Sikulifuta Azimio la Arusha - Mwinyi

Sikulifuta Azimio la Arusha - Mwinyi

It is true that Mzee Mwinyi did not kill Arusha Declaration rather he abandoned every principle stated on Arusha Declaration!

LOL!! naona umetumia fatuma sasa!

Nilisema mnamwonea huyu naona umekubali!-Mtu pekee ambaye angelichukua AD na kubadilika na wangestahili hukumu ni Sokoine au Kawawa,

Wala hakujiangaisha kusoma na kukariri kanuni zenu, alichukua nchi na ku-assume ndiyo anaanza!! LOL!

Hivi nani ana clue kwa nini Kawawa hakuwa rais? baada ya JKN?
 
LOL!! naona umetumia fatuma sasa!

Nilisema mnamwonea huyu naona umekubali!-Mtu pekee ambaye angelichukua AD na kubadilika na wangestahili hukumu ni Sokoine au Kawawa,

Wala hakujiangaisha kusoma na kukariri kanuni zenu, alichukua nchi na ku-assume ndiyo anaanza!! LOL!

Hivi nani ana clue kwa nini Kawawa hakuwa rais? baada ya JKN?

Wabz,

Wacha uchro yakhe, ilikuwa lazima Rais atoke visiwani ati!

On Mzee Mwinyi, what he has given is a careful calculation to help CCM retake and claim ownership to Azimio. Itrully believe he has seen the signs on the wall and after his work with CCM probe team on Mvurugano Bungeni, he has realized he will be better off to wash his hands like Pontius Pilate!

He never senteced or signed the death Warrant of Azimio la Arusha, he left the fate of Azimio in vague state!

Sasa kelele za kutaka Azimio lirudi likianzia na mambo ya maadili humu ndani ya CCM, halafu kina Kishoka, Mwanakijiji na Sikonge wanadai tulitazame Azimio jipya hasa katika kuujenga Uchumi upya, kwa nini watu wasishikwe na UHARO?

Mzee wa watu feels betrayed and in midst of confusion, he declares "Mimi si msaliti, mimi sikuwamo, mimi simo, ni wale, ni mchwa" Leo ukimwambia akutajie hata mchwa mmoja atakuambia hajui hata mmoja! then alijuaje kuna mchwa? aliwaona, walimng'ata?

Kama kuna Wanasiasa Wazanzibar ambao wana walakin, huyu Mzee hachelewi kushika usukano na kuwa nambari wani. heri angejikalia tuli kama Mzee mapengo Idrisa Abdul Wakil!
 
...

Sasa turudi katika kitabu cha Mtei. Katika ukurasa wa 149, yeye aliamua kuwaalika weledi wa IMF wakiongozwa na Bo Karlstrom ili washirikiane na weledi wa Wizara ya Fedha kubuni program ya kufufua uchumi. Anasema katika jopo lao, IMF walikuwa tayari kutoa mkopo wa kufufua uchumi lakini kwa masharti matatu. Mtei ameyaorodhesha hayo masharti kuwa ni; Mosi, kushusha thamani ya shilingi, pili, kuleta wawekezaji kutoka nje ya nchi, na tatu, serikali iache kusaidia kifedha mashirika ya umma na viwanda, na badala yake iyabinafsishe. Anatoa mfano wa benki ya taifa ya biashara NBC, kuwa ilikuwa ni kubwa mno iliyotishia usalama wake yenyewe.

Kyoma asante kwa summary hii: Kama ningekuwa Nyerere pia ningeona ugumu wa kukubali mapendekezo hayo. China hadi leo wanagombana na Wamarekani katika suala la kudevalue hela yao!

Mtei alirudi kumueleza Bo Karlstrom kuwa Nyerere ameyakataa masharti. Bo Karlstrom akamwambia Mtei kuwa ebu niwezeshe nionane naye hana kwa hana nitamlainisha na atayakubali. Tarehe 29 November 1979 alimkutanisha na Nyerere Msasani. Baada ya maongezi, Nyerere alimwambia Mtei kuwa awaambie warudi zao Washington kwani yeye hawezi kuruhusu nchi yake iendeshwe kwa amri kutoka Washington (Washington consensus).

Leo hii sijui hii nchi inaendeshwa na consensus ya nani tena.
 
Hata wakubwa pia wanaweza kujifunza kutoka kwa wadogo.


Wadogo wenyewe ni hawa ambao wanaweza hata kuiba fedha kutoka kwenye benki kuu yao wenyewe kwa ajili tu ya kutafuta ushindi kwenye uchaguzi. Give me a break! Nani atakubali kujifunza kutoka kwa watu kama sisi - wizi mtupu!

Tukubali tu kwamba sisi vichwa vyetu vimejaa ugali na si ubongo na hatuwezi katu kuelewa lipi ni jema kwa manufaa ya umma. Tuko tayari kulibadili lile lililo jema kwa manufaa ya umma liwe 'jema' kwa manufaa binafsi ya viongozi na wateule wachache.

Mwalimu JKN kichwa chake kilijaa ubongo hakuna lolote ambalo limo kwenye Azimio la Arusha ambalo si valid leo katika nchi yetu hii yenye asilimia 80 ya watu maskini na iliyojaa wawekezaji feki wanaohujumu uchumi wa nchi. Kuna wenzetu wanaojidai wao ni wasomi lakini kuna mambo madogo sana ya muhimu katika maendeleo na ustawi wa jamii yetu yanawapiga chenga. Ningekuwa Rais wa nchi hii leo ningelirejesha Azimio la Arusha in full force - kwa manufaa ya umma!
 
mi nadhani kuna swali la maana hapa la kujiuliza hasa tulikurudi kwenye hii mada,

hivi ilikuwa je Mwinyi akasimama na kulizungumzia Azimio la Arusha muda huu?

jibu ambalo halina shaka ndani yake ni kuwa kuna mambo ambAyo Azimio la Arusha (Nyerere) iliyaona na ambayo ni msingi mkuu wa UTU NA UBINADAMU, WALIYAONDOA (MWINYI at el), lakini sasa hali ya wananchi na hata usalama wa nchi unaelekea kuwashinda hata wao wenyewe, maana inafikia point nchi inashikwa na watu wachache ambao wanakuwa juu ya hata ya Rais,
Na baada ya kutafakuli kwa muda mrefu mzee Mwinyi akaona haya yote yametokea kwa sababu ya kuifuta hiyo miiko ya uongozi+Azimio la Arusha, ANACHOPIGANIA SASA NI KUJITOA KWAMBA SI YEYE ALIYEYASABABISHA HAYA NA WALA SI YEYE ALIYEUA MIIKO YA UONGOZI NA PIA SI YEYE ALIYEUA AZIMIO LA ARUSHA
 
Wakuu zangu,

Kwanza kabisa shukran sana kwa elimu mliyoitoa hadi hapa tulipofikia na ningependa tu kuweka vitu vichache sawa.

Azimio la Arusha ama Maazimio mengineyo yote ni mfumo halisia ya kila mrengo wa chama cha kisiasa. Nikiwa na maana ndani ya chama cha CCM, mrengo wa chama hicho kilikuwa na wanaendelea kudai kwamba ni Ujamaa na Kujitegemea. Hili ndilo lilikuwa Azimio lao kimsingi na ndilo lililotunga sheria nyingi ambazo wao CCM wenyewe walikuja zitengua..Hivyo hivyo hata Ukitazama nchi za magharibi vyama vimekuwa vikiitwa Progressive, Demokratic, Republican wana Maazimio yanayotofautina kimsingi na yanatambulika wazi kama tunavyosoma msahafu na Biblia..

Nitarudia kuyasema haya kwamba wenzetu vyama vya Siasa ni kama dini na madhehebu yake. Pamoja na kwamba lengo kuu la kila dini ni kumcha mwenyezi Mungu na kupata uzima wa milele... kila dini ina imani na ibada zake tofauti na dini ama dhehebu jingine lakini wote wakiamini kwamba njia yao ndio mbadala ktk kumcha mwenyezi Mungu na kuupata huo UZIMA wa milele ambao kisiasa kulingana na mada hii tutauita sustainable economy.. Ndivyo ilivyo ama inatakiwa kuwa ktk siasa..ilitakiwa vyama vyetu viwe na Imani na ibada zake tofauti ambazo wanachama wake wataziamini na kuzifuata kwama njia bora na pekee ya kufikia Maendeleo ya nchi, hivyo kuwa na Azimio la kupata huo uzima wa milele.

Hivyo basi hapakuwa na ubaya wowote wakati ule wa chama (dini) kimoja CCM, kuwa na Azimio ama maazimio ya Kijamaa. Tatizo ni pale tulipounda vyama vingi tukaendelea kuwa na imani moja, hapa tumeshindwa kuelewa kwa nini tuliunda vyama isipokuwa ni ushindani kama wa mpira wa miguu..

Ruksa ya sisi kuamini mirengo mingine tofauti na Ujamaa na kujitegema ilipotoshwa zaidi kwa sababu vyama vyetu hadi leo havina tofauti ya Kiimani wala kiibada na hicho chama CCM.. Tofauti ni watu ama Uongozi ndio hatukubaliani na ndio imekuwa tofauti ya CCM, Chadema CUF na vyama vinginevyo.vyama vyote vinatofautiana kama madhehebu ndani ya dini moja...Na ndio maana hadi leo kundi kubwa la wananchi Tanzania wana amini hatuwezi kwenda mbele kufika peponi pasipo siasa ya Ujamaa na Kujitegemea..

Hivyo kimsingi, lawama zote kama zipo tujiwekee sisi wenyewe na sii Mwalimu wala Mwinyi..Hao CCM bado wanaamini kuwa wao wanafuata siasa ya Ujamaa na Kujitegemea hali kiibada wanafanya kufuru kubwa tu.. Imani hiyo imebadikia ktk misahafu yao na ajabu ni kwamba sisi wote haopa bado tunazungumzia Ujamaa na Kujitegema kana kwamba imani hiyo ni ya KITAIFA...Jambo ambalo sii kweli kabisa. Chadema wanatakiwa kuwa na maazimio yao, CUF, NCCR, na vyama vingine vyote vinatakiwa kutofautiana na CCM kimrengo yaani maazimio yao ili kuleta maendeleo nchini yawe tofauti ya hayo ya CCM.. Badala yake tunachoona hapa nchi ni unazi na ushabiki wa Yanga na Simba kuwa ndio msingi wa siasa za Kitanzania..

Vyama vyetu bado vinamefuata maazimio ya CCM na ushindani sasa hivi ni UONGOZI yaani watu gani bora kutuongoza na sii mrengo wenye Maazimio tunayoyakubali kuwa msingi wa maendeleo yetu. ..Cha ajabu ni kwamba sisi hata baada ya kuwa na vyama vingi bado dira ya CCM imeendelea kuwa dira ya Kitaifa na sii ya chama hicho na yawezekana kabisa imani hiyo imetokana na kutawaliwa na CCM kwa muda mrefu..

