Siku za Shibuda ndani ya CHADEMA zahesabika

Siku za Shibuda ndani ya CHADEMA zahesabika

Shibuda anafahamika kuwa ni mmoja wa Makachero wa siku nyingi wa CCM na alitumwa pia kuja Maswa kummaliza aliykuwa Mbunge wetu Dr. Pius Ng'wandu Yasebasi.
CHADEMA wanatakiwa kuendelea kuandaa mtu makini wa kuja kurithi jimbo la Maswa Magharibi maana Shibuda muda wake umekwisha lazima atoswe mapema jamani.. Tunao wasomi kibao Maswa wanaokubalika na wenye maono ya kuleta maendeleo Maswa na si John Magale Shibuda ambaye hajafanya lolote ikilinganishwa na mambo Mazuri aliyotuachia Mzee wetu Dr. Pius Ng'wandu Yasebasi....
 
Naona unamwaga bongo flavor tu! Messi kakosea wapi? Amesema maneno ya mtu mzima Messi ana uwezo mkubwa kuliko hata katibu mkuu wako; ameongea kama mwanasiasa siyo katibu anachojua ni fitina; uwongo na majungu

Chama
Gongo la mboto DSM

ngoja mi nikujibu chama, kwa kazi aliyotumwa kuifanya imetulia. lakini kwa wanaojua kufuatilia move, washauelewa mchezo, na wewe jiunge kama yeye kusifia wanaume wenzio
 
Huhitaji kupanda hasira. NIMEKUULIZA UMEISOMA THREAD NZIMA AU HIYO POST YANGU MOJA? Naona hujanijibu hilo...sasa nikuulize tena mpinzani wa dhati anaweza kutamka haya?......"Nasikitika sana, CCM ni chama tajiri, chama cha kuigwa Afrika katika ukombozi, ni chama chenye falsafa nzuri na ni shamba darasa la kujisahihisha…lakini itakuwa ni aibu wakiacha utajiri huo ukikwapuliwa na mwewe," alisema. Na kwangu mimi hilo ndio kosa lake....kwako wewe si kosa

Kama huna majibu niache kwanza
Ninakujibu kwa swali sawa? Hivi Mbowe alipokuwa anampongeza kikwete alikuwa anamaanisha nini? Mpinzani au sio mpinzani?
 
Ninakujibu kwa swali sawa? Hivi Mbowe alipokuwa anampongeza kikwete alikuwa anamaanisha nini?

Kumpongeza kwa lipi na lini na wapi? Be specific na uelewe kuwa Mbowe sina mawasiliano naye na wala hanijui sasa kama alikwambia wewe kuwa amempongeza Kikwete basi utujuze sasa hivi
 
Ni kweli kabisa Shibuda ni mwanasiasa makini anastahili kabisa tuzo ya Ballon d'Or. Messi wa Chadema.

Hahahahaaa... Ritz na ndugu yako chama mna mtindio wa fikra. Kama shibuda ni sawa na messi mbona magamba mlimtosa? kwakuwa kwa vipimo vyenu vya akili duni mnamuona messi basi mchukueni bure hata sasahivi kama mnamhitaji mchukueni mnasubiri nini?
 
Last edited by a moderator:
Subiri bunge livunjwe kama hajarudi maswa kulima. Hata mbinu za kufanya alichotumwa CDM kufanya hamkumpa?

Ndiyo, atarudi mkulima kwa sababu hakutakuwa na wabunge tena nchini mpaka baada ya uchaguzi. Mavuno yake ya mchango wake wa ruzuku yatakuwa yamekisaidia chama kwa miaka mitano.

Hivi unaijua Maswa na nguvu ya shibuda jimboni. Fanya kwanza utafiti halafu njoo tena hapa janvini.
 

Kwa hiyo mtu kupewa mkono ndio kupongezwa?

Niambie hapa Nyerere alimpongeza Iddi AMINI vita ikiwa inanukia?

nyerere%2B%26%2BAmin.jpg


Na je huyu Mama gamba naye alimpongeza mnyika wakati kampeleka mahakamani?

juhm-mnyika1.jpg

 
Kwa hiyo mtu kupewa mkono ndio kupongezwa?

Niambie hapa Nyerere alimpongeza Iddi AMINI vita ikiwa inanukia?

nyerere%2B%26%2BAmin.jpg


Na je huyu Mama gamba naye alimpongeza mnyika wakati kampeleka mahakamani?

juhm-mnyika1.jpg

Subiri na icheck ile ya youtube nitakupatia sio mda mrefu.
 
mtoa thread anasimamia kwa kile yeye anachokiamini hata kama hakina mashiko
 
Upinzani si Ugomvi, ni kweli.. lakini Nyani hakingiwi meno, Unapoingia kwenye chama Pinzani, kuna madhaifu kadhaa wa kadha yaliyokufanya utoke chama x na kwenda chama z, na ilihali yale madhaifu yangalipo, huwezi leo ukasifia kile ulichokikimbia. tafsiri ya wazi hukupenda Kukikimbia, kama ni hivyo, kwanini usikirudie?.. ni Unafiki na usaliti kwa wananchi waliokupa kura wakidhani umeondoka chama kile kwa mapungufu unayofikiria sasa utayarekebeisha kwao lakini leo unakisifia kile walichokikataaa wananchi wako.. ni USALITI
 
Wanabodi
Mkutano mkuu wa CCM umemalizika kwa kishindo mjini Dodoma; katika mapitio ya hotuba nimeguswa sana na hotuba ya mgeni mualikwa mbunge wa Chadema mh. John Shibuda; hotuba yake imetoa hisia si kwa vyama vya upinzani tu hata kwa CCM yenyewe; Shibuda ameonyesha kukomaa kisiasa; hivi sasa kwenye medani za siasa za Chadema Shibuda anacheza kwa umahiri mkubwa kama mwanasoka Lionel Messi; wanabodi haya ndiyo maneno ya Shibuda


chama, acha kumdhalilisha Lionel Messi. Huwezi kumfaninisha mtu wa viwango kama Messi na huyo Chakubanga (Shibuda). Hana mbele wala nyuma zaidi ya kulamba miguu ya wanaume wengine ili mtari mkono uelekee kinywani. Tunza heshma ya Messi.
 
Back
Top Bottom