Hismastersvoice
JF-Expert Member
- Jan 26, 2013
- 23,261
- 28,422
- Thread starter
-
- #181
Hapo sasa naanza kuelewa hivyo CCM iliichukua shule ya serikali! Haikubaliki.Ukipita uwanja wa mpira wa zamani nadhani ndipo hapo ilipokuwa hiyo shule. Miaka ya 83 kurudi nyuma na baada ya miaka unsyoitaja wewe palikuwa na shule (of course ilikuwa ya zamani sana) ilijulikana kana Mbeya Primary.
Kama sijakosea sana mwaka 1983 hiyo primary school ilifutwa na wanafunzi wakahamishiwa shule nyingine nadhani Mabatuni na Mapinduzi halafu pale pakaanzishwa shule ya Sekondari Meta.
Ilikuwa ya wazungu ila baada ya uhuru tukawa wanafunzi wa mwanzo kusoma hapo, idadi kubwa ya walimu walikuwa ni wazungu na wanafunzi pia pamoja na wahindi wengi zaidi na waafrika....ilikuwa kama Ulaya.
Mkuu kama umesoma Sangu Sec School bila shaka utakuwa unayajua haya maeneo Msichoke Pub.. upande wa pili ukivuka barabara ya lami...kulikuwa na mishkaki na pombe za kienyeji hapo.....Savoi Bar...na Vamponji...moja kati ya maeneo ambayo tumegonga sana ulabu enzi hizo...Mimi nlisoma sangu form 1 miaka 90s
Tulidhuru hpo kimichezo
Ila kuna mzee mmoja alisomaga enzi hzo hpo iyunga ukicheki picha za kitambo kile shule ilikuwa kama iko mbele
Hata kibasila enzi hizo iko chini ya waghoaa ilikuwa nzuri
Ila mzee baba alipozitaifisha tu akashindwa ziendesha
Ova
Siku hizi kuna bweni la Mkapa? Mimi kitambo nilitoka kulikuwa hamna bweni nilikuwa linaitwa mkapa kati haya ni lipi bweni limebadilishwa linaitwa mkapa? Mgabe,Lumumba,kawawa, S.Robert,Luthuli majina mawili ya bweni nimesahau moja karibu na mgabe kama unaelekea s,Robert na lingine opposite na kawawa.
Kati ya bweni zote Luthuli A ndio baba laoMadom mengine ni Amri Abeid, Sokoine, State ya Juu na State ya Chini.... States zilikuwa bweni za wajanja ukiachilia mbali Mkapa ilipoungua.
Asante kwa picha hizi, naiona main hall, haikujengwa kiswahili lilikuwa na jukwaa kubwa lenye pazia kubwa, nakumbuka kikundi kimoja cha utamaduni toka Guinea kiitwacho Djoriba kilikuja kutumbwiza hapa, ni kikundi cha serikali kama tulichokuwa nacho Tanzania, pia naona mabweni mimi nilikuwa la kushoto kuelekea madarasani nilikuwa kwenye chumba cha attachment watu watatu, kuelekea kulia dining hall na bakery.
Mbeya Day iliwahi kutoa waziri wa ulinzi mhe. Kibona (deceased) wakati wa rais Mwinyi kama sijakosea wakati Iyunga ilitoa rais wa makaburu Botha.Mbeya day shule yangu ya O'level sidhani Kama ndio hiyo.Mbeya day imeanzishwa 1964
Lile jengo lilitumika miaka 2 kama sikosei.Mkapa ni bweni lipo nyuma ya Luthuli. Kama unaweza kuvuta picha, kuna jengo lilikuwa kule Karibu na Luthuli.
Pia kuna jengo jipya lilijengwa mbele ya Luthuli, linatizamana na mlango wa Luthuli...Lile niliondoka lilikuwa bado halijaanza kutumika.
Tumerudi nyuma babu.Sasa niwape mpangilo wa mlo kwa siku.
1. Breakfast: yai, mkate uliochomwa (toast), maziwa,uji, silesia za mkate, jamu, siagi.
2. Saa nne asubuhi: chai ya maziwa, keki, cocoa, silesi za mkate na maziwa, uchag nouzi ni wako mezani.
3. Chakula mchana: viazi mviringo ( kila siku mpiko tofauti) nyama ( kilasiku mpiko tofauti) silesi ya mkate, ndizi mbivu na pudding.
4. Saa kumi: keki, maziwa, Silesi za mkate, cocoa, chai ya maziwa.
5. Chakula cha jioni: supu, wali njegere au nyama roast, au chips au mchanganyo wa kihoteli wapishi watakavyokuwa wameandaa, Silesi ya mkate, jamu, siagi,chai ya maziwa, karanga zilizokaangwa.
Kutokana na uandaaji huu lilikuwa hakuna sababu walimu kula majumbani mwao labda tu akipenda, je, tumesonga mbele kimaendeleo au tumerudi nyuma.
Namuona bwana Mng'ong'o anasoma Risala..hahaha Maximo mbabe sana .
Mzee unasema kweli Botha alisoma iyunga?Mbeya Day iliwahi kutoa waziri wa ulinzi mhe. Kibona (deceased) wakati wa rais Mwinyi kama sijakosea wakati Iyunga ilitoa rais wa makaburu Botha.
Si kumi, ni zaidi ya elfu moja na hatutaweza kufika huko labda nchi iundwe upya.Tumerudi nyuma babu.
Tena hatau kumi nyuma ..daaah
Ndiyo, wanafunzi toka Afrika Kusini na Southern Rhodesia walikuwa wanakuja kusoma hapo wakati wa Mbeya School.Mzee unasema kweli Botha alisoma iyunga?
Hahahaa...Daaah! Naomba nijibu kwanza tumerudi nyumaSasa niwape mpangilo wa mlo kwa siku.
1. Breakfast: yai, mkate uliochomwa (toast), maziwa,uji, silesia za mkate, jamu, siagi.
2. Saa nne asubuhi: chai ya maziwa, keki, cocoa, silesi za mkate na maziwa, uchag nouzi ni wako mezani.
3. Chakula mchana: viazi mviringo ( kila siku mpiko tofauti) nyama ( kilasiku mpiko tofauti) silesi ya mkate, ndizi mbivu na pudding.
4. Saa kumi: keki, maziwa, Silesi za mkate, cocoa, chai ya maziwa.
5. Chakula cha jioni: supu, wali njegere au nyama roast, au chips au mchanganyo wa kihoteli wapishi watakavyokuwa wameandaa, Silesi ya mkate, jamu, siagi,chai ya maziwa, karanga zilizokaangwa.
Kutokana na uandaaji huu lilikuwa hakuna sababu walimu kula majumbani mwao labda tu akipenda, je, tumesonga mbele kimaendeleo au tumerudi nyuma.
Basi mzee wazazi wako walikuwa na uwezo wa kifedhaIlikuwa ya wazungu ila baada ya uhuru tukawa wanafunzi wa mwanzo kusoma hapo, idadi kubwa ya walimu walikuwa ni wazungu na wanafunzi pia pamoja na wahindi wengi zaidi na waafrika.
Kwani kuna Luthuli A na Luthuli nyingine...?Luthuli A hiyo.... Kushoto unaweza liona bweni la mkapa au disp zamaniView attachment 1107278
Luthuli B ni kule kwenye hallKwani kuna Luthuli A na Luthuli nyingine...?