Siku mbili za Halima Mdee rumande Oysterbay

Siku mbili za Halima Mdee rumande Oysterbay

Halima Mdee lazima abadilike, watanzania sasa hivi hatutaki siasa za chuki. Hata kama Rais anakosea, kuna njia nzuri za kumpinga lakini sio kama wabunge wengi wa upinzani wanavyofanya.

Kabisaa

Ila anaboa huyu ukizingatia hata hakuna analofanya la maana kwenye jimbo lake.
 
  • Thanks
Reactions: MJJ
Hata kama Rais ana element za siasa za chuki lakini sio kwa kushambuliwa kwa namna wanavyofanya wapinzani. Rais ni taasisi kumbuka.
Alichokosea Mdee ni nini hasa.. hayo maneno waliyomnukuu yana shida gani?
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Hapana mkuu. Uwezi kumwambia baba yako anaropoka anaongea hovyo ukajiona una hekima. Mbona wapo wakosoaji wengi hatuwaoni kupelekwa ndani? Kuna mbunge gani wa upinzani hakosoi raisi? Je wanawekwa wote ndani? Hapana mkuu nasomaga post zako uwa nakuamini lakini ukiunga mkono anayofanya Halima haitakuwa sawa. Ni heri kukaa kimya

Kama una ropoka hautaki kuambiwa ukweli? Kama una ropoka lazima uambiwe ukweli. Unaropoka....unakosea.
 
Ndio kamuambia sasa kuwa anakosea,huu sio mda wa kubembelezana.


Haya. Lakini nasikitika kukosa muwakilishi bungeni kwa matendo ya mbunge wangu japo sikumchangua lakini alishinda yeye ndie mbunge wangu
 
Wapinzani, upinzani sio uvunjifu wa heshima, Rais anastahili heshima yake, Huwezi kwenda kwenye media na kuongea kipumbavu namna ile, Demokrasia sio uvunjifu wa adabu, je ndio vile anavyoongeaga na baba yake?
Halima is very smart... one of the smartest person in this world... unlike watu wengine wanaojitapa kuwa wameenda shule mpaka kiwango cha juu ya gorofa huko sijui, lakini kichwani ni zero kabisa, kila wakifungua midomo yao tu, matapishi ya kinyaaa kabisa ndio yanayotoka huko midomoni mwao...
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Halima Mdee lazima abadilike, watanzania sasa hivi hatutaki siasa za chuki. Hata kama Rais anakosea, kuna njia nzuri za kumpinga lakini sio kama wabunge wengi wa upinzani wanavyofanya.
Acha unafiki, siasa za chuki mfanye nyie, wengine wanyamaze?
 
  • Thanks
Reactions: BAK
SIKU MBILI ZA HALIMA MDEE RUMANDE OYSTERBAY
Usiku wa kuamkia leo tarehe 6 Julai, 2017 ni usiku wa pili wa kulala korokoroni Mwenyekiti wa BAWACHA taifa, Mjumbe wa Kamati Kuu na Mbunge wa Kawe CHADEMA Halima James Mdee.

Katika rumande ya Polisi Oysterbay wilayani Kinondoni, Mdee ameendelea kutumikia masaa 48 aliyopewa na Mkuu wa Awilaya ya Kinondoni Ally Hapi kwa kosa la kumdhihaki Mh. Rais Dr. John Magufuli na kutoa maneno machafu yanayoweza kuvunja amani.

MATAMSHI YA MDEE
Akizungumza na waandishi wa habari Makao makuu ya CHADEMA Mdee ananukuliwa kudai kuwa Mh. Rais Magufuli amekua na "tabia ya hovyo...", "...ipo siku ataagiza watanzania (wake kwa waume) watembee vifua wazi...". Maneno mengine ni "...Rais lazima afungwe breki...",apewe semina elekezi n.k.

UCHOCHEZI
Halima Mdee anatajwa kutoa kauli za uchochezi kama vile "...woga wetu wananchi ndio unaotugharimu nchi hii..." "...watakaomfunga breki ni nyinyi wananchi...", maneno yanayotajwa kupandikiza na kuhamasisha chuki na vurugu kwa wananchi.

KUKAMATWA KWAKE
Baada ya amri ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mdee alianza harakati za kutoroka na kuruka mtego wa Polisi. Hata hivyo Jeshi la Polisi Kinondoni lilimkamata akiwa amejificha nyumbani kwa mama yake Kibamba wilayani Ubungo tayari kwa kutoroka.

RUMANDE
Halima Mdee anatajwa kuhifadhiwa katika rumande ya watuhumiwa wa uhalifu wa jinsia ya kike katika kituo cha Oysterbay Kinondoni.

BUNGE KUMUWAJIBISHA TENA
Akiwa bado anatumikia kifungo cha kutohudhuria Bunge hadi mwaka 2018, Halima Mdee ameingia tena matatani.

