Siloam church

Siloam church

Kweli ni kitru gani...??? Kwea mujibu wa nani...? Tunakubaliana wapi kuwa hii ndo kweli...??

Otorong'ong'o, Mwamini Bwana Yesu kuwa ni Mungu na kwamba aliacha utukufu wake Mbinguni na kukubali kuzaliwa kama mwanadamu ili afe na kuchukua adhabu ya dhambi zako. Ukubali pia kuwa wokovu unapatikana kwake tu, sio kupitia kwa nabii, mtume, bikira mtakatifu, Mohamed au kitu chochote kile.
 
Hiyo kweli uliyoipata yaweza kuwa inatokana na udanganyifu wa moyo wako maana kama unayabeza mambo ya rohoni hiyo kweli ya Mungu unaipataje? Kumbuka Mungu ni Roho.
Mambo ya rohoni ni yapi...? Nitajie japomatano...

Nakusubiri..
 
Mwamini Bwana Yesu kuwa ni Mungu na kwamba aliacha utukufu wake Mbinguni na kukubali kuzaliwa kama mwanadamu ili afe na kuchukua adhabu ya dhambi zako. Huyu Yesu alifufuka na alirudi Mbinguni kwa babaye. Sasa, muombe atakujulisha inakupasa kufanya nini.
Hilarious....
 
Otorong'ong'o, Mwamini Bwana Yesu kuwa ni Mungu na kwamba aliacha utukufu wake Mbinguni na kukubali kuzaliwa kama mwanadamu ili afe na kuchukua adhabu ya dhambi zako. Ukubali pia kuwa wokovu unapatikana kwake tu, sio kupitia kwa nabii, mtume, bikira mtakatifu, Mohamed au kitu chochote kile.

Yote hayo naelewa....

Sio naamini kuwa tuu Yesu ni kweli na uzima bali naamini Yesu ni Mungu....

Haya jibu yale maswali chap...
 
Hujauelewa huu mjadala, mimi sizungumzii taasisi au mtu, kinachozungumzwa hapa ni kwamba kwenye uislam hakuna mahedhebu, full stop, sasa ukianza kuniambia habari za ISIS, BAKWATA au AL-QAIDA nenda kawaulize wenyewe kwa maana hizo ni taasisi ambazo kila moja inamalengo yake.

Nadhani hata wewe hukuuelewa mjadala. Nikukumbushe, mjadala ulihusu siloam church, ukristo mmeuletaje kwenye mjadala. Siloam sio wakristo imekuwaje mmewaunganisha na wakristo. Hao majangiri wanaovaa kofia ya uislam mbona husemi mnapatana nao katika mambo gani maana wao wanaua watu, kwa kutumia maandiko ya kitabu chenu na wanadai kuutetea uislam. Kuniambia nikawaulize ni kujaribu kukwepa ukweli kuwa dini yenu ni katili mno, mnaua hovyo.
 
Acheni kufanya mambo ya kawaida magumu. Yesu alituweka huru bila masharti yoyote,alijitoa kwa hiari yake bila masharti yoyote akalipa garama ya dhambi na kufuta dhambi kwa wamwaminio.

Yesu alisema kumkubali tu unakua huru na dhambi,unakua huna hatia na dhambi. Hakuna dhambi duniani yesu alishafuta zote.

Hivi umeelewa ulichokiandika?

Kwanini Biblia inasema tutubu kila wakati?
Tukisema hatuna dhambi twajidanganya - 1Yoh1:8

Acha kufundisha watu imani za kipagani. Hakuna mwanadamu asiye na dhambi.

Maelezo yako yanathibitisha bila shaka kwamba mnamwabudu shetani.
 
Mambo ya rohoni ni yapi...? Nitajie japomatano...

Nakusubiri..

Inaelekea umedakia njiani majibu yangu kwa maelezo yaliyotolewa kwenye #106 . Sasa kama kuna mtu anaunga mkono kubezwa kwa makanisa ya 'kiroho' kama alivyoiweka Ms.Lincoln nadhani huo utakuwa ni upotoshaji. Kama wewe sio mtu wa rohoni hata nikikuambia hayo mambo ya rohoni hutayaelewa.
 
Siloam church is a cult like other cults that call themselves Christian churches.

Mafundisho yao ni uzushi, imani zao potofu, ziko kinyume na Biblia.
 