Hivyo wakuu zangu msibeze Azimio la Arusha hata kidogo ikiwa hamfahamu sababu ama maudhui ya kuwepo kwake. Azimio ndilo huzaa mwongo, sera, ilani ya chama na hata kufuatia miswada bungeni ambayo huwa sheria ya nchi..Bahati mbaya tu tumemwona Kikwete na CCM wakiweka Maazimio ya Maisha bora kwa kila Mtanzania wakasahu kuifanya ni ibada, na matokeo yake ndio haya tunayoyaona leo..

Ashanteni.....
 
Kinachotakiwa kwa serikali ni kusimamia majukumu yake ya kuongoza nchi ikiwa ni pamoja na uweka mazingira mazuri ya kustawi kwa uchumi wa nchi, hii ni kazi ya serikali. Kwa hiyo kazi ya serikali si kufanya UCHUUZI kama ilivyokuwa ikifanywa hapo awali. Hata huko umarekani serikali haifanyi UCHUUZI inahokifanya ni kutimiza wajibu kama msimamizi wa sera za ustawi wa uchumi.

Sijui kama unajua unalosema; serikali inamiliki kampuni ya Posta, inamiliki kampeni ya Reli (Amtrak), inamiliki kampuni ya Bima (FDIC), na ina miliki kampuni nyingine mbalimbali kama GM, Chrysler na hata kutoa fedha kuendesha mabenki binafsi yaliyoanzishwa na watu binafsi. Na siyo hivyo tu, kampuni imetaifisha mabenki kadhaa ambayo yalikuwa yanafeli na kuteua uongozi wake wa juu! Serikali ya marekani inafanya uchuuzi!
Hapa Mzee Mkjj huna hoja ya nguvu, hivi sasa Tanzania kuna wafanyibiashara wa kuku wangapi ukilinganisha na wakati huo? Je, wanapata wapi vifaranga? Kampuni ya kuku haikuwa na umuhimu wowote wa kumilikiwa na serikali. Serikali ilitakiwa kuwekeza katika vituo vya utafiti wa kuku na wanyama wengine na sio kufanya biashara.

Sasa kwa nini serikali ifanye utafiti huo na siyo watu binafsi?

Vituo vya utafiti ndiyo vingetumika kutoa ushauri wa jinsi ya wafugaji wanaweza kuwekeza katika biashara ya kutotoa vifaranga, ubora wa chakula cha kuku, matibabu, nk. Resources muhimu ya kufanya mambo hayo zilipotezwa kwa kuanzisha na kuiendesha kampuni hiyo. Tukubali wazo halikuwa sahihi.

Sasa, bila taasisi ya mfano utatoa ushauri kutoka wapi? Serikali ina vyuo vya Kilimo vinavyofanya utafiti na humo humo kuna taasisi za mifano zinazoendeshwa kibiashara. Sasa unataka hata hilo lisiwepo? Huwezi kuindoa serikali moja kwa moja katika kufanya biashara iwe kwa sababu ya nature ya biashara yenyewe au sababu ya unyeti wake.





Kama nilivyoeleza kazi za serikali sikuchuuza bali ni kubuni na kusimamia utekelezajiwa sera za kustawisha uchumi ambazo wananchi watazituma/watafaidika nazo katika kujiletea maendeleo yao. Kwa hiyo katika issue ya GM/ Chrysler/mabenki serikali ya umarekani ilichokifanya kutimiza kazi yake ya usimamizi (regulator mkuu wa uchumi) na wala si vinginevyo.

Ni wazi kwamba hujui Obama alichofanya; serikali ya Marekani imenunua hisa kwenye makampuni hayo, imesimamia uongozi wake na kuuteua, na licha ya kuwapa uhuru wote, bado GM na Chrysler zinasimamiwa kwa karibu na wamiliki wake (ambao mmoja wao ni serikali ya Marekani!). Serikali haikuishia kwenye usimamizi tu.

Hazina ya Marekani na ile ya Canada nao ni wamiliki; to remind you Marekani na Canada ni nchi za Kibepari!

Hali kama hiyo inaweza ikamkuta mtu yeyote yule anayefanya biashara pale ambapo biashara yake haiendi vizuri basi anaweza kuteuliwa maneja wa kuisimamia kampuni yako kwa maslahi ya wale wenye interest kwenye biashara yako kama vile wanahisa au wadogo au creditors.

siyo hivyo serikali ya Marekani na Canada zina umiliki wa GM.

Juu ya Fannie Mae na Fred Mac, haya makampuni yameanzishwa kwa malengo maalum na yana mfumo wa uendeshaji wa private mbali ya kwamba ni ya serikali.

Kwa hiyo serikali inaweza kumiliiki makampuni na kuyaendesha kibinafsi lakini chini pia ya usimamizi wa serikalki hiyo hiyo. Ni kampuni gani isiyoanzishwa kwa malengo maalum? Kuna tofauti gani kubwa kati ya Freddi, Mac na NHC au Benki ya Nyumba ya Tanzania?


Mfumo kama huo ndiyo ambao umeanzishwa Tanzania - TASAF ambapo in the long run iwe inajiendesha yenyewe kama partner wa jamii. Kwa hiyo makampuni ya Sallie Mae na Fannie Mae hayapo kwa malengo ya kufanya biashara.

Whaaat! yanafanya biashara tena biashara kubwa tu. Usidhanie yapo kwa ajili ya charity.


Swali lako linajibika kwa swali hili
Nipe mfumo ambao serikali inafanya UCHUUZI karibu katika kila jambo kuanzia Viatu, Nguo, Vyakula, Kuku, Ng'ombe, Maziwa, list ni ndefu

Sasa hili ndilo linajadilika; tulipoanza wakati wa Uhuru ni nani alikuwa na mtaji mkubwa wa kuwekeza katika sekta hizo zote isipokuwa kikundi cha watu wachache. Yaani, ulitaka kuanzia ardhi, miradi yote iishie kufanywa na kikundi cha watu wachache? Serikali ilichofanya kupitia AA ni kujaribu kutengeneza uwiano wa nafasi za kufanikiwa na kuwapa Watanzania ambao wengi wakati ule walikuwa hawana elimu ya kutosha nafasi ya kuweza kufanikiwa. Hata haya mafanikio ambayo tunayaona leo hii yametokana na nafasi hiyo iliyowekwa na Azimio.

Vinginevyo, leo tungekuwa na issues za ardhi kama za Zimbabwe (ambazo naamini kwa kadiri CCM inaendelea na sera yake mbovu tutafikia) ambapo kiasi kikubwa cha ardhi kiliwekwa mikononi mwa watu wachache huku ubepari ukitakiwa uendelee tu. Leo hii hata Afrika ya Kusini haijakubali kuuachilia ubepari ufanye upendavyo maana wanajua kabisa kwa kufanya hivyo waliokuwa nacho wataongezewa na wasio nacho wataendelea kuombea wawe nacho.

Wewe ungeamua kugombea ubunge leo hii ningekunyima kura yangu.

Bahati nzuri, sina fikra hizo hasa kama watu wenye kuwaongoza wana mawazo ya kwako; nisingethubutu kuomba kura kwako.

Nchi ilikuwa na makampuni ya serikali takribani 400 na mengi yao yanategemea ruzuku ya serikali ambayo inatokana na pesa za walipa kodi wa nchi nyingine, wanaokupa hizo pesa za kulipa mishahara ya walimu na polisi wanakuambia kuwa hatuwezi kubeba mzigo wa hasara zinazopatikana katika makampuni yako, wewe utaendelea kuwaambia kuwa nipeni tu?

Hapana unatakiwa kutumia ubongo wako na kujiuliza "nifanye nini" kukimbilia kuuza tu ni woga usiio na msingi. Busara ilitakiwa watu wakae chini (kama walivyofanya wenzenu kwenye nchi tajiri) na kusema ni makampuni yapi tuyauze, makampuni gani tubadilishe modeli ya uendeshaji wake, makampuni gani tuyaconsolidate n.k Hatukufanya juhudi zozote za kuboresha au kuokoa mashirika yetu, kwa woga wa kina Mwinyi wakaamua kuweka manyanga chini.

Busara unayoisema wewe ndiyo hiyo ambayo serikali ya Mwinyi na Mkapa iliifanya ya kuyarekebisha mashirika hayo kupitia Tume ya Rais ya Kurekebisha Mashirika ya Umma, ambapo yale yaliyokuwa mzigo na hayawezekani kurekebishwa yalipigwa chini ikiwemo Kampuni ya Kuku. Na mengine yaliuzwa. Na huo ndiyo ulikuwa uamuzi sahihi.

Bahati mbaya hawakurekebisha mashirika walikubali tu kuwa ni bora kuyauza au kuyaacha yafe wakijua kuwa wao watapata nafasi ya kuyaanzisha au kuyanunua kwa bei chee. Hawakufanya juhudi ya kuyaokoa. Leo hii wameshindwa mara mbili sasa kwenye TRL na bado wanazungumzia "kutafuta mwekezaji" yaani katika vichwa vyoa wao wanaamini wawekezaji ndio watu pekee wenye uwezo wa kuendesha mashirika yetu. Hii siyo hekima ni upumbavu.



Kwa kumalizia serikali haitakiwi kufanya biashara isipokuwa inatakiwa kutengeneza mazingira muafaka kwa akina Ruge na Kusaga waweze kuwa wabunifu, Bakhresa na Gulam Dewji waweze kutumia uzoefu wao, Profesa J, Jide na Mwana FA waweze kutumia vipaji vyao, list ni ndefu inaendelea...

Umeshakubali hapo juu kuwa kuna wakati serikali inatakiwa kufanya biashara and as a matter of fact karibu dunia nzima serikali zinafanya biashara. Jambo la msingi ni jinsi gani, namna gani, na kwa modeli gani serikali naweza kufanya biashara gani. Huwezi kukwepa serikali kufanya biashara. Hakuna nchi yoyote duniani ambayo serikali yake haifanyi biashara kabisa. NONE.
 
All in All Maazimio yote yanazungumzia CCM...!!!wakati tulipokuwa na mfumo wa chama Kimoja...!!!

Sasa ni mfumo wa Vyama Vingi ambapo vitu vingi tunahitaji kurekebisha..!!!

Mbona Mali zilizochumwa wakati wa Chama Kimoja hazirejeshwa serikalini...!!!

Wa-TZ tuamke...Tuache kuwafanya baadhi ya watu Miungu...!!! Tunapong'ang'ani Azimio la Arusha...as if serikali iendelee kupora Mali za Watu...!!! na Tuseme Turudi ktk Chama Kimoja...!!!

