Sheikh Ponda akosoa utendaji wa Rais Magufuli

Sheikh Ponda akosoa utendaji wa Rais Magufuli

Yupo sahihi shekhe Ponda huwezi kumfukuza mtumishi wa umma kwa kusema tu jukwaan watumishi wa umma wana taratibu zao na mamlaka zao za kinidhamu. Haya yanafanyika sasa si sawa.
 
Mwabieni Sheik Ponda akasome kwanza Repoti za CAG za kuanzia mwaka 2009/10 mpaka 2013/14.

Rais Magufuli na jopo lake wanachofanya ni kuzisoma hizo repoti na kutumbua majibu.

Kama vipi anaweza kuingia kwenye tovuti ya National Audit Office;

Nadhani wakati mwingine hisia zisipelekee kutupa uwezo wa kulaumu pasipo tafiti. Sijui sheikh Ponda amepata wapi taarifa kuwa raisi anafanyia kazi mambo ambayo hayajafanyiwa tafiti. sielewi kama anafuatilia hao wanaovuliwa nyazifa zao kama hawajafanyiwa uchunguzi au la!
Nadhani asemacho Sheikh kinaweza kuwa sahihi kulingana na mtazamo wake na hazuiliwi kutoa maoni yake.

Kama vipi anaweza kuingia kwenye tovuti ya National Audit Office
 
Kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni, lakini sizani kama JPM anafanya maammuzi bila kuwa na uhakika na anachokifanya.

Mungu mlinde Rais wetu JPM katika kutumbua majipu kwani tunajua maadui ni wengi sana.
 
Tunazidi kujichahnganya na kucreate division siku baada ya siku. We are only as strong as we are united, as weak as we are divided. It's time for us to face the reality that for many just see each other as enemy. We can fight it only by showing an equally strong bond of friendship and trust. Differences of worship and language are nothing at all if our aims are identical and our hearts are open. Jamii lets united by points, kuna dalili tuanakoendea kubaya kila issue ni matusi kwa kwenda mbele.
 
Anapaswa na yeye azisome hizo taarifa za Mkaguzi Mkuu za miaka ya nyuma na sasa. Vinginevyo, atakuja kulalamika tena kuwa watu wanaonewa!
 
Amekuwa mwanasiasa sasa
Katiba ya jamhuri ya muungano inaruhusu uhuru wa maoni kwa mtu yeyote:
18(1)
18.-(1) Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati.

(2) Kila raia anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio mbalimbali nchini na duniani kote ambayo ni muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi, na pia juu ya masuala muhimu kwa jamii.
 
lingeundwa jopp la wataalamu al-maarufu tume ya uchunguzi mngelalamika,hebu tulieni kwanza tuyashughulikie haya majipu ili heshima iturudi.
waswahili wanasema,ukimuona mtu analia sana wakati akikamuliwa jipu,ujue anakaribia kupona.
Mnakamua au mnafanya maigizo?
 
Na silazima kilahatua atakayochukua kufukuza wezi eti aje kutuambia,nyingine afanye na jopo lake tumeshaamua kumpa kazi. Kilakitu aje kuripoti kwetu ili iweje,atakapojiskia kusema na aseme japo vingine Ni aibu hata kusema...mf mtummoja mishahara 17 inamaana serikali iliyopita ilikuwa na uzembe wa kuchezea kodi zetu alafu walimu wakiomba nyongeza za mishahara wanaambiwa wakatafute kazi nyingine za kuwalipa vizuri eti kasungura kadogo...
Kwanza huyo ponda anayeponda yeye kawahi kufanyia hii nchi jambo gani la maana zaidi ya udini??
Walio mpa ajira niwakina nani?
 
Yupo sahihi shekhe Ponda huwezi kumfukuza mtumishi wa umma kwa kusema tu jukwaan watumishi wa umma wana taratibu zao na mamlaka zao za kinidhamu. Haya yanafanyika sasa si sawa.
Na wafanyakazi nao wafuate maadili na miiko ya kazi zao sio wanakuwa na kiburi,dharau, wezi wa mali za umma na kujiona miungu watu.
 
