Shambulizi la Lissu: Wanaomdhania dereva anahusika sio wajinga, Wana hoja za msingi. Je, anahusika?

Aisee sasa wewe kweli ndo hujaelewa kasome article ya lissu ya leo kuna risasi zilimpata lakin hazikuleta madhara makubwa maana yake kama zilimchubua tu.ila ilimkita hazikuharibu nyama.ndizo 16 zingine zilimgusa sehem nyeti zaidi.
Yani nyie jamaa lisu kawaroga sio bure,kila maelezo atakayotoa mnataka myafanye msaafu.
 
Aisee sasa wewe kweli ndo hujaelewa kasome article ya lissu ya leo kuna risasi zilimpata lakin hazikuleta madhara makubwa maana yake kama zilimchubua tu.ila ilimkita hazikuharibu nyama.ndizo 16 zingine zilimgusa sehem nyeti zaidi.
Hebu kaangalie ninayemjibu kaandika mashudu gani kabla huyo deiwaka hajaja na matusi yake. Nimemjibu kutokana na alichoandika
 
Yani nyie jamaa lisu kawaroga sio bure,kila maelezo atakayotoa mnataka myafanye msaafu.
Sawa ni maoni na mtazamo tu.sio lazima ukubaliabe na lissu au na mimi hiyo ni falsafa ya maisha.Huwezi kukubaliana na kila unayekutana nae.Ila tunaheshimu mawazo kinzani .sawa.kama ambavyo unaniheshimu na ni nakuheshimu
 
Pascal ameuliza very valid questions
Eti valid questions...nyoo, dereva wa Lissu ndiye aliyeamuru ulinzi wa Site 3 pale Area D uondolewe? Dereva wa Lissu ndiye aliyeng'oa CCTV Camera kwenye makazi ya viongozi baada ya Lissu kushambuliwa? Dereva wa Lissu ndiye aliyezuia wabunge wa CCM akiwemo na Spika Ndugai kufika hospital kumjulia Lissu hali? Dereva wa Lissu ndiye aliyezuia Bunge lisimtibu mbunge wake siyo?

Pumbavu kabisa!
 
Nakupa heko kiongozi, umesema ukweli.
Kama ingekuwa serikali na intelijensia yake ina shida ya kumwondoa huyo. Angeuawa kifo ambacho hakitoacha swali hata moja, mtu anakuja kukata uhai inaonekana baada ya kuugua muda fulani full stop.

kinafanyika kifo kisichoacha clue yeyote

NA KWANINI WAFANYE TUKIO PRECISELY 10 MINUTES BAADA YA SPEECH YA MAGUFULI KUHUSU ACCACIA ????
 
Mjadala sio walinzi,hoja ni dereva wa lisu.Kama ni walinzi pia naweza sema Dereva wa lisu,hao waliotoa camera na walinzi wanahusika au lazima wahojiwe.Kila mmoja anasehem yake ya kuhojiwa.Shida ni nyie kumfanya dereva wa lisu ni mtu asiyetakiwa kuhojiwa au kutiliwa shaka na hili ni kosa kubwa mno mnalofanya.Sijaona mwenye hoja zenye mashiko akielezea kwanini dereva asiwe suspected. Utata wa maelezo yake unatosha kuwa miongoni mwa washukiwa haijalishi kuna washukiwa wengine.
Dereva wa lissu yupo ubelgiji. Kwa maelezo ya Lissu hawajakataa kuhojiwa, Ila hawataki ahojiwe TZ kwa sasa sababu si salama. Maisha yana nafasi kubwa sana. Sijui ukweli kuhusu lissu na madai yake, Ila kama yeye aliyenusurika ana wasi wasi juu ya uhai wa dreva kama ataingia TZ, na anaamini yupo sahihi basi ni sawa akiendelea kuishi bila ukweli kujulikana kwa sasa. Sijasikia maelezo ni kwann ni vigumu kuwahoji wakiwa huko walipo. Ila kwa sasa ngoja dreva aendelee kuivuta pumzi ya MUNGU mpaka itakapopatikana njia sahihi. BTW hakuna sababu ya kuingia risk kwenye maisha ya mtu ambaye anaweza kuwa si mkosaji bali ni dreva tu. Aendelee kuishi, serikali inaweza endelea na uchunguzi na endapo ikijiridhisha kuwa anahusika kuna taratibu za kumpata. Wabelgiji si maadui, watatusikiliza watamleta.
 
