Siku walipokwenda kwa mara ya kwanza gesti

Siku walipokwenda kwa mara ya kwanza gesti

NI SHIIDA!-11

ILIPOISHIA
"Abee mama! Shikamooo!"
"Sitaki shikamooo yako!"
"Niambie ulikuwa wapi?"
"Mama nisamehe nilikuwa..."

Kabla Juliana hajamalizia kujibu alishangaa kupigwa vibao mfululizo kutoka kwa mama yake.
"Usifikiri sijui chochote, najua kila kitu, niambie ukweli ni nani ulikuwa naye gesti..."
PAA NAYO SASA...

Kifupi ni kwamba, mama Juliana alimsikia mwanaume akizungumza lakini hakujua kama ni Bitungu, ila kilichomshangaza sana ni kubaini kumbe binti yake ameanza kuwa na uhusiano wa kimapenzi na wanaume.

"Mama nisamehe."
"Niko tayari kukusamehe, niambie ulikuwa na nani?"
"Nilikuwa na kijana mmoja hivi."
"Anaitwa nani? Hana jina?"
"Mama mi simjui jina lake."

"Wee, koma kama ulivyokoma kunyonya kwenye ziwa langu, uingie na mwanaume gesti halafu uwe humjui jina?"
Juliana aliamua kumdanganya mama yake akiamini si vizuri kumtaja jina Bitungu...
"Anaitwa Sylvester."
"Anaishi wapi?"
"Kigamboni."

"Mmeanza uhusiani tangu lini?"
"Siku ya tatu leo."
"Umeshalala naye mara ngapi?"
"Mara ya kwanza leo."
"Ina maana amekutoa usichana wako?"
"Hakuweza mama."

"Kwa sababu gani asiweze?"
"Hakuweza tu."
"Unataka nikukague?"
"Hapana mama."

"Sasa kwa nini unanidanganya?"
"Sikudanganyi mama."
"Kwanza hebu niambie, hiyo gesti iko wapi?"
"Ipo Sinza."
"Ipo Sinza? Ina maana wewe hapo muda huu unatokea Sinza?"
"Ndiyo mama."

"Sinza sehemu gani?"
"Mimi siyo mwenyeji sana wa Sinza mama," alijibu Juliana bila kujua kuwa, mama yake alitaka kujua Sinza sehemu gani kwa sababu na yeye alitoka huko muda si mrefu....
"Shekilango unapajua?"
"Ndiyo mama."

"Ukitoka Shekilango ni kituo cha ngapi?"
"Sikumbuki, nilikwenda na bodaboda."
"Hebu nenda ndani haraka sana. Usije ukarudia tena," alisema mama Juliana huku akiiseti simu yake vizuri ili kumtwangia Bitungu. Lakini huku akiwaza...

"Isije ikawa alikuwa na Bitungu! Halafu isijekuwa Bitungu ndiyo yule Bitu wa kwenye simu yake akasema ni Bitte alikosea kusevu? Huyu mtoto isije ikawa anatuchanganya mimi na mwanangu?
"Lakini haiwezekani. Kwa mechi tuliyoicheza leo pale kitandani sidhani kama angeweza kumudu mchezo mwingine tena."

Simu ya Bitungu ilipokelewa, mama Juliana akaanza kumuuliza maswali...
"Baby, wewe ni msaliti kwangu siyo?"
"Wala, kwa nini baby?"
"Huna mpenzi mwingine kweli wewe?"
"Wala! Nani amekwambia?"

"Sijaambiwa na mtu, nawaza mwenyewe tu."
"Ondoa hayo mawazo mpenzi, mimi ni wako peke yako."
"Kweli mpenzi wangu?"
"Kabisa mpenzi."

"Basi nimefurahi sana kusikia hivyo," alisema mama Bitungu na kukata simu. Roho yake ikawa imefarijika kwa siku hiyo.

***
Asubuhi ya siku iliyofuata, Juliana aliamka akiwa na wogawoga wa kuonana na mama yake ana kwa ana. Lakini alipokumbuka kuhusu ile hereni aliyoiona gesti akiwa na Bitungu ambayo ni moja kati ya hereni alizomnunulia mama yake, aliamua kuanza upelelezi wake hapo.

Kwanza alimvizia mama yake amekwenda kuoga, yeye akazama chumbani maana baba yake naye alishakwenda kazini mapema.

