Shukran zangu nyingi kwa Members wa JF

Shukran zangu nyingi kwa Members wa JF

LOGORIDDIM

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2013
Posts
1,626
Reaction score
1,207
‎Salaam. Nembo niliyoibuni (nembo A) ilifanikiwa kuingia 3 bora shindano la Rajamu ya Taifa (Nation Brand Mark) - MADE IN TANZANIA. Shindano lilikuwa na jumla ya washiriki 83.

‎Kama member wa JF, nilikuja hapa kuomba support yenu katika zoezi la upigaji kura ambapo members wengi walinipigia kura.

‎1. Ninamshukuru sana Mola Muumba kwa kunijaalia kupata ushindi wa pili.
‎2. Ninawashukuru sana members wote walionipigia kura. Namuomba Mola Muumba awajaalieni nyote afya njema, umri mrefu na mali yenye manufaa. Mbarikiwe sana.

‎Aidha kongole kwake kijana wetu wa UDOM Bw. Lucas Allen Haule (nembo C) aliyepata ushindi wa kwanza. Bila kumsahau Bw. Odero (nembo B) aliyeibuka na kuwa mshindi wa 3.
‎Mola Muumba awajaalie wote hawa mafanikio zaidi.
Screenshot_20250618-111231_1.jpg
Screenshot_20250611-231813_1.jpg
 
Mwenye nembo A ndie alietakiwa kushinda sasa sijaelewa hapo imekuajekuaje yaan hao majaji waliangalia nini?
 
LOGORIDDIM hongera sana mkuu toka kwa mbunifu mwenzako (nimelalia kipaji na umri ushasogea), naona miaka imepita bado upo kwenye game...

Nakumbuka ulivyoingia JF nilikuwa mtu wa mwanzo mwanzo kukupa moyo na sasa umefika mbali sana...

Kwa jicho langu naona logo A ambayo bila shaka ndio ya kwako ina ubunifu zaidi ya logo C au B, lakini yote ya yote kongole kwa wote...
 
Nembo A ipo vizuri sana imekaa kwa muonekano wa peke yake inavutia na rahisi kuitambua
 
Mimi ningemchukua B kwa vile kaweka na ka ramani ka Tanzania kwa mbali!
 
Back
Top Bottom