Siamini kama kuna Mtanzania middle class Marekani

Siamini kama kuna Mtanzania middle class Marekani

Huu uzi naweza kujifunza kitu. Mkuu unapoongelea middle class ni mambo gani unaangalia na mtu anatakiwa awe na sifa zipi ili akolifai kuitwa middle class or lower class. Tupe darasa mkuu
 
Una matatizo ya kusoma na kuelewa kilichoandikwa na ndio maana SIAMINI kama Watu ninyi mnaweza kuwa Middle class Marekani, kwa maana Nchi zilizoendelea unalipwa kulingana na IQ yako yaani uwezo wako wa kutatua Matatizo, na hii inakwenda moja kwa moja na kiwango cha Elimu yako, hivyo kama tu unashindwa kusoma na kuelewa kilichoandikwa hapa JF, unawezaje kupata kazi ambayo unatakiwa kutumia akili kuisadia Kampuni kupata faida na kusonga mbele?

Hizo kazi zako za kubeba Maboksi hata ubebe kwa masaa 24 kwa siku kamwe hauwezi kupanda daraja na kuwa Middle class kwenye nchi zilizoendelea, yaani nchi zinazotumia technolia ili kuendelea!
Hizo kazi ni za lower class!
Ka-thread haka bwana,kana ukweli wa kufikirisha.Lakini mtu akiambiwa hali halisi ilivyo kwa wa-tz walio huko watabisha.Kuna waliopiga maisha ki-ukweli,nawafahamu jamaa kama 4 hivi na kati ya hao yupo kijana kabisa anayefanya kazi kwenye kampuni kubwa kabisa marekani(ni moja kati ya makampuni 10 makubwa duniani),ila wengi huku ni hand to mouth,ila tukirudi bongo mbwembwe nyingi na kiingereza cha kuzungumzia puani,kama vile YOU KNOW,WANAMSAPU,YEEE,OKKK!!!na I-pad kubwa masikioni muda wote ikiwa pamoja na kutembea upande upande kama basi la zuberi limekata spring.
:A S-rap:
 
Nadhani wengi mnaojibu hamjajiongeza au hamuwezi kujiongeza. Kwa mujibu wa mleta uzi nilichojiongeza ni kwamba, hakuna uhusiano kati ya kipato na class. Limetumbuka nisahihishe kama siko na wewe. Ila kama ni hivyo, very interesting. Yaani unaweza kuwa na kipato cha chini still ukawa mido klas. Dah!!!! acha nifie Mabibo.:msela:
 
Upo so wrong we jamaa,

Kuna wadau wengi tu wanapiga kaz kwenye Hiz NGO zenye makao makuu huko , ni wabongo na walianzia bongo ila wamekuwa promoted had level za seniors .ni wengi wengi.

Kuna madaktar wengi tu,wafanyabiashara wengi tu na hata wanamichezo wanapiga mzgo huko na kuingiza mpunga mrefu kuliko wa Us wazawa wengi..Ooh Acha kukariri broh! Fanya maisha yako.
 
wewe usiseme mambo ambayo huyajui kiundani bora unyamaze kimya, kuna madaktari ambao wanazo sehemu zao wenyewe tena, tena mmoja ni wa meno 50% kwa mtanzania unatibiwa kwenye sehemu yake, kuna wenye kampuni za kuwahudumikia wagonjwa, vizee, mataahira, kuna wenye daycare, gereji za kweli,kuna ambao mabosi kabisa ofisini wanatengeneza mpka dola 40 kwa saa, kuna wafanyabiashara wanasafiri kila miezi mitatu wapo tz, yaani wengi tuu. na ambao wapo katika kujiendeleza. usilete maada ambao huijui bora kuuliza.
sio rahsi kumuona mtanzania yaani kakaa anasubiri kugaiwa, kijana changamka ila usije kumkata panga mzee wako ili uende marekani kutakushinda utarudi mwenyewe.
 
Hakuna Mtu Middle class Marekani anayefanya kazi masaa 24 kwa siku, hizo kazi ni za lower class, na hata ufanye nini huwezi kuingia middle class kwa kazi hizo!

Una uhakika unachokisema kuhusu masaa ya kazi?

