Shujaa wa gesi aliyepigwa risasi-rip mr.karim

Shujaa wa gesi aliyepigwa risasi-rip mr.karim

R.I.P mkuu, kazi yako hapa duniani umeimaliza, haijalishi nini sisi tunasema hapa duniani, ila Mungu aliyekuleta hapa duniani kwa makusudi yake yeye anajua zaidi, kila la heri kwa kuwapigania wana Mtwara na raslimali za watanzania kwa ujumla.

Nadhani umepanda mbegu ya mapambano.

Serikali iliyopo madarakani mnalo la kujibu juu ya damu za watanzania zinazomwagika eti tu kwa sababu ya maamuzi yenu.
 
Vita ya maumau ilipiganwa na wazalendo lakini pia vibaraka wa watawala walikuwa nao wapo! leo hii hawa sumu, m23,enoah, kibwete na likes ndo vibaraka wa watawala wafisadi!
 
alikuwa anapigania chadema huyu na sio gesi ya mtwara haya R.I.P kamanda
 
hao ndiyo mashujaa wetu!!!! R.i.p wanajeshi wetu, walikuwa wakitekeleza wajibu wao dhidi ya maadui wa nchi yetu, wasioitakia mema tz yetu. Haki inaweza kudaiwa lkn c kwa kuleta uvunjifu wa amani. Chungulia drc uone raha ya vita mkuu!

Vita ya kwenda kuua wanamtwara na Mungu kajua mapema na bora waondoke wao mapema! Order imekuwa reversed!
 
Vijana wa Tanzania wanavyotumiwa kuleta vurugu na kupelekea vifo na uharibifu wa mali sababu tu hawajitambui,Ona hata humu JF wajinga wanavyoshabikia vurugu za Mtwara.Kijana aliekufa alikuwa anategemewa na watu wangapi leo kapoteza maisha kwa jambo ambalo halina faida kwake, wachochezi wako salama yeye anaambulia R.I.P.!Dhamana ya Taifa hili iko mikononi mwetu Vijana hivyo tusitumike vibaya tujitambue, Tafakari chukua hatua sahihi.

Tuthibitishie wanavyotumika maana sasa imefika kwa mtu kujitambua na kudai haki yake mnakimbilia kudai wanatumika
 
amekufa kwa ujinga wake mwenyewe

sisiemu wanazidi kujipalia makaa ya moto, hakuna damu ya mtu isiyokuwa na hatia itakayopotea bure lazima watalipa iwe leo kesho au hata kiama mbele za mungu.

R.I.P & mapambano yanaendelea
 
R. I. P kamanda damu yako ndiyo itakayoitetea mtwara na Tz kwa ujumla na itawadidimiza wote wanaotimiza yote haya
 
na mta kufa sana vijanaa kwa sababu ya ujinga mnatumiwa huku hamjui ngoja muendele kutumika wenyewe watakuja baadae na kujinufaisha wao alafu mtaanza tena wapiga hao hao mabwana zenu.
 
Nawaombeni wana Mtwara mkae hata kwa dakika moja kila mmoja wenu popote alipo ajiulize na kujijibu hv hii vurugu ni kwa manufaa ya Mwananchi wa kawaida wa mtwara au ni faida ya chama fulani ama kundi linalotaka kutumia mgongo wa wanachi kujiimakisha ki siasa? Tafakarini huku mkiweka maslahi ya watanzania wenzenu mbele
 
HUU UJUMBE NI MUHIMU SANA KWA UMMA WETU WOTE WA KITANZANIA. TUSAHAU ITIKADI TUJENGE TAIFA LETU. Vyombo hivi tunavyopashana habari (JF etc) Vitusaidie pia kuelimishana elimu chanya ya kutufanya tuwe wazima.

Vijana wa Tanzania wanavyotumiwa kuleta vurugu na kupelekea vifo na uharibifu wa mali sababu tu hawajitambui,Ona hata humu JF wajinga wanavyoshabikia vurugu za Mtwara.Kijana aliekufa alikuwa anategemewa na watu wangapi leo kapoteza maisha kwa jambo ambalo halina faida kwake, wachochezi wako salama yeye anaambulia R.I.P.!Dhamana ya Taifa hili iko mikononi mwetu Vijana hivyo tusitumike vibaya tujitambue, Tafakari chukua hatua sahihi.
 
kwa umri wake hata mtoto hana bora slaa ndio kaanza kulea vichanga tayari ataacha alama nchi hii huyu kijana kaacha nini au ndio sifa za kijinga za humu jf
 
Ushujaa wake ni upi? Elezea kidogo tumuelewe marehemu!
Ni kuwa mstari wa mbele kutetea rasilimali ya gesi inawanufaishe wana Mtwara bila uoga.
Heri yeye amekufa amesimama kuliko wewe unaeishi huku umepiga magoti, ukilamba watu miguu.
 
Tuthibitishie wanavyotumika maana sasa imefika kwa mtu kujitambua na kudai haki yake mnakimbilia kudai wanatumika

kaka huyu jamaa ni like a virus but non poison ni vema kumuacha aendelee kupiga round. kama yeye na watu wa ukoo wake ni kati ya wanufaika wa mradi wa gesi basi akae akijua safari hii watakufa na njaa na trip za kwenda shoping london zitazima ukoo wao waote. Gesi ya mtwara ni mali asili ambayo mungu amewapa watu wa mtwara kwa manufaa yao na watanzania wenzao wanahaki ya kuipigania mpaka tone la mwisho la damu yao, By the way sisiemu wakimaliza miradi yote ya kugawa, kubadilishana na kuuza mali zetu, Hawatashindwa kutuuza hata sisi kama tukiendelea kucheka cheka, We have to show how we are strong to Detect Our Property huo ndio uwanaume.
 
amekufa kwa ujinga wake mwenyewe

sina imani na upeo wa akili yako na kama unaakili timamu basi unaweza ukawa teja au msangaji, tumia akili yako usishikiwe hakika unakuwa mpumbavu hadi unaenda kaburini
 
Ni kuwa mstari wa mbele kutetea rasilimali ya gesi inawanufaishe wana Mtwara bila uoga.
Heri yeye amekufa amesimama kuliko wewe unaeishi huku umepiga magoti, ukilamba watu miguu.
Dah! Bonge la answer Link ya ku like ipo wapi nikulike na user zangu 7 zote
 
Back
Top Bottom