Nataka kujua CV ya Sheikh Ponda ni sawa tu na wale wachungaji wenye elimu ya dini tu bila elimu ya utawala alitakiwa kujua Urais na Uwaziri ni vitu tofauti kabisa. Rais vyombo vyote viko chini yake anajua kila mtanzania amelalaje na ameamkaje ndio Maana Majambazi wanachapwa risasi tu. Sasa anataka kufanya siasa elimu yenyewe ya kujua mambo ndogo Duh Waislamu wamuombee tu! Na uzuri waislamu wasomi hawawezi kumpinga wala hawawezi kumfuata atabakia na kakundi kadogo tu kanakomzunguka. Maana Hii elimu bure nawasiwasi Viongozi baadhi hasa wabunge wataachwa wenyewe kwenye Majukwaa
Soma katiba ya nchi ndio urudi hapa
 
Yupo sahihi shekhe Ponda huwezi kumfukuza mtumishi wa umma kwa kusema tu jukwaan watumishi wa umma wana taratibu zao na mamlaka zao za kinidhamu. Haya yanafanyika sasa si sawa.

Msichokijua nyie mliokimbia umande,hao wote tuhuma zao zilikuwa mezani siku nyingi,isipokuwa yule jamaa yenu mpigaji alikuwa hana ubavu wa kufanya chochote kwa vile na yeye alikuwa akipiga kama wao,huku nyie wapuuzi mkiendelea kuachama midomo na nzi wanafanya maskani vinywani mwenu

Nani asiyejua hali ilivyokuwa inaendelea kuwa mbaya kwenye uchumi wa nchi yetu,huku hao mnaowasifia wakiishi kama wateule.Nchi ina kila kitu,lakini watu tunaendelea kuwa maskini kwa ajili ya wapigaji.

Kwa taarifa yenu ,huyo Ponda amegundua amepoteza umaarufu anatafuta atoke vipi ili watu tujue yupo,bahati mbaya anaripoka utumbo na nyie wenye akili finyu kama yeye mnashangilia kama mazuzu.Pumbavu
 
Huyu Ponda naye ni jipu ambalo limekuwa likiisumbua Bakwata na Taifa kwa ujumla
Ponda hana mamlaka ya kimaadili kuweza kufundisha MTU mwingine kufuata sheria na utaratibu wakati yeye aliwahi kuongoza uvamizi kwenye Mali za bakwata kinyume cha sheria na akaishia lupango! Hili jipu inabidi litumbuliwe faster!
 
Kitu ambacho Ponda hakijui ni kuwa hao anaowaita wataalam, ndio wanufaika wa ufisadi na wangetoa ripoti safi!
Ponda akumbuke kuwa wakati wa sakata la Richmond, ripoti ya wataalam wa Takukuru ilisema hakukuwepo na dosari wala rushwa kwenye mkataba wa Richmond! Hadi tume ya Mwakyembe ya bunge ilipochimbua na kukuta mambo ndivyo sivyo!
Ponda anataka kuvamia eneo ambalo hana upeo nalo kabisa, ukizingatia ukweli kuwa pia anatuhumiwa kuogopa umande wakati wa utotoni!
 
Anatafuta kiki maana alipotea kwenye ulingo wa watu maharufu hapa bongo
 
Sijawahi kumuelewa huyo wa kuitwa Ponda na wala sitakuja kumuelewa. Hana la maana analozungumza ni chuki tu zinamsumbua.
 
Huo ndio ukweli tutaingia kwenye gharama za kuwalipa wahanga soon,
Kumbe na masheikh huwa wana akili.
Kaka they are clever ila shida ni kwamba kuna mentality kuwa hawajui kitu na ni watu washari basi but not true at all, maana kwa mawakili wetu hawa sijui tungoje tuone
 
Back
Top Bottom