Nikiamini kwamba wewe kweli ni mhitimu wa sheria (ingawaje si lazima uwe mwanasheria), nilitarajia uelewe hata basic principle ya sheria kwamba mahakama hufikia maamuzi ya kutia mtu hatiani pale mtu anapokuwa amethibitisha tuhuma dhidi ya mshitakiwa kwa kiwango muafaka (beyond reasonable doubt)
.
.....................Huyu mzee kuna siku yatakuja kumpata ya kumpata.
QUOTE]
Bro, may you pls reverse the mode to present your ideas. This sounds so utopian and magic to practical readers.
KGBtz usiwalaumu JF members kwamba wanamhukumu Millya Mahakama ndiyo iliyomuhukumu Millya hakukuwa na vivid evidence ya kumtia Sendeka hatiani kwa maana hiyo Millya ni muongo kaidanganya mahakama kuwa alipingwa na sisi tuna base kwenye hiyo hukumu wewe unayesema kaonewa kwa nini hukupeleka ushahidi mahakamaniTHIS IS WRONG. Kwasababu tu ya umaskini wake ndiyo maana asipate haki yake? Hayo mambo ya kufikirika kuwa aliahidiwa nini au nini, haitusadii, lets deal with the facts na tumhukumu kama mtanzania mwingine yoyote. Sijui kama mtu mmejaribu kufikiria kupigwa hadharani mpaka ukaanguka chini, its a very humilitiang incident, na hiyo ilitokea na ndiyo maana sendeka alienda kwa wazee wa kimila wamuombe msamaha, kama asingempiga, asingeenda kwa wazee. Sasa leo tunaingiza siasa za kina EL na Mengi kumkandamiza this educated young man, its just not fair! Fikiria tu angekuwa ndugu yako. I love my country, and then I hate my country and then I love it even more. Its painful and exciting at the same time.
kwanza jamii pls ondoeni hii option ya kuquote wakati mmoja wetu anajibu inachukua muda sana lakini haya ni mani yangu.
ole millya mwachie mungu tu kwani huonekani kama legal man for real,asingekushinda huyu mahakamani. na kukata rufaa hutoshinda maana you must have a new and profound evidence nayo utaipata wapi wakati principal witness wamegeuka. achilia mbali,
muundie kesi ingine maana tabia haina dawa atarudia tena.
Binafsi nimefarijika sana kama aliyosema Milya ni kweli kuwa Sendeka alipata Div-0. Hii ina maana moja tu, the guy is exceptional! kama anaweza kujenga hoja zenye nguvu na kutikisa bunge kiasi kile, kama anaweza kusimamia principle bila ya kuweweseka, kama anaweza kusimamia rasilimali za nchi kwa kiwango anachosimamia na kama anaweza kuongoza kwa kutoa michango bungeni yenye mashiko, then I will go for Sendeka badala ya wapuuzi waliojaa kwenye cabinet na PhD feki.
Ina maana Millya kahamia kwenye nyumba ya Lowassa mwaka jana baada ya kufungua kesi tupe data vizuri naona sasa unaanza kuelekea kuzuriKuweka facts sawasawa, millya anaishi kwenye nyumba ya rafiki zake ambao wamepanga kwenye hiyo nyumba ya sakina tangu miaka ya 2000, yeye millya amehamia hapo mwaka jana tu.
Excellent mkuu. Kupata kwake ziro si kwamba hakuwa na akili, kumbuka kule Simanjiro ndipo kitovu cha tanzanite. Utajuaje kama Sendeka alikuwa pia anazamia migodini na kusoma pia hivyo muda wake ukagawanyika?? Kumbuka kuwa ni wenzetu wengi ambao tulisoma nao ambao walikuwa wanafanya kazi za ziada ili kupata senti za kusaidia wazazi na wadogo zao?? Nakumbuka enzi zetu kuna watu walikataa kuendelea form Six wakaamua kufanya kazi maana maisha yalikuwa magumu kwa famila zao ili wapate japo kale kamshahara kuwasaidia, wengine walikuwa wanaishia form six wanaahirisha kwenda chuo ili wafanya kazi kidogo kuwasaidia ndugu zao. Unajua kwa wakati huu ni wachache sana ambao wamezaliwa kwa familia maskini ambao wako chuo!!! Kule vyuo vya elimu ya juu majority ni watoto ambao wazazi wao kwa namna moja wana uwezo. Wale ambao wako sekondari za kata ni wachache sana ambao wataendelea na kupata elimu nzuri na kufika elimu yajuu??? Shule zile za kata hazina facilities na waalimu wa kutosha!!! Shule ya kata waalim wawili vs sitini wa mjini!! Wapi na wapi??
Enzi za kina Sendeka ukifaulu kwenda Sekondari jua kuwa wewe ni cream kabisa!!!! Huyo Milya ni chipukizi la mafisadi na hakuna lolote la kutuambia, after all academic qualification ya kuwa mbunge minimum ni form four!!! Sasa yeye na digrii yake ya sheria ni kwa nini hakutambua kuwa ukipika kesi na hakimu akiamua kuivalia nzuga akatenda haki mbona aibu ndiyo matokeo??
