Siku mbili za Halima Mdee rumande Oysterbay

Siku mbili za Halima Mdee rumande Oysterbay

kamatwa kwa mbunge wa upinzani nchini Tanzania Halima Mdee kwa madai ya kumtusi rais John Magufuli kumeshutumiwa pakubwa huku wakosoaji wakisema kuwa ni ishara ya hivi karibuni kwamba serikali inatumia mamlaka yake vibaya ili kukandamiza uhuru wa kujieleza.

Msemaji wa chama cha upinzani Chadema Tumaini Makene ameambia BBC kwamba chama hicho kitakwenda mahakamani dhidi ya hatua ya mkuu wa Wilaya ambae aliagiza kukamatwa kwake pamoja na makamishna wengine wote wanaokiuka sheria.

Bi Mdee ni mwanachama wa Chadema, chama kikuu cha upinzani katika aifa hilo la Afrika mashariki.

Alituhumiwa na Ally Hapi, mkuu wa wilaya ya Dar es Salaam kwa kumtusi rais na kuchochea ghasia baada ya kudai kwamba rais anafikiri kwamba matamshi yake ni sheria na kwamba siku moja atawaagiza Watanzania kukaa utupu.

Muungano wa mabadiliko na uwazi unaongozwa na Zitto Kabwe ulisema kuwa hatua hiyo ni uendelevu wa utumiaji mbaya wa mamlaka.

''Sheria inayompatia mkuu huyo wa Wilaya uwezo wa kuagiza kukamatwa kwa mtu, hailingani na sababu ya kukamatwa kwa bi Mdee'',alisema.

Watu kadhaa wamekamatwa katika siku za nyuma kwa kuchapisha ujumbe katika mitandao ya kijamii ambayo mamlaka inadai inaingilia kisiasa.

Mamlaka inaamini kwamba inafuata sheria na kuchukua hatua za kuhakikisha kwamba hakuna ''migogoro yoyote miongoni mwa wananchi'' nchini Tanzania.

Bwana Magufuli alishinda uchaguzi wa urais wa mwaka 2015 na licha ya kukosolewa na upinzani pamoja na makundi ya wanaharakati anaungwa mkono na Watanzania wengi.
 
Kwahiyo Rais ana ruhusiwa kushambulia wenzake lakini wengine hawaruhusiwi kumshambulia?
kisu cha ngariba: kama una ubavu, vua koti la hiyo ID, utoke hadharani uyasema maneno ambayo wewe unaamini ni sahihi kuyasema ukimshbulia Rais.
 
Kabisaa

Ila anaboa huyu ukizingatia hata hakuna analofanya la maana kwenye jimbo lake.
We nawe ovyo kweli! Kwenye majimbo mengine hasa yale yanayoongozwa na Ccm lipi la maana limefanyika? Mijitu ya mtera haijitambui kama mbunge wao!
 
Hata kama Rais ana element za siasa za chuki lakini sio kwa kushambuliwa kwa namna wanavyofanya wapinzani. Rais ni taasisi kumbuka.
Angeanza kutambua yeye kwamba nafasi yake ni taasisi,Hata nyumbani baba akianza kukosa adabu mbele ya watoto wake,si ajabu na watoto kuanza kumkosea adabu mbele yake.
 
Hivi kati ya Rais na Mdee nani ana siasa za chuki?
Wewe kisu cha ngariba waweza kumtukana hata mama yako mzazi kwa jinsi ilivyo, lazima Rais wa nchi aheshimiwe hata kama hukumchagua. Ni sawa na kumheshimu mama yako aliyekuzaa hata kama kakukosea namna gani. Hivyo wanajamvi tusiwe kama hatuna maadili au hatujalelewa na wazazi.
 
A man who rages, threats, demand and commands his people as a way to intimidate them, is nothing more than a cowardly bully, who choose to use abuse as a method to get his way and have control.

This is not the definition of a man, it is an immature weak little child trying to appear big, tough, superior and powerful.

Time will tell, never accept any form of bullying.
 
Sishangai wengi humu kuunga mkono upuuzi wa Mdee maana hata alivyomtusi Spika 'acha Ufala' mlishangilia sana.
kama alifanya vitu vya kifala unafikiri angeambiwaje?Ndugai alistahili na bado anastahili kuitwa alivyoitwa,Mtu anayeshindwa hata kujifunza kutoka kwa wenzake waliomtangulia kufanya kazi hiyohiyo moja?Bunge badala kuendelea kuwa bora linaendelea kuwa uozo?Waache wanaoweza kusema ukweli wawaambie ukweli.
 
Wewe kisu cha ngariba waweza kumtukana hata mama yako mzazi kwa jinsi ilivyo, lazima Rais wa nchi aheshimiwe hata kama hukumchagua. Ni sawa na kumheshimu mama yako aliyekuzaa hata kama kakukosea namna gani. Hivyo wanajamvi tusiwe kama hatuna maadili au hatujalelewa na wazazi.

Nani kamtukana Rais? Unaweza kuleta hayo matusi?
 
Endelea kupiga makofi na kushangilia,ndio ujira wako.
Nawe endelea kubwabwaja tuhumu jamvini - debe tupu. Kama unamwonea huruma na kwa uwezo ulionao wa maneno humu jamvini, jitokeze ukamtoe pale kituoni.

Hivi ulikuwa wapi hadi anakamatwa?
 
Screenshot_2017-07-06-14-06-11.png
 
Wewe kisu cha ngariba waweza kumtukana hata mama yako mzazi kwa jinsi ilivyo, lazima Rais wa nchi aheshimiwe hata kama hukumchagua. Ni sawa na kumheshimu mama yako aliyekuzaa hata kama kakukosea namna gani. Hivyo wanajamvi tusiwe kama hatuna maadili au hatujalelewa na wazazi.
Mimi ninaamini kuna namna mwenye taasisi akijirekebisha hata hawa wanao mkosoa kwa namna ambayo yeye mwenyewe na mnao mzunguka hampendi,watajirekebisha pia.Vinginevyo kwa kadri atakavyo endelea kuwa hivi ndivyo na idadi ya wakosoaji wa namna hii msiyo ipenda ndivyo itakavyokuwa inaongezeka.
 
Ndio sheria kandamizi hizi ambazo makoloni aliziacha na bado magamba wanazikumbatia ili kiwakomboa wapinzani halafu wanasema huyu rais hana mfano ni wa kuigwa eti Africa.
 
Back
Top Bottom