Dan Zwangendaba
JF-Expert Member
- Apr 25, 2014
- 5,506
- 7,502
Sifuri kivipi na dira gani iliyopotea mpaka sasa? Magufuli alikuwa na agenda kuu 4, SGR, Bwawa la Mwalimu Nyerere, ujenzi wa makao makuj Dodoma na Air Tanzania. Ndani ya mwaka mmoja mama anaendeleza ujenzi katika vipande vyote vya Reli, na kazi inaendelea.Kama huyu mama anaweza kuongoza nchi basi hii nchi haina sifa za kuiongoza, yoyote anaweza kuiongoza.
Wapiga debe mtapiga sana ila ukweli ni kwamba huyu mama ni sifuri. Huhitaji elimu ta form six kuona kua hili taifa limepoteza dira chini ya huyu Mzanzibari. Muda ni mwalimu mzuri, muda utasema tu.
SGR katika kipindi cha mwaka mmoja ni kama amefanya double ya hatua iliyofikiwa katika ujenzi wa Bwawa. Air Tanzania zinaendelea kuaibgezeka na kufanya safari kama kawaida. Ndani ya mwaka mmoja amejenga vituo vya afya vingi kuliko Rais yoyote aliyewahi kumtangulia. Ndani ya mwaka mmoja Samia amejenga madarasa mengi kuliko Rais yeyote aliyemtangulia. Ndani ya mwaka mmoja amekamilisha mradi wa Megawati 85 pale Ubungo ambapo magufuli aliutelekeza akituaminisha kuwa gesi yote imeuzwa. Ni Samia Huyu kwa mara ya kwanza ameitoa bajeti ya Kilimo toka bilion 200+ hadi 900+; Ni Samia Huyu aliyefungua ten ajira baada ya msoto wa miaka 7.
Ni wapi unapata ujasiri wa kumpa sifuri kwenye uongozi wake. Punguzeni chuki Samia tries her best despite the difficult moment facing the world.