By the way nawapongeza Wakatoliki kuanzisha Bank yao. hii itapunguza msongamano ktk Bank zilizopo na itaongeza ushindani wa Bank zinavyoshindwa kuwasaidia wananchi wake... tahadhari tunatoa WAISLAM wakianzisha ya kwao...wasije wengine kusema nchi inataka kusilimishwa!!!

Tunachohitaji maisha bora kwa Kila mtanzania, barabara zetu mbovu..watu hatuna nyumba bora...haya mabenki yaje suluhuhisho la kuwasaidia kweli watz.
 
Wadogo wenyewe ni hawa ambao wanaweza hata kuiba fedha kutoka kwenye benki kuu yao wenyewe kwa ajili tu ya kutafuta ushindi kwenye uchaguzi. Give me a break! Nani atakubali kujifunza kutoka kwa watu kama sisi - wizi mtupu!

Tukubali tu kwamba sisi vichwa vyetu vimejaa ugali na si ubongo na hatuwezi katu kuelewa lipi ni jema kwa manufaa ya umma. Tuko tayari kulibadili lile lililo jema kwa manufaa ya umma liwe 'jema' kwa manufaa binafsi ya viongozi na wateule wachache.

Mwalimu JKN kichwa chake kilijaa ubongo hakuna lolote ambalo limo kwenye Azimio la Arusha ambalo si valid leo katika nchi yetu hii yenye asilimia 80 ya watu maskini na iliyojaa wawekezaji feki wanaohujumu uchumi wa nchi. Kuna wenzetu wanaojidai wao ni wasomi lakini kuna mambo madogo sana ya muhimu katika maendeleo na ustawi wa jamii yetu yanawapiga chenga. Ningekuwa Rais wa nchi hii leo ningelirejesha Azimio la Arusha in full force - kwa manufaa ya umma!

Utalirejesha in full force na kulitelekeza kwa namna gani, kama sheria?
 
Mzee Mwanakijiji;857634]Sijui kama unajua unalosema; serikali inamiliki kampuni ya Posta, inamiliki kampeni ya Reli (Amtrak), inamiliki kampuni ya Bima (FDIC), na ina miliki kampuni nyingine mbalimbali kama GM, Chrysler na hata kutoa fedha kuendesha mabenki binafsi yaliyoanzishwa na watu binafsi. Na siyo hivyo tu, kampuni imetaifisha mabenki kadhaa ambayo yalikuwa yanafeli na kuteua uongozi wake wa juu! Serikali ya marekani inafanya uchuuzi!

Nafikiri unashindwa kuelewa nini lengo la serikali ya Marekani katika hayo makampuni uliyoyataja. Serikali inachokifanya ni ku regulate economy na wala si kuyandesha na kuyaikili mashirika hayo kama tulivyokuwa tunafanya sisi. Ni muhimu kuelewa hilo. Kilichotokea Marekani kinaweza kufanywa na Serikali yetu kunapotokea matatizo kama yalivyotokea Marekani lakini yote inategemea na uwezo wa kifedha wa serikali husika. Kwa mfano katika nyakati tofauti serikali imeweza kuingilia uendeshaji wa mabenki yaliyokuwa na matatizo kama vile GreenLand, Meriadian-Biao na ile bank ambayo ilibadilishwa kuwa Azania Bancorp. Uingiliaji wa shughuli hizo ni mahsusi kwa ajili ya kuprotect au regulate economy only na si uingiliaji wa kudumu

Sasa kwa nini serikali ifanye utafiti huo na siyo watu binafsi?

Mara nyingi researches hutumia fedha na si biashara ya uhakika kwamba utaweza kupata faida kama zinavyofanyika biashara zingine. Traditionally researches huwa funded na maeneo fulani kama vile serikali, Mashirika ya Kimataifa, nk. Kwa hiyo si rahisi kwa wafanyibiashara kufanya kazi hizo kwa sababu nilizozieleza hapo. Serikali inawajibu wa kuaandaa mazingira mazuri ya kukua kwa uchumi ikiwemo ku-fund researches ambazo zitatumika katika kuendeleza biashara na mambo mengi yanayohusiana na sekta hiyo.

Sasa, bila taasisi ya mfano utatoa ushauri kutoka wapi? Serikali ina vyuo vya Kilimo vinavyofanya utafiti na humo humo kuna taasisi za mifano zinazoendeshwa kibiashara. Sasa unataka hata hilo lisiwepo? Huwezi kuindoa serikali moja kwa moja katika kufanya biashara iwe kwa sababu ya nature ya biashara yenyewe au sababu ya unyeti wake.

Ndiyo maana nilisema kuwa kama wewe utataka kuwa mwakilishi wangu kwa jambo kama vile mbunge sintokupa kura yangu kwa sababu mawazo yako ya kuwa na taasisi za mfano kama Kampuni ya Kuku siyakubali kwani hayana tija na yanatumia resources muhimu za walipa kodi ambazo zingekwenda kwa wanataaluma kufanya tafiti mbalimbali juu ya kuku.






Ni wazi kwamba hujui Obama alichofanya; serikali ya Marekani imenunua hisa kwenye makampuni hayo, imesimamia uongozi wake na kuuteua, na licha ya kuwapa uhuru wote, bado GM na Chrysler zinasimamiwa kwa karibu na wamiliki wake (ambao mmoja wao ni serikali ya Marekani!). Serikali haikuishia kwenye usimamizi tu.

Hazina ya Marekani na ile ya Canada nao ni wamiliki; to remind you Marekani na Canada ni nchi za Kibepari!

The do it kwa sababu ni kazi ya serikali kusimamia policies zote iwe za uchumi, afya, viwanda, ulinzi, nk. Serikali ya Marekani inaweza kuchukua hatua hizo katika ku-regulate uchumi wa nchi yake kwa namna ambayo wanaweza, nayo kuwa na fedha ya kuweza kufanya hayo. Kama huna fedha huwezi kuiga wanayofanya Marekani, fedha yetu ya kufanya mambo kama hayo ndiyo hiyo tunategemea kulipana mishahara na kana kwamba haitoshi inabidi tupewe msaada wa kulipa mishahara hiyo kutoka kwa donors. Kwa mtaji huo huwezi kufanya yale ambayo nchi tajiri kama Marekani inayafanya.


siyo hivyo serikali ya Marekani na Canada zina umiliki wa GM.



Kwa hiyo serikali inaweza kumiliiki makampuni na kuyaendesha kibinafsi lakini chini pia ya usimamizi wa serikalki hiyo hiyo. Ni kampuni gani isiyoanzishwa kwa malengo maalum? Kuna tofauti gani kubwa kati ya Freddi, Mac na NHC au Benki ya Nyumba ya Tanzania?


Tofauti kubwa ni kwamba hayo makampuni ya Marekani yanaendeshwa kwa ufanisi wakati hayo ya kwetu yamekuwa yakiendeshwa bila ya ufanisi wa kuridhisha, hatimaye benki kama THB ikayeyuka na NHC kujikita kuwa shirika la Upangishaji Nyumba.




Whaaat! yanafanya biashara tena biashara kubwa tu. Usidhanie yapo kwa ajili ya charity.

Primarily si mashirika ya kibiashara na ndiyo maana surplus zake zinakwenda kwenye foundation zinazozisimamia kwa ajili ya re-investment.




Sasa hili ndilo linajadilika; tulipoanza wakati wa Uhuru ni nani alikuwa na mtaji mkubwa wa kuwekeza katika sekta hizo zote isipokuwa kikundi cha watu wachache. Yaani, ulitaka kuanzia ardhi, miradi yote iishie kufanywa na kikundi cha watu wachache? Serikali ilichofanya kupitia AA ni kujaribu kutengeneza uwiano wa nafasi za kufanikiwa na kuwapa Watanzania ambao wengi wakati ule walikuwa hawana elimu ya kutosha nafasi ya kuweza kufanikiwa. Hata haya mafanikio ambayo tunayaona leo hii yametokana na nafasi hiyo iliyowekwa na Azimio.

Samahani, mawazo yako hayaleti maana yeyote, unadhani kulima shamba la kijiji watu 100 ndiyo kupata tija? Uchumi unatufundishaje juu ya Marginal Returns and Marginal Cost? Nchi yetu ili iendelee kiuchumi na kuwa na uchumi imara tunahitaji wafanyibiashara wakubwa wachache tu na with time wafanyibiashara wadogo na wakati wangejijenga kutokana na mazingira mazuri ya kufanya biashara na shughuli zingine. I don't believe serikali ilitakiwa kumiliki njia kuu za uchumi kwa maana ya kuzuia private participation katika nyanja hiyo. Haikuwa sahihi kwa serikali kuchukua mabenki, makampuni ya bima, na mengine kama hayo kwani hapo ndipo tulipoharibu.

Vinginevyo, leo tungekuwa na issues za ardhi kama za Zimbabwe (ambazo naamini kwa kadiri CCM inaendelea na sera yake mbovu tutafikia) ambapo kiasi kikubwa cha ardhi kiliwekwa mikononi mwa watu wachache huku ubepari ukitakiwa uendelee tu. Leo hii hata Afrika ya Kusini haijakubali kuuachilia ubepari ufanye upendavyo maana wanajua kabisa kwa kufanya hivyo waliokuwa nacho wataongezewa na wasio nacho wataendelea kuombea wawe nacho.

Kama nilivyosema hapo awali serikali ilitakiwa kubuni mikakati ya kweli ya kustawisha uchumi lakini badala ilileta mikakati ambayo haikuwa sustainable na ndiyo maana leo hii tumerudi nyuma kuanza pale ambapo 1966/67 tulipochepukia. Laiti kama serikali ingekuwa inaelewa kuwa uchumi ni muhimu kumilikiwa na wananchi hata kama ingechukua miaka 30 baada ya uhuru lakini tungestawi kwa kuwa wazalishaji zaidi na watanzania wengi wangekuwa wanashiriki katika kuendesha uchumi wa nchi yao leo hii. Hayo mambo ya kusema kuwa tungekuwa na matatizo ni mambo ya kijinga na woga usiokuwa na maana kwa kukwepa kuwajibika katika mambo ya kweli na yenye manufaa kwa nchi na wananchi. Kujenga uchumi imara hakuna short cut.


Bahati nzuri, sina fikra hizo hasa kama watu wenye kuwaongoza wana mawazo ya kwako; nisingethubutu kuomba kura kwako.

Ni kweli maana ungejaribu tu usingepata kitu kwa maana ungezidi kuturudisha nyuma na hatimaye ukishindwa unaangukia kwenye rushwa kama short cut kujenga wealth badala ya kuweka sera makini za kukuza uchumi


Hapana unatakiwa kutumia ubongo wako na kujiuliza "nifanye nini" kukimbilia kuuza tu ni woga usiio na msingi. Busara ilitakiwa watu wakae chini (kama walivyofanya wenzenu kwenye nchi tajiri) na kusema ni makampuni yapi tuyauze, makampuni gani tubadilishe modeli ya uendeshaji wake, makampuni gani tuyaconsolidate n.k Hatukufanya juhudi zozote za kuboresha au kuokoa mashirika yetu, kwa woga wa kina Mwinyi wakaamua kuweka manyanga chini.

