Shujaa: Maj Gen Mwita Chacha Marwa "Kambale" Afariki

Sielewi vizuri lengo la post hii, ila nataka kufahamisha kuwa Kiaro na Musuguri walipanda cheo kimoja baada ya kingine kuanzia private mpaka walipofikia. Mwaka 1972, tulipigina kidogo na Amin pale Mutukula, na alieyongoza mapigano yale alikuwa Colonel (wakati huo) Musuguri. Mpaka mwaka wa 1985 wakati bado najaua mambo ya jeshi letu, vyeo vya maofisa wote wa jeshi vilikuwa vinatolewa kwa ridhaa ya rais ambaye ndiye amiri jeshi mkuu. Hata hivyo utoaji wa vyeo vya kuanzia junior na senior officers, yaani 2nd. Lt. had Lt. Col. ilikuwa ni lazima recommendation itolewe na Ngome, halafu Rais anabariki. Baada ya hapo, vyeo vya juu (superior officers, yaani wenye alama nyekundu kwenye collar) kuanzia colonel na kuendelea vilikuwa vinatolewa na rais kwa kushauriana na CDF pamoja na Chief of Staff tu; na superior officers waliokuwa wakipandishwa vyeyo kwa njia hii ilikuwa ni kuanzia Colonel na Brigadier tu. Vyeo vyote vilivyokuwa vinatolewa kukiwa na baraka za jeshi vilikuwa vinathamini sana uwezo wa mtu kijeshi, ingawa katika miaka ya themanini siasa zilianza kuharibu kidogo utaratibu huu ambapo makada wa Chama (kama akina Nsa Kaisi) walipewa vyeo vya ukanali from nowhere. Zaidi ya kuvurugwa kidogo na hizo siasa, ni lazima tukubali kuwa watu waliopanda ngazi baada ya ngazi hadi kuwa mabrigadier walikuwa na uwezo mkubwa sana wa kuongoza jeshi. Musuguri, Marwa, na Kiaro ni baadhi ya maofisa waliopanda namna hiyo.

Juu ya Brigadier, yaani Major General, Luteni Gen na General ni vyeo vilivyokuwa vinatolewa na rais tu kwa kushauriana na mashushushu wake, na wala havikuwa na mkono wa mtu yeyote jeshini; ni kama vyeo vya kuteuliwa. Mara nyingi inasemekena kuwa utoaji wa vyeo hivyo ulifuata popularity jeshini (hii ilikuwa ni muhimu sana ili kuridhisha wapiganaji), royality (katika miaka hiyo ambapo majeshi yalikuwa yanaweza kuangusha utawala wa kiraia). Hakukuwa na formula yoyote juu ya utoaji wa vyeo hivyo. Generel Twalipo alipandishwa cheo na Nyerere kutoka Luteni Kanali hadi kuwa Major General (akiruka vyeo vya Kanali na Brigadier) kwa vile alitoa siri ya mapinduzi yaliyokuwa yamepikwa na sarakikya, kwa hiyo alikuwa ni Royal kwa Nyerere.

Kuna wasomi wengi sana ambao hawakupata kuteuliwa kushika vyeo vya juu sana kutokana na ubovu wa muundo wa jeshi letu wakati huo. Brigadier ilikuwa ni lazima awe Brigade commander, kwa hiyo ilikuwa lazima awe na Brigade yake. Wasomi na wataalam wengi wa kijeshi wakawa wanaishia kwenye Ukanali ambacho ndicho kilikuwa cheo cha juu kutolewa chini ya recommendation ya Ngome na hakikuwa na ulazima wa kuwa batallion Commander. Hii ilikuwa ni unfortunate sana, kwa mfano unakuta kuwa kwa vile Colonel Lupogo ndiye alikuwa mtaalam mkuu wa kupanga vita, position yake ile ilikuwa ni ya muhimu sana kwa jeshi zima kuliko kumfanya awe Brigade commander wa brigade moja; kwa hiyo akaendelea kubaki kama Kanali na mkuu wa mipango ya kivita
.

Thanks Kichuguu,

Hizi evidence ndio wenzangu wanakosa zaidi ya kuleta story za mtaani. Appointment za ngazi ya juu kabisa ya jeshi sehemu nyingi hata Marekani huwa ni ridhaa ya rais ambayo mara nyingi haijali elimu ya Havard au WestPoint!
 
Kiaro na Msuguri hawajuhi kusoma wala kuandika. Washauri unaosema wewe ndio watendaji wa kazi za kila siku. Hao wazee walikuwa wanaogopa kwenda likizo kwa kuogopa nafasi zao kuchukuliwa.

