Simanjiro: James Millya vs Ole Sendeka

Excellent mkuu. Kupata kwake ziro si kwamba hakuwa na akili, kumbuka kule Simanjiro ndipo kitovu cha tanzanite. Utajuaje kama Sendeka alikuwa pia anazamia migodini na kusoma pia hivyo muda wake ukagawanyika??

once again we are discussing about the merit of people instead of issues

Sielewi Mdondoaji unam challenge nini Maane, Maane alisema kupata kwake Div 0 si kwamba Sendeka hakuwa na akili wewe ukamwambia asi discuss Merit a discuss issues nikakwambia issue ya Div0 ni Millya mwenyewe kaileta nafikiri mlaumu Millya na si mwingine afterall naona hata wewe sasa unaongelea yaleyale
 

Millya araise kesi mara ngapi alikataa ushauri wa wazee wa kimila akasema mahakama itatoa haki sasa haki imetolewa anasema hakuridhika anakimbilia media naona anatapatapa tu mwisho wake uko karibu sana
 
Maane na Luteni someni biography ya 7th president wa US anaitwa Andrew Jackson aliyeongoza miaka 8 marekani tafuteni kama alisoma hata darasa moja.
Naona wewe huna hoja mimi nasema Sendeka ameonyesha uwezo wa kujenga hoja bungeni kuwazidi walio na PhD sasa what is the difference with your argument au unataka ligi tu isiyo na mbele wala nyuma hata Maane amejaribu kuelezea hivyo hivyo wewe ndiyo ukasema asi discuss issue hiyo which is which sasa
 
Join Date: Sat Mar 2010
Posts: 8
Thanks: 1
Thanked 11 Times in 6 Posts
Rep Power: 0


Huyu amejoin juzi tu, wenye akili wanajua ni kwa nini!

Huu ndiyo ujinga ambao tuwahi kujadili huko nyumba.
Mtu ku-join jana inamaanisha alikuwa hasomi post za jf?.
Badala ya kuuda hoja na tujadili,mtu anaanza kuangalia mtu ali join lini?.
 

tuko pamoja mkuu samahani sana kwa kukuelewa vibaya respect!!!
 
...watanzania wengi inaonekana wana akili za rojo rojo, kuthibitisha hili angalia habari za magazeti mengi ya kila siku,ndio maana si ajabu kuitikia mwaliko wa mpumbavu mwenzao kujadili UPUMBAVU!!!
 

Ole Sendeka ameshinda kesi yake. Kama katumia fedha za Mengi au zake mwenyewe huo ndio utamaduni uliopo Tanzania siku hizi. Money speaks! Millya katika taarifa yake amesema:
sasa nashikilia nafasi ya Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Arusha na Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya UVCCM Taifa.

Huyu unayem-brand umaskini aliwezaje kupata nafasi ya kuwa Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Arusha wakati tunaelewa dhahiri kwamba vyeo ndani ya CCM havipatikani bila kutumia pesa? Kama maskini alitoa wapi pesa za kuweza kushinda na kuwa Mwenyekiti. Acheni kutudanganya. Lisemwalo lipo. Huyu kijana inaelekea anatumiwa tu! Nani asiyejua makundi yaliyopo ndani ya CCM?

Ilishasemwa hapo awali kwamba kama Millya ni Morani, Morani huwa hawalii-lii hovyo hadharani! Yeye bado kijana, kama anaipenda nchi yake na chama chake aachane na kutafuta kumshinda Ole Sendeka badala yake aelekeze nguvu zake kwenye shughuli za UVCCM kwa manufaa ya umoja huo na CCM kwa ujumla.
 
Millya pole sana ila tangu siku ile pale steers Dar ukiwa na wapambe wako akiwamo tule mwanamke mwana CCM niliwasikia maongezi yenu nikashindwa kujua kama kweli hata ka tone ka elimu mlikuwa nako .Niliwasikia mkipanga na kujitapa juu ya kumliza Sendeka . Kama unasoma kumbuka mlikuwa watu 3 na yule mwanamke wa Arusha mnajitapa mwezi ulio pita kabla hamjaangushwa mahakani. That was very low kwa mtu kama wewe kuongea na kuwa na plan zile . Nakuhakikishia kama ume ajiriwa shikilia ajira na achana kabisa na Siasa maana si wewe wala wapambe wako wanajua la kufanya .Hutashinda hatama kama ulidai na yule mwanamke kwama Sendeka hakupewa Jimbo na Mungu . Mbinu chafu tokea steers will never help you na sasa unakimbilia kwenye media unaharibu zaidi .

