Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,427
- 154,270
Kitabu cha mithali 31 kuanzia msitari wa 10
hadi 31 kimeelezea sifa mbalimbali za mke
mwema, tuangalie kwa uchache sifa hizo
kwa kuzichambua katika maeneo tofauti.
1. Imani
Mithali 31:26, 29, 30
Mke mwema anayashika na kuyafanyia kazi
maneno ya Mungu na ni mtu ambaye
anamtumikia Mungu kwa moyo wake wote
na akili yake yote. Anatafuta makusudi ya
Mungu katika maisha yake na kuyafuata.
Zaburi 119;15
2. Ndoa
Mithali 31:11-12, 23, 28
Mke mwema humuheshimu mume wake na
anahakikisha anamtendea mambo mema
siku zote za maisha yake. Ni wa kuaminika
na msaidizi kwa mume wake. Efeso 5:22-24,
1Petro 3
3. Malezi
Mithali 31: 26, 28
Mke mwema anawafundisha watoto wake
njia za Mungu na pia anawatunza kwa
upendo. Huwafundisha kwa hekima na
kuwaelekeza njia iwapasayo kuiendea.
Mithali 22:6
4. Huduma
Mithali 31:12-15, 17, 20
Mke mwema anamhudumia mume wake na
familia yake yote kwa ukarimu na upendo.
Anahakikisha wanapata chakula kilicho bora
na chenye afya. Ni mtu mwenye huruma na
ukarimu.
5. Mali
Mithali 31:14, 16, 18
Mke mwema anatafuta kwanza ushauri wa
mumewe kabla ya kutumia fedha na pia
anafanya manunuzi kwa hekima. Ni
muangalifu kununua bidhaa zenye ubora
kulingana na mahitaji ya familia yake.Efeso
5:23
6. Nyumba
Mithali 31:15, 20-22, 27
Mke mwema ni mtu anayeifanya nyumba
iwe mahali pa kuishi. Anatengeneza
mazingira ya kuvutia kwa familia yake na
wageni wote na anawahudumia watu wake
wote kwa ukarimu. 1pet 4:9, Ebrania 13:2
7. Muda
Mithali 31:13, 19, 27
Hutumia muda wake vizuri na kuhakikisha
anakamilisha kazi zake za kila siku. Kamwe
hapotezi muda katika kufanya mambo
ambayo hayampendezi Mungu na yasiyo na
faida.
8. Uzuri / Urembo
Mithali 31:10, 21-22, 24
Ni mrembo na mwenye thamani, ana uzuri
wa ndani unatoka kwa Yesu Kristo.
Anatumia ubunifu wake na utanashati wake
kuleta uzuri katika maisha yake na ya watu
wake.
Mungu atusaidie ili maisha yetu yaonyeshe
kweli tunamjua na kumwamini yeye.
Ubarikiwe na Bwana Yesu!
hadi 31 kimeelezea sifa mbalimbali za mke
mwema, tuangalie kwa uchache sifa hizo
kwa kuzichambua katika maeneo tofauti.
1. Imani
Mithali 31:26, 29, 30
Mke mwema anayashika na kuyafanyia kazi
maneno ya Mungu na ni mtu ambaye
anamtumikia Mungu kwa moyo wake wote
na akili yake yote. Anatafuta makusudi ya
Mungu katika maisha yake na kuyafuata.
Zaburi 119;15
2. Ndoa
Mithali 31:11-12, 23, 28
Mke mwema humuheshimu mume wake na
anahakikisha anamtendea mambo mema
siku zote za maisha yake. Ni wa kuaminika
na msaidizi kwa mume wake. Efeso 5:22-24,
1Petro 3
3. Malezi
Mithali 31: 26, 28
Mke mwema anawafundisha watoto wake
njia za Mungu na pia anawatunza kwa
upendo. Huwafundisha kwa hekima na
kuwaelekeza njia iwapasayo kuiendea.
Mithali 22:6
4. Huduma
Mithali 31:12-15, 17, 20
Mke mwema anamhudumia mume wake na
familia yake yote kwa ukarimu na upendo.
Anahakikisha wanapata chakula kilicho bora
na chenye afya. Ni mtu mwenye huruma na
ukarimu.
5. Mali
Mithali 31:14, 16, 18
Mke mwema anatafuta kwanza ushauri wa
mumewe kabla ya kutumia fedha na pia
anafanya manunuzi kwa hekima. Ni
muangalifu kununua bidhaa zenye ubora
kulingana na mahitaji ya familia yake.Efeso
5:23
6. Nyumba
Mithali 31:15, 20-22, 27
Mke mwema ni mtu anayeifanya nyumba
iwe mahali pa kuishi. Anatengeneza
mazingira ya kuvutia kwa familia yake na
wageni wote na anawahudumia watu wake
wote kwa ukarimu. 1pet 4:9, Ebrania 13:2
7. Muda
Mithali 31:13, 19, 27
Hutumia muda wake vizuri na kuhakikisha
anakamilisha kazi zake za kila siku. Kamwe
hapotezi muda katika kufanya mambo
ambayo hayampendezi Mungu na yasiyo na
faida.
8. Uzuri / Urembo
Mithali 31:10, 21-22, 24
Ni mrembo na mwenye thamani, ana uzuri
wa ndani unatoka kwa Yesu Kristo.
Anatumia ubunifu wake na utanashati wake
kuleta uzuri katika maisha yake na ya watu
wake.
Mungu atusaidie ili maisha yetu yaonyeshe
kweli tunamjua na kumwamini yeye.
Ubarikiwe na Bwana Yesu!