Sijaona waziri anaeshirikiana na jamii kwa moyo wa kujitolea bila makamera kumzidi Dkt Dorothy Gwajima, Her Responsibility exceeds her power

Sijaona waziri anaeshirikiana na jamii kwa moyo wa kujitolea bila makamera kumzidi Dkt Dorothy Gwajima, Her Responsibility exceeds her power

Hakuna anapojitahidi, ni muoga sana. Wanawake wa chadema na waandishi wa habari walipigwa pale mahakamani siku ya kesi ya lissu, akaombwa achukue hatua, akatumiwa na videos, lakini alikaa kimya hata kuzungumzia tu aliogopa

Anachagua matukio
Ooooooohooooo...!Tena?
 
Kujua matatizo ya wananchi kwa ukaribu ni msingi wa utatuzi wa kweli. Ni muhimu kwa viongozi kuwa karibu na waathirika moja kwa moja badala ya kutegemea tu ripoti kutoka kwa viongozi wa chini. Mara nyingi ripoti hizi huwa zimepunguzwa au kuhaririwa kwa nia ya kulinda maslahi ya viongozi hao wa chini, kundi kubwa zaidi hata hawafuatilii wala kujishughulisha (wavivu) wanasubiri mishahara wanatunga chochote, hivyo kuficha hali halisi ya matatizo yanayowakumba wananchi.

Katika mazingira haya, napenda kukiri kuwa Dkt. Dorothy Gwajima ni miongoni mwa viongozi wachache wanaojitahidi kuwasiliana moja kwa moja na wananchi ili kuelewa changamoto zao kwa undani. Anaonekana kuwa na dhamira ya dhati ya kufuatilia matatizo ya kijamii kutoka kwenye vyanzo vya moja kwa moja. Silaha yake kubwa imekuwa matumizi ya majukwaa ya mitandao ya kijamii, jambo ambalo linadhihirisha kuwa anaendana na wakati na ana nia ya kweli ya kusikiliza wananchi.

Kwa mfano, katika jukwaa la JamiiForums, mara kadhaa nimeona Dkt. Gwajima akianzisha mijadala, akichangia, na kureply maoni mengi ya wananchi. Hili si jambo rahisi kwa kiongozi wa ngazi yake, lakini linaonyesha jinsi anavyothamini maoni ya watu wa kawaida. Pia katika mitandao mingine kama Facebook, anaendelea kuwa na uwepo wa dhati, si tu kwa kutoa taarifa, bali pia kwa kujibu maswali na kutoa mrejesho wa moja kwa moja kwa wananchi.

Uwajibikaji wake unazidi mamlaka aliyopewa, jambo linalomtofautisha sana na viongozi wengi ambao wanajulikana zaidi kwa vyeo vyao kuliko kwa kazi wanazozifanya. Dkt. Gwajima ameonyesha kuwa cheo si pambo, bali ni nafasi ya kuwatumikia wananchi kwa uwazi, uwajibikaji na moyo wa dhati.
In fact ndiye kiongozi pekee pendwa nchi nzima! Uzuri wa Dkt. Gwajima D kajaliwa kusikiliza sauti za watu, yaani inaonekana ni kiongozi anayeishi maisha ya mtanzania wa kawaida, yaani pamoja na ukubwa wa madaraka alionao ila hajasahau maisha ya mtanzania wa kawaida. Hata mume wake atakuwa ana enjoy u Baba nyumbani
 
Hakika.
Dkt. Gwajima D ni waziri pekee ambaye si yupo karibu na jamii tuu, bali ni mwanajamii mzuri.
Hongera sana na Mungu azidi kukubariki.

Kiongozi mzuri ni yule anayependa "kujamiika", maana kwa kufanya hivyo, ndipo anajua changamoto zilizopo kwenye jamii na namna ya kuzitatua.

Mfano mzuri, hapa Jamii Forums, kuna michango mizuri sana ambayo ikichukuliwa na kufanyiwa kazi kwa wakati, naamini changamoto nyingi zingepatiwa ufumbuzi kwa haraka na urahisi.
 