Huhitaji kusema unatumia ubongo tu pia unaangalia facts zilizopo mbele yako. Serikali imekuwa ikiruzuku almost mashirika yote kwa gharama za walipa kodi na fedha za wafadhili. Wafadhili wanakuambia hatukupi tena pesa ya kufidia hasara ya mashirika yako, at the same time huna pesa ya kutosha ya kulipa mishahara ya wafanyakazi wa serikali, kweli bado utang'ang'ana? Unless you dumb!!!! Uamuzi wa kurekebisha mashirika haukuweza kuepukika kwani kwa namna yeyote ile mashirika mengine yalikuwa ni lazima yafe yanataka hayataki (wapi KAMATA? wapi NAFCO? wapi Kampuni ya Baiskeli NABCO? wapi Kampuni ya Vyombo vya Nyumbani HOSCO? Dartex? Natex? na utitiri wa makampuni ya kama hayo ambayo hayakuwa na ulazima wowote)


Bahati mbaya hawakurekebisha mashirika walikubali tu kuwa ni bora kuyauza au kuyaacha yafe wakijua kuwa wao watapata nafasi ya kuyaanzisha au kuyanunua kwa bei chee. Hawakufanya juhudi ya kuyaokoa. Leo hii wameshindwa mara mbili sasa kwenye TRL na bado wanazungumzia "kutafuta mwekezaji" yaani katika vichwa vyoa wao wanaamini wawekezaji ndio watu pekee wenye uwezo wa kuendesha mashirika yetu. Hii siyo hekima ni upumbavu.

Si kupingi katika serikali kumiliki shirika kama la reli, lakini hata hivyo ni vema serikali ikaweka nafasi yake wazi katika mustakabali wa kudumu wa shirika kama hilo na ma mengineyo ya mawasiliano. Uzoefu duniani kote unaonesha kuwa Mashirika ya mawasiliano si muhimu tu kwa malengo ya kiuchumi pekee bali pia kiusalama. Kwa hiyo serikali labda ingechukua upande wa kuwa na hisa nyingi si lazima majority na kutengeneza mgawanyo mwingine wa hisa nyingi kwa induvidual private owner na zinazobaki kwa public. Lakini hata hivyo hayo yote yanawezekana endapo tu mashirika hayo yatakuwa profitable kwani hisa zake zitauzwa kwa mujibu wa sheria.





Umeshakubali hapo juu kuwa kuna wakati serikali inatakiwa kufanya biashara and as a matter of fact karibu dunia nzima serikali zinafanya biashara. Jambo la msingi ni jinsi gani, namna gani, na kwa modeli gani serikali naweza kufanya biashara gani. Huwezi kukwepa serikali kufanya biashara. Hakuna nchi yoyote duniani ambayo serikali yake haifanyi biashara kabisa.

That's how you think, lakini ninakurudisha nyuma kuwa serikali ndiyo msimamizi wa policies zote ziwe za uchumi, ulinzi, elimu, maji, kilimo, nk. Kwa hiyo serikali ina kazi zake nazo ni ku-regulate mambo haya. Sasa unapoona wana regulate uchumi ukatafsiri ni lazima wafanye biashara, basi huo ni mtazamo wako unahitaji mjadala mwingine.
 
Nafikiri unashindwa kuelewa nini lengo la serikali ya Marekani katika hayo makampuni uliyoyataja. Serikali inachokifanya ni ku regulate economy na wala si kuyandesha na kuyaikili mashirika hayo kama tulivyokuwa tunafanya sisi. Ni muhimu kuelewa hilo. Kilichotokea Marekani kinaweza kufanywa na Serikali yetu kunapotokea matatizo kama yalivyotokea Marekani lakini yote inategemea na uwezo wa kifedha wa serikali husika. Kwa mfano katika nyakati tofauti serikali imeweza kuingilia uendeshaji wa mabenki yaliyokuwa na matatizo kama vile GreenLand, Meriadian-Biao na ile bank ambayo ilibadilishwa kuwa Azania Bancorp. Uingiliaji wa shughuli hizo ni mahsusi kwa ajili ya kuprotect au regulate economy only na si uingiliaji wa kudumu

Sasa ndugu yangu wewe unataka kubishi for the sake of kubisha. Amtrak ni kampuni ya biashara huduma yake ni usafiri; FDIC ni shirika la bima na huduma yake ni bima; Freddie Mac na Fannie zinahusiana na kutoa mikopo ya nyumba nafuu. Haya yote ni makampuni ya serikali yanafanya BIASHARA. Na serikali hiyo ni ya kibepari ya Marekani. Sasa sijui ni kipi hapa kigumu kuelewa kuwa serikali inaweza kufanya biashara?


Serikali inawajibu wa kuaandaa mazingira mazuri ya kukua kwa uchumi ikiwemo ku-fund researches ambazo zitatumika katika kuendeleza biashara na mambo mengi yanayohusiana na sekta hiyo.

Serikali inapata wapi wajibu huu ambao private sector haiwezi? Yote ya research unayoyasema yanaweza kufanywa (na yanafanywa) vile vile na private sector. Kwanini serikali ifanye research ambayo ingeweza kuacha ifanywe na private sector? Unless.. utasema kuwa there are some instances when the state has some certain interests to protect.



Ndiyo maana nilisema kuwa kama wewe utataka kuwa mwakilishi wangu kwa jambo kama vile mbunge sintokupa kura yangu kwa sababu mawazo yako ya kuwa na taasisi za mfano kama Kampuni ya Kuku siyakubali kwani hayana tija na yanatumia resources muhimu za walipa kodi ambazo zingekwenda kwa wanataaluma kufanya tafiti mbalimbali juu ya kuku.

Uwe unaelewa basi; Sisemi kwamba leo tuwe na makampuni ya kuku au mbuzi ya serikali. Ninachosema ni kuwa kuna wakati serikali yaweza kuendesha makampuni kwa ajili ya kutengeneza mazingira fulani bora ya kibiashara. At the time kulikuwa na ulazima wa kuwa na makampuni fulani ambayo baadaye ulazima huo haukuwepo tena. Lakini huwezi kuondoa haja na ulazima wa serikali kushiriki biashara hasa kama kwa kufanya hivyo kunalinda maslahi makubwa ya jamii nzima. Ukilielewa hili hutapata shida sana.




The do it kwa sababu ni kazi ya serikali kusimamia policies zote iwe za uchumi, afya, viwanda, ulinzi, nk. Serikali ya Marekani inaweza kuchukua hatua hizo katika ku-regulate uchumi wa nchi yake kwa namna ambayo wanaweza, nayo kuwa na fedha ya kuweza kufanya hayo. Kama huna fedha huwezi kuiga wanayofanya Marekani, fedha yetu ya kufanya mambo kama hayo ndiyo hiyo tunategemea kulipana mishahara na kana kwamba haitoshi inabidi tupewe msaada wa kulipa mishahara hiyo kutoka kwa donors. Kwa mtaji huo huwezi kufanya yale ambayo nchi tajiri kama Marekani inayafanya.

Sasa kama hili ni kweli, uchumi wetu binafsi unaweza vipi kuhimili kuachiwa kufanya mambo yote wakati hauna uwezo kama wa Marekani? Kuna mambo ambayo tulipopata uhuru tusingeweza kuyaacha sekta binafsi iyafanye, haikuwa na uwezo huo na ni serikali tu ndiyo ilikuwa na uwezo.



Tofauti kubwa ni kwamba hayo makampuni ya Marekani yanaendeshwa kwa ufanisi wakati hayo ya kwetu yamekuwa yakiendeshwa bila ya ufanisi wa kuridhisha, hatimaye benki kama THB ikayeyuka na NHC kujikita kuwa shirika la Upangishaji Nyumba.

Sasa hiki unachosema ndicho kiini. Tatizo lako ni kuwa makampuni yetu yalikuwa hayaendeshwi kwa ufanisi kwani kama yangekuwa yanaendeshwa kwa ufanisi nina uhakika usingekuwa na tatizo nayo. Kumbe tatizo siyo umiliki per se bali ni ufanisi. So if this is true (which I totally presume it to be), basi wenye akili hawakimbilii kuuza tu mashirika au kuyaua wanajiuliza how can we run them efficiently. So, tungeenda kujifunza Wamarekani, Wachina, Waingereza wanaendesha vipi makampuni ya serikali kwa ufanisi katika mazingira ya ushindani binafsi wa kibiashara. Na kutoka hapo na sisi tunafanya hivyo.

Kina Mwinyi, Mkapa na sasa Kikwete hawana fikra za kutafuta ufanisi; wao tatizo ni hili ulilokuwa nalo mwanzoni yaani umiliki. Kumbe jibu siyo kubadilisha umiliki (linaweza kuwa sehemu ya jibu) lakini jibu liko kwenye ufanisi.

Primarily si mashirika ya kibiashara na ndiyo maana surplus zake zinakwenda kwenye foundation zinazozisimamia kwa ajili ya re-investment.

the functional word here is "primarily".


Samahani, mawazo yako hayaleti maana yeyote, unadhani kulima shamba la kijiji watu 100 ndiyo kupata tija? Uchumi unatufundishaje juu ya Marginal Returns and Marginal Cost? Nchi yetu ili iendelee kiuchumi na kuwa na uchumi imara tunahitaji wafanyibiashara wakubwa wachache tu na with time wafanyibiashara wadogo na wakati wangejijenga kutokana na mazingira mazuri ya kufanya biashara na shughuli zingine.

you see.. ukiruhusu hilo utadevelop monopolies, na hakuna nchi ya kibepari ambayo imekubali kuachilia monopolies zikue. Halafu si kweli kwamba tunahitaji "wafanyabiashara wakubwa wachache" yaani hao wafanyabiashara wamiliki vitu gani? Mwisho utataka hao wafanyabishara wakubwa wachache ambao watakuwa na uwezo mkubwa watamiliki sehemu kubwa ya uchumi.

Matokeo yake utataka tuwe na watu wengine wakiwa watumishi wa hawa wengine.. hii ni mentality ya kurudisha ukoloni kwani ni katika ukoloni ndipo wafanyabishara wakubwa walikuwepo huku mamilioni ya wananchi wakiwa pembezoni mwa uchumi wao.

I don't believe serikali ilitakiwa kumiliki njia kuu za uchumi kwa maana ya kuzuia private participation katika nyanja hiyo. Haikuwa sahihi kwa serikali kuchukua mabenki, makampuni ya bima, na mengine kama hayo kwani hapo ndipo tulipoharibu.