Tuna kila sababu ya Kuwaenzi maKamanda wetu,Lakini Ndugu zangu pale kwenye Ukweli ni lazima Usemwe.Nakubaliana kabisa na Bin Maryam kuwa kulikuwa na Walakini kwenye Uwezo wa Kielimu wa Mzee Kiaro,Sina Uhakika na Mzee Msuguri,lakini kwa macho yangu nimeshuhudia Mzee Kiaro akishindwa kusema "Organization Of African UNITY".Jambo hili lilitokea Oljoro JKT wakati wa kumuaga Waziri Salim alipokuwa anakwenda kutumikia Ukatibu Mkuu wa Jumuiya hiyo.

Kwa kujua Uwezo wa Mkuu wa Majeshi,Kamanda Karubi(Mkuu wa kambi ya Oljoro kwa wakati huo)aliwaelekeza Vijana kupiga makofi na kushangilia pale Mzee Kiaro atakapokosea kiswahili au jambo lolote,Nina imani kuna vijana humu walikuwepo kwenye Shughuli hiyo na watakubaliana na hilo.

Kwa sababu nilizosema hapo awali ni kweli kwamba kuna baadhi ya Viongozi wakuu wa Jeshi walifikia vyeo walivyopata kwa ajili ya Utumishi ulotukuka na sio Elimu yao.

Pamoja na yote ni vyema tuutambue na Kuuheshimu Mchango Mkubwa ulotolewa na Makamanda wetu kuilinda Nchi dhidi ya Hujuma kutoka Nje.Mwenyezi mungu amlaze Mahali Pema Peponi Shujaa Mwita Marwa "Kambale"
 
Mwafrika,

..aliyeleta habari ya Kaduma na Kuhanga ni Kithuku. Uteuzi wao ulizingatia siasa kuliko taaluma na matokeo yake yanajulikana. lets stick kwenye mada.

Imetokana na aliyeleta analogy ya VC wa UDSM na mwalimu wa shule ya msingi, nikamsaidia tu kumwongezea taarifa hiyo imchagize katika kufikiri.

Tukirudi katika mada, hakuna aliyeweza kuthibitisha ulazima wa kiongozi yeyote kuwa na elimu ya juu kuliko watu wote anaowaongoza. Kiongozi anapaswa kuwa na sifa na uwezo wa kuongoza utakaokidhi viwango vilivyowekwa na ile mamlaka inayompa madaraka hayo. Hadi sasa hakuna hata mmoja aliyeweza kuthibitisha kuwa hao maafande wanaotajwa hawakustahili madaraka waliyopewa ya ukuu wa majeshi kwa vipndi tofauti.

Hebu tuzungumze objectively, ni sifa zipi anapaswa kuwa nazo CDF (na kwa mujibu wa nani, tupewe references), kisha tutajiwe katika hao maafande waliopita, nani hakuwa na sifa hizo (ushahidi mbele). Wenye hoja karibuni.
 
Ninarudi kusema hawajui kusoma na kuandika.

Bin Maryam,

Kwa vile unasema ulizaliwa Barracks, inawezekana kuwa mmoja wa wazee hawa alikuwa kamanda wa wazazi wako. Sasa kama katika shughuli zao za kijeshi alimpiga mzazi wako kwata nyingi sana, hiyo ilikuwa ni sehemu ya kazi na wala usimchukie.
 
Mwafrika,

..wako wakuu wa Majeshi ambao waliteuliwa kutokana na long service and loyalty. hawakuwa na formal education. hawakuwa commisioned from any re-known military academy. hawakuwa na utaalamu wa mambo kama logistics na planning.

..vilevile katika kuteuliwa kwao waliwaruka wanajeshi ambao walikuwa na vigezo nilivyovitaja hapo juu.

..kichuguu ameeleza vizuri jinsi promotions zilivyokuwa zinawakwaza askari wasomi, wataalamu.

..nadhani nilichokosea mimi nikuwa specific na kutaja majina ya beneficiaries wa mfumo mbaya wa promotions uliokuwepo jeshini.

..kila nilichokisema nimefanya hivyo in good faith. kama kuna aliyekwazika samahani sana.
 
Tuna kila sababu ya Kuwaenzi maKamanda wetu,Lakini Ndugu zangu pale kwenye Ukweli ni lazima Usemwe.Nakubaliana kabisa na Bin Maryam kuwa kulikuwa na Walakini kwenye Uwezo wa Kielimu wa Mzee Kiaro,Sina Uhakika na Mzee Msuguri,lakini kwa macho yangu nimeshuhudia Mzee Kiaro akishindwa kusema "Organization Of African UNITY".Jambo hili lilitokea Oljoro JKT wakati wa kumuaga Waziri Salim alipokuwa anakwenda kutumikia Ukatibu Mkuu wa Jumuiya hiyo.

Kwa kujua Uwezo wa Mkuu wa Majeshi,Kamanda Karubi(Mkuu wa kambi ya Oljoro kwa wakati huo)aliwaelekeza Vijana kupiga makofi na kushangilia pale Mzee Kiaro atakapokosea kiswahili au jambo lolote,Nina imani kuna vijana humu walikuwepo kwenye Shughuli hiyo na watakubaliana na hilo.

Kwa sababu nilizosema hapo awali ni kweli kwamba kuna baadhi ya Viongozi wakuu wa Jeshi walifikia vyeo walivyopata kwa ajili ya Utumishi ulotukuka na sio Elimu yao.

Pamoja na yote ni vyema tuutambue na Kuuheshimu Mchango Mkubwa ulotolewa na Makamanda wetu kuilinda Nchi dhidi ya Hujuma kutoka Nje.Mwenyezi mungu amlaze Mahali Pema Peponi Shujaa Mwita Marwa "Kambale"

Kushindwa kutamka maneno ya kiingereza sio kipimo cha elimu ya mtu. Watu wenye elimu kubwa tu wanashindwa kutamka maneno, tena yale yanayomaanisha majina ya fani zao. Hapa nina jamaa kutoka Uganda ana masters, lakini anasema fani aliyosomea inaitwa "ansoporochee", akimaanisha "anthropology", yuko profesa wa kihindi anayetamka "wayabiliti" akimaanisha "viability", na mifano iko mingine mingi.

Narudia, lafudhi sio kipimo cha elimu. Hoja hii naikataa, na ninaamini wengine wataikataa pia. Tafuta ushahidi mwingine, huu haukubaliki hata kama ulishuhudia "kwa macho" akitamka ndivyo sivyo!
 
Tuna kila sababu ya Kuwaenzi maKamanda wetu,Lakini Ndugu zangu pale kwenye Ukweli ni lazima Usemwe.Nakubaliana kabisa na Bin Maryam kuwa kulikuwa na Walakini kwenye Uwezo wa Kielimu wa Mzee Kiaro,Sina Uhakika na Mzee Msuguri,lakini kwa macho yangu nimeshuhudia Mzee Kiaro akishindwa kusema "Organization Of African UNITY".Jambo hili lilitokea Oljoro JKT wakati wa kumuaga Waziri Salim alipokuwa anakwenda kutumikia Ukatibu Mkuu wa Jumuiya hiyo.

NI kweli kuwa Kyaro alikuwa na shida ya matamshi na kushindwa kutamka maneno kutokana na deep accent yake ya kikuriya. Na wala sio maneno ya kiingeraza pekee bali pia hata maneno mengi ya kiswahili. Kama unakumbuka ule ugomvi wake na mke wa mwinyi ulikopelekea Kyaro kumtukana mama kwa kikuriya!

Lakini kusema kuwa Kyaro alikuwa hajui kusoma huu ni uongo kabisa na mheshimiwa Mwawado kuna tofauti kubwa kabisa ya kushindwa kutamka maneno (kama vile bush anavyoshindwa kutamka maneno mengi kwenye speech yake) na kushindwa kusoma.

Kwa kujua Uwezo wa Mkuu wa Majeshi,Kamanda Karubi(Mkuu wa kambi ya Oljoro kwa wakati huo)aliwaelekeza Vijana kupiga makofi na kushangilia pale Mzee Kiaro atakapokosea kiswahili au jambo lolote,Nina imani kuna vijana humu walikuwepo kwenye Shughuli hiyo na watakubaliana na hilo.

Hili huwa linamtokea Bush mara nyingi sana kwenye mikutano yake ya hadhara na watu hushangilia pale anavyoshindwa kutamka maneno na wala hicho si kigezo cha kusema kuwa Bush (au Kyaro) in this case hakujua kusoma.

Kwa sababu nilizosema hapo awali ni kweli kwamba kuna baadhi ya Viongozi wakuu wa Jeshi walifikia vyeo walivyopata kwa ajili ya Utumishi ulotukuka na sio Elimu yao.

