Sasa hapo mnajichanganya, alipokuja huyo Mfalme wa Morocco,wengi tulimsikia Magufuli akiomba tujengewe msikiti na kiwanja cha mpira Dodoma.Dunia haina siri, waislamu wamefunguka kwamba ule msikiti ambao JPM alikuwa anatamba kuwaombea waislamu wajengewe kumbe ni kazi iliyoanza enzi ya JK mpaka Mufti akasafiri kwenda kwa nchi iliyofadhili ili wakajadiliane...
Sasa mbona kwenye majibu ya huyo Mfalme kwenye suala la msikiti hakusema alishaambiwa na Kikwete na analijua!
Lakini la ajabu ni kweli kwa wingi wa matajiri wa kiislamu nchi hii walikuwa na sababu ya kuomba kujengewa msikiti?