Bwana Mengi hakikisha huyu kadogoo Milya anasafisha jina lako. Hivi kweli kama swahiba wangu anapatwa na matatizo nitaacha kwenda kumtia moyo kisa naogopa maadui zake?? Swahiba wa kweli ni yule akufaaye wakati wa dhiki!
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Machi 14, 2010
....................................................Katika maisha yangu nimeweza pia kuwa kiongozi katika ngazi mbalimbali. Kwa sasa nashikilia nafasi ya Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Arusha na Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya UVCCM Taifa. Nafasi hizi nimezipata kutokana na historia ya uwajibikaji wangu usiotiliwa shaka na moyo wangu wa kujitoa katika kusaidia kufanikisha majukumu yanayokuwepo mbele yetu katika taasisi yoyote niliyobahatika kufanya nayo kazi. ........................James MillyaHistoria yangu
Ushauri wa ziada kwa Ole Milya,
1.Sababu za kutupwa kesi ni ushahidi dhaifu ambao umeshindwa kuestablish prima facie.
2.Serikali haiwezi kukata rufaa kwa weak case kama hii, kama hata yeye mwenyewe Ole Milya ameshindwa kuithibitishia mahakama alipigwa kofi/ngumi shavu gani, hakumbuki kama ni la kulia au kushoto!. Wala kwenye maelezo yake ya awali, hakuripoti kutishiwa bastola!.
3. The only remedy ni yeye Ole Milya kujipanga upya, afungue kesi ya madai, civil suit dhidi ya Sendeka, anadai milioni kadhaa, kesi itadrag mpaka baada ya uchaguzi, Sendeka atashinda uchaguzi na atashinda tena hiyo kesi, na hapa itakuwa ndio the begining of an end kwa Ole Milya.
once again we are discussing about the merit of people instead of issues
Mdondoaji what are the issues want be discussed hoja ya Div 0 ni moja ya issue ambayo Millya ka raise kwa nini tusiijadilionce again we are discussing about the merit of people instead of issues
.
Mzee Mengi na Media Zake ni kikwazo kikubwa sana katika demokrasia ya nchi hii.Huyu mzee kuna siku yatakuja kumpata ya kumpata.
Tatizo kubwa hapa jf,wengi ni washabiki na hawamjui huyu mzee kwa undani alivyo yeye na media zake..
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Machi 14, 2010
...... Vyombo vya IPP, vilinihusisha mimi kutumwa na wanasiasa na hasa Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa kwenda kumshtaki Sendeka.
Mdondoaji what are the issues want be discussed hoja ya Div 0 ni moja ya issue ambayo Millya ka raise kwa nini tusiijadili
Ha ha ha!!! Which merits without issues!!!! We need to substantiate merits by backing them with issues!!
Hili la kutumiwa sio jambo geni au jipya kwa bw.Millya.
Kwa wale wasiomfahamu vizuri huyu Millya, huyu mmasai ni mtu anayependa kutumika sana na wanasiasa, huwa hajali maslahi ya wengi anaangalia tu upande wake.
Tukio linalonifanya niseme hivyo ni Mmaka 2004 wakati serikali iko kwenye mchakato wa kupeleka bungeni muswada wa sheria ya kuanzisha bodi ya mikopo. Baada ya kubainika kuwa muswada ulikuwa na mapungufu meni sana hasa kutokana na kutoshiriishwa kwa wanafunzi, viongozi wa wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu tullikutana na kutoa tamko na mapendekezo yetu. Huyu milya ndiye pekee alisimama kutetea muswada huo na kutoa bla bla kadhaa ( wakati huo alikuwa rais wa wanafunzi Tumaini university Iringa) alikuwa ni mtu aliyetumika sana na waziri Ng'wandu wakati huo kudhoofisha jitihada za wanafunzi kuwa na sauti ya pamoja.
Baada ya kutokea mkorogano kikaitishwa kikao cha marais wa vyuo vya elimu ya juu(vyuo vya umma na binafsi) unguja chuo kikuu cha zanzibar ( zanzibar university) na milya akashambuliwa sana na washiriki, kimsingi kikao kiliwaka moto karibia watu washikane mashati hadi ikabidi tumshauri mwenyekiti aahirishe kikao kwa muda ili kutuliza munkari ya wajumbe na kweli baada ya kurudia kikao jazba zikawa zimeisha na kikao kikaendelea lakini milya akaaga na kuondoka.
Baada ya hapo ikafika wakati muswada umepita na serikali imekubali wanafunzi kuwakilishwa kwenye bodi ya mikopo, Milya akadanganywa tena kwamba atpewa nafasi ya kuwa muwakilishi kwahiyo badala ya taasisi tuliyokuwa tumeianzisha (TAHLISO) kusimamia mchakato wa kuwapata wawakilishi Milya akaitisha kikao tena na baadhi ya watu wa vyo binafsi na kutoka na msimamo tofauti na wengine. Baada ya kuligundua hilo tukaendelea kutia presha wizara hadi ikakubaliana na mapendekezo ya TAHLISO kuwakilisha wanafunzi na kwa kuanzia mmoja wa wajumbe akateuliwa bw. Saidi Mkasiwa (alikuwa makamu m/kiti wa tahliso) sasahivi ni mheshimiwa hakimu kule bwagamoyo.
Kwahiyo milya sijaribu kudanganya umma, yeye ni mtu wa kutumiwa na ni mzoefu katika eneo hilo.