Hiyo kweli uliyoipata yaweza kuwa inatokana na udanganyifu wa moyo wako maana kama unayabeza mambo ya rohoni hiyo kweli ya Mungu unaipataje? Kumbuka Mungu ni Roho.

Kuhukumu wenzenu ndio haiba yenu.Nimebeza mambo ya rohoni kivipi? Kumtuza mchungaji kama mtumbuizaji nalo hilo ni jambo la rohoni? Mungu sio BABA enu peke yenu, mbinguni utawakuta usiowategemea na sihami kanisa.Ukumbuke pia mambo ya nguvu za giza ni ya rohoni pia...
 
Inaelekea umedakia njiani majibu yangu kwa maelezo yaliyotolewa kwenye #106 . Sasa kama kuna mtu anaunga mkono kubezwa kwa makanisa ya 'kiroho' kama alivyoiweka Ms.Lincoln nadhani huo utakuwa ni upotoshaji. Kama wewe sio mtu wa rohoni hata nikikuambia hayo mambo ya rohoni hutayaelewa.

Shida ni kuwa unafikiri hayo mambo ya rohoni unayajua peke yako na kanisa lako.Sio kila wakati makanisa hayo mnayoyaita ya kiroho yapo sahihi.Na sio yote ni chimbuko la uovu.Kweli huijui peke yako.Injili ni ya Yesu kristo masia, sio yako.Usidhani wewe ndio upo karibu na
Kristu zero distance na wengine wapo miles away kisa unaabudu kwenye so called kanisa la kiroho.Kwanza hamna kanisa la kimwili.Sipendi watu wanaodharau imani za watu wengine hasa walokole na Alshabab.
Mnakimbilia kulaani na kupindisha ukwelimSijapotosha kitu na simtuzi mchungaji katu izo mbwembwe za Ngwasuma tuwaachie Wenyewe.Nimemaliza.Na kama unadhani nimepotoka sana niombee sio kunitisha na kujiinua kama malaika while wewe na mimi ni damu na nyama.
Ova.
 
Inaelekea umedakia njiani majibu yangu kwa maelezo yaliyotolewa kwenye #106 . Sasa kama kuna mtu anaunga mkono kubezwa kwa makanisa ya 'kiroho' kama alivyoiweka Ms.Lincoln nadhani huo utakuwa ni upotoshaji. Kama wewe sio mtu wa rohoni hata nikikuambia hayo mambo ya rohoni hutayaelewa.

Vipi mpendwa...Yani umegoma kunitajia mambo ya rohoni...Au umeropoka tuu kumbe na wewe huyajui ila umekariri tuu mambo ya rohoni..

Mkuu au mambo ya rohoni ni kule kuropika rikandaraboshika rabarabaraaaaa.....ndo hiyo mkuuu...??
 
Mwamini Bwana Yesu kuwa ni Mungu na kwamba aliacha utukufu wake Mbinguni na kukubali kuzaliwa kama mwanadamu ili afe na kuchukua adhabu ya dhambi zako. Huyu Yesu alifufuka na alirudi Mbinguni kwa babaye. Sasa, muombe atakujulisha inakupasa kufanya nini.

Naona umeanza kuleta hoja nyingine, okay tuendelee kukumbushana tu,
1. Mimi kwanza namuamini yesu (Issah) kama mtume aliyekuja kabla ya Mtume Muhammad (s.a.w) na sio mungu kwasababu hana sifa za kuwa mungu ila wewe kama unazo hizo sifa unaweza kunieleza,
2. Yesu hakuwahi kufa ila alipaa mbinguni na hapo baadae atarudi na moja ya lengo la kurudi ni kuja kubainisha kuwa yeye ni nani, ni mungu au alikuwa ni mtume kama mitume mingine tu.
3. Siamini kwamba mungu au mtume anaweza kuchukua dhambi za mtu, ila naamini kwamba kila mtu atalipwa kulingana na kile alichokitenda hapa duniani.
4. Mimi naamini kuwa wakuombwa ni Mungu mmoja tu, na sio Yesu (Issah) wala Mtume (S.A.W), hivyo mimi na wewe tunapaswa kumuomba mungu kupitia mafundisho ya hao mitume na sio kuwaomba wao.
5. Unasema yesu aliacha utukufu wake mbinguni na kukubali kuzaliwa kama mwanadamu ili afe na achukue dhambi zako alafu hapohapo unasema alipofufuka alirudi kwa baba yake (sio kwenye utukufu wake tena), okay. swali, kipindi mungu (yesu) amekufa (kabla hajafufuka) dunia ilikuwa inaendeshwa na mungu yupi?
NB; hatugombani ila ni kueleweshana tu. Ahsante.
 
