Changalucha
JF-Expert Member
- Oct 19, 2011
- 505
- 582
Mwanasiasa huyu kutoka visiwani aliwahi kushika wadhifa wa juu kabisa katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar alipoteuliwa na Rais Aman Abeid Karume mnamo mwaka 2000 kuwa Waziri Kiongozi wa SMZ akiwa na umri wa miaka 38.
Mnamo mwaka 2010-2015 aliteuliwa na Rais Jakaya Kikwete kuwa mbunge (wa kuteuliwa) na baadaye Waziri wa Mambo ya Ndani wa Serikali ya Muungano.
Wakati tukisubiri taarifa ya Tume maalumu iliyoundwa kufuatiliaji mauaji yaliyofanywa na Polisi kwa kijana mfanyabiashara wa madini baada ya kuporwa mamilioni ya fedha zake na polisi huko Mtwara (na kwingineko), mabadiliko makubwa yanatarajiwa na watanzania kufanyika katika Wizara ya Mambo ya ndani na Jeshi la Polisi hapa nchini.
Je, Uteuzi huu wa Mbunge Shamsi Nahodha ni maandalizi ya kushika tena nafasi ya Wizara hiyo?
Mnamo mwaka 2010-2015 aliteuliwa na Rais Jakaya Kikwete kuwa mbunge (wa kuteuliwa) na baadaye Waziri wa Mambo ya Ndani wa Serikali ya Muungano.
Wakati tukisubiri taarifa ya Tume maalumu iliyoundwa kufuatiliaji mauaji yaliyofanywa na Polisi kwa kijana mfanyabiashara wa madini baada ya kuporwa mamilioni ya fedha zake na polisi huko Mtwara (na kwingineko), mabadiliko makubwa yanatarajiwa na watanzania kufanyika katika Wizara ya Mambo ya ndani na Jeshi la Polisi hapa nchini.
Je, Uteuzi huu wa Mbunge Shamsi Nahodha ni maandalizi ya kushika tena nafasi ya Wizara hiyo?