Shujaa wako mwaka 2012

Shujaa wako mwaka 2012

Zitto Kabwe, kwani hoja ya kutokua na imani na wazir mkuu ilisaidia kwa kiasi kikubwa baadhi ya mawazir vilaza kuondolewa na hii hoja fedha za uswiss nayo itatusaidia kuondoa mianya ya fedha haramu kama zitto anavyoshauri sheria ipitiwe kuhusu utoaji wa fedha nje ya nchi! Jamaa ni jembe lenye uwezo mkubwa.
 
Zitto ndye shujaa wangu, pamoja na kuchafuliwa na shushushu Ben Saanane bado ameibuka bingwa na ataibuka bingwa milele. 'cobra' Jiandae tu kumuomba radhi.
 
Last edited by a moderator:
mnafichuliwa ujinga mliokuwa mnafanya mnakuja kupongezana hapa ,............hapa ni kwa MA GREAT THINKER ningekuona wewe mleta mada na wenzio ben saakumi na juliana shonza wote ningewa tandika viboko liwalo na liwe .humjui mnatetea nini tumbo ,chama au taifa .........
 
Shujaa wangu 2012 ni mimi mwenyewe sababu nimehangaika kivyangu na nimejipatia maendeleo, great thanks to god!
 
Shujaa kwenye nini mtoa mada mbona huwi specific ?
 
Dr.SLAA ni shujaa namba1. DAUDI MWANGOSI namba2. Akina Lissu , Mnyika na Lema wanashika nafasi ya tatu.
Naomba tuwatangaze mashujaa wetu bila upendeleo wowote. Awe mwana siasa au mwananchi wa kawaida aliyefanya kazi nzuri kwa ajili ya kuleta maendeleo ya Nchi yetu. Aliyefichua uovu kwa faida ya chama na wananchi nk

Mimi naomba pasipo aibu wala ubinafsi nimtangaze Saa nane Umefanya kazi nzuri sana! uwe umetumwa au hapana lkn imenisaidia kujua mengi kuhusu siasa na imani yangu imezidi kuwa Imara. Kuna mambo mengi umesaidia yasiharibike kuliko ungekaa kimya. Katika hili wewe ni shujaa!

Mungu akupe heri na kukupigania!
 
Nakapanya,ameweza kutimiza malengo mengi na kusaidia wengine pia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom