sinza pazuri
JF-Expert Member
- Aug 16, 2014
- 2,525
- 7,374
Diamond Platinumz msanii namba moja Africa ni zaidi ya msanii.
Mimi namuita mwanamapinduzi au kwa kilami wanasema game changer na anaendelea kulionesha ilo kwa vitendo.
Jambo lolote ambalo lilionekana haliwezekani kwenye industry yetu ya burudani yeye alibadilisha mtazamo na kuwa inawezekana.
Kautoa muziki wetu mbali kutoka kuwa muziki wa masela na mwanangu mwanangu mpaka kuwa industry yenye wafanyabiashara.
Kila mtu alimshangaa miaka zaidi ya kumi nyuma aliposema hawezi kufanya show chini ya dau la million 10 leo hii tunaona wasanii wanafanya shows za dollar elfu 50.
Amekuwa mfanyabiashara mkubwa wa music lebo, media, betting, real estate na kuna biashara nyingine kubwa anakuja kumtambulisha mwaka huu.
Uzuri wasanii wengi wanaiga mazuri yake na si vibaya kujifunza kwa waliofanikiwa kinachowashinda tu uwa ni consistency.
Diamond Platinumz anaanzisha wengine wanafata mwana mapinduzi.