Tatizo lako sijui kama hujui historia au hutaki kukiri historia ilivyokuwepo. As a new nation we could not have left mabenki, makampuni ya bima na mengineyo kuwa moja kwa moja mikononi mwa watu binafsi. Rudi nyuma uangalia ni mikopo gani ilitolewa na kwanini tangu uhuru 1961 hadi lilipotangazwa azimio (ambapo waliachiwa waendeshe makampuni hayo) matokeo yalikuwa ni mabaya kwa mamilioni ya watu wetu. Ilichofanya serikali ni kile ambacho kimefanywa majuzi na wengine nacho ni kuhakikisha kuwa taasisi hizo nyeti haziwezi kuendelea kufanya kazi bila uangalizi wa moja kwa moja wa serikali.

Binafsi naamin tatizo kubwa siyo kwa serikali kuyachukua, tatizo langu (na hata leo bado ni hilio hilo) serikali haikuwa na uwezo wa kuyaendesha kwa ufanisi kama tunavyoona hata leo hii. Hili linahusiana na model ya umiliki na uendeshaji wa makampuni hayo ya umma. Binafsi ningefanya tofauti more kwa style ya Obama, Uingereza n.k

Jambo jingine hata hivyo ni kuwa unataka kuacha impression kuwa hakukuwa na makampuni binafsi; yalikuwepo na mengine yame survive hadi leo hii.


Kama nilivyosema hapo awali serikali ilitakiwa kubuni mikakati ya kweli ya kustawisha uchumi lakini badala ilileta mikakati ambayo haikuwa sustainable na ndiyo maana leo hii tumerudi nyuma kuanza pale ambapo 1966/67 tulipochepukia.

Once again, you choose to ignore history. Matukio yote yale hayakutokea in a vaccuum. Hata leo hii sijui kama unataka kusema kuwa tunaendesha uchumi wetu vizuri zaidi compared to wakati ule au la? I would argue, no we are not.
Laiti kama serikali ingekuwa inaelewa kuwa uchumi ni muhimu kumilikiwa na wananchi hata kama ingechukua miaka 30 baada ya uhuru lakini tungestawi kwa kuwa wazalishaji zaidi na watanzania wengi wangekuwa wanashiriki katika kuendesha uchumi wa nchi yao leo hii.

This is not true; otherwise, Kenya ingekuwa mbali sana, Congo (zaire) ingekuwa mbali sana, Ghana ingekuwa mbali sana na hata Nigeria zingekuwa mbali sana! Nchi hizo zote hazikufuata Azimio la Arusha! Zilikuwa na sekta binafsi.. lakini zilifika wapi? Tatizo haliko kwenye sekta binafsi tu au la.

Hayo mambo ya kusema kuwa tungekuwa na matatizo ni mambo ya kijinga na woga usiokuwa na maana kwa kukwepa kuwajibika katika mambo ya kweli na yenye manufaa kwa nchi na wananchi. Kujenga uchumi imara hakuna short cut.

The way it sounds wewe unafikiri private sector ni panacea ya matatizo yetu. Kwamba tukiondoa umiliki wa serikali na kuruhusu sekta binafsi ifanye ipendavyo basi matatizo yetu yote yataondolewa. Si kweli.




Ni kweli maana ungejaribu tu usingepata kitu kwa maana ungezidi kuturudisha nyuma na hatimaye ukishindwa unaangukia kwenye rushwa kama short cut kujenga wealth badala ya kuweka sera makini za kukuza uchumi

Si kweli.. Mbona leo hatuna Azimio na Rushwa imekomaa; mbona Wamarekani hawana Azimio la Arusha na corruption ipo vile vile. Rushwa haihusiani hata kidogo na umiliki wa uchumi!



Huhitaji kusema unatumia ubongo tu pia unaangalia facts zilizopo mbele yako. Serikali imekuwa ikiruzuku almost mashirika yote kwa gharama za walipa kodi na fedha za wafadhili. Wafadhili wanakuambia hatukupi tena pesa ya kufidia hasara ya mashirika yako, at the same time huna pesa ya kutosha ya kulipa mishahara ya wafanyakazi wa serikali, kweli bado utang'ang'ana? Unless you dumb!!!!

Then.. serikali inatakiwa ifikirie jinsi gani iendeshe mashirika yapi na kwa namna gani. Serikali kutoa ruzuku siyo jambo geni duniani. I know utakubali nchi nyingine kufanya hivyo isipokuwa Tanzania. Tatizo ni mfumo wa uendeshaji wa makampuni hayo na aina ya makampuni ambayo ni kwa maslahi ya nchi kwa serikali kuyaendesha.

Uamuzi wa kurekebisha mashirika haukuweza kuepukika kwani kwa namna yeyote ile mashirika mengine yalikuwa ni lazima yafe yanataka hayataki (wapi KAMATA? wapi NAFCO? wapi Kampuni ya Baiskeli NABCO? wapi Kampuni ya Vyombo vya Nyumbani HOSCO? Dartex? Natex? na utitiri wa makampuni ya kama hayo ambayo hayakuwa na ulazima wowote)

Yalikuwa na ulazima wakati ule na labda hata sasa. Leo hii tunaagiza baskeli kutoka ng'ambo, tunaagiza vitu ambavyo zamani tulishaanza kuvitengeneza wenyewe. Badala ya kujaribu kuyabadiilsha mashirika yale kuyaingiza kwenye private sector tukaamua yafe. Kina Mwinyi hawakutumia Hekima; kina Mkapa hawakuta kufikiri. Kwao kushindwa ilikuwa ni rahisi zaidi kuliko kujaribu kushinda. Ndio maana kauli yangu ni kuwa uongozi mara zote ni uwezo.




Si kupingi katika serikali kumiliki shirika kama la reli, lakini hata hivyo ni vema serikali ikaweka nafasi yake wazi katika mustakabali wa kudumu wa shirika kama hilo na ma mengineyo ya mawasiliano. Uzoefu duniani kote unaonesha kuwa Mashirika ya mawasiliano si muhimu tu kwa malengo ya kiuchumi pekee bali pia kiusalama.

Lakini yanaendeshwa na serikali; kwani sekta binafsi haiwezi kusimamia mashirika ya usalama? Kwa hiyo, unakubaliana na mimi kuwa kuna wakati ambapo "uzoefu" unataka baadhi ya mashirika yamilikiwe na serikali! mashirika yanayofanya biashara kama Reli!

Kwa hiyo serikali labda ingechukua upande wa kuwa na hisa nyingi si lazima majority na kutengeneza mgawanyo mwingine wa hisa nyingi kwa induvidual private owner na zinazobaki kwa public. Lakini hata hivyo hayo yote yanawezekana endapo tu mashirika hayo yatakuwa profitable kwani hisa zake zitauzwa kwa mujibu wa sheria.

kati ya yote uliyosema hili uko na mimi pamoja. Tatizo siyo umiliki tatizo ni suala la efficiency. Na pale inapohusu umiliki swali kubwa ni jinsi gani tunaweza kutengeneza umiliki uliobora. Kwa mfano, kwanini serikali haikujaribu kutumia wazo hilo lako (which I absolutely and unconditionally claim to be mine too!) kuokoa:

Ubungo Farm Industries
TRL
Tanesco
Mwatex n.k?

Jibu ninalo: Hakukuwa na mtu aliyetaka kuyaokoa au kuyafanya makampuni hayo kuwa ya faida. It was to these individuals interest kuyaua ya kwetu ili wageni wapate nafasi. This has been their template for years now. Ndio maana wamefikia hata kubinafsisha kazi za Polisi!



That's how you think, lakini ninakurudisha nyuma kuwa serikali ndiyo msimamizi wa policies zote ziwe za uchumi, ulinzi, elimu, maji, kilimo, nk. Kwa hiyo serikali ina kazi zake nazo ni ku-regulate mambo haya. Sasa unapoona wana regulate uchumi ukatafsiri ni lazima wafanye biashara, basi huo ni mtazamo wako unahitaji mjadala mwingine.

Ninafahamu vizuri tofauti ya kuregulate na kuendesha kampuni. Nadhani wewe ndio hutaki kukubali kile ambacho unakiona na unakikubali (sehemu nyingine hapo juu).
 
Leo hii sijui hii nchi inaendeshwa na consensus ya nani tena.

Mzee Mwanakijiji! heshima mbele mkubwa wangu. Bado nchi yetu inaendeshwa kwa amri kutoka Washington. Umesahau malengo ya milenia na uchafu mwingine? si sera tu, kibaya zaidi, hata baadhi ya sheria zinazoendesha nchi zinatungwa kwa msukumo kutoka nje, na wananchi wanalazimishwa kuzikubali na kuzitii.

Si unakumbuka 2006/2007 Serikali ya Denmark kupitia kwa balozi wake Carsten Pedersen, ilisitisha msaada wa zaidi ya shilingi bilioni 3.16 kwa serikali ya Tanzania mpaka hapo serikali ya Tanzania ingepeleka Muswada wa rushwa Bungeni. Si unajua fedha (si msingi bali ni matokeo ya maendeleo). Hoops! Nimekosea, fedha ndiyo msingi wa maendeleo. Hivyo, Serikali ya Tanzania ilifyata mkia na kupeleka Muswada wa rushwa Bungeni.

Ni kipindi hicho hicho ambapo, Wabunge ambao ni (wawakilishi wa wananchi) Hoops! ambao ni wawakilishi wa vyama vya siasa, ambavyo ndivyo vinawakilisha wananchi, waliikaba koo Serikali iweke wazi mikataba ya madini ili angalau waisome tu. Si unajua ati kazi yao ni kuisimamia na kuiwajibisha Serikali kwa niaba ya nani tena? Serikali iliwakejeli na kusema mikataba ni siri. Mmmh! jambo usilolijua ni kama usiku wa giza. Sasa utasimamia na kuwajibisha wakati uko gizani? Wawakilishi wakitaka chochote wanatoka kapa, lakini Mzungu akitaka chochote kinafanyika.

Unakumbuka mkutano wa IMF uliofanyika Dar mwaka jana, ambapo kimwana wa CNN aliwauliza wajumbe wa mkutano walioamini kuwa amri kutoka Washington sasa basi. Rais Kikwete alinyoosha mkono, lakini Waziri wake wa Fedha, machale yalimcheza na kuuchuna (alijua ni usanii). Haya bana, swali la pili (kimwana naye..mmmh), sasa Rais Kikwete hutapokea tena amri kutoka Washington (Manake watoa amri wamevurunda uchumi wao), una mawazo/mikakati gani ya kuendesha nchi? Rais wetu alijibu kuwa ataendelea kufanya vilevile, yaani anavyofanyafanya, yaani yaani, si unajua tena kiaina?

