BigTall
JF-Expert Member
- Mar 9, 2022
- 422
- 1,049
Katika Mji wa Bariadi Makao makuu ya Mkoa wa Simiyu, mapema Leo Asubuhi kumekumbwa na Changamoto ya upatikanaji wa Mafuta ya Petroli.
Nimetembelea vituo vya Mafuta 8 ambavyo vimekuwa vikitoa huduma ya mafuta ambapo vituo vyote 7 havina Mafuta huku kituo kimoja tu Total Energies ndicho chenye mafuta.
Licha ya kukosekana kwa Petroli, Mafuta ya Dieseli yanapatikana kwenye vituo hicho na huduma kwa watumiaji wa Mafuta hayo ambao siyo wengi zinaendelea kutolewa.
Baadhi ya vituo, vimeweka matangazo yanayoelezea kuwa hakuna huduma ya mafuta ya Petroli, huku vingine vikibandika matangazo yenye ujumbe kuwa Petroli Hamna.
Waendesha Pikipiki za Abiria (Bodaboda) wamelalamikia Hali hiyo, wakidai kuwa wametembelea vituo vyote na hawajapata huduma.
" Toka Asubuhi Mji mzima wa Bariadi, Mafuta ni kama Dhahabu, kimebaki kituo kimoja tu Cha Total ndicho chenye mafuta, vituo vingine vyote havina Mafuta", Amesema mmoja wa Bodaboda.
Pia soma EWURA: Tuna mafuta ya kutosha Nchini, wenye vituo lazima wawe na mikataba na waagizaji
Nimetembelea vituo vya Mafuta 8 ambavyo vimekuwa vikitoa huduma ya mafuta ambapo vituo vyote 7 havina Mafuta huku kituo kimoja tu Total Energies ndicho chenye mafuta.
Licha ya kukosekana kwa Petroli, Mafuta ya Dieseli yanapatikana kwenye vituo hicho na huduma kwa watumiaji wa Mafuta hayo ambao siyo wengi zinaendelea kutolewa.
Baadhi ya vituo, vimeweka matangazo yanayoelezea kuwa hakuna huduma ya mafuta ya Petroli, huku vingine vikibandika matangazo yenye ujumbe kuwa Petroli Hamna.
Waendesha Pikipiki za Abiria (Bodaboda) wamelalamikia Hali hiyo, wakidai kuwa wametembelea vituo vyote na hawajapata huduma.
" Toka Asubuhi Mji mzima wa Bariadi, Mafuta ni kama Dhahabu, kimebaki kituo kimoja tu Cha Total ndicho chenye mafuta, vituo vingine vyote havina Mafuta", Amesema mmoja wa Bodaboda.
Pia soma EWURA: Tuna mafuta ya kutosha Nchini, wenye vituo lazima wawe na mikataba na waagizaji