Alifungua kwenye kikopo ambacho mama yake anakitumia kuwekea hereni zake, hakuona hereni hata moja. Akaangalia juu ya dressing table, akaiona hereni moja tu, akatingisha kichwa huku akisema moyoni...

"Ile niliyoiona gesti hii mwenzake, kwa vyovyote vile. Ina maana mama ndiye mwanamke aliyekuwa na Bitungu gesti...itakuwa yeye na ndiyo maana alinibana kuhusu Sinza sehemu gani niliyokuwepo mimi," alisema moyoni Juliana huku akichomoka kutoka chumbani humo.

Aliendelea na mambo yake mengine lakini kuanzia muda huo akawa hamwogopi tena mama yake kufuatia kubaini uozo wake na Bitungu.

Jiliana alianza kufanya utafiti wake kwa kutumia akili ya kujiongeza. Aliamua kwamba siku mama yake akitoka na yeye atoke, amfuate kwa nyuma kwa siri mpaka atakapoingia na yeye aingie.
Lakini pia aliamua kuendelea na uhusiano na Bitungu akiamini kwamba, atatumia akili yake ya ziada ili kijana huyo ammwage mama yake.
 
NI SHIIDA!-12

ILIPOISHIA
Lakini pia aliamua kuendelea na uhusiano na Bitungu akiamini kwamba, atatumia akili yake ya ziada ili kijana huyo amwage mama yake.
DONDOKA NAYO SASA...


Akili ya kujiongeza aliyokuwa nayo Juliana ilikuwa ni kuhakikisha kila mama yake anapopigiwa simu yupo pembeni akisikiliza japo kwa kujificha. Alishajitoa mhanga kwa lolote...
"Haiwezekani hata siku moja, kama kula tutaendelea kula wote tu, lakini kwa nini mama anizidi akili? Hata kama ni mama yangu haiwezekani!"

Maisha ya Juliana na mama yake bado yalikuwa ya kuwindana, Juliana hakutaka kumuachia mama yake hata sekunde, kila simu ilipokuwa ikipigwa Juliana hakosi, kama siyo pembeni yake basi atakuwa eneo hilohilo akisikiliza ni nani amepiga.
Siku moja Juliana akiwa katika kufanya usafi katika chumba cha mama yake alisikia simu ya mama yake ikiita, kipindi hiki mama yake alikuwa bafuni akioga.
"Juliana!"

"Abee mama"
"Niletee simu yangu!" Mama Juliana alikuwa tayari ameshaisikia simu yake ikiita, akili yake ilishajiweka ni lazima atakuwa Bitungu, hakutaka hata kidogo Juliana aishike lakini kutokana na kujua kuwa yupo chumbani kwake karibia na hiyo simu akifanya usafi ikambidi amuagizie tu.
"Mbona huji?"

"Nakuja mama, halafu simu yenyewe imeshakata!"
alisema Juliana huku akihema na kusogelea eneo la bafuni alipokuwepo mama yake, jina la kwenye simu iliyokuwa ikiita kwa mama yake lilimkera sana kiasi cha kuamua kuikata kwa makusudi, alikuwa ni Bitungu.
"Shika mama, lakini imeshakatika"
"Alikuwa nani?"

"Hata sikuangalia mama, nadhani atapiga tena!"
"Unadhani? Embu nipe huko!"
Alisema mama Juliana kwa jazba huku akishika simu ile na mapovu ya sabuni mkononi sambamba na majimaji. Harakaharaka akaangalia ‘missed call' lakini hakukuwa na jina alilodhani zaidi ya kukutana na jina la Mama Zai.

"Ina maana Mama Zai ndiyo alikuwa amepiga?"
"Sijui mama, wala sikuangalia jina!"
Alichokifanya mama Juliana ni kuangalia sehemu ambazo simu ile imepokelewa na kugundua kuwa alifanyiwa mchezo na Juliana. Mchezo wa kukatiwa simu ya Bitungu.
"Kwa nini umekata simu yangu!"

"Hapana mama iliita yenyewe na kukatika!"
"Ina maana miye mjinga sijui simu? si nakuuuliza?"
"Kweli mama!"