Nawashangaa Wabongo wanaodai Rais wetu ni "kigulu na njia". Sasa afanye nini nchini wakati sera na sheria za kuendesha nchi zinasukumwa kutoka nje?

Alafu hawa "viongozi bora" kabla hatujawachagua wanasema ni "vichwa kweli kweli" yaani ni "moto" wa kuotea mbali kwa "mawazo na ubunifu" wao. Tena wengine tunawajua ni wajinga tu, lakini nasikia siku wanapochanguliwa/teuliwa kuwa "viongozi bora", basi akili, busara, PHD na nini tena... vyoote vinawaangukia papo kwa papo. Lakini wanapotakiwa kutuliza bori na kuchanga bongo zao hizo ili kubuni mbinu, sera, dira na mikakati kabambe ya kutukwamua, wanaona maluilui na kukimbilia Washington kwa akina IMF, WB, WTO na kadhalika, ati kuhemea.

Tukiwauliza mmeleta nini kutoka Washington? Hawasemi, ila tunaona watu wanahamishwa kutoka katika ardhi zao ili kuwapisha "wawekezaji". Yaani mambo yaleyale ya Abushiri. Tofauti ni kwamba Abushiri hakuwa na PHD. Pia Abushiri hakwenda Washington. Umesahau hivi majuzi, Rais Obama alimsifia Rais Kikwete kuwa anafanya kazi nzuri isiyo kifani, kama ambavyo Rais Reagan na Bush walivyomsifia Rais Mobutu kuwa ni mfano wa kuigwa Afrika. Si unajua Wamarekani hawana rafiki yakhe. Wana maslahi. Ukitaka fedha, watakupa. Ukitaka mabomu watakuvurumushia. Ukitaka misifa, watakumwagia kebekebe, ilimradi tu wametimiza haja yao.

Tuliambiwa kuwa mnaona! Obama kamsifia Kikwete, sasa wawekezaji watanyesha Tanzania kama mvua za masika. Hata hivyo, baada ya Kikwete kumpa kisogo tu Obama, Serikali ya Obama imetoa ripoti kwa Wamarekani na dunia nzima kuwa "aka ka nchi ka Tanzania kanakoongozwa na Kikwete kananuka rushwa". Hivi vilemba vya ukoka bwana! lakini vinalipa, si unajua wabongo kwa kubabaika. Juzi anti yangu ananipigia simu kuwa Kikwete na Obama pete na kidole. Na huu ni msimu wa uchaguzi. Na kale ka asilimia sabini ketu kanako fuata upepo, mmmh! yetu macho.

Anyway, Haya masharti ya IMF ambayo Bo Karlstrom alitaka kumuingiza mkenge Nyerere ni upuuzi mtupu. In fact, Rais Mwinyi aliyakubali yote na mengine ya ziada -kama cost-sharing katika elimu na afya. Walimpa dose ya kuvizika kabisa viwanda na mashirika ya umma, kuididimiza elimu na idara ya afya. Hiyo dose iliitwa SAPs - Structural Adjustment Programs.

Of course, hata kilaza anajua kuwa unaposhusha thamani ya shilingi wakati unaagiza malighafi na mafuta kutoka nje, unavizika viwanda, siyo unavifufua. Unapokata mipango ya elimu na kupunguza fedha za kununua vifaa vya mahabara, vitabu vya ziada na kiada, mishahara ya waalimu na kadhalika, unakuwa umewekeza katika bora elimu na siyo elimu bora. Matokeo yake, ama unakuwa na asilimia kubwa ya wanafunzi wanaopata zero, au unakuwa na idadi kubwa ya watu wasiojua kusoma wala kuandika.

Dira ya Azimio la Arusha inasema kuwa mtu anaweza kutetea haki zake bara-bara kama haki hizo anazijua, na anazijua sheria zinazomlinda kitaifa na kimataifa. Ndiyo maana ukatoka mkakati wa Msoma (Azimio la msoma)-Elimu kwa wote. Matunda yake yalionekana na matunda ya SAPs tunayaona leo.

Nasikia Obama anarudisha mikopo ya wanafunzi serikalini kutoka katika mabenki binafsi. Sasa Serikali itaimiliki kwa asilimia 100 na itapanua wigo wa kuwasomesha Wamarekani wasiyo na uwezo bure. Sisi tunaambiwa hatuwezi kuwasomesha watu wetu bure kwa sababu inabidi fedha inayopatikana baada ya kukusanya kodi iende kulipa madeni. tena madeni mengine tulikopa kutunza vyura vya Kihansi. Yaani watu wasiende shule ili vyura wapone.

Unakumbuka miaka ya 2000, nchi masikini zililalamika kuwa masharti ya SAPs yalizitia kilema cha maisha na kudai yaondolewe. Well, February 2003 na March 2005, nchi tajiri zilikutana na kupitisha maazimio ya Rome 2003 na Paris 2005 ili kupunguza makali ya masharti. Rais Mkapa alimtuma Kikwete (waziri wa mambo ya ndani-wakati ule) atuwakilishe. Hayo maazimio hayatekelezwi na bado wanaendeleza ubabe tu mpaka hapo tutakapo damka kutoka usingizini.

Azimio la Arusha ilikuwa dira, kama vile ngazi ambayo mtu anaweka ukutani ili imwezeshe kufika paani. Katika msukosuko wa upepo, anakuja Mzungu, tena yuko paani, anakwambia itupe hiyo nganzi nitakutupia kamba alafu nikuvute. Ukiiangalia ngazi unaona imebuniwa na mswahili mwenzako na kamba imebuniwa na mzungu, tena yuko paani unapotaka kwenda. Unaitupilia mbali hiyo ngazi na kubakia kubembea kwenye kamba. Mzungu anavuta kidogo alafu anaiachia unadondoka puu!. Anakwambia kabla ujaishika tena kamba, nitupie hilo embe, unamtupia, nitupie Hindi la kuchoma, unamtupia na yeye anakula. Na hivi ndivyo wanavyotufanya. Nasi tunashangilia Hoyeeeee!
😎
 
Azimio la Arusha ilikuwa dira, kama vile ngazi ambayo mtu anaweka ukutani ili imwezeshe kufika paani. Katika msukosuko wa upepo, anakuja Mzungu, tena yuko paani, anakwambia itupe hiyo nganzi nitakutupia kamba alafu nikuvute. Ukiiangalia ngazi unaona imebuniwa na mswahili mwenzako na kamba imebuniwa na mzungu, tena yuko paani unapotaka kwenda. Unaitupilia mbali hiyo ngazi na kubakia kubembea kwenye kamba. Mzungu anavuta kidogo alafu anaiachia unadondoka puu!. Anakwambia kabla ujaishika tena kamba, nitupie hilo embe, unamtupia, nitupie Hindi la kuchoma, unamtupia na yeye anakula. Na hivi ndivyo wanavyotufanya. Nasi tunashangilia Hoyeeeee!
😎

Kyoma.. tatizo letu hatuna watu wetu wenye msimamo unaotakana na kufikiria; what I have noticed as of late ni kuwa kuna kizazi kipya cha wasomi ambao wanaangalia falsafa ya azimio na wanajua kwa nini waliobahatika kupewa nafasi ya kulitekeleza. Hawakuwa na uwezo wa kina wa kuelewa kile ambacho umeksima hapo juu. Walifikiria azimio ni mwisho. Kwamba tumeshatangaza sasa tuanze kuvuna. Hawakulichuklia kama dira jinsi ambavyo Mwalimu alilichukulia.
 
Bw. Kyoma maelezo yako ni sawia kabisa.

Hizi SAPs za IMF na WB tulizikurukupukia tu lakini waliozileta walikuwa na malengo yao, na sasa tunayaona matunda. Serikali imepoteza ushawishi ktk rasilimali zake kwa kasi ya kutisha, kwa kisingizio cha uwekezaji. Wasiwasi wangu ni kuwa baada ya muda wa miaka 40-50 sijui tutakuwa tumebakiwa na kitu gani!

Azimio la Arusha ilikuwa dira, kama vile ngazi ambayo mtu anaweka ukutani ili imwezeshe kufika paani. Katika msukosuko wa upepo, anakuja Mzungu, tena yuko paani, anakwambia itupe hiyo nganzi nitakutupia kamba alafu nikuvute. Ukiiangalia ngazi unaona imebuniwa na mswahili mwenzako na kamba imebuniwa na mzungu, tena yuko paani unapotaka kwenda. Unaitupilia mbali hiyo ngazi na kubakia kubembea kwenye kamba. Mzungu anavuta kidogo alafu anaiachia unadondoka puu!. Anakwambia kabla ujaishika tena kamba, nitupie hilo embe, unamtupia, nitupie Hindi la kuchoma, unamtupia na yeye anakula. Na hivi ndivyo wanavyotufanya. Nasi tunashangilia Hoyeeeee!

Nimependa hapa ulivomalizia..
 
hakuna kitakacholiondoa Azimio la Arusha katika mioyo ya wapenda Tanzania na rasilimali zake
 
Anyway, Haya masharti ya IMF ambayo Bo Karlstrom alitaka kumuingiza mkenge Nyerere ni upuuzi mtupu. In fact, Rais Mwinyi aliyakubali yote na mengine ya ziada -kama cost-sharing katika elimu na afya. Walimpa dose ya kuvizika kabisa viwanda na mashirika ya umma, kuididimiza elimu na idara ya afya. Hiyo dose iliitwa SAPs - Structural Adjustment Programs.


!
😎

Mkuu umenena vyema kuhusu u-dira wa Azimio na kuwa lilidharauliwa simply kwa sababu ni product yetu 'siyo ya ulaya'

Lets then discuss in this way, lets assume Nyerere angeendelea mpaka 1995, na hakutaka kufuata mipango ya IMF au WB unafikiri nchi yetu ingeendelea kwa kiasi gani , na toa sababu ya jibu lako. You can take example in Kenya.

Angalia nchi ilipokuwa at that time mwaka 1985 AND reflect hali hiyo mpaka 1995 tungekuwa mbele au nyuma kwa kiasi gani.

any one may help on this
 
Lets then discuss in this way, lets assume Nyerere angeendelea mpaka 1995, na hakutaka kufuata mipango ya IMF au WB unafikiri nchi yetu ingeendelea kwa kiasi gani , na toa sababu ya jibu lako. You can take example in Kenya. Angalia nchi ilipokuwa at that time mwaka 1985 AND reflect hali hiyo mpaka 1995 tungekuwa mbele au nyuma kwa kiasi gani. any one may help on this

Mzee Waberoya. heshima yako mkuu. Haswa! haya ndiyo maswali ya kujadili na siyo hotuba ya Mwinyi inayoitwa Azimio la Zanzibar. Azimio la Zanzibar liko Washington, ndiyo maana hatujawahi kuliona, na wala hatujawahi kuuliza liko wapi zaidi ya kushabikia tu kana kwamba ni Simba na Yanga. Zanzibar walikaa kuangalia jinsi ambavyo wangetumia mianya ya masharti ya IMF kutunga sheria mpya ili wajinufaishe binafsi kutokana na mali iliyokuwa ikimilikiwa na umma.