Ila pia kumbuka sisi tunacheka maana CCM baada ya kutula sasa mbinu zenu chafu mnaanza kuonyeshana wenyewe kwa wenyewe . Laana kubwa inakuja juu yenu .
 

Mkuu,

Sasa wewe hujatofautiana na Sendeka.Mara muachie Mungu mara Muundie kesi nyingine.

Hapa mkuu msimamo ni upi?hayo hapo juu ni kama mafuta na maji
 
Tanzania kuna siasa za chuki na majungu sana. Wanasiasa jamani leteni maendeleo katika Taifa hili na sio majungu na chuki zitakazoingiza taifa katika machafuko. Historia inaaonyesha kuwa sehemu zilizowahi kuwa na machafuko na mauaji ya raia Afrika kwa asilimia kubwa inasababishwa na wanasiasa.
Tuijenge Tanzania isiyo na siasa za chuki na majungu jamani
 
Millya kama kweli wewe ni lawyer basi mtoto wangu bora asome uhandisi.
 

Sasa bw. mdondo, mbona unaongea huku unajing'ata ng'ata?

Kama sendeka alimtishia na kweli ni kosa kisheria kutishia, na bw.millya akaamua kwenda mahakamani baada ya kudharau ushauri wa wazee wa kimasai kutaka wayamalize, sasa analalamika kitu gani? Yani leo ndio anakumbuka vyombo vya habari na kutafuta public sympathy? sisi tunaomfahamu bw millya wala hatuna sababu ya kumhurumia hata kidogo, kwakuwa aliyataka mwenyewe kusikiliza ushauri wa mzee wa richmond sasa akaze msuli sio kulialia.

Kama anadhani vyombo vya habari vya mzee mengi ndivyo vimemuangusha mahakamani si atumie radio five na ABC tv (kama imeanza kuruka hewani) ili kukabiliana na IPP media!!

Kama iktokea Millya akamshinda Sendeka kwenye kura za maoni ndani ya ccm na wakaamua agombee ubunge simanjiro, hilo litakuwa jimbo litakalochukuliwa na upinzani kwa uhakika na kwa ulaini.

Tatizo la bw. milya ni uwezo wake bado ni mdogo, pamoja na kutwambia ana LL.M, cha msingi aendelee tu na ajira aliyonayo bad hajaiva kisiasa.
 
Milya Olesendeka kwa hili kakuzidi maarifa tafuta mbinu nyingine, kung'ang'niza mbinu hii moja kuta kushushia hadhi wewe bado kijana mdogo una safari ndefu mno kisiasa usijichafue mapema hivi.
Jifunze mbinu mpya.
 
jamani lazima watanzania tuwe na shukrani, huyu mzee mengi ndo aliyetufungua macho, Tanzania kulikuwa hakuna TV lakini huyu mzee alituwezesha na kutufix kwenye nchi zenye ustaarabu, sasa kwa kuwa cku hizi kuna series ya TV then mnamuona is a scambag, hey folks, kumbukeni tulikotoka and figure out
 
..naona watu kama hawako impartial ktk taarifa hizi.

..CCM wameamua kupatana, kwamba sasa hivi mafisadi na "wapiganaji" wamekuwa kitu kimoja kuelekea uchaguzi mkuu. hii ndiyo strategy ya CCM dhidi yetu wananchi.

..Ole Sendeka vs Ole Millya ni masuala binafsi. wanagombea ulaji tu hao. hakuna yeyote kati yao anayeweza kudai ameisaidia jamii yake kupiga hatua ya maendeleo. jimbo lina utajiri kibao lakini limechoka kama nini.
 
IMEKAA KAAJE SHAHIDI MUHIMU WA MASHTAKA KUANDAA MAPOKEZI YA MSHTAKIWA?