Nadhani hata wewe hukuuelewa mjadala. Nikukumbushe, mjadala ulihusu siloam church, ukristo mmeuletaje kwenye mjadala. Siloam sio wakristo imekuwaje mmewaunganisha na wakristo. Hao majangiri wanaovaa kofia ya uislam mbona husemi mnapatana nao katika mambo gani maana wao wanaua watu, kwa kutumia maandiko ya kitabu chenu na wanadai kuutetea uislam. Kuniambia nikawaulize ni kujaribu kukwepa ukweli kuwa dini yenu ni katili mno, mnaua hovyo.

Ni sahihi mjadala unahusu ''Siolam Church'', hivyo kama great thinker lazima tujadili zaidi ya hapo ilimradi kuwe na mahusiano na kile tunachokijadili, hivi ndivyo inavyokuwa mkuu, nachofahamu mimi dini yetu sisi sio katili bali ni dini yenye huruma kubwa kwa mwanadamu kuliko dini nyingine zote, kila jambo lilioamrishwa linafaida kubwa na hasara kiduchu au hasara isiwepo kabisa (ukisoma ndio utaelewa ila usiposoma hautakaa uilewe hii dini) Mf. tendo la mtu aliyendani ya ndoa kupigwa mawe hadi kufa linaonekana ni jambo la kikatili mno, lakini hii hukumu ni sahihi kulingana na athari za tendo au kosa lenyewe. kwanza kabisa tuanze kubainisha faida na hasara za tendo hili. kwa upande wa faida, binafsi siioni faida yeyote zaidi ya kukidhi matamanio ya nafsi kwa njia isiyo halali, hali yakuwa una mwenza wako nyumbani, (kama unafaida nyingine unaweza kunieleza), kwa upande wa hasara hata mia zinafika kama we GT utakubaliana na hili. (sihitaji kukutajia) lakini nyingi zitaangukia kwenye magonjwa, mauaji ya alaiki, chuki, uhasama, visasi, familia zisizo rasmi, ukosefu wa maadili n.k. Natumaini utakuwa umenielewa sasa.
 
Kweli haitafutwi kwa kuhama makanisa bali inatafutwa kutokana na nia ya ndani ua kumjua Mungu na Neno lake na kulitenda pasipo sahau kumwomba akusaidie....Sidanganyiki ng'oo! Wala simtuzi muhubiri jukwaani.

Hili la kumtunza sijui kutuza muhubiri akiwa jukwaani kwakweli huwa silielewi kabisa na sitalifanya to be honest.........
 
Hujauelewa huu mjadala, mimi sizungumzii taasisi au mtu, kinachozungumzwa hapa ni kwamba kwenye uislam hakuna mahedhebu, full stop, sasa ukianza kuniambia habari za ISIS, BAKWATA au AL-QAIDA nenda kawaulize wenyewe kwa maana hizo ni taasisi ambazo kila moja inamalengo yake.

Ndugu kimbwe
Usilazimishe watu wakubaliane na hisia zako. Uislam una madhehebu. Na hilo linajulikana dunia nzima. Hiyo exclusiveness unayoionyesha ni dalili ya extremism katika imani. Na huo ni upotofu.
 
soma hapa anavyomuita ......Mjumbe wa mapenzi ya Mungu AD2 MUNGU wa majeshi ....... anaitwa mungu wa majeshi! mtu akiishakutoa kwenye Biblia tu umepoteza dira. Mimi mtu yeyote ashike Biblia yake nami yangu tuombe ukianza sijui majini mahaba sijui nabii nani hatuelewani

Binadamu anapoamua kuwa mjinga anakuwa mjinga kweli kweli .....!!
 
Nimegundua pia wanapenda kucheza na maneno, mfano; bibilia wakishaichana front cover wanaita kitabu cha neno sijui, ndoa wanaita agano, yani ni mchezo fulani wa kisaikologia. wenyewe watusaidie, kanisani hatuwezi kuja kama mnashindwa kutueleza juu ya imani yenu hapa.
 
Back
Top Bottom