NI UJINGA WA KIWANGO CHA LAMI

1. Kuamini kwamba serikali ilihitaji makomandoo wengi tena wenye AK47 kumuondoa Lisu uhai. Kimsingi JASUSI mmoja tu mwenye mafunzo haba kabisa anatosha kumuondoa Tundu Lisu duniani, Tena bila mpuuzi mwingine yeyote yule kujua.

2. Kuamini kuwa pale bungeni MAJASUSI walishindwa kumuwekea sumu kwenye kiti akakalia KAMA AMBAVYO ILISEMEKANA D.R MWAKYEMBE ALIWEKEWA NA MAMVI (Na mpaka leo bado haijajulikana)

3. Kuamini kuwa wangeshindwa kumsubili barabarani wakamsukumia roli la taka ikawa ajali kama ile ililoua watalii kule Arusha

4. Kuamini kuwa Majasusi (TISS) walikosa dawa ya usingizi ya kupulizia ambayo wangeweza kwenda nyumbani kwake wakapuliza kisha wakamchomba syringe ya sumu na wakati wezi tu wa kijingajinga huku mtaani wanayo na wanatumia kuiba majumbani

5. Kuamini kuwa Majasusi (TISS) walikosa food poison ya kumuwekea dereva wa Lisu ili akilewa na kuzidiwa barabarani gari lipinduke.

6. Kuamini kuwa Majasusi (TISS) walishindwa kubuni A silent assassination method waje kumsubiri nyumbani na kupiga kelele nama AK47 ...UPUUZI.

Mimi sijawahi kwenda hata JKT lakini nina uwezo wa kubuni mbinu zaidi ya 50 za kum-eliminate MBOWE ukiachialia mbali Tundu Lisu..

TUNDU LISU hana ulinzi wa kuwapa shida watu wa TISS kama wanania ya kumuondoa.

Hao Tiss unaowasifia hivi wangekuwa na huo uwezo nchi yetu isingeingia mikataba ya kipuuzi iliyokuwa ikipigiwa kelele miaka nenda rudi. Unadhani kila tiss anakubali kushiriki uovu? Wanaweza kukalia kimya uovu lakini sio lazima waunge mkono upuuzi.
 
Muuaji hutumia risasi moja au mbili kwisha kazi, target ni moyo au kichwani.
Tukiongea kisayansi, kiitelijensia na kibinadamu upo sahihi mkuu. Ila inawezekana maisha yana siri nyingi sana tusizozijua. Hata fumbo la uhai ni kitu gani bado hatujalifumbua. Tunaishi tu na wakati mwingine tunaondoa uhai bila kujua ni nini haswa tumekiondoa.
 
Maswali fikirishi


1.Mbowe ana uwezo wakuondoa walinzi waliokozamu siku ile?


2 Je camera ameondoa mbowe kuficha ushahidi?


3 kwann mbowe na timu yake waliamua kumpeleka nairobi badala ya muhmbili?walikuwa wana hofu nn?


4 kwakuwa nia ya mbowe ni kumdhuru tundulisu km wanavyodai upande wapili je kwakuwa yupo mikononi mwake nairobi ameshndwa nn kumdhuru?


5.km nia ya serikali ni nzuri kwnn wamekataa uchunguzi huru?wakati chadema wako tayari?


6.je jeshi la police haiwez kufanya uchunguzi bila kuwepo dereva wa tundulisu?je km angekufa wangemhoji nani au wangeacha kufunwya uchunguzi?


7 je police walishawah kuwahoji walinz wa zamu siku hyo?walikuwa wapi siku hyo?
 
Muuaji hutumia risasi moja au mbili kwisha kazi, target ni moyo au kichwani.

NGOJA NIKUPE SIMULATION YA ASSASSINATION KAMA KWELI SERIKALI INGETAKA KUMUUA.

1. Siku 3 kabla ya tukio lenyewe, umbali wa mita 300 kutoka kwenye nyumba ya Lisu kwenye paa la nyumba ya mbunge fulani (WA UPINZANI) Television network (Dish) ingesumbua.

2. Mbunge huyo (Wa upinzani) angepiga simu kwenye king'amuzi husika na wao wangemwambia tutakuja ndani ya siku mbili acha taarifa kwa mlinzi

3. SIKU YA TUKIO wafanyakazi fake wa king'amuzi (Snipers) wangefika na bunduki zao zenye viwambo vya kuzuia sauti na kupanda juu ya paa la huyo mbunge fulani kutengeneza dishi at the same time Lisu anashuka kwenye gari..anakula risasi moja tu ya kichwa.

4. Wiki moja baadae kungetengenezwa theory kwamba mbunge huyo wa upinzani na Tundu Lisu walikuwa wanagombea mwanamke au mteja wa kumuwakilisha mahakamani.
 
Hao Tiss unaowasifia hivi wangekuwa na huo uwezo nchi yetu isingeingia mikataba ya kipuuzi iliyokuwa ikipigiwa kelele miaka nenda rudi. Unadhani kila tiss anakubali kushiriki uovu? Wanaweza kukalia kimya uovu lakini sio lazima waunge mkono upuuzi.

Unadhani kila Mwanajeshi anayeenda vitani ANAPENDA mbali ya kuwa ameahapa kuilinda nchi yake???? Tumia kichwa chako acha kuchosha vyakwetu.
 
NI UJINGA WA KIWANGO CHA LAMI

1. Kuamini kwamba serikali ilihitaji makomandoo wengi tena wenye AK47 kumuondoa Lisu uhai. Kimsingi JASUSI mmoja tu mwenye mafunzo haba kabisa anatosha kumuondoa Tundu Lisu duniani, Tena bila mpuuzi mwingine yeyote yule kujua.

2. Kuamini kuwa pale bungeni MAJASUSI walishindwa kumuwekea sumu kwenye kiti akakalia KAMA AMBAVYO ILISEMEKANA D.R MWAKYEMBE ALIWEKEWA NA MAMVI (Na mpaka leo bado haijajulikana)

3. Kuamini kuwa wangeshindwa kumsubili barabarani wakamsukumia roli la taka ikawa ajali kama ile ililoua watalii kule Arusha

4. Kuamini kuwa Majasusi (TISS) walikosa dawa ya usingizi ya kupulizia ambayo wangeweza kwenda nyumbani kwake wakapuliza kisha wakamchomba syringe ya sumu na wakati wezi tu wa kijingajinga huku mtaani wanayo na wanatumia kuiba majumbani

5. Kuamini kuwa Majasusi (TISS) walikosa food poison ya kumuwekea dereva wa Lisu ili akilewa na kuzidiwa barabarani gari lipinduke.

6. Kuamini kuwa Majasusi (TISS) walishindwa kubuni A silent assassination method waje kumsubiri nyumbani na kupiga kelele nama AK47 ...UPUUZI.

Mimi sijawahi kwenda hata JKT lakini nina uwezo wa kubuni mbinu zaidi ya 50 za kum-eliminate MBOWE ukiachialia mbali Tundu Lisu..

TUNDU LISU hana ulinzi wa kuwapa shida watu wa TISS kama wanania ya kumuondoa.
Ukienda Google ukaandika CIA failed missions utashangaa kukuta missions nyingi CIA walizofeli, hiyo ni CIA sasa sijui huu upuuzi wetu unaoitwa TISS na ujinga mwingine umeshafeli missions ngapi.UJINGA WA KIWANGO CHA LAMI katika UBORA WAKE
 
Mjadala sio walinzi,hoja ni dereva wa lisu.Kama ni walinzi pia naweza sema Dereva wa lisu,hao waliotoa camera na walinzi wanahusika au lazima wahojiwe.Kila mmoja anasehem yake ya kuhojiwa.Shida ni nyie kumfanya dereva wa lisu ni mtu asiyetakiwa kuhojiwa au kutiliwa shaka na hili ni kosa kubwa mno mnalofanya.Sijaona mwenye hoja zenye mashiko akielezea kwanini dereva asiwe suspected. Utata wa maelezo yake unatosha kuwa miongoni mwa washukiwa haijalishi kuna washukiwa wengine.