Pamoja na yote ni vyema tuutambue na Kuuheshimu Mchango Mkubwa ulotolewa na Makamanda wetu kuilinda Nchi dhidi ya Hujuma kutoka Nje.Mwenyezi mungu amlaze Mahali Pema Peponi Shujaa Mwita Marwa "Kambale"

Ni kweli issue hapa ni Marwa na inabidi alale kwa amani huko kokote aliko
 
Mwafrika,

..wako wakuu wa Majeshi ambao waliteuliwa kutokana na long service and loyalty. hawakuwa na formal education. hawakuwa commisioned from any re-known military academy. hawakuwa na utaalamu wa mambo kama logistics na planning.

..vilevile katika kuteuliwa kwao waliwaruka wanajeshi ambao walikuwa na vigezo nilivyovitaja hapo juu.

..kichuguu ameeleza vizuri jinsi promotions zilivyokuwa zinawakwaza askari wasomi, wataalamu.

..nadhani nilichokosea mimi nikuwa specific na kutaja majina ya beneficiaries wa mfumo mbaya wa promotions uliokuwepo jeshini.

..kila nilichokisema nimefanya hivyo in good faith. kama kuna aliyekwazika samahani sana.

Mimi binafsi sijakwazika mkuu ila nilikushangaa tu!
 
ni kweli kabisa kuwa kina marwa na musuguri walikuwa na tatizo la accent..hii haimaanishi kushindwa kutamka maneno ni kushindwa kusoma na kuandika....kina maryam hawajui historia za hwa makamnda wa mwanzo...hawa ni makamanda ambao waliingia jeshini mwaka 1945 wametumikia jeshi karibu miaka 50..mara ya kwanza wameingia jeshini kama drop out wa class 4..waliokimbilia kuchunga ngombe na walikuwa wakiwa recruited kwa kukamatwa kwa nguvu huko maporini tena bila ridhaa za wazazi wao...hakuna anayewafikia...majenerali wa leo average wanatumikia jeshi miaka 30 kufikia cheo hicho...

mimi najua wasomi wengi tu wenye kiswahili kibovu....kama kuongea kiswahili kilichonyooka ingekuwa usomi ..nafikiri wengi wangeitwa wasomi....

amenikumbusha mmoja hapa hotuba za jenerali kiaro..atasema hivi.."CHIJANA CHIPOO..CHINA NGUVU ..KAKAMAVU KAPSAA..." and something like that..it was interesting...accent..lakini watu walikuwa hawajali hilo...
 
Kiaro na Msuguri hawajuhi kusoma wala kuandika. Washauri unaosema wewe ndio watendaji wa kazi za kila siku. Hao wazee walikuwa wanaogopa kwenda likizo kwa kuogopa nafasi zao kuchukuliwa.

Hii ni hearsay tena toka kwa mtu ambaye inaelekea hata hajui jeshi wanafanyeje kazi.

Jeshi utaogopa kwenda likizo? Kazi ipi hiyo itakayochukuliwa?
 
Bin Maryam,

Kwa vile unasema ulizaliwa Barracks, inawezekana kuwa mmoja wa wazee hawa alikuwa kamanda wa wazazi wako. Sasa kama katika shughuli zao za kijeshi alimpiga mzazi wako kwata nyingi sana, hiyo ilikuwa ni sehemu ya kazi na wala usimchukie.


Sina chuki lakini kumbuka vijana wengi hapa wamesoma mada nzito kufikia atomic level na huwezi kutoa hoja kuwa Jenerali wa Tanzania asiyeweza kusoma na kuandika aliweza kuongoza majeshi ya Tanzania katika vita vilivyotumia logistic na sophistication ya aina kupata ushindi.

Pamoja na utu uzima mnaotaka kuonyesha hapa baadhi yenu mko indoctrinated, na hamtumii muda wenu kufuta mavumbi.
 
Kwa kuwa mada ishakuwa blown out of proportion twendeni hivyo hivyo ... haya mimi naomba shule ya Ukanali wa Jakaya Kikwete,Luteni Lowasa?, Luteni Makamba, Kanali Kinana, Kapteni Jaka Mwambi, Kanali Nsa Kaisi, Brigedia Hashim Mbita, Kanali Ayoub Shomari Kimbau, Bridegia Hassan Ngwilizi, Brigedia Ahmed Chitete, Bridegia Muhidin Kimario, Meja Sigela Nswima etc.

RIP Maj Gen Marwa
 
Sina chuki lakini kumbuka vijana wengi hapa wamesoma mada nzito kufikia atomic level na huwezi kutoa hoja kuwa Jenerali wa Tanzania asiyeweza kusoma na kuandika aliweza kuongoza majeshi ya Tanzania katika vita vilivyotumia logistic na sophistication ya aina kupata ushindi.

Pamoja na utu uzima mnaotaka kuonyesha hapa baadhi yenu mko indoctrinated, na hamtumii muda wenu kufuta mavumbi.