Naomba unipe siku mbili nimalize project zangu alafu nikujibu. Si unajua mshika mbili?. Nitakujibu kwa mifano hai kwa sababu iko tele. Kitakacho nirahisishia mjadala huu baina yangu na wewe ni ukweli usiopingika kuwa Azimio la Arusha siyo dini. Ni sayansi ya jamii ya kufikiri. Kama zilivyo sayansi nyingine za mwili wa binadamu, uchumi, siasa, fizikia, hisabati na kadhalika. Hizi Sayansi zote ni rahisi kudhibitisha kwa hoja na mifano. Kama ambavyo wanasayansi wanachukuwa dutu au utovu wa zambarau (Litmus), ambao hugeuka rangi ya samawati (blue) katika asidi na nyekundu katika alkali. Isipobadilika, basi tunasema kuna kasoro.

Dini ni imani. Kama hakuna imani hakuna dini. Ndiyo maana mijadala ya dini huwa naihepuka kwa sababu mwisho wake ni matusi na maswumbwi. Kwa sababu hakuna dini unayoweza kuichovya katika tindikali ikabadilika rangi na kuwa samawati, basi tukasema hii ndiyo itakupeleka mbinguni. Na hakuna mwanadamu wa kawaida aliyewahi kufa na akarudi kutuambia ni dini gani haitambuliwi na Mungu. Kwa hiyo inabidi tuamini tu. Atakaye kushika mbonini unamtwanga ngumi.

Kwa sababu Azimio la Arusha ni dira iliyojengwa kwa sayansi ya kufikiri, sitarajii tushikane mashati katika mjadala huu. Ngoja nitoe mfano mmoja ili uone nitakapo kujibu nitaanzia wapi. Mfano; dila ya Azimio la Arusha inasisitiza kujitegemea (na sijuhi wanaokataa kujitegemea wanataka nini). Kuna mambo mengi hapo, labda leo nitaje elimu. Ili kujitegemea na kuwa huru (siongelei uhuru wa bendera), lazima watu wetu wote wapate elimu bila ubaguzi na upendeleo wowote. Hivi ndivyo dila inavyosema.

Sasa tufanye je? Ndipo jopo la weledi lilipoangalia mazingira halisi na hali za watu wetu, na kubuni mikakati ya kuhakikisha kila raia anapata elimu. Wengine walikwisha kuzidi umri wa kwenda shule. Hao ni kisomo cha watu wazima. Kuna vizingiti gani vinavyoweza kuwazuia watu wetu au vitu vitakavyowawezasha watu wetu kupata elimu bora. Wakavitaja. 1. Umande-ikatungwa sheria kali ya waogopa umande. 2. Ada-Serikali kwa kukusanya kodi ikawalipia wanafunzi wote kuanzia chekechea mpaka chuo kikuu. Pia ikatungwa sera na sheria ya kuhimiza hilo.

3. Lishe bora kukuza ubongo wa mwanafunzi - Kodi ya wananchi ndiyo ilitumika kuwalisha wanafunzi wote mashuleni. 4. Nauli na fedha za kujikimu na kula njiani- Kodi iliwasafirisha wanafunzi kutoka Karagwe to Dar na kadhalika. 5. Waalimu, vifaa vya Mahabara, vifaa vya elimu ya kujitegemea kama vyerehani, vitabu na dispensari zenye madawa za huduma ya kwanza mashuleni na kadhalika. 6. Mila na destuli za kuwazuia watoto wa kike wasiende shule, ikatungwa sera na sheria.

Haya yote na mengineyo yalifanyika kuanzia miaka ya 1970 mpaka kufifia kwake, na pengine kufa kabisa miaka ya 1990, ambapo SAPs ilianza kukolea. Nikirudi nitakutajia katika kilimo, viwanda na uchumi kwa ujumla. Nitazitaja sheria muhimu zilizotungwa kutokana na Azimio la Arusha (si sheria zote zilizohusu Azimio la Arusha-mfano za wakuu wa wilaya kuweka watu jela ulikuwa ni ujinga wa Nyerere. Hazina mahusiano yoyote na Azimio la Arusha). Pia nitazitaja sheria muhimu zilizotungwa kwa maelekezo ya IMF ili kuvunja zile zilizotokana na dila ya Azimio la Arusha. Baada ya hapo ndipo tutaangalia, kama tungeendelea na mtindo huo tungekuwa wapi hivi sasa.

Naonya (ha haaa!) usije ukaniletea mambo ya Sembe ya njano na foleni na viatu vya matairi na takataka nyingine sijuhi nini tena ambalo ni tunda la madhara ya vita ya kagera, ukame na kupanda kwa bei ya mafuta. Hakuna mfumo wowote duniani ambao haupati msukosuko. Vita ya Kagera tuliigaramia kwa fedha yetu iliyotokana na viwanda vyetu vichanga (si jasema ilikuwa halali au la). Waangalie wamarekani na utajiri wao, walipigana vita ya Iraq kwa mkopo, deni la taifa limewafika pomoni na uchumi wao ulianguka, sembuse sisi?

Tulikula Sembe? si afadhali sisi tulikula Sembe. Umesoma kuhusu Great Depression? watu walikufa kwa utapia mlo, hawakuwa na mahala pa kulala, wengine walijiua kutokana na hasara waliyoipata. Waliishi hivyo miaka nenda rudi mpaka wakajitoa katika kipindi kigumu. Hawakukimbia mtikisiko na kutupa dira yao ya taifa. Watu huwa hawakimbii matatizo. Huyakabili kwa kuchanga bongo siyo kuazima bongo. Ndiyo maana hizi ngonjera huwa sitaki kuzisikia. Kwa hiyo mzee, vuta subira, nitarudi na majibu yenye mifano hai, kwa sababu hii ni sayansi siyo dini.
 
Refer my question again na nasubiri jibu mkuu Kyoma, kumbuka unayemjibu ni muumini wa AD.
 
Mwinyi hawezi kukwepa lawama, chini yake walilizika Azimio

Lula wa Ndali-Mwananzela
Machi 24, 2010


RAIS wa Pili wa Jamhuri yetu, Mzee Ali Hassan Mwinyi hawezi kamwe kukwepa lawama ya maziko yasiyo na swala ya Azimio la Arusha kule Zanzibar.

Hawezi, leo hii, kutuambia kuwa walioliua azimio hilo walikuwa wengine wakati yeye ndiye aliyekuwa Rais na Amiri Jeshi Mkuu. Kama vile Mkapa asivyoweza kukwepa lawama ya ufisadi mkubwa uliofanyika chini ya utawala wak,e na Rais Kikwete asivyoweza kukwepa lawama ya yale yanayotokea chini yake.

Kama vile Mwalimu Nyerere anavyobebeshwa lawama ya yale yaliyotokea chini yake, vivyo hivyo na hawa wengine wawe tayari kukubali makosa yao.


Kwanini Azimio la Zanzibar lilibadilisha Azimio la Arusha?

Baada ya minong'ono kuwa hatimaye Azimio la Arusha limezikwa Zanzibar, Rais Mwinyi alizungumza na wazee wa Jiji la Dar es Salam, Februari 25, 1991, kuelezea kile kilichojiri kwenye kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa kilichofanyika Zanzibar.


Katika maelezo yake, jambo la kwanza Mzee Mwinyi aliwahakikishia wananchi kuwa "kuna hofu kwamba Azimio la Arusha linageuzwa. Kwa hiyo, tokea mwanzo, kabla ya kusema lolote, nataka tuelewane kwamba siasa yetu bado ni ile ile ya Ujamaa na Kujitegemea. Haikugeuka, wala hatutazamii kuigeuza.

"Kwa hali yoyote, sisi wanachama wa Chama Cha Mapinduzi hatutaigeuza siasa hii. Kule Zanzibar tulizungumza mambo mengi, miongoni mwao, ni kutoa tafsiri ya baadhi ya vipengele vya Azimio ili vifanane na wakati tulionao."


Hivyo ndivyo alivyosema Mzee Mwinyi hiyo Februari 25, 1991. Kwa hiyo, kwanza kabisa, Mzee Mwinyi alituhakikishia kuwa nchi yetu bado ni ya Kijamaa na sera yake ni Kujitegemea. Na akaahidi kabisa kuwa siasa yetu hiyo haijageuka na wala "hatutazamii kuigeuka".

Hili ni jambo muhimu kulielewa kwani miezi michache tu iliyopita tumewasikia watawala wa leo wakiiruka Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea huku wakidai kile kile kilichodaiwa na Mzee Mwinyi kwamba ni wakati wa "kwenda na wakati".


Mzee Mwinyi akaelezea hilo kwa kusema kuwa "Ndugu Wazee, Msahafu wa Waislam unasema ‘LIKULLI AJALIN KITABU". Mwingereza mmoja kaitafsiri aya hiyo hivi: '
TO EVERY AGE ITS BOOK" yaani "Kila zama ina Kitabu (Mwongo) chake".

"Na sisi Wana-CCM tunakubali kuwa "kila Zama zinahitaji kuwa na Mwongozo wake". Azimio la Arusha ni Mwongozo wetu wa msingi. Ni dira inayoongoza mwelekeo wa jamii yetu. Lakini tafsiri zake zinabidi zirekebishwe kila inapohitajika ili zisipitwe na wakati. Miongozo ina tabia moja: inakuja ili kufafanua, kuelekeza au kukemea hali mbaya inayojitokeza."


Kwa hiyo, hadi mkutano ule wa Zanzibar CCM waliendelea kudai kuwa Azimio ndiyo mwongozo wa msingi na kwamba kinachohitajika ni tafsiri. Sasa angalau tunaweza kumpa pongezi Mzee Mwinyi kwa kujaribu kutafuta tafsiri mpya ya Azimio kulingana na mazingira ya wakati ule.


Lakini alipoingia Mkapa yeye hakutaka kuangalia Azimio kama dira na kujaribu kutafuta tafsiri mpya na vile vile hata Kikwete naye hajaliangalia Azimio na kuona tafsiri yake.

Tafsiri ya Azimio si lazima ilikane Azimio hilo?

Mojawapo ya mambo ya msingi ambayo watu wanahitaji kuyajua ni kuwa kutafuta tafsiri ya Azimio siyo lazima kukana Azimio hilo. Wakati mwingine ile misingi ya Azimio ndiyo tunahitaji kuirudia zaidi na wakati wa Mzee Mwinyi walichokifanya siyo kutafsiri upya Azimio; bali kuvunja vunja misingi ya Azimio hilo.