Mtani huu utetezi wako kwenye hili suala la Lissu naona ni kama ubaruka sarakasi ukiwa umefunga msuli kwa mama mkwe. Bora ujikite kwenye kusifia SGR, stiegler gorge maana ndio pekee mlilo nalo. Huu utetezi wa dereva wa Lissu naona unajichoresha tu.

Hakuna anayetetea dereva wa Lissu kuhojiwa bali ni mazingira ya Dereva kuhojiwa. Dereva tuko tayari kuhojiwa na sio dereva tu hata Lissu maana yuko hai. Polisi wetu hawana weledi zaidi ya kupiga na kujenga hofu, police hawa hawa wanaopiga watu wanaotaka kumuombea Lissu tena kwa amri toka juu kwa hao hao wanaoshukiwa? Tunashukuru Mungu Lissu amepona kwani ingepigwa propaganda mfu kama kifo cha Wangwe. Tulitarajia uchunguzi ungeanza kwa hao walinzi waliokuw eneo la tukio maana wao wapo hapa hapa, kisha CCTV camera zingetumika na huyo Dereva wa Lissu walikuw hapo Nairobi muda mrefu tu, na isotoshe tuna uhusiano mzuri na Ubeligiji watumwe wapelelezi.

Nikushauri kitu mtani, hili shambulio la Lissu ni kama pembe la ng'ombe halifichiki, hata ufanyeje liko wazi. Sema Lissu yuko upande wa makali hivyo hatopata lolote. Lakini waliotenda hawana utata. Usipoteze MB zako maana naona hapa unatafuta kupandisha jazba tu lakini mchezo umeshapoteza huu. Katetee ndege tu jamaa yangu.
 
Ukienda Google ukaandika CIA failed missions utashangaa kukuta missions nyingi CIA walizofeli, hiyo ni CIA sasa sijui huu upuuzi wetu unaoitwa TISS na ujinga mwingine umeshafeli missions ngapi.UJINGA WA KIWANGO CHA LAMI katika UBORA WAKE

ZAMANI, Tulikuwaga na UJINGA mmoja hivi wa kusema " SAA YANGU NDIO IKO SAHIHI INAENDA SAWA NA RADIO" Bila kujua kuwa kule kwenye radio ni mtu ana saa kama yako anaangalia hahahaaaa.

UJINGA MWINGINE ni huu wa kuja humu na HOJA za GOOGLE.

Hivi unadhani hivyo vitu huko GOOGLE vimewekwa na YESU?? CIA wafeli critical mission wakuwekee wewe google? wanakuwekea upuuzi wanaojua hauna effect kwao..Vinginevyo uwe ni umbea tu wa vyombo vya habari.
 
Wala tusiumize vichwa jamani,waliomtwanga risasi lisu,walikuwa na baraka zote za system,
Hii ni copy and paste,duniani kote,ya serikali za ovyo,hivi waliomtesa Mbunge Boby wine,hawajurikani?si serikali ya UG,hizi ni modus operandi za serikali zote za hovyo
 
Unadhani kila Mwanajeshi anayeenda vitani ANAPENDA mbali ya kuwa ameahapa kuilinda nchi yake???? Tumia kichwa chako acha kuchosha vyakwetu.

Hapa naona unakimbiza tu mbuzi mweusi gizani. Hili la Lissu Katafute kazi nyingine, kinachosaidia ni vitisho tu kuzima ukweli huu lakini kila kitu kiko peupe.
 
Hili ni bandiko la maswali kwa Tundu Lissu na dereva wake, kufuatia shambulio la Lissu,
Shambulizi la Lissu, Wanaomdhania Dereva Anahusika, Sio Wajinga!, Wana Hoja za Msingi!. Jee Anahusika?.
Maswali haya ni kufuatia hoja za Lissu kwenye bandiko hili.
Mhe. Tundu Lissu,
Kwanza pole sana kwa yaliyokusibu.
Umezungumza mengi kuhusu kilichotokea mwaka mmoja uliopita, ila watu wanaohoji kuhusu dereva wako, nakuomba sana usiwaite wajinga, au wametumwa, kwa sababu mashaka yao ni very valid.

Kwa vile mashuhuda ni nyinyi wawili tuu, wewe na dereva wako, then kuna mambo tungependa kujua kutoka kwa Lissu mwemyewe na dereva wake.

