DOKEZO Shinyanga: Kuna Wafanyakazi wa Idara ya Ardhi wanatengeneza mazingira ya rushwa waziwazi

DOKEZO Shinyanga: Kuna Wafanyakazi wa Idara ya Ardhi wanatengeneza mazingira ya rushwa waziwazi

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Wafanyakazi wa Idara ya Ardhi Mkoa wa Shinyanga na wale wa Manispaa ya Shinyanga wanafanya kazi zao kwa mazoea sana huku wakitengeneza mazingira ya kupokea rushwa kutoka kwa wananchi.

Kama week mbili zilizopita kulikuwa na zoezi la urasimishaji wa ardhi katika kata ya Kizumbi, kijiji cha Nhalegani, zoezi lililoratibiwa na watajwa hapo juu, wananchi walitakiwa kufika kwenye kituo kilichoandaliwa katika shule ya msingi Nhalegani wakiwa na nyalaka muhimu ili waweze kufanya utaratibu wa kupewa hati miliki za viwanja vyao.
Tatizo lilianza tu siku ya mwanzo kwa sababu zoezi zima lilikuwa disorganized huku watumishi wakiwa kama miungu watu pale mwananchi anapohitaji huduma zao na hili lilisabishwa na wao kutaka kutengeneza mazingira ya rushwa.

Kufupisha story ni kuwa baada ya mambo yote mwananchi alitakiwa kufunguliwa maombi kupitia mfumo wa e-ardhi na hapo kupokea control number ya kulipia maombi hayo shilingi 5000/= na baada ya hapo mwananchi anapokea control number nyingine kwa ajili ya kulipia hati.

Watu wote walilipia 5000/=hizo control number hazikuwa na shida lakini control number kwa ajili ya kulipia hati hapo watumishi hao walianza kutengeneza mazingira ya rushwa kwamba kama haujaongea nao vizur hawakupi control number, wanakwambia subiri, nenda nyumbani itaingia kwenye simu.

Sasa ni week ya tatu inaingia na bado watu wengi hawajapokea control number wanataka wananchi wawafuate ofisini kwao pale Manispaa ili wawaombe rushwa.

Hata ukifika pale ofisi kwao hakuna msaada wanajifanya wapo bize tu.

Tafadhali mamlaka husika liangalie hili jambo, watu wanateseka, wazee wanateseka kwenda kufuatilia jambo ambalo halikutakiwa kuwa na usumbufu wa hivyo kwa sababu huu ni mradi ambao kwa taarifa tulizo nazo unafadhiliwa na World Bank.

Kama hawatabadilika nitarudi hapa kuwataja majina watumishi wanao omba rushwa kwa wananchi.
 
Watumishi awamu hii hatupo nyuma


 
Hii ndio Tanganyika y CHURA a.k.a Dalali maskini hana chake KABISA. Tujipange kuteseka mpk 2030.
KAZI ni kipimo cha utu
 
Mwananch baada ya kulipa control number ya jiji yaan 5k pia anapaswa kutumiwa control number nyingine ya malipo ya wizara na inachakatwa na afsa ardhi mteule ambao kimfumo wapo wachache kulinganishwa na idadi ya kazi yaan viwanja vinavyopaswa kurasimishwa.

Huo upenyo wa uchache imetengeneza burgoise ambao hutengeneza mianya ya rushwa hivyo kudidimiza lengo la urasimishaji kwa wananchi, japo kwa serikali wanakua hawana hasara kutokana ulivyofanyiwa tu usajil na kuilipa ile 5k tayar ushaingia kweny register ya mlipa kodi(pango) hivyo tayar utakua ushaanza kukadiriwa pango la ardhi na kila mwaka utakua na deni na unapaswa kulilipa.

Kisheria unapokaa miaka mitatu bila kuilipa hio pango ya ardhi basi kami kamishina wa ardhi anayomalaka ya kutengua umiliki wako wa ardhi(revocation)under the power of president.Japo sheria hii huaga haifatwi mara nyingi ila ukitaka kuijua ipo na inaweza fuatwa zinguana na CCM ndo utajua au hujui.

Mwisho, urasimishwaji uliletwa haswa kwa hoja ya dead capital as purported by Desotho, also gvt management as you can't manage what you don't know and other trivial reasons. Japo lengo kuu la kuweka huduma na mazingira kua formal yaan kua na barabara, maji etc bado halijafikiwa kabisa na hata pia kuwapa watu hati halijafikiwa kwa asilimia walau 60 kwasababu ya sababu kama hizo za watumishi wasio waadilifu na sababu za kimifumo.
 
Wizara ya Ardhi hizi kero huwa mnachukua kweli???

Ni mambo ya ajabu sana unaenda kufata hati unaambiwa wewe anza tu kuomba kibali cha ujenzi uendelee hati utaipata tu
 
Hapo ukitoa 50K unapata hiyo control number unaipata siku hiyo hiyo wenyewe wanaiita facilitation fee..........wanatumia gap la waombaji kuwa wengi kujinufaisha, nina uzoefu nao
 
Back
Top Bottom