Sheikh Ponda akosoa utendaji wa Rais Magufuli

Sheikh Ponda akosoa utendaji wa Rais Magufuli

Mzushi tu hana lolote lile, yy kwa akili yake anadhani JPM anafanya kazi kwa mawazo yake bila kushirikisha wataalamu? labda kwa taarifa tu ni kwamba hizo taarifa zipo nyingi tu pale ikulu wala hazisubiri hizi za juzi, kimsingi zilikuwa hazifanyiwi kazi na ndo JPM kaanza nazo, nadhani Ponda kapotoka2.
Zinasubiri Tv na Magaazeti?
 
rais magufuli hata afanye mazuri yote, ila asipowatoa wale masheikh wa uamusho zanzibar kwa huyu sheikh ponda rais atakua hajafanya chochote.
Maigizo ndio kitu hakitakiwi serekali ya Tv na Magazeti
 
lingeundwa jopp la wataalamu al-maarufu tume ya uchunguzi mngelalamika,hebu tulieni kwanza tuyashughulikie haya majipu ili heshima iturudi.
waswahili wanasema,ukimuona mtu analia sana wakati akikamuliwa jipu,ujue anakaribia kupona.
 
Ngoja nipite maana apa kuna vuguvugu la nanihii ukichangia tu lazima uonekane wewe ni wa chama au mpinga ponda

Sent from my BlackBerry 9790 using JamiiForums
 
Anatafuta kiki,,,,mtu una mishahara 17 tunahitaji report gani tena? Yale mazoea ya kuunda unda tume za wataalamu enzi yake ishapita
 
Mkuu nchi hii ukijifanya msemakweli unapotezwa,bora katafute riziki ya wanao rudi shimoni kwako lala..ukitaka kugombana na serikali za kiafrika endekeza mdomo na ndicho anachokifanya Ponda,mwambieni atulie kashika makali hajashika mpini.
kwake hiyo ni sehemu ya maisha wala hajali, lazima aseme anachokiamini, ww muoga tulia na mkeo shimoni kwako
 
SHEIKH Ponda Issa Ponda, Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam Tanzania, amekosoa utendaji wa Rais John Magufuli, hasa dhana ya kutumbua majipu, akisema ina kasoro za kiutawala.

Akizungumza leo, Sheikh Ponda amesema utendaji wa Rais Magufuli ni wa kulipualipua.

“Ni kweli kwenye serikali kulikuwa na matatizo mengi, lakini lazima utaratibu kamili wa kuchukulia watu hatua ufuatwe,” amesema na kuongeza:

“Huwezi kuchukulia hatua watu bila kuwa na ripoti ya kitaalamu. Huko ni kufanya kazi kwa kulipuka.

Watanzania watafurahi zaidi kama serikali haitaingia hasara kutokana na kazi hiyo iliyo na shaka katika utekelezaji wake.”

Amesema ingekuwa bora kwa Rais Magufuli kusubiri ripoti za wataalamu wake, na si ‘kutumbua majipu’ kabla ya kupata ripoti.

Anasisitiza, “Jambo hili halipo sawa hata kidogo.”
Anasema dhamira ya kurejesha nidhamu serikalini ni nzuri na inahitajika sana, lakini namna ya utekelezaji wa dhamira yake hakuuanza vizuri.

“Juzi Rais Magufuli amepokea ripoti kutoka kwa Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali. Angepaswa kuanza kuifanyia kazi ripoti hiyo ili kuepuka madhara kama yale ya kukamata meli ya uvuvi kwenye Pwani ya Dar es Salaam mwishowe serikali ikaingia gharama,” amesema Sheikh Ponda.
Hakuna aliefukuzwa kazi.
Wanasimamishwa kupisha uchunguzi. Pia jamani mwacheni mkuu apige kazi
 
Kwahy anataka rais atoe reference kuwa wewe nimekutumbua kutokana na ripoti ya a na be na che
 
ukiona mtu mzima analia ujue kuna jambo,maneno haya hua yana maana wakati fulan sasa huyu mzee mtandao wake wote umevurugwa na magu maana kila anaye muona unamwambia magu kashaharibu system ama ya ukabila ama ya udin hivyo maisha ni magum sana.ushauri muelezen mzee huyu kuwa hata wengne wameharibiwa ila tofaut yake ni kwamba wanakufa kama kondoo kimya kimya,kama yy pameuma mwambie nchi hii ni ya watanzania wote sio wachache na kama wapo ndo hao wanalialia hum atulia.
 
