Sheria ya Jeshi kuhusu mavazi ni ya kishamba na kizamani sana

Nimemsikiliza askari aliyekuwa akihojiwa na CloudsTV anasema sheria ya mavazi ya jeshi unasema;-
"Ni marufuku raia kuvaa sare za jeshi ama mavazi yanayofanana na sare za jeshi". Ili iweje?

Yaani ktk zama hizi za sayansi na teknolojia bado jeshi letu linataka kujitofautisha na raia kwa mavazi? Mwanajeshi ajitofautishe kwa umahiri wa kung'amua na kuzima nia na jaribio la adui kutaka kuivamia nchi yetu. Baasi! Siyo hizi blah blah za kuwalingishia raia gwanda za jeshi.

Kule nchi za watu mpk walevi na mateja wanavaa mavazi yanayofanana na sare za majeshi ya nchi zao. Mbona hatujasikia wakipata shida ya kiusalama?

Tuachane na ushamba huu. Nakumbuka hata bendera ya taifa kabla ya Kikwete kuwa rais ilikuwa ni marufuku kukutwa hata na leso inayofanana na bendera yetu ya taifa. Mhe. Kikwete akaondoa ushamba huu.

Ni wakati wa kuondoa ushamba wa kuzuia raia mavazi yanayofanana na sare za kijeshi sasa.
Ndugu, sipingi maoni yako kwamba ni Mambo ya kizamani.Kama unaona ni Mambo yaliopitwa na wakati,hakuna aliyekukataza kuvaa.Jeshi halijakurupuka kutangaza jambo hili.Imefika wakati wa kutoufautisha matamko ya kisiasa na ya kijeshi.Nawashauri wanaoona kwamba haya ni Mambo ya kizamani WAVAE Weekend njema
 
Sijasema wapige raia ila naona sio sawa raia kuvaa sare zinazofanana na majeshi.
Mbona CCM huvaa magwanda ya kijani wakati JWTZ nao Wana rangi hizo hizo?

Hoja hapa ni kuwa rangi ya vazi la raia fulani kufanana na rangi ya vazi ya jeshi haiwezi kuwa ni sababu ya kutosha kusema "amevaa vazi la jeshi"

Huu ndio ujinga na ushamba mkubwa kuliko wote unaosemwa na mleta hoja Sexless otherwise watuambie mstari wa vazi la jeshi na raia kwa kigezo cha rangi tu unauchorea wapi hasa kabla kuhukumu watu?
 
asanteni watanzania, hii inaonyesha watu wameelimika... mkoloni mweusi ajiandae naona watu vichwa vimeanza kupata moto. Walikuwa polis na sasa hata wanajeshi wameanza kuchafua taswira kwa wananchi. Huwezi ukampiga raia et kisa kavaa vazi ambalo hajaliiba ila tu limefanana na lako... hayo mavazi wanavaa kwa sababu ya kodi zetu halafu wanaleta mambo ya hovyo... jeshi umefika muda mbadiri sheria na taaribu zenu muda hauwasubiri oooooh,
 
Mtu aliyevaa nguo zinazofanana na za jeshi huwa anavimba kuliko mjeda.

Wanaopenda kuvaa sare wakanunue za simba na yanga zinafaa kuvimba pia.
Nimeshona mpk sofa za mabakamabaka sasa kwa taarifa yako.
IMG-20230905-WA0000.jpg
 
Hivi imagine Kila kitu kinafanana kasoro nembo huoni Kwa tz inaweza kutumika kutapeli au kuonea watu...huko vijijini raia wanajua kweli mambo ya nembo?
Umeshafanya utafiti ukajua tatizo ni kiasi gani au unatumia hisia tu na mawazo binafsi?

Hizi nguo ziko duniani kote mitumba na Mpya na dunia nzima majeshi yanatumia nguo zenye mwelekeo huo.
 
Mtu aliyevaa nguo zinazofanana na za jeshi huwa anavimba kuliko mjeda.

Wanaopenda kuvaa sare wakanunue za simba na yanga zinafaa kuvimba pia.
Yaani mnalifanya kama vile nitatizo la kitaifa wakati ktk Watu 60 unaweza kukuta wenye nazo hawazidi hata 500
 
Hakuna anayekomalia. Tunachosema hakuna uhalali Wala sababu ya jeshi kuacha majukumu yake ya msingi na kuanza kugombana na raia eti kisa wamevaa mavazi yanayofanana na sare zao. Ni ujuha.

Mavazi ya jeshi yana nembo. Raia akivaa sare za jeshi (vazi lenye nembo ya jeshi ) hapo akikamatwa Sina nongwa. Lkn akivaa vazi halina nembo ya jeshi, ikn linafanana rangi na kila kitu cha jeshi, hilo siyo mali ya jeshi. Ni ujinga.
Kaa kimya kama hujui.

Kombati ya jwtz ina nembo gani.

Hata sare zingine zina nembo gani,

Hiyo midomo yenu na Maandishi mnatumie vizuri

Vaa uone
 
Eti usajili wakikukuta na Tattoo napo wanasema umedisqualify,ukiuliza tatoo ina shida gani hawana majibu.

Wenzetu huko majeshi yao yana watu wana tatoo za hatari na wanatumikia jeshi safi bila tatzo,ishu ipo huku kwetu
Huko wanapokea hadi Mashoga, vp hapa kwetu nao wapokelewe?
 
Waambiwe ukweli.
SARE sio jeshi.
Jeshi ni mafunzo, teknolojia, akili, saikolojia, falsafa, vifaa, n.k

Ni ushamba wa kijinga sana.

Halafu pia nguo kuwa na mabaka mabaka, haiwi nguo ya jeshi.

Je, wanajeshi wasiovaa sare, wanakuwa raia au wanakoma kuwa wanajeshi?!

Ni ujinga wa kiwango cha karibu na upumbavu.
Nadhani haujui madhara ya unachokitetea.
 
Lakini Kwa nini na wewe raia utake mavazi ya jeshi lakini??? SI uchokozi huoo ni kumshika mwanaume matako huko
Sio sare ya jeshi tu bali sare ya taasisi yoyote kama wewe sio mhusika unaivaa ili iweje? Hata sare shule kama wewe sio mwanafunzi kwanini uvae sare ya shule? kwa hali yoyote ile unataka kufanya ualifu ili ujifiche kwenye sare husika.Kama kuvaa sare inakupendeza vaa ya Mgambo basi.
 
asanteni watanzania, hii inaonyesha watu wameelimika... mkoloni mweusi ajiandae naona watu vichwa vimeanza kupata moto. Walikuwa polis na sasa hata wanajeshi wameanza kuchafua taswira kwa wananchi. Huwezi ukampiga raia et kisa kavaa vazi ambalo hajaliiba ila tu limefanana na lako... hayo mavazi wanavaa kwa sababu ya kodi zetu halafu wanaleta mambo ya hovyo... jeshi umefika muda mbadiri sheria na taaribu zenu muda hauwasubiri oooooh,
Wao wenyewe wameshaona,kizazi kimeshaamka.
 
Back
Top Bottom