Muoga huyo, wanawake waliopigwa mahakamani siku ya kesi ya lissu alikaa kimya, alitumiwa ushahidi wote Ila akaogopa hata kuongea tu
Alifanya vizuri kukaa kimya. Serikali tuliyonayo ni ya kisasi na uovu. Yaani kuna kikundi cha wajinga walishajipenyeza kumharibia Dkt Samia so kiongozi yeyote akipinga wanatoa maelekezo anafukuzwa kazi
 
Hakika.
Dkt. Gwajima D ni waziri pekee ambaye si yupo karibu na jamii tuu, bali ni mwanajamii mzuri.
Hongera sana na Mungu azidi kukubariki.

Kiongozi mzuri ni yule anayependa "kujamiika", maana kwa kufanya hivyo, ndipo anajua changamoto zilizopo kwenye jamii na namna ya kuzitatua.

Mfano mzuri, hapa Jamii Forums, kuna michango mizuri sana ambayo ikichukuliwa na kufanyiwa kazi kwa wakati, naamini changamoto nyingi zingepatiwa ufumbuzi kwa haraka na urahisi.
Anachagua matukio. Siku ya kesi ya lissu aliogopa hata kuzungumzia tu jinsi wanawake walivyopigwa na kudhalilishwa
 
Alifanya vizuri kukaa kimya. Serikali tuliyonayo ni ya kisasi na uovu. Yaani kuna kikundi cha wajinga walishajipenyeza kumharibia Dkt Samia so kiongozi yeyote akipinga wanatoa maelekezo anafukuzwa kazi
Kwa maana hiyo hizi sifa anazopewa hapa hastahili
 
Kujua matatizo ya wananchi kwa ukaribu ni msingi wa utatuzi wa kweli. Ni muhimu kwa viongozi kuwa karibu na waathirika moja kwa moja badala ya kutegemea tu ripoti kutoka kwa viongozi wa chini. Mara nyingi ripoti hizi huwa zimepunguzwa au kuhaririwa kwa nia ya kulinda maslahi ya viongozi hao wa chini, kundi kubwa zaidi hata hawafuatilii wala kujishughulisha (wavivu) wanasubiri mishahara wanatunga chochote, hivyo kuficha hali halisi ya matatizo yanayowakumba wananchi.

Katika mazingira haya, napenda kukiri kuwa Dkt. Dorothy Gwajima ni miongoni mwa viongozi wachache wanaojitahidi kuwasiliana moja kwa moja na wananchi ili kuelewa changamoto zao kwa undani. Anaonekana kuwa na dhamira ya dhati ya kufuatilia matatizo ya kijamii kutoka kwenye vyanzo vya moja kwa moja. Silaha yake kubwa imekuwa matumizi ya majukwaa ya mitandao ya kijamii, jambo ambalo linadhihirisha kuwa anaendana na wakati na ana nia ya kweli ya kusikiliza wananchi.

Kwa mfano, katika jukwaa la JamiiForums, mara kadhaa nimeona Dkt. Gwajima akianzisha mijadala, akichangia, na kureply maoni mengi ya wananchi. Hili si jambo rahisi kwa kiongozi wa ngazi yake, lakini linaonyesha jinsi anavyothamini maoni ya watu wa kawaida. Pia katika mitandao mingine kama Facebook, anaendelea kuwa na uwepo wa dhati, si tu kwa kutoa taarifa, bali pia kwa kujibu maswali na kutoa mrejesho wa moja kwa moja kwa wananchi.

Uwajibikaji wake unazidi mamlaka aliyopewa, jambo linalomtofautisha sana na viongozi wengi ambao wanajulikana zaidi kwa vyeo vyao kuliko kwa kazi wanazozifanya. Dkt. Gwajima ameonyesha kuwa cheo si pambo, bali ni nafasi ya kuwatumikia wananchi kwa uwazi, uwajibikaji na moyo wa dhati.
Mama yeyote asiyependa kujipodoa podoa ujue yuko serious na kazi.Anachukizwa sana na unyanyasaji wa watoto wa kike na wakiume kingono.Laiti angelikuwa na kofia mbili na ile ya upolisi.Wabakaji wangelitafuta hifadhi nje ya nchi
 
Back
Top Bottom