Mama Juliana aliiweka pembeni ya bafu simu ile na kumfukuza Juliana arudi chumbani aendelee na kazi ya usafi.
Juliana alijirudia zake ndani akiwa amejiongeza vya kutosha, alishaelewa picha kamili juu ya kitakachotokea mbeleni. Alichoamua ni kwenda kuchukua simu yake na kumpigia Bitungu.
"Haloo!"

"Yes baby! Nimekumisi upo wapi sasa hivi?"
"Nipo maeneo ya mbali kidogo!"
"Si uniambie tu hata kama mbali, mbali mbinguni bwana"
"Sweet niko Bagamoyo lakini kesho nategemea kurudi!"
"Bagamoyo? Umeenda lini?"

"Embu subiri kwanza kuna simu ya bosi wangu inaingia, ntakupigia."
Aliongea Bitungu kisha akamkatia simu Juliana. Juliana aliishiwa pozi, penzi la Bitungu lilishamkolea, alijifariji na kuona kuwa huenda ni kweli Bitungu atakuwa amepigiwa simu na bosi wake. Akiwa bado anatafakari kuhusu Bitungu kwa mbali akasikia sauti ya mama yake ikiongea na simu. Hatua kwa hatua akasogelea hadi eneo la sebuleni ambapo mama yake alikuwa na kanga moja tu ametoka kuoga huku akiongea na simu.

"Niambie moja nijue nikukute wapi?"
"Utakuja moja kwa moja hadi gesti ya Tupendane ipo mtaa wa Mchopanga huku Bagamoyo,"
"Kwa nini mpenzi wangu umeamua kwenda mbali huko! Embu njoo mjini bwana!"

"Hukuhuku ndiyo safi na kuna amani kuliko huko kuwa na hofu kibao, kwanza dakika 40 tu umeshafika!"
"Haya ngoja nivae haraka nakuja, nilivyo na hamu asikwambie mtu na leo nataka mechi ya kikubwa, sitaki mechi za mchangani za kuishia nusu saa."
"Kwa hilo usijali, miye ndiye Bitungu!"

"Haya mpenzi nipe saa moja nitakuwa nimeshafika hapo."
Maneno ya Mama Juliana aliyokuwa akiongea kwenye simu yalimuumiza sana Juliana, alijinyong'onyea huku akiwa bado amejificha kwa kujibanza kwenye ukuta wa sebuleni kwao, mama Juliana hakutambua kama Juliana ameyasikia yote aliyoongea kwenye simu.

Alichokifanya Juliana ni kukimbia chumbani kwake na kujiandaa tayari kwa kumfuatilia mama yake hadi atakapoelekea, lengo lake kubwa lilikuwa ni kuhakikisha anamtenganisha Bitungu na mama yake.
"Juliana!"
"Abee mama!"

"Natoka ila nitawahi kurudi mwanangu, nimeitwa sehemu kuna mwenzetu anatakiwa kufanyiwa kicheni pati hivyo nimeitwa kushirikiana nao katika kuandaa."
"Sawa mama!"

"Nakuona unameremeta tu, sitaki utoke na wala sichelewi narudi mchana huuhuu nikukute!"
"Sawa mama!"
Aliitikia Juliana huku akiwa ameshapendeza bila mama yake kujua kuwa wapo safari moja huko aendapo.
 
NI SHIIDA!-13

ILIPOISHIA
Haloo... wee Juliana!"
"Sawa mama!"
Aliitikia Juliana huku akiwa ameshapendeza bila mama yake kujua kuwa wapo safari moja huko aendapo.
SEREBUKA NAYO SASA...

Kitendo cha mama Juliana kutoka kuelekea kupanda bodaboda hadi kituo cha Mwenge ndipo akapande daladala za kwenda Bagamoyo, huku nyuma Juliana alizuga kwa dakika chache na kuufunga mlango kisha akampigia simu Bitungu.
"Haloo"
"Ndiyo sweet!"

"Mbona hukunipigia tena ulipomaliza kuongea na bosi wako!"
Juliana alimtega Bitungu makusudi.
"Ohh! Sorry Sweet, nilijisahau hata hivyo simu yangu inaelekea kuisha chaji muda si mrefu itakatika na huku nilipo hakuna umeme!"
"Jamani! Hata Jenereta hamna baby!
"Ndiyo..."

