Umeweka mtiririko mzuri na binafsi sikujua kama alikamatiwa kwa mama yake na kitendo cha kuwa kwa mama yake ni namna mojawapo ya kutaka kutororka.
Jambo moja ni wazi nalo ni kuwa kila mtu anataka kumfurahisha Mheshimiwa Raisi kwa kadri inavyowezekana.Wateule wote wameshasoma ni kitu gani ambacho aliyewateua anataka na wanaitumia nafasi hiyo kiukamilifu,ni jambo jema kwani wanajihakikishia kula kwao na wapendwa wao.
Mkuu wa wilaya ametumia mamlaka yake kikatiba na tunaamini saa 48 zitaisha na atatoka sasa tuangalie huyu wa Dodoma naye kimemuumiza nini?Hivi kweli kwa matamshi hayo ukilinganisha na yule aliyesema bungeni watu wanalala tu ni nani kaliabisha bunge zaidi?
Binafsi naomba JPM asimame tena katika uchaguzi wa 2020 na upinzani wapate wabunge wachache mno na ikiwezekana wakosekane kabisa, si ajabu tukapiga hatua kubwa mno katika nchi hii.