peno hasegawa
JF-Expert Member
- Feb 24, 2016
- 12,829
- 21,460
Kampuni ya Yapi Markezi haina uwezo tena wa kifedha kuendeleza huu mradi na ni wazi kuna mambo yanafichwafichwa sana juu ya nini chanzo na nani yuko nyuma ya hili jambo baya kabisa kuwahi kutokea. Yaani hela za mradi zimeibwa halafu tunakwenda kukopa nyingine kufidia zilizoibwa!.
Mradi huu una mikopo lukuki na yote tulitangaziwa hapa na tunajua fedha zote za kukamilisha mradi huu zilipatikana zote na ili kuweka angalizo kwa watanzania tunawakumbusha kuwa huu ni mkopo na watakaolipa ni watanzania hawa masikini.
Leo mradi umesimama na mkandarasi kaweka wazi kuwa hana fedha!. tunachukulia jambo hili kiwepesi sana na kama ni jambo dogo na hakuna shida yoyote lakini leo nataka niseme kuna WIZI MKUBWA sana umefanyika kwenye huu mradi mpaka mkandarasi kakosa fedha kuendelea na mradi na kazi imesimama. Hii ni kashfa kubwa sana na hatuwezi kukaa kimya hata iweje.
Vyanzo vyetu vinasema MAJIZI hayo yakichukua hela yao "in advance" mara tu mkataba uliposainiwa na ndiyo maana Yapi Markezi wamefika mahali hela waliyotoa rushwa kwa lazima imeleta nakisi kwenye utekelezaji.
Hatuwezi kulitazama hili kirahisi tu na kuona ni jambo la kawaida na sasa tunatafuta nkopo mwingine kama nchi ili kumalizia mradi! Swali ni kuwa nani kaina fedha za mwanzo? Nani yuko nyuma ya hii michezo kiasi kwamba anaogopwa kutajwa na kushughulikiwa mpaka nchi inaingia kwenye mchakato wa kutafuta mkopo mwingine kumalizia mradi? Huyu MWIZI special hivi ni nani mpaka anapewa ulinzi wa hivi?
CAG hivi upo kweli? Yaani huu mradi kinachojufanya usiukague ni kitu gani? Bunge hivi mpo kabisa yaani na haya yanatokea mnaona sawa tu? Mnashindwa nini kutoa azimio la kumtaka CAG akague na kuweka wazi shida iko wapi?
Sisi tunajua nani yuko nyuma ya hasara hii kubwa kwa hili taifa na tunajua nguvu inatumika kumficha na kumlinda lakini watanzania hawa pamoja na ujinga wao na ulofa wao hawapaswi kupitishwa kwenye njia hii na kama vyombo husika hasa wewe CAG hamtachunguza hili basi tutawasaidia ifikapo 1 January 2024 siku ya mkesha wa mwaka mpya! (Siku hii utakuwa ni ukurasa mpya unafunguliwa)
Haiwezekani kuwatia watanzania kwenye shida ya deni jingine kubwa hivi huku tunamjua mtu aliye katikati ya haya madili na tunaogopa kumsema!. Watanzania siyo malofa na wajinga kiasi hicho hata kama wanakaa kimya.
Hatuwezi kukaa wa watu kama Kadogosa pale TRL badala ya kufanya kazi wao wako hapo kwa ajili ya kusaidia watu kuiba fedha za watanzania na wanaogopa kuwasema kwa kuwa wanataka kulinda nafasi zao na vyeo vyao na wengine wameahidiwa ubunge kama Kadogosa. Nyie kama mnawaogopa ni vizuri lakini sisi Kigogo Media hatujawahi kumuogopa mtu na hili linajulikana na tutasema waziwazi ili kila mtu ashinde mechi zake.
Watanzania kuna wizi na kashfa ya kutisha kwenye mradi wa SGR na chanzo cha Yapi Markezi kukwama kuendelea na kazi ni mabilioni ya fedha yamekwapuliwa na wakubwa wakati wa kuwapa tenda sasa hawana hela tena.
Mradi huu una mikopo lukuki na yote tulitangaziwa hapa na tunajua fedha zote za kukamilisha mradi huu zilipatikana zote na ili kuweka angalizo kwa watanzania tunawakumbusha kuwa huu ni mkopo na watakaolipa ni watanzania hawa masikini.
Leo mradi umesimama na mkandarasi kaweka wazi kuwa hana fedha!. tunachukulia jambo hili kiwepesi sana na kama ni jambo dogo na hakuna shida yoyote lakini leo nataka niseme kuna WIZI MKUBWA sana umefanyika kwenye huu mradi mpaka mkandarasi kakosa fedha kuendelea na mradi na kazi imesimama. Hii ni kashfa kubwa sana na hatuwezi kukaa kimya hata iweje.
Vyanzo vyetu vinasema MAJIZI hayo yakichukua hela yao "in advance" mara tu mkataba uliposainiwa na ndiyo maana Yapi Markezi wamefika mahali hela waliyotoa rushwa kwa lazima imeleta nakisi kwenye utekelezaji.
Hatuwezi kulitazama hili kirahisi tu na kuona ni jambo la kawaida na sasa tunatafuta nkopo mwingine kama nchi ili kumalizia mradi! Swali ni kuwa nani kaina fedha za mwanzo? Nani yuko nyuma ya hii michezo kiasi kwamba anaogopwa kutajwa na kushughulikiwa mpaka nchi inaingia kwenye mchakato wa kutafuta mkopo mwingine kumalizia mradi? Huyu MWIZI special hivi ni nani mpaka anapewa ulinzi wa hivi?
CAG hivi upo kweli? Yaani huu mradi kinachojufanya usiukague ni kitu gani? Bunge hivi mpo kabisa yaani na haya yanatokea mnaona sawa tu? Mnashindwa nini kutoa azimio la kumtaka CAG akague na kuweka wazi shida iko wapi?
Sisi tunajua nani yuko nyuma ya hasara hii kubwa kwa hili taifa na tunajua nguvu inatumika kumficha na kumlinda lakini watanzania hawa pamoja na ujinga wao na ulofa wao hawapaswi kupitishwa kwenye njia hii na kama vyombo husika hasa wewe CAG hamtachunguza hili basi tutawasaidia ifikapo 1 January 2024 siku ya mkesha wa mwaka mpya! (Siku hii utakuwa ni ukurasa mpya unafunguliwa)
Haiwezekani kuwatia watanzania kwenye shida ya deni jingine kubwa hivi huku tunamjua mtu aliye katikati ya haya madili na tunaogopa kumsema!. Watanzania siyo malofa na wajinga kiasi hicho hata kama wanakaa kimya.
Hatuwezi kukaa wa watu kama Kadogosa pale TRL badala ya kufanya kazi wao wako hapo kwa ajili ya kusaidia watu kuiba fedha za watanzania na wanaogopa kuwasema kwa kuwa wanataka kulinda nafasi zao na vyeo vyao na wengine wameahidiwa ubunge kama Kadogosa. Nyie kama mnawaogopa ni vizuri lakini sisi Kigogo Media hatujawahi kumuogopa mtu na hili linajulikana na tutasema waziwazi ili kila mtu ashinde mechi zake.
Watanzania kuna wizi na kashfa ya kutisha kwenye mradi wa SGR na chanzo cha Yapi Markezi kukwama kuendelea na kazi ni mabilioni ya fedha yamekwapuliwa na wakubwa wakati wa kuwapa tenda sasa hawana hela tena.