WINGER_TEREZA
JF-Expert Member
- Jul 31, 2015
- 242
- 450
Habari, Jana msanii tajika sana nchini Tanzania, Afrika Mashariki na kati na pengine kuliko wote kusini mwa jangwa la Sahara Naseeb Abdul, maarufu kama Diamond Platnumz, alisaini dili kubwa na moja kati ya recording label kubwa ya muziki dunia, Warner Music Group, kuhusu usambazaji wa kazi za muziki wake na Wasanii walio katika label yake ya WCB WASAFI.
Muda mfupi baada ya Diamond kusaini mkataba huo alitumia page za mitandao ya kijamii ya Instagram na Twitter kutoa shutuma kwa kampuni kubwa ya Kimarekani inayojihusisha na tafiti za kubaini watu wenye ukwasi (UTAJIRI), FORBES, kuwa hawakufanya tathimini vizuri juu ya ukwasi aliona kupitia ile list waliyoitoa last week inayonesha Wasanii matajiri zaidi barani Afrika ambapo kwenye list hiyo Naseeb hayumo hata kwenye top 20!
Sio mara ya kwanza hawa FORBES kulalamikiwa na baadhi ya watu juu ya takwimu zao kwa mfano ni mwaka jana tu rapper Mkubwa toka "STATE", Kanye West, alilalamika na kuwapa makavu hao FORBES kwa kumkadilia kiduchu juu ya utajiri wake kitu achapo kilizua gumzo sana Dunia nzima na ikapelekea kwa hao FORBES kuingia chimbo kumkadilia tena Kanye na hatimaye wakamtangaza kuwa yuko katika orodha ya Ma-rapper billionares sambamba na Jay Z, P.Diddy na Dr Dree.
Kwa huku kwetu Tanzania, kila mwaka FORBES wamekuwa wakitoa orodha ya watu matajiri zaidi nchini na kwa mara zote wamekuwa wakimtaja Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya Mohammed Enterprises (METL), Mohammed Dewji - Mo, kuwa ndiye billionaire kinara hapa kwetu na pengine ndiye billionare kijana kuliko wote Afrika. Hii imekuwa ikipingwa na baadhi ya watu hasa katika "vijiwe vya kahawa" kwani wengine wanaamini kuwa mmiliki wa Makampuni ya Said Salim Bakhresa (SSB Group of Companies) - Saidi Bakheresa kuwa ndiye mwenye pesa nyingi kuliko wote hapa Tanzania kwani ana mali zisizo amishika zinazo onekana na kujilikana na kila mtu tofauti na huyo MO.
Kwa scenerio hizo, nami kama naanza kuamini hayo maneno ya Vijiweni kuwa Bakhresa ndiyo tajiri namba moja hapa kwetu Tz kwani kila mtu anaziona mali zake kama Wiwanda vyake kila kona hapa nchini na kwa DSM Mfano ni pale Buguruni, Mwandege, Uwekezaji Mkubwa pale Chamazi - Azam complex, kuleze Zanzibar ana uwekezaji mkubwa sana sitaweza kutaja wote ila chukulia mfano wa Hotel Verde na ule Mji wa kitalii wa Fumba. Ana mradi mkubwa wa uzalishaji wa miwa pale Bagamoyo ambapo itapelekea kuanzishwa kwa kiwanda kikubwa cha sukari nchini. Pia bidhaa za Azam zimekuwa nambari moja katika nchi nyingi za Afrika na ni nadra sana kwa Mtanzania wa kawaida kupita siku bila kutumia bidhaa hata moja ya Azam hasa za Vyakula na Vinywaji!.
Mwisho napenda kuhitimisha kuwa pengine Diamond yuko sahihi kuwa Forbes memkadilia vibaya na pia Forbs wamemkadilia vibaya Bakhera (kwa Bakhersa nina asilimia kubwa hii ni kutokana na hulka yake ya kutopenda kuweka mambo yake hadharani na huwa hapendi kujionesha wala kuonekana onekana tofauti na MO au matajiri wengine tunao wajua).
Nawasilisha na asanteni.
Muda mfupi baada ya Diamond kusaini mkataba huo alitumia page za mitandao ya kijamii ya Instagram na Twitter kutoa shutuma kwa kampuni kubwa ya Kimarekani inayojihusisha na tafiti za kubaini watu wenye ukwasi (UTAJIRI), FORBES, kuwa hawakufanya tathimini vizuri juu ya ukwasi aliona kupitia ile list waliyoitoa last week inayonesha Wasanii matajiri zaidi barani Afrika ambapo kwenye list hiyo Naseeb hayumo hata kwenye top 20!
Sio mara ya kwanza hawa FORBES kulalamikiwa na baadhi ya watu juu ya takwimu zao kwa mfano ni mwaka jana tu rapper Mkubwa toka "STATE", Kanye West, alilalamika na kuwapa makavu hao FORBES kwa kumkadilia kiduchu juu ya utajiri wake kitu achapo kilizua gumzo sana Dunia nzima na ikapelekea kwa hao FORBES kuingia chimbo kumkadilia tena Kanye na hatimaye wakamtangaza kuwa yuko katika orodha ya Ma-rapper billionares sambamba na Jay Z, P.Diddy na Dr Dree.
Kwa huku kwetu Tanzania, kila mwaka FORBES wamekuwa wakitoa orodha ya watu matajiri zaidi nchini na kwa mara zote wamekuwa wakimtaja Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya Mohammed Enterprises (METL), Mohammed Dewji - Mo, kuwa ndiye billionaire kinara hapa kwetu na pengine ndiye billionare kijana kuliko wote Afrika. Hii imekuwa ikipingwa na baadhi ya watu hasa katika "vijiwe vya kahawa" kwani wengine wanaamini kuwa mmiliki wa Makampuni ya Said Salim Bakhresa (SSB Group of Companies) - Saidi Bakheresa kuwa ndiye mwenye pesa nyingi kuliko wote hapa Tanzania kwani ana mali zisizo amishika zinazo onekana na kujilikana na kila mtu tofauti na huyo MO.
Kwa scenerio hizo, nami kama naanza kuamini hayo maneno ya Vijiweni kuwa Bakhresa ndiyo tajiri namba moja hapa kwetu Tz kwani kila mtu anaziona mali zake kama Wiwanda vyake kila kona hapa nchini na kwa DSM Mfano ni pale Buguruni, Mwandege, Uwekezaji Mkubwa pale Chamazi - Azam complex, kuleze Zanzibar ana uwekezaji mkubwa sana sitaweza kutaja wote ila chukulia mfano wa Hotel Verde na ule Mji wa kitalii wa Fumba. Ana mradi mkubwa wa uzalishaji wa miwa pale Bagamoyo ambapo itapelekea kuanzishwa kwa kiwanda kikubwa cha sukari nchini. Pia bidhaa za Azam zimekuwa nambari moja katika nchi nyingi za Afrika na ni nadra sana kwa Mtanzania wa kawaida kupita siku bila kutumia bidhaa hata moja ya Azam hasa za Vyakula na Vinywaji!.
Mwisho napenda kuhitimisha kuwa pengine Diamond yuko sahihi kuwa Forbes memkadilia vibaya na pia Forbs wamemkadilia vibaya Bakhera (kwa Bakhersa nina asilimia kubwa hii ni kutokana na hulka yake ya kutopenda kuweka mambo yake hadharani na huwa hapendi kujionesha wala kuonekana onekana tofauti na MO au matajiri wengine tunao wajua).
Nawasilisha na asanteni.