Shule za miaka ya 1980 na 1990 mwanzoni

Shule za miaka ya 1980 na 1990 mwanzoni

ndekarishia

Senior Member
Joined
Feb 9, 2012
Posts
106
Reaction score
22
Nimekuwa nikizikumbuka shule za miaka ya 80 na 90 ambazo kila mzazi alitamani mwanae asome mojawapo kati ya hizo. Mimi binafsi nilifaulu std VII kwenda Mawenzi sec Moshi lakini mzee wangu alinihamishia Umbwe mapema sana, hiyo ilikuwa 1992. Najiuliza kipindi kile shule hizi zilikuwa na nini na kwa sasa hazisikiki tena?

Shule hizo ni Umbwe, Weruweru, Ashira, Usagara, Galanos, Pugu, Ilboru, azania, Jangwani, Mazengo, Msalato, Iringa Girls, Tosamaganga,, Loleza, Mbeya Sec, Mzumbe, Kibaha, Tanga Tech, Minaki, Nganza, Songea Boys/girls, old Moshi, nk...

Kilichozipoteza shule hizi nini?
 
Mbona hizo shule heshima yake iliishia 2002 sio 1980-1990
Zilikua shule kweli kweli ,na tabora boys ,kilakala,
 
Baadhi hata sasa zina rock japo zinakumbwa na matatizo mengi
 
Masikini umbwe shule yangu .......

Mkuu msg yako imenipa hisia kali sana...nakuona umeikumbuka Shule uliyosoma....hapo lazima wazo limekuijia na kukumbuka Siku za nyuma za life yako enzi za Shule,

Huwa inahuzunisha sana mtu ukiwaza maisha ya Shule hasa kama umri wako umesogea kidogo..
 
Mara secondary, Musoma Alliance, Bwiru boys na girls, nk
 
Kilichozipoteza shule hizo na nyingine nyingi ni siasa! Siasa imeingilia Elimu kiasi kwamba hakuna ufanisi tena kwenye elimu. Kama mwanafunzi asiyejua kusoma na kuandika anaenda sekondari,unategemea shule hizo zibaki kuwa bora?
 
kwl mkuu, shule nyingi za zaman hasa ilboru, mzumbe, kibaha, tabora boy, tabora girls, kilakala na msalato siku hz zmekosa ufuatiliaji mzur na watoto wengi wanaopelekwa hapo wengi ni mabogus coz watoto wengine wasio na vipaji vya akil huamia hapo na kuleta aibu kwenye shule hizo hasa za vipaji maalum, pia mazingira ya shule ni magumu kwa walimu na maslahi ya walimu hayasimamiwi ndo maana shule kongwe nyingi zinafanya vibaya, serikal inapaswa iwe makin kuziangalia na kuzikumbuka shule kongwe maana viongoz wengi wa nchi hii hasa wa serikal kuu wametoka kwenye shule kongwe, kipindi cha nyuma ilikuwa ikitajwa ilboru tanzania nzima inatetemeka kwa performance yao lakini sasa hv watu wanaona ni ya kawaida maana imepoteza umaarufu wake, walimu wa shule hizo kongwe jitahidin kujituma walau sifa zirud, pia watoto wanaopangwa hapo wajitume ile kurudisha heshima za shule kongwe, pia na wadau mlotoka ktk shule kongwe kumbuken kuzitembelea ili kujua kuna shida gan na kitu gan kifanyike ili kuboresha taaluma za shule hizo
 
Nimekuwa nikizikumbuka shule za miaka ya 80 na 90 ambazo kila mzazi alitamani mwanae asome mojawapo kati ya hizo. Mimi binafsi nilifaulu std VII kwenda Mawenzi sec Moshi lakini mzee wangu alinihamishia Umbwe mapema sana, hiyo ilikuwa 1992. Najiuliza kipindi kile shule hizi zilikuwa na nini na kwa sasa hazisikiki tena?

Shule hizo ni Umbwe, Weruweru, Ashira, Usagara, Galanos, Pugu, Ilboru, azania, Jangwani, Mazengo, Msalato, Iringa Girls, Tosamaganga,, Loleza, Mbeya Sec, Mzumbe, Kibaha, Tanga Tech, Minaki, Nganza, Songea Boys/girls, old Moshi, nk...

Kilichozipoteza shule hizi nini?
Mkuu wingi wa shule binafsi na kata zimeua umaarafu na ubora wa shule hizi. Siasa ndani YA wizara YA Elimu ndio tatizo
Tuliosoma miaka hiyo tunafahamu ubora wa shule tajwa.
 
Back
Top Bottom