Viroja tu ndio vimebaki, hoja sifuri na name callings kibao ukitumia hearsay!
 
........................................ Kama mnakumbuka ndege yetu iliyotunguliwa na majeshi yetu wenyewe kwa bahati mbaya, rubani wake akiwa mtoto wa Nyerere. ....................................................

Ninawapongeza wapinganaji wote na makamanda wote waliojitolea kulinda nchi yetu dhidi ya 'Nduli' Amin.

Sahihisho kidogo hapo.
Rubani wa kijeshi aliyetunguliwa kwa makosa na JWTZ alikuwa ni Capt. Alexander Kaleya Mshana na siyo Capt. Andrew JK Nyerere kama ilivyoashiria hapo. Andrew alimaliza vita salama.

Nilibahatika kuwafahamu hao watajwa pale Ngerengere - Morogoro mara baada tu ya kundi lao kurudi kutoka mafunzoni China miaka ya early 1970s.

Kuna upotofu kiasi fulani kwa baadhi ya postings hapa, ila Kichuguu anajitahidi sana kuweka hali katika picha halisi ya mambo yalivyokuwa.

Nahisi kuwa Bin Maryam kipindi hicho (Late 1970s to mid-1980s) alikuwa ni mtoto mdogo, na ufahamu wake unatokana na 'stories' za kambini baina ya watoto. We all know how mis-guiding such stories can be, sometimes.
 
Hii ni hearsay tena toka kwa mtu ambaye inaelekea hata hajui jeshi wanafanyeje kazi.

Jeshi utaogopa kwenda likizo? Kazi ipi hiyo itakayochukuliwa?

Mtanzania yani nakuambia kuna mambo hapa ukisoma inabidi ucheke tu maana hata watoto wa chekechea wangetoa hoja vizuri. Eti jeshi mtu aogope kwenda likizo! As if kuna mtu atapindua na kuchukua nafasi ya mkuu wa majeshi!

Yaani mie naenjoy explosion tu hapa.
 
Kwa kuwa mada ishakuwa blown out of proportion twendeni hivyo hivyo ... haya mimi naomba shule ya Ukanali wa Jakaya Kikwete,Luteni Lowasa?, Luteni Makamba, Kanali Kinana, Kapteni Jaka Mwambi, Kanali Nsa Kaisi, Brigedia Hashim Mbita, Kanali Ayoub Shomari Kimbau, Bridegia Hassan Ngwilizi, Brigedia Ahmed Chitete, Bridegia Muhidin Kimario, Meja Sigela Nswima etc.

RIP Maj Gen Marwa

kaka masatu hao uliotaja hapo juu ni maafisa wenyewe wapiganaji wanawaita " maafisa mananga wa vitabu" au "political commisers"

hapo watoe wawili tu ndio role yao mstari wa mbele inaeleweka MEJA GENERAL MUHIDIN KIMARIO na brigedia GENERAL HASSAN NGWILIZI....wapiganaji waliosave msumbiji..wanaikubali kazi ya ngwilizi kimedani....ni askari mzuri!!! ngwilizi ndie aliyekuwa mkuu wa bregedi iliyokuwa msumbiji..iliyoongoza ile operesheni ya mwisho ya kuwasafisha wareno waliobakia bakia na renamo..kama sikosea ilikuwa christened OPERESHENI SAFISHA SAFISHA au kitu kama hicho......

hao waliobaki kina kikwete ,lowassa,mwambi na wenzake ambao walikuwa groduates wakati wa vita hawakuwa mstari wa mbele bali walibaki kufundisha siasa vikosini na baadhi wakifundisha mgambo....

kuna wengine kama BRIG GEN MOSES NNAUYE huyu alishiriki kama muhamasishaji ..ni muhimu sana..akiwa ni vikosi vya bendi na burudani...[ie mwenge jazz,na kwaya ya luteni komba...]hwa walikuwa na wajibu wa kuhakikisha askari wanaburudishwa na kuliwazwa baada ya kazi ngumu...na kuwatia hamasa...na propaganda za ushindi...
 
Mtanzania yani nakuambia kuna mambo hapa ukisoma inabidi ucheke tu maana hata watoto wa chekechea wangetoa hoja vizuri. Eti jeshi mtu aogope kwenda likizo! As if kuna mtu atapindua na kuchukua nafasi ya mkuu wa majeshi!

Yaani mie naenjoy explosion tu hapa.

Jeshini kwenda likizo unatakiwa kujaza fomu. Kama hujui kusoma fomu utajaza vipi?
 
Back
Top Bottom