Shujaa wa gesi aliyepigwa risasi-rip mr.karim

Shujaa wa gesi aliyepigwa risasi-rip mr.karim

Vijana wa Tanzania wanavyotumiwa kuleta vurugu na kupelekea vifo na uharibifu wa mali sababu tu hawajitambui,Ona hata humu JF wajinga wanavyoshabikia vurugu za Mtwara.Kijana aliekufa alikuwa anategemewa na watu wangapi leo kapoteza maisha kwa jambo ambalo halina faida kwake, wachochezi wako salama yeye anaambulia R.I.P.!Dhamana ya Taifa hili iko mikononi mwetu Vijana hivyo tusitumike vibaya tujitambue, Tafakari chukua hatua sahihi.

Siamini mawazo ya Mtu huyu eti anasema "kapoteza maisha kwa jambo ambalo halina faida kwake," kweli huyu anajua nini hitaji la wana Mtwara? La hasha huyu hafahamu msaidieni.
 
Huyu kijana wana mtwara tukishinda suala la gesi tutajenga mnara kumuenzi..............

575583_505907989457681_421588064_n.jpg


Ukikimbia nchale ukitembea nchale, Pole sana kamanda.
 
kweli hawajitambui hata ukiangalia hiyo haki wanayosema wanapigania ni ipi hata mfano gesi ikibaki mtwara watu wa aina yake sana sana kazi watakazo ambuliia kwenye hiyo ajira ya gesi ni umesenja, ufagizi, na zifananzao na wanao wachochea wakiwa vivulini. tena kwa hiyo alama aliyoonyesha no wonder mzee wa onyo yuko kimya kwa sababu anajua chimbuko lake. Taabu kwelikweli na hizi ziro zinazoongezeka kila mwaka vijana wanazidi kuwa gizani.
Jaribu kufikiria 'kwa sauti',gesi ikibaki Mtwara na mitambo ya umeme na usindikaji ikajengwa Mtwara uchumi wa Mtwara hautashtuka? Wafanyakazi 'skilled' kutoka maeneo mengine watanunua mahitaji toka kwa kina nani? Mahitaji ya shule bora,hospitali bora,hoteli bora,viwanja vya ndege,viwanda vya vyakula hayatakuwepo? Wakazi wenye kipato cha kati hawataongezeka? Bodaboda hazitapata abiria? 'Wageni' hawatajenga 'rest houses' Mtwara badala ya ku-shuttle Dar kila siku? Jiulize Savannah Plains International School huko Shinyanga ilijengwa kwa ajili ya nini? Tuache kuwa 'narrow minded'..
 
Nawaombeni wana Mtwara mkae hata kwa dakika moja kila mmoja wenu popote alipo ajiulize na kujijibu hv hii vurugu ni kwa manufaa ya Mwananchi wa kawaida wa mtwara au ni faida ya chama fulani ama kundi linalotaka kutumia mgongo wa wanachi kujiimakisha ki siasa? Tafakarini huku mkiweka maslahi ya watanzania wenzenu mbele

Nasi tunaojadili humu tujiulize, kwani suala la Mtwara limetokea ghafla au dukuduku zake zimesikika mapema hata Kabla ya haya? Kwanini serikali yetu sikivu isiwasikilize kwanza na kuwapatia Elimu sababu Za msingi kwanini gesi ipelekwe Dar na sio Mtwara. Sasa hapa usikivu wa serikali hii uko wapi?
 
mkuu AINE, Alikubali kutumiwa. Liwe somo kwako na wengine, vijana tusikubali kutumika kama ngazi ya wengine.......poleni wafiwa, r.i.p!!
alitumiwa na nani? kiukweli tunataka kumjua anayetumia vijana hawa hadi wanakumbwa na umauti huu, nasikitika sana
 
Jaribu kufikiria 'kwa sauti',gesi ikibaki Mtwara na mitambo ya umeme na usindikaji ikajengwa Mtwara uchumi wa Mtwara hautashtuka? Wafanyakazi 'skilled' kutoka maeneo mengine watanunua mahitaji toka kwa kina nani? Mahitaji ya shule bora,hospitali bora,hoteli bora,viwanja vya ndege,viwanda vya vyakula hayatakuwepo? Wakazi wenye kipato cha kati hawataongezeka? Bodaboda hazitapata abiria? 'Wageni' hawatajenga 'rest houses' Mtwara badala ya ku-shuttle Dar kila siku? Jiulize Savannah Plains International School huko Shinyanga ilijengwa kwa ajili ya nini? Tuache kuwa 'narrow minded'..



Unafikiri hayajui yote hayo Mkuu?Basi tu kaamua kujifanya punguani lakini hilo wala halihitaji kwenda shule kujua faida watakazopata wanamtwara endapo madai yao yatasikilizwa.
 
Serikali hii bwana badala ya kujadili jinsi ya kumaliza tatizo na wananchi wa Mtwara wao wamekalia kuangalia chama gani kinachochea!

Tumikieni wananchi waliowaweka madarakani na sio kuwabeza maoni yao na kutowasikiliza Kabisa

Maamuzi mnaamua ninyi sawa tuelimisheni tuelewe sio kutunuruza buruza.

Ubabe mnaofanya Mtwara na maeneo mengine ya Tz tunaona na kutafakari juu ya usikivu mnaoudai kuwa serikali yenu inao katika kutenda hiki kwa wananchi wake.
 
Siamini mawazo ya Mtu huyu eti anasema "kapoteza maisha kwa jambo ambalo halina faida kwake," kweli huyu anajua nini hitaji la wana Mtwara? La hasha huyu hafahamu msaidieni.