Kufuatia matamshi ya Mdee na waandishi wa habari Makao Makuu ya Chadema, Spika wa Bunge Job Ndugai ameagiza kamati ya Kinga na Madaraka ya Bunge kukutana haraka kujadili kitendo cha Mbunge huyo kutoa matashi ya kulifedhehesha Bunge. Akikutwa na hatia huenda akaongezewa adhabu nyingine.
Ajifiche kwa kipi kipya hapo?ujinga na upumbavu tatizo kubwa sana kwa watanzania kusema ukweli imekuwa shida
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Wangoje zamu yao wawe na rais saiz wanaumia bure kwa kuona wanasifiwa
 
Halima ana hoja nzuri...ila anakoseaga namna ya kuziwasilisha..angekua anapunguza jazba ingemsaidia mno.
 
Mi sio mnafiki, ukweli unabaki kuwa ukweli, Sina chuki kama wewe mchina,Ila upinzani ni roho, tena roho inayotoka kwa shetani, ukiwa nayo utatumia vivuli vingi kupinga kila kitu, ndio asili yake.
...ndugu, maandishi yako humu yanaonyesha wewe ndio unayeongozwa na roho ya shetani... kufunga watu midomo, ubabe, uongo, unafiki, kujipendekeza, kulazimishia heshima (kumbuka, respect is earned), double standards, kuminya haki za wengine etc, yote haya ni mambo ya kishetani, maana matokeo ya haya mambo hapo baadaye yanajulikana tumeona sehemu mbali mbali duniani. Pole sana kwa hiyo roho... but its not too late...
 
Kabisaa

Ila anaboa huyu ukizingatia hata hakuna analofanya la maana kwenye jimbo lake.
Toa mfano wa la maana analofanya mbunge yeyote wa CCM, au afanye kama yule anayepiga selfie ya kuokoa wahanga wa mafuriko huku kashikiliwa asidondoke?
 
SIKU MBILI ZA HALIMA MDEE RUMANDE OYSTERBAY
Usiku wa kuamkia leo tarehe 6 Julai, 2017 ni usiku wa pili wa kulala korokoroni Mwenyekiti wa BAWACHA taifa, Mjumbe wa Kamati Kuu na Mbunge wa Kawe CHADEMA Halima James Mdee.

Katika rumande ya Polisi Oysterbay wilayani Kinondoni, Mdee ameendelea kutumikia masaa 48 aliyopewa na Mkuu wa Awilaya ya Kinondoni Ally Hapi kwa kosa la kumdhihaki Mh. Rais Dr. John Magufuli na kutoa maneno machafu yanayoweza kuvunja amani.

MATAMSHI YA MDEE
Akizungumza na waandishi wa habari Makao makuu ya CHADEMA Mdee ananukuliwa kudai kuwa Mh. Rais Magufuli amekua na "tabia ya hovyo...", "...ipo siku ataagiza watanzania (wake kwa waume) watembee vifua wazi...". Maneno mengine ni "...Rais lazima afungwe breki...",apewe semina elekezi n.k.

UCHOCHEZI
Halima Mdee anatajwa kutoa kauli za uchochezi kama vile "...woga wetu wananchi ndio unaotugharimu nchi hii..." "...watakaomfunga breki ni nyinyi wananchi...", maneno yanayotajwa kupandikiza na kuhamasisha chuki na vurugu kwa wananchi.

KUKAMATWA KWAKE
Baada ya amri ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mdee alianza harakati za kutoroka na kuruka mtego wa Polisi. Hata hivyo Jeshi la Polisi Kinondoni lilimkamata akiwa amejificha nyumbani kwa mama yake Kibamba wilayani Ubungo tayari kwa kutoroka.

RUMANDE
Halima Mdee anatajwa kuhifadhiwa katika rumande ya watuhumiwa wa uhalifu wa jinsia ya kike katika kituo cha Oysterbay Kinondoni.

BUNGE KUMUWAJIBISHA TENA
Akiwa bado anatumikia kifungo cha kutohudhuria Bunge hadi mwaka 2018, Halima Mdee ameingia tena matatani.

Kufuatia matamshi ya Mdee na waandishi wa habari Makao Makuu ya Chadema, Spika wa Bunge Job Ndugai ameagiza kamati ya Kinga na Madaraka ya Bunge kukutana haraka kujadili kitendo cha Mbunge huyo kutoa matashi ya kulifedhehesha Bunge. Akikutwa na hatia huenda akaongezewa adhabu nyingine.
Political gain/grave in young age.

You shall reap what you sowed
 
...ndugu, maandishi yako humu yanaonyesha wewe ndio unayeongozwa na roho ya shetani... kufunga watu midomo, ubabe, uongo, unafiki, kujipendekeza, kulazimishia heshima (kumbuka, respect is earned), double standards, kuminya haki za wengine etc, yote haya ni mambo ya kishetani, maana matokeo ya haya mambo hapo baadaye yanajulikana tumeona sehemu mbali mbali duniani. Pole sana kwa hiyo roho... but its not too late...
Ulichoandika tu kinaonyesha wewe ni mtu wa aina gani.
 
Back
Top Bottom