mshikachuma
JF-Expert Member
- Dec 2, 2010
- 2,853
- 638
Mkandara una nilet down mkuu!...jitahidi kucontrol hasira zako. Pia kukaa kimya nako ni dhahabu
Unaweza kutupa ushahidi wa madai haya? maana kama wewe umesikia lazima ipo copy ya hotuba hiyo na haiwezekani watu wote hapa JF wasiwe nayo. Please iwekeni hapa tumchambue huyu Sheikh Ponda. napenda sana kuwajua viongozi hawa wa dini hasa wanapozungumza maneno kama haya..
Samahani natoka kidogo lakini nitarudi kukusoma tafadhali niwekee ile kitu muhimu sana kwangu. Ni tag please.
Haya ndio mambo sinisiyataka miye. Mimi nimekuomba uniwekee hotuba yake ambayo wewe umeisikia ili nami pamoja na watu nwengine wachangi juu ya hotuba hiyo...Hivi Mkandara unataka uambiweje? Hivi humu JF hakuna hiyo thread inayohusiana na Shehe Ponda? Mbona watu huwa wanachangia wakati radio hiyo iko hewani. Kwa sababu watu hawajaweka sauti yake ndiyo huamini? Tafuta hiyo thread tena utakuta hata baadhi ya waislam wenzako wana support hiyo kauli ya Ponda.
Mkuu ni nia yangu mtu ashtakiwe kwa mujibu wa sheria kama ulivyosema na si kwa kuisiwa au kwa chuki na kumkomoa kwa kuwa anabishana na serikali katika utaratibu ambao serikali haitaki kuifuata hata kama ni haki yake mtu huyo.Mkuu wangu sielewi kabisa ila navyosoma hapa JF inaonyesha kwamba kuna tuhuma ama ushahidi kuwa Sheikh Ponda anahusika na mauaji ya Mbagala. Lakini hizi tuhuma ni za hapa JF sielewi ukweli ni upi ktk kukamatwa kwake na kama amehusika kweli ipo kila sababu ya kukamatwa na kupelekwa mbele ya sheria lakini kinyume cha hapo kama ni sababu ya yale maandamano ya kupinga sensa, akasimama kuiomba serikali iwaachie huru waumini wa Kiislaam waliokamatwa - hapo sioni kama lilikuwa kosa la watu kushabikia kiasi hiki maana hata Dr.Slaa, Mbowe Lema, Tundu Lissu wote wameisha kamatwa kwa makosa ya kutetea wafuasi wa Chadema ambao walikisiwa kufanya vurugu.
Wananchi wana kila haki na Uhuru wa kutoa maoni yao (freedom of expression). Ikiwa leo seirkali inapingana na maoni ya wananchi kwa sababu ya dini yao basi hiyo katiba mpya sijui itakuwaje. Na kila siku mnabishana na kina Ritz na Zomba humu mnawaita wao ndio wajinga, washenzi na wapumbavu wa kuitetea serikali. Serikali imekuwa ikitafuta ushahidi wa kumkamata Sheikh Ponda kutokana na mgomo na maandamano ya waislaam yalofanyika kupinga sensa ile hata kufikia kuharibu sensa nzima ya watu nchini...
Ifike mahala wanaChadema myapime maswala kwa kutazama makalio yenu wenyewe. Mnaiona Haki viongozi wenu wanawatetea wanaChadema lakijni hamuioni haki pale kiongozi wa Kiislaam anapopingana na Uongozi wa CCM. Kama Sheikh Ponda amehusika na njama zozote dhidi ya Wakristu na sio mfumo unaowakandamiza Waislaam basi nifahamisheni ili nami nishiriki ktk harakati hizi za kuwachambua viongozi hawa wa dini wanaosababisha UDINI..All I know Sheikh Ponda huikaripia serikali ya CCM kwa kuwakandamiza Waislaam kwa lugha ambayo hutoa hatadhari ya kwamba itafikia wakati Waislaam na wakristu watakuwa maadui..
Wapi nime onyesha hasira? kusema hawa watu wakizibwa midomo wanaweza ongea kwa makalio?.. hapana mkuu wangu huu ni usemi tu ambao mtu anaulizwa swali hana jibu lakini anapenda tu kuongea ili mradi aonekane kaandika japokuwa pumba. Hii ndio maana yake sawa na kusema masaburi..Mkandara una nilet down mkuu!...jitahidi kucontrol hasira zako. Pia kukaa kimya nako ni dhahabu
Sasa isiwe akamatwe kwa sababu wameamua kumtoa kafara; Ponda hajaanza leo kusema anayoyasema. Kama muda wote (miaka yote) wameweza kumvumilia imekuwaje leo waamke na kusema wanamkamata?
Kama kosa ni yale ya Mbagala au anayoyasema ukweli ni kuwa itakuwa ni kumuonea! Kosa ni la serikali inayotawala. Ukiacha mlango wazi kwenye zizi kila sikuw watu wanakuambia chui ataingia na kula mbuzi nawe ukapuuzia siku chui akiingia na kula utalaumu zizi kwanini halikufungwa?
Kuhusu swala la kuhamasisha Waislaam wasihesabiwe sijasema sio makosa isipokuwa binafsi yangu namuunga mkono kama navyomuunga mkono DR.Slaa na Mbowe ktk kuhamasisha M4C. Je, ni makosa kisheria? itategemea wewe uko upande gani..Mkuu ni nia yangu mtu ashtakiwe kwa mujibu wa sheria kama ulivyosema na si kwa kuisiwa au kwa chuki na kumkomoa kwa kuwa anabishana na serikali katika utaratibu ambao serikali haitaki kuifuata hata kama ni haki yake mtu huyo.
Nisichokielewa ni kwa vipi huelewi sheikh ponda ana makosa hata kwa huko kuhamasisha watu wasihesabiwe kwenye sensa. Huko ni kukiuka sheria. Kama ni sheria kuchukua mkondo wake basi kuna haki kumkamata. Amekamatwa kwa makosa ambayo anatuhumiwa kuyatenda na ni mara nyingi tu watu wamehamaki dhidi ya serikali hata wale wasiopenda haki ya mtu kukiukwa kwamba kwanini serikali haimkamati na kumfungulia sheik Ponda mashtaka kwa sababu anavuruga umoja wa kitaifa na kuleta chuki kati ya jamii ili watu wagawanyike kidini.
Nikuulize tu swali dogo. Hivi hakuna watu ambao watafaidika na mgawanyiko wa kijamii hasa kidini ukitokea? Kama wapo Sheikh Ponda na msimamo wake huawezi kuwa kati ya watu wanaotaka mgawanyiko huo au kuna watu wako nyuma yao ili watimize azma zao za kula hata kama ni kwa gharama ya damu ya watanzania?
Hizo ni technics za JK kuona kasema vibaya Mbagala sasa kuneutralize his bad speech iliyoelekea kukubali kitendo cha kuchoma makanisa DAWA NI KUMKAMATA PONDA KUONYESHA JK HAKUBALIANI NA KITENDO CHA KUCHOMA MOTO MAKANISA...
Wachangiaji wa Jamii kuweni makini JF itachomwa moto pia