Kabla Bitungu hajamalizia kuongea akaikata simu na kuizima kwa makusudi, alijua ameshamdanganya Juliana na wala hawezi kujua lolote. Alijiweka sawa akimsubiri mama Juliana. Aliamini baada ya muda ataiwasha simu na kumuelekeza alipo.

Kwa upande wa mama Juliana presha ilikuwa juu, alionyesha kuchanganyikiwa. Alishafika kituoni Mwenge na kumpigia simu Bitungu ikawa haipatikani, akashindwa afanye nini.
"Ndiyo nini ananifanyia! Kama alikuwa hataki kuonana na mimi leo si angeniambia?"
Alijisemea mama Juliana huku hasira zikimzidi, hakuonyesha kukata tamaa kwa sababu maji alishaamua kuyavulia nguo, alichokifanya aliendelea kupiga simu ya Bitungu mara mbilimbili huku ikiwa haipatikani, mara ikaita.

"Haloo!"
"Tushaonana watoto sasa!" Aliuliza mama Juliana kwa jazba.
"Hapana chaji mpenzi, vipi umefika wapi?"
"Nipo kituoni Mwenge, tena una bahati nilikuwa nataka kurudi nyumbani nikalale!"
"Ahhaa!! Usinifanyie hivyo mpenzi utaniua panda daladala uje!"
"Nishuke wapi!"

"Shuka Bagamoyo mwisho, nitakuja kukuchukua stendi, halafu tuelekee hadi eneo ilipo gesti."
Maneno yale yalimpa faraja moyoni mama Juliana, aliona anapendwa kuliko hata mume wake anavyompenda, mwili wake ulikuwa umepatwa na mshtuko kama wa radi na Bitungu tu ndiyo alikuwa fundi wa kurekebisha mshtuko huo. Haikuchukua muda mama Juliana akawa ameshaingia kwenye daladala ya kuelekea Bagamoyo.

Wakati mama Juliana akiwa ndani ya daladala, Juliana naye alikuwa tayari ameshauona mchezo mzima pale kituoni, alikodi bodaboda ya kumpeleka hadi Bagamoyo.
"Hakikisha daladala ile pale mbele yetu haituachi hata chembe!"
Juliana alimwamuru dereva bodaboda.

Kila kituo daladala ilipokuwa ikisimama, dereva bodaboda alikuwa akisimama kwa nyuma yao kidogo. Baada ya mwendo wa zaidi ya nusu saa hatimaye wakaingia Bagamoyo.
"Tusimame hapahapa!" Juliana alimuamuru dereva.

Mahesabu ya Juliana yalikuwa sahihi, alishuhudia mama yake akishuka kwenye daladala moja kwa moja na kufuatwa na Bitungu ambapo walikumbatiana kisha wakaingia kwenye bajaji na kuchomoka.
"Tuwafuate, mpaka nitajua mwisho wake, haiwezekani nifanyiwe mchezo mchafu huku nashuhudia!"
Aliongea Juliana huku dereva bodaboda akiendelea kuwafuatilia bila kujua kama anayemfuatilia Juliana ni mama yake mzazi.

Baada ya mwendo mfupi, ile bajaji ikawa imeshasimama, mama Juliana alitoka sambamba na Bitungu na kuelekea katika gesti ya Tupendane.
"Nimerudi tena!!"

Aliongea Bitungu, akimwambia mhudumu wa mapokezi katika ile gesti huku akielekea kwenye chumba alichopangiwa na kufikia moja kwa moja kwenye kitanda.
"Mpenzi nilikwambia huku kumetulia!"
"Kweli, lakiniii..."

"Lakini nini tena!! Umeshaanza kulalamika!"
"Hapana Bitungu, itabidi tufanye haraka nirudi si unajua huku ni mbali!"
"Najua!"

Mama Juliana alivua nguo zake na kufungua kimkoba alichokuwa nacho na kutoa khanga na kuivaa, kisha akatingisha mwili wake kwa makusudi mbele ya Bitungu aliyekuwa akimtolea macho.
"Twende basi tukaoge mpenzi!"
"Mhh, unajua wewe ni mzuri asikwambie mtu! Utamu ulionao ni zaidi ya kitu chochote!"
Aliongea Bitungu huku akivua suruali yake na kuchukua taulo la gesti na kumshika Mama Juliana hadi bafuni kwenda kuogeshana.