Japo wakati anazungumza na wazee wale hatukujua ukali na kina cha uvunjifu huo wa misingi ya taifa, leo hii tukiangalia nyuma tunaweza kuona pasipo shaka jinsi gani misingi hiyo iliporomoshwa.

Tuangalie baadhi ya mapendekezo ya Azimio la Zanzibar na kuona kama inaendana na misingi ya Azimio la Arusha.


1: Azimio lilitaka tujitegemee:


Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere akizungumza miezi michache baada ya Azimio la Arusha kutangazwa alielezea ifuatavyo juu ya dhana ya kujitegemea:

"Kumbe kujitegemea maana yake nini basi, na kutaleta matatizo gani katika siasa yetu ya siku za baadaye? Kwanza kabisa kujitegemea maana yake ni kwamba hatuna budi kujitegemea sisi na amali yetu wenyewe katika kuleta maendeleo. Amali hizo ni ardhi, na watu."

Akaendelea kusema: "Kujitegemea maana yake siyo kujitenga, ama katika mambo ya uchumi, ama katika mambo ya siasa. Maana yake ni kwamba tutajitegemea wenyewe, hatutawategemea watu wengine".


Sasa kule Zanzibar Mzee Mwinyi alitambua tatizo ambalo bado hatukufanikiwa kulishughulikia. Alielezea hivi "Wakati Azimio la Arusha lilitutaka tujitegemee, hali halisi ni kuwa tumekuwa wategemezi wakubwa. Maana Taifa letu hivi sasa, kwa pato lake lenyewe la fedha za ndani, linaweza kujitegemea kwa kipindi cha miezi saba tu katika mwaka.


"Tunategemea watu wengine, kwa njia ya ruzuku na mikopo, kumalizia miezi mitano inayosalia katika mwaka. Hii ni hatari. Lazima tuendelee kubuni mbinu za kuondokana na hali hiyo."


Kwa hiyo, tunaona kuwa lengo la Azimio la Zanzibar ilikuwa ni kurudisha Taifa kwenye kujitegemea? Je lilifanikiwa hivyo?


Leo hii tuna ushahidi usio kifani wa fikra tegemezi zilivyozama kiasi kwamba Rais wa Jamhuri yetu, Jakaya Kikwete anatembea duniani akiimba wimbo kuwa bila "wawekezaji hatuwezi kuendelea" na kuwa kwa namna fulani maendeleo yetu yanategemea hisani ya watu hawa wa nje.


Matokeo yake leo hii wenyewe tunajiita tumeendelea kwa sababu tunaweza kuagiza (siyo kuzalisha) vitu vingi kutoka ng'ambo. Tumefikia mahali hata matunda na vitunguu vinavyouzwa nchini vingine ni vya kutoka ng'ambo!


Ukifika kwa maduka ya kifahari sijui ni mangapi yanauza vitu vya ndani ya nchi yetu. Maofisi yetu (tena hasa ya Serikali) ni mangapi yanatumia samani zilizotengenezwa nchini? Mazulia, vitasa, hadi mapazia tunaona fahari ya kuwa tumenunua ng'ambo! Angalia vigae tunavyotumia kujengea na kupamba nyumba zetu!

Ukiondoa vitu kama vileo, sigara, na vitu vingine vichache vinavyozalishwa nchini, vitu vingi bado tunategemea kutoka ng'ambo! Ni kweli kuwa uchumi wetu ni tegemezi mno!


Binafsi ningependa kujua ni kiasi gani tunachozalisha ndani kinaliwa ndani ya nchi na kwa kiasi gani tunaweza kutosheleza mahitaji yetu. Kama wakati wa Mwinyi uwezo wetu wa ndani ulikuwa ni kuweza kujiendesha kwa miezi saba tu, ningependa kujua kama tukiondoa misaada yote ya kigeni ya moja kwa moja kwenye bajeti (direct budgetary support) tuna uwezo gani leo hii kuiendesha serikali yetu? Mara kadhaa sasa tumesikia Bunge likilazimika kupitisha "bajeti ya ziada"!

Walipolikataa Azimio la Arusha na msingi wa kujitegemea taifa letu likabakia la watu kujigemea na kuendeleza utegemezi hadi wa kifikra!


Lakini wao walilivunja Azimio. Waliamua kuificha ramani ya taifa letu na sasa wamebakia kusingizia kuwa "lilishindikana".
Miaka 20 kujenga nchi?

Mojawapo ya hoja za kipuuzi ni kuwa ati tulijaribu kujenga taifa kwa misingi ya Azimio lakini tulishindwa. Ukweli ni kwamba hatukujaribu!


Wengi wa wazee wetu walimtegemea Nyerere kifikra na kiushawishi hawakuwa waamini wa Azimio la Arusha. Wale wachache walioamini hawakuwa kwenye madaraka. Na ukweli wa haya tumeyaona baada ya wao kulizika Azimio kule Zanzibar; wale ambao walikuwa karibu na Mwalimu kumbe ndio mabepari wenyewe na ndio wanyonyaji wenyewe!

Tumejaribu kujenga taifa tulipoona ugumu tukakata tamaa! Hakukuwepo watetezi wa namna ya maisha yetu.


Leo hii wapo watu wanahusudu China ilivyopiga hatua wakati ni nchi ya Kikomunisti, ya chama kimoja na bado ina makampuni mengi tu ya serikali! Wamarekani hawailazimishi China kuwa nchi ya Kibepari (japo misingi ya ubepari inaota mizizi).

Lakini watu hawataki kukubali kuwa mabadiliko ya China yalichukua muda na yalikuwa na watetezi wake! Katika Tanzania hatuna watetezi kwa sababu tunaogopa kujitahidi!


Kina Mwinyi na wasaidizi wake badala ya kufanya mkutano wa kisomi na kiutendaji wa nini cha kufanya ili kutekeleza Azimio la Arusha, wakaamua kwa woga wao kuweka manyanga chini.

Kama vile Mkapa baadaye alivyoingia na suala la madini na sasa Kikwete kwenye nishati, wote hawataki kufanya maamuzi magumu na kuyasimamia. Wanataka rahisi rahisi!


Na sisi Watanzania ndio kabisa! Hatutaki kutoka jasho sana; hatutaki kupatwa na kazi ngumu na kufanya mambo ya maendeleo ambayo yanaweza hata kugharimu maisha yetu.

Mtu mmoja aliniuliza juzi kuhusu Azimio kuwa kwani "ilikuwa ni lazima watu wafe wakati wa Azimio"!? Mtu huyo nilimuuliza kama anajua kama Marekani ilipofikia hapa ni maelfu ya Wamarekani walikufa kujenga nchi yao?


Katika kuutetea Muungano wa Marekani, Abraham Lincoln aliamuru majeshi ya Kaskazini kupigana na ndugu zao wa Kusini waliotaka kujitenga. Zaidi ya Wamarekani laki sita walikufa katika vita ile ya wenyewe kwa wenyewe.

Leo hii watu wanashangaa Rwanda inavyopiga hatua pole pole lakini hawajui kuwa Rwanda imeonja uchungu wa kukaribia kupoteza kila kitu.


Sasa Tanzania tunaambiwa ati miaka 20 tumeshindwa! Mwinyi alizungumza kuwa ati hali ilikuwa ngumu sana tukashindwa kutetea Azimio. Miaka mingine karibu ishirini baadaye tuko bado na matatizo yale yale na hakuna kiongozi ambaye anaweza kutunyanyulia ramani ya taifa letu na kusema "jamani turudi tumepotea".

Nyerere alijaribu kuwakumbusha pale Uwanja wa Sokoine kuwa huwezi kuvunja misingi ya Taifa ukabakia salama. CCM wameivunja misingi hiyo na sasa hawana cha kushikilia.


Tukiwadokeza hili wanakuja juu; ati tunapandikiza mbegu za chuki. Kumbe kipo kizazi kipya cha Watanzania ambacho bado kinatambua na kukubali kuwa hatuwezi kujenga uwanja wetu bila kufuata ramani; hatuwezi kujenga nyumba yetu bila kufuata michoro ya ujenzi. Hatuwezi kujenga taifa letu bila kuangalia misingi ya taifa hilo. Vinginevyo tutabahatisha.

Nimalizie kwa maneno ya mwisho ya hotuba ya Baba wa Taifa pale Chuo Kikuu Mlimani, Agosti ile ya 1967. Maneno haya yabakie kuwa changamoto kwa kizazi kipya watetezi wa misingi ya taifa letu. Yawe kama maneno ya unabii ambayo yanarudi leo kama mwangi kutufikia kizazi cha karne ya 21. Nyerere alihitimisha kwa kusema:


"Kwa hiyo swali lenyewe la kuuliza ni: je, kama kila mmoja wetu yu tayari kuupokea wajibu wa kujenga nchi ambamo hakuna mtu anayeona aibu kwa sababu ya umaskini wake anaoulinganisha na utajiri wa mtu mwingine; wala hakuna anayeonea aibu pato lake kwa sababu ya umaskini wa mwingine? Je, tu tayari kujenga taifa ambamo kila mtu atamhesabu mwenzake kuwa sawa naye kabisa, katika moyo wa ushirikiano?

Kila mmoja wetu lazima alijibu swali hilo; lakini vijana wanaowajibu maalumu. Vile vile vijana wenye elimu wana vishawishi maalumu; maana katika nchi za kibepari hao ndio wangalikuwa mabwana kuwakandamiza wengine.


Naamini kwamba vijana wa Tanzania, waliosoma na wasiosoma, watakubali mzigo huo.

Kuubeba mzigo huo haitakuwa rahisi, wala haliwezi kuwa jambo la kupendeza kila siku. Ili kuumudu mzigo huo lazima vijana waelewe kabisa, wakubali shabaha na misingi ya zimio la Arusha, ili kusiweko kukata tamaa, na shida za kila mtu zisiwavunje moyo.

Lazima itambulike kwamba iko kazi ya kufanywa, kazi ambayo mara nyingi itakuwa ngumu, na ambayo inataka mtu aziweke kando starehe zake.

Lakini hatimaye kazi hiyo itakurudisha kwamba umetimiza wajibu wako katika kujenga taifa la Ujamaa kwa faida ya watoto wetu, na wajukuu wetu."


Laiti ningepata majina ya vijana waliokuwa Chuo Kikuu siku ile wakimsikiliza Mwalimu, ningewauliza wamefanya nini na mzigo waliobebeshwa? Maana wengine ndio waliokuwa wakiliaga kwa tabasamu Azimio wakati wanalizika kule Zanzibar!

Walishindwa kuufikisha mzigo kwa kizazi kingine. Sasa sisi wengine tumeamua kuubeba wenyewe!

Lidumu Azimio!
 
Back
Top Bottom