1800
JF-Expert Member
- Dec 27, 2010
- 2,215
- 611
Nipo katika viunga vya mahakama ya mkoa wa Morogoro, nimeona ulinzi mkali umeimarishwa na helicopter ya polisi kutoka Dar es salaam ikiwasili mnamo mida ya saa tano.
Habari ni kuwa helicopter hiyo ilimleta Sheikh Ponda kuja kusomewa mashtaka yake, mashtaka ambayo hayakuzidi hata nusu saa kusomwa, na mnamo saa sita na dakika 28 mchana helicopter hiyo iliondoka na kurejea D.s.m.
Bado haijajulikana kama imeondoka na Sheikh Ponda au vipi.
Hivi kweli Ponda amekua threat kiasi hiki?
Habari ni kuwa helicopter hiyo ilimleta Sheikh Ponda kuja kusomewa mashtaka yake, mashtaka ambayo hayakuzidi hata nusu saa kusomwa, na mnamo saa sita na dakika 28 mchana helicopter hiyo iliondoka na kurejea D.s.m.
Bado haijajulikana kama imeondoka na Sheikh Ponda au vipi.
Hivi kweli Ponda amekua threat kiasi hiki?
Ktk mahakama ya Mkoa wa Morogoro ameletwa Sheikh Ponda kuja kusomewa shitaka la uchochezi.
Nimeshangaa kuona umati wa askari kanzu, FFU na wale wa Usalama barabarani. Pesa ya walipa kodi inateketea kwa mambo ya kijinga kama haya inatia uchungu sana.
Kwa sasa chopa inawashwa na sheikh anarudishwa Dar.
![]()
Sheikh Issa Ponda Akiwa mahakamani mkoani Morogoro asubuhi ya leo Sheikh Ponda Amesomewa Mashtaka Matatu katika Mahakama ya mkoa wa Morogoro Likiwemo la uchochezi alilolitoa Kwenye Mkutano wa Hadhara Tarehe 10 mwezi huu Ambapo Inadaiwa alisema kwamba ''Ndugu waislamu Msikubali uundwaji wa kamati za ulinzi na usalama za Misikiti kwani kamati hizo zimeundwa na Bakwata ambao ni vibaraka wa Serikali ''katika viwanja vya shule ya kiwanja cha ndege Mkoani Morogoro.Baada ya kusomewa Mashitaka hayo Mahakama imesema Upelelezi Umekamilikaa Dhamana Imefungwa na Amerudishwa Rumande Mpaka tarehe 28 mwezi huu ambapo kesi hiyo itaanza kusikilizwa katika Mahakama ya Mkoa wa Morogoro.
![]()
Sheikh Ponda akiondoka Mahakamani Mpaka Aug 28 2013
![]()
Ulinzi wa POLISI