Bongolander
JF-Expert Member
- Jul 10, 2007
- 5,067
- 2,197
Wakuu Great thinkers, napenda mijadala ya kwenye jukwaa hili maana wachangiaji na wakosoaji wanaotumia hoja na busara kuchangia, kukosoa, kushauri na kurekebisha. Watunga sera makini wanafuatilia sana jukwaa hili, kwa kuwa wachangiaji, hata kama si wote wenye weledi, walio wengi si mbumbumbu na vilaza. Kwa hiyo wanaweza kuiangalia nchi yetu kwa kioo cha jukwaa hili.
Nakumbuka sana wakati wa serikali iliyopita ni jukwaa hili ulikuwa unaanikwa uozo mwingi uliopo kimfumo na uliotudunisha kwa muda mrefu kama taifa. Kulikuwa hakuna kushambulia watu, ila kushambulia matendo na kauli zao. Tulishambulia ujinga ule, na wengi wenye akili walikuwa wanasema Tanzania, kwanza na utanzania kwanza. Na baada ya awamu ya tano kuingia madarakani, mengi tuliyokjuwa tunalalamikia huo yamefanyiwa kazi, na mengine hata yamezidi matarajio. (Kumbukeni madili yaliyokuwa yanapigwa kutokana na safari za rais nje ya nchi ambazo hadi leo hii gharama zake anajua Mungu- JPM Ametatua kabisa na kufanya maajabu) The point is hoja zetu zenye maana huwa zinasikilizwa na kufanyiwa kazi, hata kuliko zinazoongewa kwenye mikutano.
Ningependa turudi kwenye njia ile, ili manjuka wajue kuwa mijadala ni hoja zinazolenga issues, na sio mashambulizi ya wasifu binafsi. Au hata kuingia kwenye mambo cheap wakati nchi yetu inahitaji macho makali kwenye mambo makubwa.
Nimekuwa nafuatilia posts naona kama watu wanolalamikia sana serikali, wanawalenga watu, wakisema mambo yanayofanyika sasa yanafanya hali iwe ngumu. Lakini badala ya kueleza mibadala na kuchambua kwa picha kubwa, wanagusa vidone vodone na kuacha mbali picha kamili ya nchi yetu, na kuanza lugha za matusi.
Tujaribu kuangalia ni nini kilikuwepo before JPM, na sasa tukoje. Miaka minne iliyopita sio mbali sana. Kuna ukweli kuwa baada ya hela za dawa za kulevya kuondolewa mitaani, na baada ya hela za ufisadi kupungua sana mitaani, hali iko tofauti. Ndio maana baadhi ya watu wanasema bora wakati wa JK maana hela ilikuwa nje nje, lakini tunasahau kuwa ile hela ilikuwa chafu. Kumbukeni kuwa Eddo alikimbizwa U-PM kutokana na uozo wa madili ya ajabu, Mh Pinda alikuwa kwenye hati hati sababu kasi yake ya kudeal na mambo yanayogusa kutatua taabu za wananchi ilikuwa ndogo. Licha ya changamoto zilizopo sasa mambo yamebadilika sana.
Our country was in verge of becoming a banana republic, we averted that. So we need to do better than throwing cheap shots.
Nakumbuka sana wakati wa serikali iliyopita ni jukwaa hili ulikuwa unaanikwa uozo mwingi uliopo kimfumo na uliotudunisha kwa muda mrefu kama taifa. Kulikuwa hakuna kushambulia watu, ila kushambulia matendo na kauli zao. Tulishambulia ujinga ule, na wengi wenye akili walikuwa wanasema Tanzania, kwanza na utanzania kwanza. Na baada ya awamu ya tano kuingia madarakani, mengi tuliyokjuwa tunalalamikia huo yamefanyiwa kazi, na mengine hata yamezidi matarajio. (Kumbukeni madili yaliyokuwa yanapigwa kutokana na safari za rais nje ya nchi ambazo hadi leo hii gharama zake anajua Mungu- JPM Ametatua kabisa na kufanya maajabu) The point is hoja zetu zenye maana huwa zinasikilizwa na kufanyiwa kazi, hata kuliko zinazoongewa kwenye mikutano.
Ningependa turudi kwenye njia ile, ili manjuka wajue kuwa mijadala ni hoja zinazolenga issues, na sio mashambulizi ya wasifu binafsi. Au hata kuingia kwenye mambo cheap wakati nchi yetu inahitaji macho makali kwenye mambo makubwa.
Nimekuwa nafuatilia posts naona kama watu wanolalamikia sana serikali, wanawalenga watu, wakisema mambo yanayofanyika sasa yanafanya hali iwe ngumu. Lakini badala ya kueleza mibadala na kuchambua kwa picha kubwa, wanagusa vidone vodone na kuacha mbali picha kamili ya nchi yetu, na kuanza lugha za matusi.
Tujaribu kuangalia ni nini kilikuwepo before JPM, na sasa tukoje. Miaka minne iliyopita sio mbali sana. Kuna ukweli kuwa baada ya hela za dawa za kulevya kuondolewa mitaani, na baada ya hela za ufisadi kupungua sana mitaani, hali iko tofauti. Ndio maana baadhi ya watu wanasema bora wakati wa JK maana hela ilikuwa nje nje, lakini tunasahau kuwa ile hela ilikuwa chafu. Kumbukeni kuwa Eddo alikimbizwa U-PM kutokana na uozo wa madili ya ajabu, Mh Pinda alikuwa kwenye hati hati sababu kasi yake ya kudeal na mambo yanayogusa kutatua taabu za wananchi ilikuwa ndogo. Licha ya changamoto zilizopo sasa mambo yamebadilika sana.
Our country was in verge of becoming a banana republic, we averted that. So we need to do better than throwing cheap shots.