Siku za Shibuda ndani ya CHADEMA zahesabika

Siku za Shibuda ndani ya CHADEMA zahesabika

dosama

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2010
Posts
912
Reaction score
959
Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kimesema kimechoshwa na kauli tata za Shibuda na siku zake zinahesabika ndani ya chama.

Hayo yanesemwa kwa nyakati tofauti katika mikutano ya chama chao mikoani walipoulizwa na wanananchi. Kati ya walionyeshwa kuchoshwa na kauli za Shibuda ni Tundu Lissu na Mbowe

Source: Mtanzania
 
kalipwa ubwabwa na nyama tu kwa kazi ya upandikizi aliyopewa iliyomshinda kabla hajaianza..he is stuck in the middle!
 
shibuda ni gamba kuu alivuliki ni kama lile la kobe ukilivua nae anakufa ngoja alejee kwenye dini yake ya mafisadi
 
Yuko kikazi zaidi Chadema. Anaijua kazi yake ni ipi aliyotumwa kuifanya huko na atahama akiimaliza.
 
Shindwa Shibuda Shindwa..na uTOKE Chadema Tokaa..huna mamlaka ya kuvuruga,rudi kwa aliyekutuma..SHINDWA SHIBUDA
 
Yuko kikazi zaidi Chadema. Anaijua kazi yake ni ipi aliyotumwa kuifanya huko na atahama akiimaliza.

labda aende TLP ndo atafanya hiyo kazi aliyotumwa sio CHADEMA...
 
Nafikiri cdm.wasitumie nguvu sana kwa shibuda kwanza nikiweka pandikizi jimboni kwake.akiisha aishe moja kwa moja
 
Niliposoma heading nikajua Chadema wamemfukuza Shibuda kumbe maigizo tu...Chadema hawana ubavu wa kumfukuza Shibuda hata siku moja Shibuda ni Kamanda sio diwani wa Arusha utamfukuza kwa barua.
 
miaka 2 tu ameshatibua mambo namna hii, akiachwa miaka 3 iliyobaki si ndo ataharibu kabisa,
 
Source Mtanzania

Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kimesema kimechoshwa na kauli tata za Shibuda na siku zake zinahesabika ndani ya chama.

Hayo yanesemwa kwa nyakati tofauti katika mikutano ya chama chao mikoani walipoulizwa na wanananchi. Kati ya walionyeshwa kuchoshwa na kauli za Shibuda ni Tundu Lisu na Mbowe

Anazo tabia Kama za popo huyu mtu,bora aondolewe.
 
CHADEMA haina uwezo wa kumfukuza Shibuda.

Nakuuliza mleta mada, Mchagga anaweza kumfukuza anaemuingizia fedha? Maawee!
 
Source Mtanzania

Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kimesema kimechoshwa na kauli tata za Shibuda na siku zake zinahesabika ndani ya chama.

Hayo yanesemwa kwa nyakati tofauti katika mikutano ya chama chao mikoani walipoulizwa na wanananchi. Kati ya walionyeshwa kuchoshwa na kauli za Shibuda ni Tundu Lisu na Mbowe
you will never tired of democracy tundu acha kuchemsha
 
Nafikiri cdm.wasitumie nguvu sana kwa shibuda kwanza nikiweka pandikizi jimboni kwake.akiisha aishe moja kwa moja

Ni kweli inahitajika busara kidogo tu kummaliza huku kukiwa na matayarisho mbadala jimboni kwake, CDM wasisubiri 2015 bali wanachotakiwa ni kuanza kumpekecha taratiiiibu kote alikoshika ili akidondoka basi asinyanyuke tena, CCM kwenyewe hawamtaki kwani wanamjua alivyo kinyonga ndumila kuwili, Mwanzoni Shibuda alivyokuwa anahangaika akiwa ndani ya CCM kugombea nafasi mbalimbali na kuzikosa mie nilikuwa namhurumia sana kumbe ilikuwa haki yake,

Shibunda hana faida na chama wala wapiga kura wake bali yeye huwaza ntakunywa pombe na nani ndani ya chama au ntakunywa pombe na mpiga kura yupi na sio kuwazia matatizo ya wapiga kura wake na ndio maana akakomalia posho bungeni utafikiri kitu posho ni mama yake.
 
Avue GWANDA avae GAMBA! Maana ameamua kudandia meli inayozama.
 
Back
Top Bottom