Shule ya Serikali Pwani kupewa jina la Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo

Daisy Llilies

JF-Expert Member
Apr 19, 2019
1,017
2,154
1590925297517.png


Waziri wa TAMISEMI Selemani Jafo amemuagiza Mkurugenzi wa halmashauri ya Kisarawe kuisajili shule mpya ya wasichana Kisarawe kwa jina la mkuu wa wilaya hiyo, Joketi Mwegelo.

Jokate amepokea taarifa hiyo kwa hisia na kusema hiyo ni heshima kubwa ambayo kuifikia amevumilia mengi ikiwemo baadhi ya watu kujaribu kumbeza na kumvua utu wake.

"Nilipoteuliwa wapo walibeza na wengine kujaribu kunivua utu wangu. Niliwaelewa lakini. Pwani wanasema Aso Mtu Ana Mungu. Namshukuru Mungu wangu kwa kunitetea. Mhe Waziri Jafo kamuelekeza DED kuisajili hii shule ya kihistoria Kisarawe na iitwe Jokate Mwegelo Girls Secondary School", Ameandika mkuu huyo wa wilaya aliyepata pia kuwa mshindi wa pili kwenye mashindano ya Miss Tanzania mwaka 2006.
 
Kwanza nitangulize shukrani zangu za dhati kwako mkuu wa wilaya yetu ya Kisarawe!

Napenda juhudi zako,u bunifu wako na fighting spirit chanya juu ya wilaya yetu.

Sambamba na juhudi zako ndani ya muda mfupi kumekuwa na mabadiliko mazuri ndani ya wilaya, nakupongeza sana.
Nije kwenye kiini cha uzi wangu;

Shule yetu mpya inayotarajiwa kutoa elimu hivi karibuni IWE YA O'LEVEL YA WASICHANA WENYE UFAULU MZURI KUTOKA DARASA LA SABA.

Iwe inachukuwa japo wasichana watatu toka kila shule wilaya nzima. Hii itasaidia sana kuwawezesha watoto waliokuwa na uwezo kuendeleza taaluma zao bila ya kukumbana na changamoto za kimazingira na vishawishi.

Pia watoto wahusishwe moja kwa moja kwenye programs mbalimbali mathalani kilimo cha mboga mboga, uhifadhi wa mazingira pamoja na uzalishaji wa miche ya mazao kama minazi, maembe, mikorosho, michungwa na mipapai.

Kuwepo na mkuu wa shule mtendaji hasa atakaye simamia taaluma, nidhamu, mazingira na projects mbalimbali shuleni
 
Umeshauri vema sana mkuu hilo LA kuchukua watoto watatu sikubalian nawe katika kila shule kikubwa waweke wastani fulan ambao watoto wafikie ili wachaguliwe kujiunga hapo

Unajua kuna shule nyingne za msingi unakuta ufaulu wa wanafunz huwa hafifu sana mfano unaweza kuta shule A mtoto wa 1 kapata alama 200 mtoto wa 2 kapata 198 watatu kapata 196 mtoto wa 4 kapata 195

Lakini shule B wakwanza 190 wapili 180 wa tatu 177

Huoni hapo utakuwa hujawatendea haki mtoto wa shule A aliyepata wastan wa alama195 ambapo kamshinda had wa kwanza kutoka shule B.

HONGERA SANA DC JOKATE
 
Hivi hii shule imejengwa kwa kodi zetu au au jokate ndyo katoa pesa?

Jk na mkapa wamejenga mamia ya shule za kata ila kibinafsi sijasikia hata moja inajina la Mkapa au JK.

Kigogo inabidi atueleze usiku wa siku ya kuweka jiwe ikulu ya chamwino alikuwa wapi.
 
Kajenga kwa kuokoteza michango kutoka kwa wadau mbali mbali mpaka Shule imekamilika.Nyie wakati anachangisha mlimtukana,leo kafanikisha ujenzi wa Shule mnaoji.Zile bilioni alizochangiwa na watu pamoja na Pierre kuchangia Madawati angezitafuna mgehoji.Kapambana na hiyo ni legacy yake kutokana na juhudi zake.

Umefika wakati ukipewa nafasi lazima ujitume kuacha legacy nyuma.Hongera Jokate hata Wilaya ingebadilishwa ipewe jina lako sawa.Toka tupate Uhuru Kisarawe Ni Wilaya za mwanzo kabisa lakini wewe Umefanikiwa kuleta maji. Wabongo vizavizabina ukichutama watasema ukisimama watasema.Jifunze kujituma na kufanya kazi kwa bidii acha Majungu.
 
Hivi hii shule imejengwa kwa kodi zetu au au jokate ndyo katoa pesa?

Jk na mkapa wamejenga mamia ya shule za kata ila kibinafsi sijasikia hata moja inajina la Mkapa au JK.

Kigogo inabidi atueleze usiku wa siku ya kuweka jiwe ikulu ya chamwino alikuwa wapi.
Nachoelewa shule imejengwa kutokana na kampeni ya tokomeza zero ambayo aliiendesha mwenyewe na kupitia influence yake kama celebrity ikafanikiwa. Hata ikiitwa jina lake sio mbaya maana ni legacy yake mwenyewe kama mkuu wa wilaya
 
Kajenga kwa kuokoteza michango kutoka kwa wadau mbali mbali mpaka Shule imekamilika.Nyie wakati anachangisha mlimtukana,leo kafanikisha ujenzi wa Shule mnaoji.Zile bilioni alizochangiwa na watu pamoja na Pierre kuchangia Madawati angezitafuna mgehoji.Kapambana na hiyo ni legacy yake kutokana na juhudi zake.Umefika wakati ukipewa nafasi lazima ujitume kuacha legacy nyuma.Hongera Jokate hata Wilaya ingebadilishwa ipewe jina lako sawa.Toka tupate Uhuru Kisarawe Ni Wilaya za mwanzo kabisa lakini wewe Umefanikiwa kuleta maji.Wabongo vizavizabina ukichutama watasema ukisimama watasema.Jifunze kujituma na kufanya kazi kwa bidii acha Majungu.
kwel kabisa
 
Kwanza nitangulize shukrani zangu za dhati kwako mkuu wa wilaya yetu ya Kisarawe!

Napenda juhudi zako,u bunifu wako na fighting spirit chanya juu ya wilaya yetu.

Sambamba na juhudi zako ndani ya muda mfupi kumekuwa na mabadiliko mazuri ndani ya wilaya, nakupongeza sana.
Nije kwenye kiini cha uzi wangu;

Shule yetu mpya inayotarajiwa kutoa elimu hivi karibuni IWE YA O'LEVEL YA WASICHANA WENYE UFAULU MZURI KUTOKA DARASA LA SABA.

Iwe inachukuwa japo wasichana watatu toka kila shule wilaya nzima. Hii itasaidia sana kuwawezesha watoto waliokuwa na uwezo kuendeleza taaluma zao bila ya kukumbana na changamoto za kimazingira na vishawishi.

Pia watoto wahusishwe moja kwa moja kwenye programs mbalimbali mathalani kilimo cha mboga mboga, uhifadhi wa mazingira pamoja na uzalishaji wa miche ya mazao kama minazi, maembe, mikorosho, michungwa na mipapai.

Kuwepo na mkuu wa shule mtendaji hasa atakaye simamia taaluma, nidhamu, mazingira na projects mbalimbali shuleni
Jokate apitie hapa
 
Back
Top Bottom