Hoja kuwa tumetoka naye mbali hivyo tunaaminiana, hazina mashiko mbele ya watu na kazi zao. Lissu alipotoka na dereva wake, anaweza kujilinganisha Dr. Slaa na mlinzi wake Kagenzi walipotoka?, halafu what happened?!. Kwenye mambo ya assignment, anaweza hata akatumika mke wako aliyekuzalia wanao, sembuse itakuwa dereva tuu mliotoka nae mbali!.
Baadhi ya maswali ni haya...
  1. Baada kuona kuna gari linawafuatilia, mlichukua hatua gani?.
  2. The common sense ya kufuatiliwa inaelekeza, uki note you're followed, hatua ya kwanza ni kumpote anaye kufollow kwa makusudi, ili kwanza kujiridhisha kuwa anakufollow.
  3. Ukiisha jiridhisha you are followed, una change direction kumpoteza maboya.
  4. Ukimuona bado yupo, then kama uko fit, unamlengesha mahali kwenye kona ambapo hawezi kuchomoka, mnamalizana!.
  5. Kama hauko fit, unamlengesha kwenye safe area ,usually sehemu open kwenye makundi ya watu na kumripoti kunakohusika.
  6. Baada ya kuona mnafuatwa, kwa nini mliendelea kuelekea nyumbani?.
  7. Mlipofika mkasimama, mkawaona watu wawili wanashuka na AK 47, kitendo tuu cha kujua tuu bunduki zile ni AK 47, hii maana yake ni close proximity, kwenye shooting that close!, risasi 38!, dereva huyu amesalimikaje asipitiwe hata na moja?.
  8. Ametokaje kwenye gari na kujificha chini ya gari ya jirani bila kugundulika?!.
  9. Anafichwa nini kuhojiwa?, kuna nini kinafichwa?.
  10. Maswali yataendelea
Huko nyuma niliisha wahi kuzungumza haya kuhusu dereva wa Lissu.

Mpaka sasa the situation ya shambulio la Lissu as it is, limefanywa na watu wasiojulikana. Serikali yetu imeshindwa kuwabaini, lakini sisi watu wa media, tunaweza kusaidia kama nilivyosema hapa.
WanaJF, Je tuisaidie Serikali yetu inaposhindwa au tusubiri ishindwe, tuibeze na kuizomea kuwa haiwezi? - JamiiForums
Hitimisho.
The only defence ya Dereva wa Lissu has nothing to do na hiyo shooting, ni uzito tuu wa serikali kugoma kuita wachunguzi wa nje. Ingekuwa ni inside job ya Chadema, tungeshuhudia serikali fasta ingechunguza!.

Lakini kwa vile wasiojulikana ni hawa
Shambulio la Lissu: Wajue Wasiojulikana Watakaojulikana na 'Wasiojulikana' Ambao Kamwe, Hawatajulikana!. - JamiiForums

Tusitegemee lolote jipya hapa.
Tundu Lissu, just get well soon, na sasa inakubidi uchangue kati ya uanaharakati na kuishi.

Pole.
P.
Rejea
Tuacheni Ramli Chonganishi: Tusihukumu, Tusije Tukahukumiwa!. "Karma Ndio Pekee Hutoa Hukumu ya Haki Hapa Duniani!. - JamiiForums

Handling of Serious Security Issues: Kama CHADEMA Takes Things For Granted Kwa Uzembe Hivi!, Jee Ikulu Yetu Wangeiweza?! - JamiiForums

Tundu Lissu: Polisi wa Tanzania hawana mamlaka ya kunihoji nikiwa Kenya au kwingineko nje ya mipaka ya Tanzania - JamiiForums

P.
Acheni unafiki jamani, mbona kwenye hayo maswali hujauliza ni nani aliondoa CCTV camera kwenye eneo la nyumba za mawaziri na naibu spika zenye ulinzi mkali wa serikali?
 
Bila kupepesa macho maswali yangu kwako waliotoa cctv ni dereva wa Lissu?je.walinzi wa getini aliwaondoa dereva wa Lissu?vitu vingine tumieni akili tu ya kawaida tunaambiwa kila nyumba ina walinzi lakini that day hakukuwa na walinzi hayo je ni dereva alihusika?
 
Back
Top Bottom