Muda wote Juliana alikuwa yupo nje ya gesti ya Tupendane, presha kwake ilikuwa kubwa, hakujielewa ni njia gani atatumia kujua chumba walichokuwa Bitungu na mama yake mule ndani.
"Kuna vyumba!"

Aliongea Juliana akimwambia mhudumu yule wa mapokezi.
"Ndiyo, unataka single au double?"

"Kwanza shilingi ngapi? Na ingekuwa vizuri kwanza niweze kuviona na ukubwa wake!"
Aliongea Juliana huku akijijua kabisa hakuwa na uwezo wa kulipia chumba kutokana na pesa kidogo aliyokuwa amebeba. Yule mhudumu wa mapokezi alimwelekeza chumba kimoja baada ya kingine huku akikiruka kile chumba ambacho yupo Bitungu na mama yake.
"Mbona vingine hunionyeshi?"

"Ukiona hivyo ujue vina watu ndani yake."
"Kwani?? Yule mama aliyeingia humu ndani na kijana mmoja hivi kama dakika kumi zilizopita kaingia chumba gani?"

Juliana alimuuliza yule mhudumu kimitego.
"Chumba hiki hapa tulichokiacha!"

Alijibiwa Juliana huku akili yote ikimuhama, akaachana na yule mhudumu na kuelekea chumba alichokuwa ameelekezwa, moja kwa moja akaufungua mlango wa kile chumba, haukuwa umefungwa hivyo akaingia moja kwa moja na kuzama ndani.
"Lakini huko si nimekwambia kuna watu!"
"Hata kama!! Nawafahamu ngoja niwasalimie kwanza!"
 
NISHIIDA!-14

ILIPOISHIA
Alijibiwa Juliana huku akili yote ikimuhama, akaachana na yule mhudumu na kuelekea chumba alichokuwa ameelekezwa, moja kwa moja akaufungua mlango wa kile chumba, haukuwa umefungwa hivyo akaingia moja kwa moja na kuzama ndani.

"Lakini huko si nimekwambia kuna watu!"
"Hata kama!! Nawafahamu ngoja niwasalimie kwanza!"
SEREBUKA NAYO SASA...

Aliongea Juliana huku akiwa ameshaingia ndani na kumuacha mhudumu nje akiwa mdomo wazi. Kitendo cha kuingia kwenye kile chumba alikikuta kitupu, macho ya Juliana yaligongana na nguo za mama yake sambamba na mkoba uliokuwa kitandani pale, hakujiamini mara mbilimbili kama alikuwa ni mama yake.

"Lazima watakuwa wameingia kuoga tu!"
Alijiongelea Juliana huku akipiga hatua kuelekea kwenye bafu ambalo lilikuwa ndani mulemule. Alipokaribia katika mlango wa lile bafu aligundua kuwa haukuwa umefungwa, hivyo akausukuma kidogo na kuchungulia kwa jicho moja. Alimshuhudia mama yake akiwa anamsugua mgongo Bitungu, Bitungu naye akimsugua mama Juliana huku wakifurahia kwa kupigana mabusu.

Baada ya kusuguana kwa muda wakajimwagia maji kuondoa mapovu kisha Bitungu akataka kufanya mambo mulemule bafuni...
"Mhh sasa naona mechi yetu kama tukaihamishie kule kwenye uwanja mkubwa maana nahisi huu si uwanja mzuri..."

"Kwani una nini sweet!"
"Wee huoni, vichuguu kila kona, hata mashuti unayopiga nashindwa kuyadaka vizuri!"
"Ni kweli sweet lakini ngoja kwanza nikijikwaa tu ndiyo tuh..."
"Ukijikwaa nini, sitaki kusubiri mpaka ujikwae, miye nainuka bwana!"
"Hapana Sweet subiri kwanza!"

Muda wote Juliana alikuwa akiwapiga jicho kupitia kaupenyo kadogo kwenye mlango, mzuka ulionekana kumpanda hata lile wazo la kutaka kuwafumania likakaukia kwenye ubongo wake kwa muda mfupi.
"Inamaana Bitungu ndiyo mchezo wake enhh!, kwangu miye anajifanya kunibania kwa mama anampa vyote!"

