hiyo 61% ni hesabu za ki NGO cha kwenye brifcase kinaitwa PEW,
CIA wao data yao ya mwanzo ni 30%,
so baadae walihitaji ku update data,wakatumia za PEW.
LAKINI ukicheki update za CIA kwa mwakahuu,naona iko blank means hawana vyanzo vya uhakika
Elungata,
Mwaka wa 2011 nilialikwa Chuo Kikuu Cha Iowa kufanya muhadhara
katika mambo haya haya tunayojadili hapa Majlis.
Muhadhara ulikwenda vizuri na niliielewasha hadhira mchango wa
Waislam katika kupambana na ukoloni kuanzia vita vya Maji Maji
1905 hadi kufikia siasa za uzalendo kuanzia 1929 ilipoasisiswa AA
hadi kuja kuundwa kwa TANU 1954.
Hii kwao wao ilikuwa historia ngeni hawakupatapo kusoma mengi
niliyoyaweka hadhir pale.
Katika kujumuisha nikaeleza hali inayowakabili Waislam baada ya
uhuru kupatikana na misuguano iliyopata kutokea kwa Waislam
kupambana na polisi katika mitaa ya Dar es Salaam kwa kupinga
dhulma.
Ukumbi ulikuwa kama umemwagiwa maji baridi.
Hii ilikuwa historia mpya kwao hawakupata kusikia kabla.
Sasa ikawa maswali na majibu.
Hadhira yangu ilikuwa ya wasomi wa African History na miongoni
mwao wako wajuzi walioandika vitabu kuhusu Afrika na Tanzania
kama
Michael Lofchie, James Brennan, Jonathon Glassman,
James Giblin na vijana wanaonyanyukia katika siasa za Afrika
wakifanya Ph D zao.
Michael Lofchie
Kiasi bado kama dakika tano kumaliza muhadhara wakaja na swali
waliloniwekea mwisho ili nisitoke pale kichwa juu kwani nilikuwa
Alhamdulilah nimewaweka pale walipostahili kuhusu Uislam katika
Tanzania.
Wengi wao walikuwa na fikra kuwa Tanzania ni nchi ya Kikristo.
Swali likaja kwa kutoka kile wanachoita, ''religious distribution'' kati ya
Waislam na Wakristo.
Wakanambia, ''Nyie Waislam ni wachache Tanzania hamuwezi mkapata
fursa sawa na Wakristo ambao ni majority.''
Nimesimama pale juu peke yangu naangalia sura za Wazungu ambao
zilionyesha kufurahishwa na swali lile kama vile wanasema tumempata.
Ningeliweza kuja na takwimu zangu kutoka vyanzo tofauti na vile vya CIA
waliokuwa wakitegemea wao lakini nikaona hapana itakuwa, ''their word
against mine.''
Nilijiambia hapa lazima nije na kitu hata wao bado hawajakifikiria.
Nikawaambia ingekuwa Wakristo ni wengi Tanganyika Vita Vya Maji Maji
kupinga dhulma za Wajerumani visingeongozwa na Waislam akina
Sultan
Abdul Rauf Songea Mbano.
Nasema maneno hayo nikimwangalia
Prof. Giblin Mkuu wa Idara ya Historia
Chuo Kikuu Cha Iowa na ndiye aliyenialika chuoni hapo na mwenyewe ameandika
kitabu kuhusu Maji Maji.
Nikaendelea nikasema ingekuwa Wakristo ndiyo wengi Tanganyika uhuru wa
Tanganyika usingeletwa na Waislam.
Nikamaliza kwa kusema, ''Nionyesheni nchi yeyote duniani ambayo ilikombolewa
kutoka katika ukoloni na ''minorities,'' iwe Asia au Afrika.
Hapa nikasimama kusubiri jibu.
Ukumbi mzima kimya.
Nikasema, ''Tanzania Waislam ni wengi na hii inawatisha walioshika serikali na ndiyo
maana waliondoa kipengele cha dini katika sensa ili kuficha ukweli.''
Ukumbi mzima ulikuwa umesinyaa hadhira ilikuwa imepwelewa.
Ungedondosha pini ungelisikia mlio wake.
Jonathon Glassman hapo hapo akanialika kwenda kufanya muhadhara mwingine
chuoni kwake Northwestern University, Evanston Chicago.
Hiki ndicho chuo kinachoongoza dunia nzima katika African History.
Hawa ndiyo mabingwa wa historia ya Afrika.
Nilizungumza katika Ukumbi wa
Eduardo Mondlane.