Speed of light
JF-Expert Member
- Nov 8, 2014
- 313
- 285
Fikra za udini zinajidhihirisha wazi wazi hususan hoja inapotolewa na mwenye imani ya dini ya kiislam utaona mtoa hoja anashambuliwa yeye mwenyewe binafsi na sio hoja yake inayojadiliwa utafikiri anayeshambuliwa si mwananchi
Fikra za namna hii hazijengi wala kuleta umoja na mshikamano bali hujenga uadui na chuki zisizo na tija kwa taifa
Kuna dhana kwa siku kadhaa sasa imekuwa ikisambazwa mitandaoni baada ya wahisani kutunyima msaada wao dhana hiyo ikiwataka wananchi wote kwa ujumla kama Taifa tujitegemee kiuchumi tusiwe omba omba
Dhana hiyo ni nzuri lakini haiwezi kuwa na matokeo mazuri kama kuna baadhi ya wananchi bado wana fikra za kubaguana kwa misingi ya udini
kuwa wenye itikadi fulani za kidini hawana haki ya kutoa maoni yao
Ubaguzi wa aina yoyote wenye kiashiria cha kudhalilisha kundi fulani ni sumu ya maendeleo popote pale duniani
Dhana ya kujitegemea itakuwa
ni nyimbo isiyo na manufaa yoyote ikiwa ubaguzi wa kidini utaachwa uendelee kushamiri
Fikra za namna hii hazijengi wala kuleta umoja na mshikamano bali hujenga uadui na chuki zisizo na tija kwa taifa
Kuna dhana kwa siku kadhaa sasa imekuwa ikisambazwa mitandaoni baada ya wahisani kutunyima msaada wao dhana hiyo ikiwataka wananchi wote kwa ujumla kama Taifa tujitegemee kiuchumi tusiwe omba omba
Dhana hiyo ni nzuri lakini haiwezi kuwa na matokeo mazuri kama kuna baadhi ya wananchi bado wana fikra za kubaguana kwa misingi ya udini
kuwa wenye itikadi fulani za kidini hawana haki ya kutoa maoni yao
Ubaguzi wa aina yoyote wenye kiashiria cha kudhalilisha kundi fulani ni sumu ya maendeleo popote pale duniani
Dhana ya kujitegemea itakuwa
ni nyimbo isiyo na manufaa yoyote ikiwa ubaguzi wa kidini utaachwa uendelee kushamiri