Vijiji vingi unakuta kila mji kuna kuku kadhaa, maana kuku wa kienyeji wanajifuga wenyewe na hakuna mishe za wizi, kwa hiyo akifika mgeni wa heshima kuku lazima atembee.
Sisi tukiwa wadogo ilikuwa kama kuna mgeni kaja na hatujala nyama muda mrefu tunaforce king, unakuta tunamuuliza maza mbele ya mgeni, "Mama tukamate kuku". Hapo mama anakuwa hana ujanja, ila mgeni akiondoka mtaimba kwa fimbo.
Ila kuna wageni hata huulizi, maana unakuta naye kaja na mzigo kama wa mahindi, vitunguu, au chochote tu, bush hakuna uchoyo wa misosi, labda miaka hii.