Aliendelea kujisemea Juliana huku akiwa bado kauinamia mlango.
Ndani ya muda mchache Bitungu na mama Juliana walikuwa katika mapumziko ya mechi yao, mama Juliana alikuwa hoi hajiwezi huku Bitungu akishughulika kwa kumvalisha khanga yake.
"Vaa basi jezi yako, tukapumzikie kule!"
"Baby!"

"Nambie!"
"Usinivalishe hiyo khanga kwanza!"
"Kwa nini?"
"Hivi umeniroga ama nini?"
"Kwani vipi sweet?"

"Yaani haiwezekani hata mechi ya kwenye uwanja mbovu uwe unaijulia kiasi hiki!"
"Nilishakwambia miye fundi wa mipira iliyokufa, kiwanja chochote unachokitaka tunaweza kucheza na nikatoka na ushindi tena ule wa kishindo." Aliongea Bitungu kwa kujisifu.

Maneno yale yalipata kusafiri hadi kwenye ubongo wa Juliana, akayanasa kwa hasira ya hali ya juu sambamba na macho yakimkakamaa.
"Bitungu... Bitunguuuu?"

Juliana alijikuta akitoa sauti ya ukali akilitaja jina la Bitungu kwa sauti ya juu, moyoni mwake alishakubaliana na lolote litokee. Alichokifanya kabla Bitungu na mama Juliana hawajatoka mle bafuni, alifungua kitasa cha mlango ule na kutaka kuingia ndani.
"Unafanyaje chumba hiki?"

Sauti nene na kali ya kiume ilimhoji Juliana. Juliana akageuka na kuisikia sauti ile inapotokea, kisura hakuweza kumfahamu zaidi ya kuambulia kumjua yule mhudumu wa mapokezi aliyekuwa amefuatana naye.

"Nilimwambia chumba hicho kina watu akasema anafahamiana nao," alijitetea yule mhudumu wa mapokezi akimuelezea yule kaka mbele ya Juliana.
"Dada hivi unajua utaratibu katika gesti hii?"
"Jamani si nilishawaambia kuwa nawafahamu?"

"Hata kama unawafahamu ndiyo uwachungulie tena wakiwa bafuni?"
"Haya tusubiri watoke muone kama hawanijui!" Aliongea Juliana kwa kujiamini lakini yule mkaka hakutaka kabisa kuaminiana naye, alichokifanya alimshika Juliana mkono na kumtoa katika kile chumba.
"Nimesema sitoki, hata mfanyaje mpaka wa huku bafuni wanione?"
Aliongea Juliana kwa kujiamini.

"Utatoka tu! Wee nani mpaka usitoke na kwanza hivi umelipia hata chumba humu ndani?"
"Sijalipia lakini sitoki!"
Juliana alitolewa kwa nguvu huku akiburutwa mpaka kwenye korido ya mule ndani ya gesti.

***
Wakati yote hayo yakiendelea si Bitungu wala mama Juliana aliyekuwa anajua kinachoendelea. Ndiyo kwanza mama Juliana alikubali kuendelea na kipindi cha pili baada ya kuchanganywa na mechi iliyopigwa kipindi cha kwanza japokuwa uwanja ulikuwa mbovu.
"Bitu mpenzi!"

"Niambie sweet!"
"Nasikia kuna makelele kweli nje na sauti ya dada kama analia kwa mbali?"
"Achana nao wanaweza wakawa watu wamefumaniana hao lakini kwa hapa, hapana! Sidhani kama kuna mambo hayo!"
"Nina wasiwasi Bitu!"

"Achana nao kwanza hayatuhusu tumekuja kula raha zetu hapa na siyo kufuatilia mambo ya watu."
Aliongea Bitungu huku akimvalisha mama Juliana ile khanga yake. Walikuwa tayari wameshatosheka kwa mechi kali mbili. Kitendo cha kutoka bafuni na kuelekea kitandani ile sauti iliyokuwa ikilia ndiyo kwanza ikazidi.

"Bitu, wacha nikaone anayelia mbona sauti kama ya mwanangu!"
"Mwanako? Afuate nini huku? Embu jifute tuagize chakula tupumzike kidogo urudi hayo mambo mengine waachie hukohuko hayatuhusu."
"Bitu kwangu miye nahisi kama yananihusu."

ITAENDELEA JUMATANO...!!!!
 
nimecheka alipoingia chumbani kutaka kuwasalimia waliopo ndani..,, nice move!!
 
Back
Top Bottom