kama kawaida yangu mimi ni msema kweli japo najua hampendi ukweli lakini nitasimamia ukweli Daima zifutazo ni sababu zinazonifanya nisikubaliane na Chadomo kuwa James Kinyasi Millya anaweza kuwa mbunge wa Simanjiro,
1.kwanza k
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...otice-cdm-wakija-na-tamko-jingine-refu-2.html
Sasa kama hana "hasari" unabwabwaja nini kwa mtu asiye na "hasari" Get a life dude
........
kama kawaida yangu mimi ni msema kweli japo najua hampendi ukweli lakini nitasimamia ukweli Daima zifutazo ni sababu zinazonifanya nisikubaliane na Chadomo kuwa James Kinyasi Millya anaweza kuwa mbunge wa Simanjiro,
1.kwanza kabisa Millya anajinadi kwa Wananchi wa Simanjiro kuwa yeye ni mwanaseria aliyetunukiwa cheti cha juu kabisa cha taaluma huyo, wananchi wasimanjiro huwa wanajiuliza inakuaje mtu mwenye taaluma hiyo ya sheria aliwahi kupigwa makofi hadharani na Mh mbunge wa Simanjiro, pamoja na kwamba anasema yeye amesoma zaidi kuliko Olesendeka alishindwa kufua dafu kwa mtetezi wa haki za wa nyonge Olesendeka, sasa huwa tunajiuliza kama elimu yake imeshindwa kumsaidia yeye mwenyewe itawezaje kuwasaidia wana simanjiro?
2.pili wazee wa kimila waliwahi kumuomba James Olemilya atoe kesi mahakamani wakamalize kijadi nyumbani kwani wamasai huwa wanamahakama zao na wanatumia kuwapatanisha waliogombana, ikiwa ni pamoja na vongozi wa kiserikali wanatokea kwenye makabila hayo. James Millya aliwajibu wazee hao kuwa yeye hana imani na mahaka za kijadi hivyo yeye ni mwanasheria anaimani na mahakama, japo aliishia kulalamika kuwa mahakama haija mtendea haki huku akisema atakata rufaa japo sifahamu kilicho mzuiya kukata rufaa baada ya kuongea na wandishi wa habari Dar es salaam, inashangaza na haingii akilini kama mh huyu alikuwa hana imani na mahakama ya wazee ambao ndiyo watakaye mpa kura sasa sijui atawambiaje watu ambao hana imani nao wamwamini wampe jukumu la kuwawakilisha kwenye Bunge la jamuhuri ya muungano.
3.James Millya anataka kuwagawa wanasimanjiro kwa rika zao, mpambe wake ambaye najua atakukuja hapa kujitapa Frank Oleleshwa aliwahi kuwambia wananchi wa Simanjiro hasa mamurani wa Korianga kuwa Millya ni Korianga hivyo anahitaji makorianga wote wawe chadema na ahakikishe watapambana na wazee waliotungoza siku zote bila kutupatia maendeleo, hili ni tatizo maana wazee wote wanaamini Millya na wapambe wake wanataka kuwajengea chuki wanasimanjiro wachukiane na hata mamurani hawapendi kuchonganisha na baba zao.
hizo ndizo sababu kuu zinazomfanya mh Olesandeka asimuwaze kijana huyu kuwa atakuwa nahasari yeyote kwenye uchaguzi ujao, pamoja na kwamba kamanda huyu wa chadema juzi alikwenda Orkesment na Gideon Sanago kuwahonga wazee wenye njaa kali na hapa nileweke walikuwa ni wazee fulani walevi wasio na mbele wala nyuma hata kura hawapigi, kwenda kumjengea boma ya nyasi eti kwa ishara kuwa atakuwa kiongozi wa simanjiro ilikuwa ni bure na haina madhara yeyote kwa ccm, wanasimanjiro wataendelea kuamini kuwa Millya ni mtovu wa nidhamu na alistahili kupigwa kofi.