Sijawahi kufikia wala kuvuka uzito kg 60!

Sijawahi kufikia wala kuvuka uzito kg 60!

Keyboard_Warrior

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2015
Posts
6,327
Reaction score
11,026
Familia, hii kitu kuna wakati inanikera. Kiasi kwamba siku hizi nikiona mzani mbele yangu nahisi kama nimeona adui.

Iko hivi, urefu wangu ni 182cm, uzito wangu sasa...58kg.

Aisee, maisha yangu yote sijawahi kuvuka hiyo kilo 58, sanasana kuna wakati nashuka mpaka kilo 56.

Natamani sana kuongezeka uzito, angalau na mimi niwe na hata kilo 60. Nini nifanye kuongeza uzito!?

NOTE: Sina ugonjwa sugu wowote, siumwi mara kwa mara, ni zaidi ya miaka mitatu sasa sijakanyaga hospitali.
 
Screenshot_2026-01-13-17-54-34-24_40deb401b9ffe8e1df2f1cc5ba480b12.jpg


Nipo kwa underweight hapo!!!
NJANO
 
Familia, hii kitu kuna wakati inanikera. Kiasi kwamba siku hizi nikiona mzani mbele yangu nahisi kama nimeona adui.

Iko hivi, urefu wangu ni 182cm, uzito wangu sasa...58kg.

Aisee, maisha yangu yote sijawahi kuvuka hiyo kilo 58, sanasana kuna wakati nashuka mpaka kilo 56.

Natamani sana kuongezeka uzito, angalau na mimi niwe na hata kilo 60. Nini nifanye kuongeza uzito!?

NOTE: Sina ugonjwa sugu wowote, siumwi mara kwa mara, ni zaidi ya miaka mitatu sasa sijakanyaga hospitali.
Basi wewe huli kwa urefu wa kamba yako!Na pengine sii chawa pia.
 
Kula ugali mkubwa , kunywa supu na chapati kila asubuhi , kisha usukutue mdomo na kama safari mbili za baridi , pata muda wa kupumzika , achana na stress za mapenzi na mikopo .

Note: kiriba tumbo Sio poa bwashee
 
Kula ugali mkubwa
Nakula sana!
kunywa supu na chapati kila asubuh
Hii nafanya sana.
kisha usukutue mdomo na kama safari mbili za baridi
Hapa sijawahi kufikiria, ila kama inaweza kunifikisha katika 60kg, nadhani nitajaribu.
pata muda wa kupumzika
Muda wa kupumzika napata.
achana na stress za mapenzi na mikopo
Nina stress za kiwango cha kawaida tu, sidhani kama zinaweza kuwa na impact kubwa kwenye uzito wa mwili wangu.
 
Niliwahi kuwa na tatizo hilo ingawa wewe kwako ni kubwa zaidi. Nina urefu wa 180cm ila nilikuwa na 70kg. Nikaenda gym yule trainer akanishauri nile sana na kunyanyua chuma. Alinisisitiza yaani hata ule muda niko kitandani nataka kulala nitafune hata popcorn. Kimsingi nile sana. Niliongezeka vizuri nikawa na umbo lililojengeka vyema.

Nilikuja kuharibu nilivyoacha gym na kujikuta nimenenepa hatari kufika kilo 97. Ndo ikabidi nianze mazoezi ya kukimbia na kurudi 88kg.
 
Back
Top Bottom