Kwanza nini kinachopima hizo class ni masaa unayofanya kazi? Kiopato cha mwaka mzima? au aina ya kazi? Ukijua majibu ya hayo maswali hamtabishana tena.

Sababu mnabishana bure tu bila kujielewa
 
Umefanya utafiti wako lini na wapi? au huamini tu bila ya kuwa na kigezo chochote kile cha hiyo imani yako? Kwa taarifa yako tu ni kwamba US na hata EU wapo Watanzania ambao wana status zaidi hiyo ya middle class lakini hawapendi kupita huku na kule kujitangaza kwamba mimi hivi mimi vile.

Najua kuna Watz wengi sana wanishi Marekani lkn binafsi siamini kama kuna yoyote yule ambaye ana kipato cha kumfanya awe Middle Class ndani ya Marekani, naamini Watz ambao labda wana hiyo status ni wale wanaofanya Ubalozini ambao wanalipwa na Serikali yetu, ama wale wa UN, lkn wengine wa Uraiani siamini kama kweli wana qualify Middle class Status ya Marekani, sema wakija Bongo wanaonekana wako juu lkn kwa Marekani wengi pmj na kuwa wana kazi lkn bado wana low income status, na Hapa siongelei Watanzania kuanzia Kizazi cha kwanza yaani waliozaliwa na Wazazi watz ndani ya Marekani, hao naamini wako wengi lkn wale Wahamiaji, SIDHANI!
 
Inategemeana na middle class unavyoifikiria, western countries describes in three parts, lower middle class, middle and upper......Wapo wengi middle class in definition but not upper middle class
 
Umefanya utafiti wako lini na wapi? au huamini tu bila ya kuwa na kigezo chochote kile cha hiyo imani yako? Kwa taarifa yako tu ni kwamba US na hata EU wapo Watanzania ambao wana status zaidi hiyo ya middle class lakini hawapendi kupita huku na kule kujitangaza kwamba mimi hivi mimi vile.

Mkuu nakushukuru kwa kutoa mwanga kwa huyu member. Kungekuwa na uweekano au kama wangeweza kutoa ruhusa nigeanza kuorodhesha hapa. Kama ulivyosema kuna watanzania wengi ambao hawataki sifa na kujitaja.

Labda tumuulize tafsiri yake ya middle class ni nini, na ni kwanini kwa mawazo yake watanzania hawapo kwenye hiyo class.

Lakini anachosema kuwa wafanyakazi wa ubalozi ndio middle class, ni uongo mkubwa. Labda aangalia na kujiuliza mapatao yao ni kiasi gani, au aeleze ni kigezo gani anachotumia kuwaona wao ni middle class.

Simple advice atembee anionee...
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Dah we mtoa mada haujawatembelea vizuri wa Tz waliopo USA. Kuna washkaji wana kampuni zao binafsi za kuuza magari mapya huko US, kuna watu wa firm za biashara zilizosimama, kuna madaktari wa clinic zao na wameajiri wazungu tupu nk
 
Ka-thread haka bwana,kana ukweli wa kufikirisha.Lakini mtu akiambiwa hali halisi ilivyo kwa wa-tz walio huko watabisha.Kuna waliopiga maisha ki-ukweli,nawafahamu jamaa kama 4 hivi na kati ya hao yupo kijana kabisa anayefanya kazi kwenye kampuni kubwa kabisa marekani(ni moja kati ya makampuni 10 makubwa duniani),ila wengi huku ni hand to mouth,ila tukirudi bongo mbwembwe nyingi na kiingereza cha kuzungumzia puani,kama vile YOU KNOW,WANAMSAPU,YEEE,OKKK!!!na I-pad kubwa masikioni muda wote ikiwa pamoja na kutembea upande upande kama basi la zuberi limekata spring.
:A S-rap:

Hahahaaaa basi la zuberi.....sipati picha...
 
Hahahaaa mwendelezo wa chuki dhidi ya wabeba maboksi....

Endeleeni kujifariji tu.
 