Anatafuta kiki,,,,mtu una mishahara 17 tunahitaji report gani tena? Yale mazoea ya kuunda unda tume za wataalamu enzi yake ishapita
Kuna mdau mmoja mwaka 2012 aliwahi kuchangia mada kwenye hii link:
Historia ya kweli ya maisha ya Sheik Ponda na Fareed ni muhimu

Chanzo cha chabari hizi kinaanza kwa kueleza kuwa, imebainika kuwa Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Sheikh Issa Ponda si raia wa Tanzania.

Uchunguzi uliofanywa na chanzo hiki nchini Burundi, Kigoma na taarifa za uhakika kutoka idara ya Uhamiaji na vyombo mbali mbali vya dola umebaini kuwababa yake Ponda mzee Issa Ponda alizaliwa mwaka 1921, na kuishi eneo la Rumonge barabara ya 6, nyumba namba 31, Bujumbura nchini Burundi, na kuhamia nchini mwaka 1957.

Mzee Issa Ponda alifikia ujiji, kwenye mji wa Ball (hivi sasa Kawawa) na kupokewa na mtanzania abaye baadaye alikuja kuwa mjomba wake Ponda anayeitwa Iddy Matata. Mara baada ya kahamia kwenye mji huo na kupewa kiwanja na mzee Matata mzee Issa ndipo alipomuoa Mariam Ally Kassa (huyu ndiye mama wa Shehe Issa Ponda) na alimzaa Shehe Ponda Mwaka 1958.
Taarifa za kiuchunguzi zinaonyesha kuwa, mzee Ponda baada ya kuoa na kupata mtoto, alianza kutafuta namna ya kuzoeleka kwenye eneo alilokuwa anaishi ili aonekane ni mzaliwa wa Tanzania na alifanikiwa kwa hilo hadi akagombea udiwani uliodumu kuanzia mwaka 1964 hadi 1965.
Taarifa za uhamiaji zinaonyesha kuwa, Ponda ambaye alipata elimu yake ya msingi Kigoma na kuishia darasa la saba, hakuwai kuukana uraia wake kama sheria ya uhamiaji inavyoelekeza, kwa hiyo bado anatambulika kama raia wa Burundi.
Hata hivyo Sheikh Ponda kwa kutumia njia anazozijua (njia za panya), mwaka 1995 alpohamia njini Dar es salaam akitokea Kigoma alikuwa anafanya biashara, alaipata hati ya kusafiria namba A0143978 (nakala chanzo cha habari kinayo) iliyotolewa Juni mwaka 1995 kwa jina la Pondamali Issa Pondamali ambayo ilitakiwa kuisha 21, June mwaka 2000, ingawa aliongezewa muda hadi 2005, na inaonyesha anuani yake ya posta ni 21842 Kigoma namba ya simu ni 21842.

Sheikh Ponda aliamia Dar es salaam baada ya tukio la kupigwa risasi mguuni na polisi wakati akisafirisha magendo ziwa Tanganyika kati ya Tanzania na Burundi, ambapo duru za kiusalama zinaonyesha kuwa, alipelekwa kwa gari hadi Mwanza na kisha kwa ndege mpaka jijini Dar es salaam na kuojiwa na aliyekuwa afisa upelelezi pamoja na aliyekuwa mkuu wa usalama wa taifa wakati huo Haidery Zuberi kabla ya kuachiwa (Ponda).
Sheikh Ponda pia amewahi kuhusishwa na uuzaji wa madawa yaliyokwisha muda wake na mara kadhaa amekamatwa akijaribu kuyavusha kuelekea nchi jirani.

Sheikh na kundi lake ni wanasadikika kutumiwa na vyama fulani vya kisiasa ili kuanzisha vurugu na uvunjifu wa amani nchini, Sheikh Ponda pamoja na wenzake walikutana 7, Septemba kwenye msikiti wa kichangani (TIC), Magomeni Mpipa jijini Dar es salaam na 8, septemba kwenye msikiti wa Mtambani Kinondoni na kupanga namna ya kufanikisha vurugu hizo, pamoja na mkakati wa kumung'oa Mufti wa Tanzania Sheikh mkuu Shabani Bin Simba.
Wanaomfahamu vizuri Ponda wameishauri idara ya uhamiaji kumrudisha kwao Burundi kwa kuwa ni kinara wa vurugu na uvunjifu wa amani hapa nchini.