Anafahamu na ndio maana anatahadharisha kufikiri kabla ya kutenda..... ni vema kujiepusha na maafa.
 
kinachotia moyo wote tutapita ktk mauti, ktk haki lazima upigane,unaweza kupona ukafaidi, au ukafa wakafaidi jamii yako kabla na wao hawajaonja mauti lkn lazima wayaonje mauti!
 
unavifahamu vita vya majimaji wewe wangai walikufa!?
lazima watu wafe ili kuleta ukombozi

kafe wewe basi tuone kweli una uchungu na nchi hii..kusema wenzenu wafe ni rahisi, ila kujitosa wenyewe kufa ni ngumu..
 
Ushujaa wake ni upi? Elezea kidogo tumuelewe marehemu!

Jakubumba, kwani hujui kama Mtwara kuna vita na wanaokufa vitani huitwa mashujaa? Kabla ya tukio la jana, askari polisi wengi tu walikuwa wameishapelekwa frontline. Jana ikaonekana polisi hawawezi kupigana vita wakapelekwa wanajeshi!!!
 
Unafikiri hayajui yote hayo Mkuu?Basi tu kaamua kujifanya punguani lakini hilo wala halihitaji kwenda shule kujua faida watakazopata wanamtwara endapo madai yao yatasikilizwa.
Mkuu suala sio kujifanya punguani kinachonisikitisha ni kuona fujo, kuharibu mali za watu wasio na hatia na umwagaji damu bila hao wanaofanya hizo fujo kujua kuwa wanatumiwa kwa faida ya watu wachache. Tanzania karibia kila mkoa una rasilimali ambazo zikutumiwa ipasavyo bila kuwanufaisha wachache ni manufaa kwa wakazi wa mikoa hiyo na watanzania kwa ujumla wake lakini kinachofanyika sasa wanaonufaika ni wachache wenye madaraka, mafisadi na tena wasio na uchungu na nchi. mfano Geita kuna dhahabu lakini angalia geita leo. Shinyanga tangu niko mdogo nasikia almasi Mwadui angalia shinyanga ilivyo, Arusha Tanzanite, na mikoa mingi mingineyo je ni kweli sisi hohehae tunanufaika nazo wakati ziko kwenye mikoa yetu? Geita nasikia sina uhakika kuwa mkataba ni miaka miamoja? baada ya hapo geita ikoje serikali haina hata hisa kwenye huo mgodi, na SHERIA ZETU NI DHAIFU ZA KULINDANA ZIMETUNGWA NA MUHIMILI AMBAO NI BUNGE. ndio manaana mtu akiboronga hapa anahamishiwa pale badala ya kuwajibishwa? tufanyeje "KATIBA MPYA"

Nini kifanyike basi tuanzishe fujo kwenye kila mkoa wenye rasilimali kwa kuchoma nyumba za watu, kuua, kuharibu barabara, kuvunja madaraja, kung'oa reli ili tupate haki zetu, kazi za wabunge wetu ni kutushawishi kufanya fujo ili wao waonekane ndio wabunge wazuri wanaotetea maslahi yetu (kujipaka mafuta kwa mgongo wa chupa) wakitudandanya ndio haki itapatikana na dunia ijue tunaonewa au kazi zao ni kuwatetea kwa nguvu zote ili ile rasilimali itunufaishe wanachi. na akishindwa tumwajibishe yeye tuliyemchagua? Maana shida hii sio Mtwara tu ni Tanzania nzima ila watu leo masikio yao yako mtwara kesho masikio yatakuwa wapi? Kahama? Mwadui, Mara, Geita, Arusha, Kilimanjaro, Serengeti, ngorongoro au wapi maana kote kuna wahanga ambao ni watanzania masikini wanaoteseka kwa mengi? maana kila mkoa unarasilimali Mungu kweli alitubaliriki lakini ndio tunaongoza kwa umasikini.

Tufanye nini basi kama na Wabunge tuliowaamini wako kiitikadi zaidi kila mmoja anataka umaarufu lakini kiukweli wako kimasilahi yao zaidi dawa ni kuwawajibisha wabunge na mawaziri ambao ni serikali kwa kusaini mikataba mibovu na kutokujali wananchi tusikubali sisi ndio tuwe chambo cha wao kupandia ngazi kwa kutochochoea tufanye fujo mimi nafikiri kila sekta iamke lakini sio kwa uvunjifu wa amani? hata kama ni mwenyekiti wa kijiji wananchi wamwajibishe pale anapoenda kinyume maana kawekwa kusimamia wananchi kwa nini agawe ardhi ya kijiji kwa matakwa yake.

Nionavyo matatizo ni makubwa zaidi lakini tutayatatua kwa jinsi wanavyofanya wanamtwara? fujo, kuua, kuchoma nyumba za watu, kuvunja madaraja? wewe unaonaje hapo? hasara ni kwa nani unapovunja daraja? kwa yule aliyevaa suti huku anapigwa na kiyoyozi au wewe unayeenda kuvunja hilo daraja? Maana wakati wewe unapoenda kuvunja yeye kapanda ungo na kuruka? Kwa nini yeye asiende nasi tukavunja hilo daraja tukiwa wote bega kwa bega tujue kweli anastahili kuwa kiongozi wetu maana yu pamoja nasi kwa shida na raha.
 
Huyo aliyepost hyo picha simuamin nan anamfaham huyo kijana kama kwel ni mwana mtwara,mnatafuta namna ya kuchafua chadema.?
 
kafe wewe basi tuone kweli una uchungu na nchi hii..kusema wenzenu wafe ni rahisi, ila kujitosa wenyewe kufa ni ngumu..

nipo tayali kufa mkuu, kunahaja gani ya kuishi kitumwa nchini kwako!
 
Back
Top Bottom