Mnadhani hapo hakuna mikakati miovu iliyofanyika?
Kwa kawaida mahakama huamua kesi kulingana na ushahidi uliowasilishwa mahakamani. Ushahidi wa kimazingira uhusishwa pale tu ambapo unahusina moja kwa moja na tukio - wakati linatokea au kabla halijatokea - kulingana na mazingira yaliyosababisha litokee. Sina uhakika iwapo ushidi wa kimazingira wa matukio yanayotokea baada ya kesi kuamuliwa yanaweza kutumika kama hoja kwenye rufaa
 
Millya: Sijatumwa na Lowassa kumshtaki Sendeka

na Mwandishi Wetu


MWENYEKITI wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Arusha, James ole Millya, amesema hakutumwa na aliyekuwa Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa, kumshtaki mbunge wa Simanjiro Christopher ole Sendeka.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dar es Salaam jana, alisema yeye alifikia uwamuzi huo baada ya kupigwa kofi na Sendeke kitu kilichomvunjia heshima mbele ya jamii.
"Lengo la kumwingiza Lowassa katika kesi hii ilikuwa kujitafutia umaarufu kwa Sendeka mwenyewe na kutafuta huruma na kusaka misaada ya kumsaidia katika kesi hasa kwa wabaya wa Lowassa.
"…Naomba nisisitize kuwa kabla ya kufungua kesi hii na kwa kuwa ilitokea katika kikao ambacho Lowassa alikuwepo mgeni rasmi, yeye binafsi na Askofu Thomas Laizer waliniita nami nikaitikia wito wa kuwaona," alisema Millya.
Alisema hivi sasa anakusudia kukata rufaa dhidi ya Sendeka kwa vile hakuridhishwa na mwenendo mzima wa kesi hiyo iliyoendeshwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha.
"Ni wazi kuwa binafsi sijaridhishwa na hukumu iliyotolewa na naamini kuwa Sendeka ana kesi ya kujibu, lakini napenda kusisitiza kuwa nina imani kubwa na mahakama na vyombo vingine vya dola, hivyo basi kuteleza katika ngazi hii si mwisho wa mahakama kutoa haki katika kesi hii.
"…Naamini mahakama na vyombo vingine vinavyohusika vya serikali vitaungana nami kama ambavyo vimefanya katika jitihada za kutafuta haki yangu mpaka ipatikane," alisema Millya.
Alisema anafikiria namna ya kuiomba serikali kwa kuwa ndiye mshtaki katika kesi hiyo kufikiria namna ya kukata rufaa kwa vile inaonyesha kulikuwa na mazingira yaliyojengwa kupoteza maana ya kesi wakati ikisikilizwa.
"Kila mmoja anaweza kuona hata tukio la shahidi mmoja aliyetakiwa kutoa ushahidi na serikali amegeuka kuwa mmoja wa wana kamati ya maandalizi ya mapokezi ya mshtakiwa," alisema Millya.
Kutokana na hali hiyo, Millya ameitaka serikali kumfungulia mashtaka kwa kuidaganya mahakama kwa vile hakuwa mkweli pindi alipotakiwa kutoa ushahidi.
Alisema baada ya yeye kwenda mahakamani, ameshuhudia mambo mengi kutokea ikiwa ni pamoja na haki ya mtu kuchezewa kwa maslahi ya mtu mmoja au kikundi fulani.
‘Baadhi ya mambo hayo ni matumizi mabaya ya vyombo vya habari ambavyo vilikuwa na lengo la kuandika habari potofu na za kunikandamizi… naelewa nia hiyo," alisema Millya.
Sendeka alikuwa akikabiliwa na kosa la shambulio la kudhuru mwili na kutishia kwa silaha. Ilidaiwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo Januari 9, mwaka jana majira ya saa 10:00 jioni katika Chuo cha Ualimu Monduli.

Maoni yangu: Huyu dogo kafulia, ajitafutie mkakati mbadala wa kutafuta ubunge kule simanjiro
 
Na nyie akina Sendeka toeni Pumba zenu..tomechoka na kulialia kwenu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…