Chanzo cha habari ni gazeti la Afrika leola Jumatano Septemba 12-18, 2012 Toleo namba 60.


Katika gazeti la Kiislamu la safina la tarehe 7, Septemba 2012 toleo namba 25, lineeleza kuwa Ponda analo genge linalomfadhili limempa ponda hadhi ya usheikh licha ya kujua kuwa hastihili kuwa sheikh.

Nanukuu: Gazeti moja linalojiweka mbele katika kudai haki za waislamu limekuwa likiandika habari zake si kwa kuwasilina naye bali kwa kupitia kumbukumbu za zamani tu.
Katika kuhakikisha malengo yao yanafanikiwa genge hili limempa Ponda, hadhi ya Sheikh wa kiislamu licha ya kujua fika kwamba Ponda si sheikh hana elimu ya dini inayompa hadhi hiyo. Baadhi ya watu wanadai sheikh huyu hajamaliza hata juzuu 30 zinzzokamilisha msahafu wa qu'raan licha ya kutojua masomo mengine yanayomfanya mtu afikie kiwango cha usheikh, kama Figh na kadhalika.

Mwisho wa kunukuu.

Tuangalie kwa ufupi mtu anayeitwa Farid Had

Farid Had ni kiongozi wa kikundi cha uhamsho au genge la vurugu na machafuko Zanzibar ambalo wengi wa wafuasi wake ni watu kutoka Pemba wenye kuutukuza uarabu. Ni mtu anayemwataka Wazanzibar wjiondoe kwenye muungano. Lakini wazanzibar wanafikiri ni mwenzao kumbe sivyo. Farid Had ana uraia wa mchi mbili, kinyume na katiba ya nchi yetu.
Yupo mtu aliyesema aliwahi kukutana na Farid kwenye mkusanyiko mmoja wa wanadini wa kiislamu nchini Mauritania akiwa anawakilisha si Zanzibar wala Tanzania, bali aliwakilisha nchi ya Oman. Hakuna anayejua mtanzania aliwezaje kupata nafasi ya kuwakilisha Oman nje ya nchi yake lakini hayo yanasemwa na sina shaka kama hayapo yanakuja, maana pafukapo moshi usikanyage moto upo.

Huyo ndiye bwana Farid Had.
 
ponda maswala hayo akamueleze jk muda huu sio wakat wake wala si mahala pake kila zama na utaratibu wake,wazungu wananizam sana kwa maswala ya nchi ni kwasababu walitokea kuwajibishana tena bila kumuangalia mtu uson leo hii kizaz na kizaz wako makin mpaka damu zao zinaelewa hivyo.nchi ina watu wa aina tofaut na kila mtu ana tabia zake sasa bhasi ni razima kutumia mfumo wa magu ili kunyoosha watu wote wawe kitu kimoja kwa sababu mfumo mnaotaka ni wa jk ambao ni very corrupt tuseme inatosha jamaniiiiiii.
 
miongoni mwa masheikh wenye hekima sheikh Ponda ni mmoja wapo sio sawa na hawa masheikh Ubwabwa
 
[
Na Suala la kukandamiza demokrasia na uhuru wa habari wewe unalichukuliaje?
QUOTE="weyuyo, post: 15748199, member: 360347"]ponda maswala hayo akamueleze jk muda huu sio wakat wake wala si mahala pake kila zama na utaratibu wake,wazungu wananizam sana kwa maswala ya nchi ni kwasababu walitokea kuwajibishana tena bila kumuangalia mtu uson leo hii kizaz na kizaz wako makin mpaka damu zao zinaelewa hivyo.nchi ina watu wa aina tofaut na kila mtu ana tabia zake sasa bhasi ni razima kumia mfumo wa magu ili kunyoosha watu wote wawe kitu kimoja kwa sababu mfumo mnaotaka ni wa jk ambao ni very corrupt tuseme inatosha jamaniiiiiii.[/QUOTE]
 
Back
Top Bottom