You are questions can be asily found in the links below, read and come back for discussion: Halafu kuna mengine umenisemea hapo, source ya kusema vile ni kuwa JKN alikuwa haambiliki na nikatoa mfano tu; so whether Mtei was right or wrong was not my argument! kuna post nimetaka wataalamu watueleze issue za hawa WB na IMF ni kwa jins gani wangeiathiri AD, that shows I have no clue in this very area!
http://www.dailynews.co.tz/home/?n=4834&cat=home
Mkuu Waberoya, heshima yako mkuu. Samahani kama sikueleweka, kwani najua maana iko kwa msomaji na siyo mwandishi. Sikukusudia kukuweka maneno mdomoni, ila nilitaka kudadisi kwa kutumia maswali. Hakika nilitaka kujua ulichoandika kuwa hayo mawazo mazuri ya Mtei yaliyokataliwa na Nyerere ni yepi na uzuri wake ni upi?
Link uliyonipa kwamba kuna majibu ya maswali yangu sikuyakuta. Nimekuta vitu viwili.
Mosi, nanukuu "Another issue that makes him happy at the moment he says, is the IMF's recent decisions which he used to push foward but were ignored when he was working at the Breton Wood institute. One of the things he proposed in the early 80's was that since poor nations paid their fees to IMF in gold, and the gold over time appreciated, the fund was supposed to give back some of the profits obtained from sell of gold to poor nations."
Hili wazo halihusiani na Nyerere. Mtei alipojiuzuru, aliajiriwa na IMF. Hapa anaongelea ushauri mzuri alioutoa kwa IMF ili kuziinua nchi masikini duniani kutokana na rasilimali za nchi hizo, lakini IMF wakaukataa. Ningeshangaa kama wangekubali kwa sababu IMF, WB na WTO hazikuundwa kuziinua nchi masikini. Katika hali ya anguko la uchumi wa dunia, ambapo dola imeshuka thamani na dhahabu imepanda thamani maradufu kwa kipindi kifupi, na baadhi ya nchi masikini zinatoa dhahabu kwa wingi, ningeshangaa kama IMF wasingekimbilia kuyatekeleza hayo mawazo kwa sababu hayazinufaishi nchi masikini. Hili nitalijadili katika kipengele tofauti kwa sababu halihusiani na maswali yangu. Hii ni Mtei na IMF siyo Mtei na Nyerere ambalo ni swali langu.
Pili, katika link uliyonipa nimekuta wazo jingine ambalo pia halijibu swali langu. Nanukuu "He says one of his 'friction' with Nyerere was that when the Ujamaa policy vividly failed in the late 70's he wanted to apply IMF's measures to rescue the situation. At independence we were neck in neck against Kenya and Uganda but we failed because we took too long to take actions after the fall of Ujamaa," he explained." Hapa hakuna mahala wanataja mawazo ya Mtei ni yepi na uzuri wake ni upi?
Katika link hiyo wanaongelea kitabu alichokiandika Mtei cha "From Goathed to Governor" kilichochapishwa mwaka jana - 2009 ambacho nimekisoma. Unless mtu anayaweka mawazo ya Mtei yaliyokataliwa na Nyerere katika maandishi, mimi nitaendelea kumuamini Mtei mwenyewe ambaye ameuweka ukweli huu katika kitabu chake. Katika kitabu chake, kuanzia ukurasa wa 146 mpaka 157, Mtei anaeleza kwa kinagaubaga Nyerere aliyakataa mawazo ya Bo Karlstrom kutoka IMF. Haya hayakuwa mawazo ya Mtei.
Anaeleza kuwa mara tu baada ya vita ya Kagera 1979, uchumi ulilegalega na ulihitaji dola milioni 375 ili kuukarabati. Anasema yeye kama Waziri wa Fedha alipewa jukumu la kuhusisha jopo la weledi ili kuukwamua uchumi dhidi ya madhara ya vita ya Kagera.
Na hili ni jambo la kawaida popote duniani. Mfano, 2008 Marekani ilikumbwa na anguko la uchumi kutokana na mchanganyiko wa sababu, mojawapo zikiwa ni madhara ya vita dhidi ya Iraq, mtikisiko wa soko la nyumba, kupanda kwa bei ya mafuta n.k. Hiyo ilisababisha baadhi ya viwanda na mabenki makubwa kufilisika na vingine kulegalega. Marais Bush na Obama, mara zote waliwataka Mawaziri wao wa Fedha kukaa na majopo ya weledi ili kubuni mbinu za kujikwamua.
Majopo yao ya weledi yaliamua kuwa baadhi ya benki (hata viwanda) ni kubwa kiasi kwamba hawawezi kuziachia kufa, na wala kuzimega katika vibaba. Walizigomboa kwa mitaji mikubwa ya kodi za wananchi, ambapo serikali inamiliki asilimia kubwa ya hisa mpaka hapo dhoruba litakapo pita na zikaanza kupata faida. IMF, WB na WTO hawaruhusiwi kunusa pua katika majopo ya Marekani ya kufufua uchumi.
Sasa turudi katika kitabu cha Mtei. Katika ukurasa wa 149, yeye aliamua kuwaalika weledi wa IMF wakiongozwa na Bo Karlstrom ili washirikiane na weledi wa Wizara ya Fedha kubuni program ya kufufua uchumi. Anasema katika jopo lao, IMF walikuwa tayari kutoa mkopo wa kufufua uchumi lakini kwa masharti matatu. Mtei ameyaorodhesha hayo masharti kuwa ni; Mosi, kushusha thamani ya shilingi, pili, kuleta wawekezaji kutoka nje ya nchi, na tatu, serikali iache kusaidia kifedha mashirika ya umma na viwanda, na badala yake iyabinafsishe. Anatoa mfano wa benki ya taifa ya biashara NBC, kuwa ilikuwa ni kubwa mno iliyotishia usalama wake yenyewe.
Mtei alirudi kumueleza Bo Karlstrom kuwa Nyerere ameyakataa masharti. Bo Karlstrom akamwambia Mtei kuwa ebu niwezeshe nionane naye hana kwa hana nitamlainisha na atayakubali. Tarehe 29 November 1979 alimkutanisha na Nyerere Msasani. Baada ya maongezi, Nyerere alimwambia Mtei kuwa awaambie warudi zao Washington kwani yeye hawezi kuruhusu nchi yake iendeshwe kwa amri kutoka Washington (Washington consensus). Kuwa Nyerere alimwambia "I will devalue the Shilling over my dead body". Na hiki ndicho kisa kilichopelekea Mtei Kujiuzulu/kuachishwa kazi.
Kwa maoni yangu, kikatiba, Rais anapomuomba Waziri mawazo katika suala muhimu, na Waziri akampeleka mtu mwingine na kumwambia Rais kuwa "msikilize huyu ndiye mwenye mawazo mazuri", haimaanishi kwamba yale ni mawazo ya Waziri. Ila inamaanisha kuwa Waziri alikuwa na mawazo yake na akayaona siyo mazuri kama ya mwenzake. Au inawezekana Waziri hakuwa na mawazo kabisa ndiyo maana akayaona ya yule mtu ni bora. Sijuhi katika issue ya Mtei ni lipi linaegemea kwake, ila katika kitabu chake, hakutaka ile ya "copy and paste" yaani kuyafanya mawazo ya IMF ni yake. Kama ambavyo hukujibu maswali yangu, na link uliyonipa haina majibu, basi nitaendelea kuamini maandishi ya Mtei mpaka hapo atakapojitokeza mdau wa kunielemisha kuhusu mawazo ya Mtei ni yapi na uzuri wake ni upi?