Shtuka..! Unaibiwa

Shtuka..! Unaibiwa

Hahahaaa. Sina kipaji cha kuanzisha uzi ujue.

Hivyo imebidi niongezee humu humu ni tujue chanzo hasa nini mpaka imefikia Brenda katoa namba. Hahaaa.
chanzo kuanzia siku inaanza au tangia walipoingia basini au tangiwa walipoanza safari au tangia walipoanza maongezi?

Yote kwa yote mwanamke akitoa namba tu ni sawa na msafiri Alofika mkuranga,aendae dar,atokae masasi
 
chanzo kuanzia siku inaanza au tangia walipoingia basini au tangiwa walipoanza safari au tangia walipoanza maongezi?

Yote kwa yote mwanamke akitoa namba tu ni sawa na msafiri Alofika mkuranga,aendae dar,atokae masasi
Chanzo kuanzia humo basini mpaka wakapeana hizo namba.
 
Ila nyinyi wa secular mnapenda kujitutumia kutaka kusjindana maumbile,ila ipo siku mtanyoosha maelezo halafu mtakuwa mmeshachelewa sana.
Mmh. Na wewe umeamua kuyasingizia maumbile tena. Heeee.

Wasiofanya je na wenye jinsia kama yenu wao kwao imekaaje?
 
Aisee! Basi mi ni tatizo, unaweza kaa na Mimi siti moja hata safari iwe ya Massa kumi no story, yaani kuna kipindi huwa najishangaa, yaani hata ukinisemesha nitaona kama unanikera tu, huwa sipendi story sijui kwa nini...! Na nikikaa na Mwanamke ndo kabisaa... Afadhari mwanaume mwenzangu tunaweza ongea mawili matatu, lakini mwanamke huwa sitaki mazoea nao niwapo safarini, waifu mwenyewe kuna kipindi akiwa ananisemesha huwa namuweka wazi tu, "naomba uniache". Ye ataenda kuendelea na shughuli zake mi ananiacha ndani
We tunafanana. Stori nikute kijiwe cha kahawa, kwenye gari/basi ni kusoma kitabu nikichoka nalala.
 
Na hili ni kwa wote na sio kwa Ke peke yake
Bila shaka kwa wote.... Mathalani mimi sijawahi kuanzisha story na mtoto wa kike ndani ya bus zaidi ya salamu.Isipokuwa mmoja tu alijaribi kulianzisha na kunipa biskuti zao za kuitwa "EAT SOME MORE".
 
Mmh. Na wewe umeamua kuyasingizia maumbile tena. Heeee.

Wasiofanya je na wenye jinsia kama yenu wao kwao imekaaje?
Nilijua tu hapa huwezi kunielewa kama nilivyo kusudia.

Maumbile ndio sisi wewe huwezi kuwa Hajar bila hilo umbile lako.

Nataka nikuulize swali,kwa sharti ulijibu kama inavyotakiwa ujibu....!
 
Hahahaaaa. Wataka mdada wa watu aangukiwe na jumba bovu.

Huwa naona mie pia ila sijui kwa nini hii tabia ipo na sijui anayekuwaga mdhaifu hapo ni nani kati ya Me na Ke maana waeza kuta ni katoto kanaenda shule na kamevaa sketi ya shule ila unakuta kanagandana na mtu kisa tu kakaa naye siti moja.

Ila hebu tujadili Wadau dawa ya hii kitu ni nini? Na ni nini inasababisha hii kitu?

Japo tusihalalishe kwamba wote wanaopeana namba lengo ni mapenzi.
Fursa adimu.

Ila jamaa mtoa mada mbona shilawadu flani
 
Hahahaaa. Nimecheka sana kwa ulichokiandika ila sijuagi kwa nini huwa mnaisingizia hiyo sijui baiolojia.

Jitahidini kuizuia hiyo tamaa sababu si wanawake wote wanajuaga kukataa. Mnawapa shida tu wanawake wa watu.

Jirani sumbai nimeona lile neno lako pendwa hapa. Hahaaaa.
Tumeumbwa hivyo. Jirani.

Its a biological factor
 
Nilijua tu hapa huwezi kunielewa kama nilivyo kusudia.

Maumbile ndio sisi wewe huwezi kuwa Hajar bila hilo umbile lako.

Nataka nikuulize swali,kwa sharti ulijibu kama inavyotakiwa ujibu....!
Hahaaa. Umefanya nicheke maana kiukweli toka nianze kukuquote kila mara lazima useme sijakuelewa duuuh!

Usiniulize maana waeza sema pia sijalielewa swali lako. 😂😂
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom