kama mtoto wa shule ya msingi!mara kadi mara epa!ebu jipange then uje kutueleza vizuri kabisa ili tuelewe unachomaanisha,kama swala la wewe kuwa na kadi mbili kwani ni siri???
Naona umekulupuka asubuhi,na kuharisha jukwaani,vipi hujakwenda kanisani leo au tangu jana tayari?
 
Jamani au macho yangu! Kuna mahali Nape amemwita JITU TAPELI baba je! Huu ubaba unatoka wapi?

Mkuu kwa hili sioni tatizo liko wapi- ni suala la maadili tu kijana kumuita mtu mkubwa baba, mama, kaka n.k
 
Marando ana makosa mengi, na watu wa aina hii wanatuvurugia sana nchi yetu wamekuwa wanatuma vibaya fursa hii ya kidemokrasia kutaka kujinufaisha, wamekuwa si wa kweli kwa Taifa hili,wamewajaza vijana ujinga, wanatumia waandishi njaa kuandika uozo wao hii mbaya sana.....Marando elimu yako itumie kujenga nchi usiitumie kwa kujitazama mwenyewe madhara yake ni makubwa sana....Chunga kuchafuka kisiasa hakutokusaidia bali kutkupoteza .........

Tuhuma zipi? za kuwatetea Mafisadi? Kwani anaye takiwa kudhibitisha kwamba huyu mtu anamakosa ni nani? Acha Porojo za asubuhi
 
Kama huku ndio kuwa katibu wa itikadi na uenezi wa chama basi mtu yeyote tu anaweza, ilimradi tu asiwe na aibu aropoke tu ili kufurahisha watanzania wenye upeo wa chini wa kufikiri, wale waliozoea kugawiwa khanga kipande na chumvi mfuko na kisha wakateswa miaka mitano huku wakilaumu tu halafu wakasahau tena punde tu msimu wa khanga na chumvi unapowadia.

Sioni namna unavyotumia elimu na upeo wako kuendeleza chama chako zaidi ya kuongelea watu na kuleta mipasho na kejeli zisizo na maana.

Sijui upuuzi huu utaisha lini!?
 
NAPE kama hujuwi basi leo nitakueleza jambo, watanzania wa leo wanaakili kuliko wewe unavyodhani, ndio maana hapo mwanzo ulipokuja na kahoja kako ka kuwavua magamba mafisadi umma ulianza kukuthamini.

L
akini umma huo huo kwa kuwa ni waelewa baada ya kuona huna msimamo katika mambo ya msingi umekurudi na sasa wengi hawakuungi mkono.

USHAURI: kwa kuwa uwezo wako wa kuelewa masuala ya sheria ni mdogo hebu tafuta mtaalamu wa sheria ili aweze kukushauri, wakili ni nani, kazi yake ni nini, na kwa nini mtuhumiwa anahaki ya kujitetea na kutetewa.

Ndio maana tukichukuwa nchi(wananchi) toka kwa mafisadi sio kuwa "tutawachinja" tu wale tunaoamini ni mafisadi bali watafikishwa mahakamani nao pia watakuwa na haki ya kutetewa na itakapo bainika wana makosa watachukuliwa hatua kwa mujiwa wa sheria.

Nadhani huna hoja za msingi katika hili, jipange halafu uje na hoja yenye mashiko, sisi lengo letu ni moja tu, kuhakikisha kila mwananchi anathaminiwa utu wake na anaishi kama binadamu anavyopaswa kuishi, kutengeneza kizazi chenye kujiamini na sio kujipendekeza kwa wala rushwa.

NA HASA KUHAKIKISHA MAGAMBA YOTE YALIYO KUSHINDA YANAFIKISHWA KWENYE VYOMBO VYA SHERIA, NA KUWAVUA MAGAMBA YAO.
 
Nimeshangazwa sana na shutuma za Marando juu yangu binafsi, Mwakyembe na Mzee Samweli Sitta.. Shutuma hizi zimenukuliwa kwenye baadhi ya vyombo vya habari likiwemo gazeti la TanzaniaDaima.......

Nape vipi Kuhusu Miezi Sita? tutarajie nini? au Ndo ngonjera za siku 90? Ila kisheria wewe unaonaje Marando kuwatetea watuhumiwa.

Kwani anaye weza kuthibitisha makosa ya Mtuhumiwa ni Nani? Ni CCM? ni mahakama? au ni watu wa mtaani? wewe hujaona mtu anafanya kosa mbele ya hakimu na bado anaweka mawakili kumtetea? basi ingekuwa ukifanya kosa mbele ya Mahakimu unapelekwa Gerezani moja kwa moja
 
Back
Top Bottom