Ndugu, jifunze kutafuta maarifa kutoka kwenye vyanzo vya kuaminika. Usitegemee mambo ya kijiweni tu. Kuna hata mitandao siku hizi inatoa maarifa mengi sana. Usikae tu ukiwaangalia watu wanaotamba mabarabarani wakitoka majuu ukajua kwamba hao ndiyo wote huko majuu.
Kitu cha kwanza ulitakiwa ujitosheleze kwa kupata maana ya "middle class." Hujasema lolote. Tukusaidie basi. Kwenye wikipidia wanasema hivi: The following is a list of occupations one might expect to find among this class: Accountants, Professors (Post-secondary educators), Physicians, Engineers, Lawyers, Architects, Journalists, Mid-level corporate managers, Writers, Economists, Political Scientists, Urban planners, Financial managers, High school teachers, Registered Nurses (RNs), Pharmacists and analysts, etc...
Hapo tu kwanza jiulize kweli Wabongo wote walio Marekani, hakuna wa profession hizo? Katika tovuti nyingine nilisoma kwamba middle class wana vipato kuanzia $50,000 (lower middle class) hadi $600,000 (upper middle class). Jiulize tena hapo.
Wengi wanaishi huko maisha yao bila makuu wala kujionyesha. Kuna mtu aliwahi kuuliza kwenye forum tutaje hata watatu tu waliofanikiwa kuwa vinara katika nyanja mbalimbali. Tuliweza kuwataja wasomi wahandisi, executive ktk makampuni makubwa, nk. Na wapo wengi sana.
Jielimishe!!!

Najua kuna Watz wengi sana wanishi Marekani lkn binafsi siamini kama kuna yoyote yule ambaye ana kipato cha kumfanya awe Middle Class ndani ya Marekani, naamini Watz ambao labda wana hiyo status ni wale wanaofanya Ubalozini ambao wanalipwa na Serikali yetu, ama wale wa UN, lkn wengine wa Uraiani siamini kama kweli wana qualify Middle class Status ya Marekani, sema wakija Bongo wanaonekana wako juu lkn kwa Marekani wengi pmj na kuwa wana kazi lkn bado wana low income status, na Hapa siongelei Watanzania kuanzia Kizazi cha kwanza yaani waliozaliwa na Wazazi watz ndani ya Marekani, hao naamini wako wengi lkn wale Wahamiaji, SIDHANI!
 
Mkuu mleta mada naona kuna maswali ya muhimu umekacha kuyajibu lakini yale mepesi umeweza kujibizana...

Je daraja la kati kwa Marekani hupimwa vipi?

Je thamani ya mtu wa dajara la kati kwa Marekani ukilinganisha na thamani ya mtu wa daraja kama hilo Tanzania kuna utofauti gani?

By the way hayo uliyoyaandika nadhani yanawagusa zaidi Watanzania waliopo Far East haswa miji kama Macau, Guangzhou na HongKong, kule Watanzania kweli wanahenyeka haswa....
 
Kwa jinsi wazee wa box mlivyobabaisha kumjibu jamaa napata picha labda anachokisema ni kweli. Mmekuja na zile za kiujumla kuwa Kuna washkaji mabosi, Wako wengine wanapiga kazi kubwa na blabla kibao lakini hakuna hata mmoja aliyetoa evidence kumpinga jamaa. Yeye karusha jiwe gizani naona limewapata, hakuna hata mmoja aliyesema "Mimi Ni middle class" kipato changu Ni zaidi ya 50,000 USD kwa mwaka au Fulani anamkwanja huo
 
Kuna watu hiyo hela uliyoweka hapa wanavuta times 4, na hiyo ni baada ya kodi. Evidence kwani hapa tuko mahakamani!? Kama unataka kuamini sawa kama hutaki kuamini pia sawa.


Kwa jinsi wazee wa box mlivyobabaisha kumjibu jamaa napata picha labda anachokisema ni kweli. Mmekuja na zile za kiujumla kuwa Kuna washkaji mabosi, Wako wengine wanapiga kazi kubwa na blabla kibao lakini hakuna hata mmoja aliyetoa evidence kumpinga jamaa. Yeye karusha jiwe gizani naona limewapata, hakuna hata mmoja aliyesema "Mimi Ni middle class" kipato changu Ni zaidi ya 50,000 USD kwa mwaka au Fulani anamkwanja huo
 
Back
Top Bottom