Shairi la Leo...........

Fikiri ukila mbuzi, nyunyiza na pilipili
Fikiri wake mchuzi, ndimu weka ya ukali
Fikiri simtie nazi , itaharibu misuli
Fikiri akigoma mbuzi, itumie four wheeli
Fikiri nimefikiri, utamu nikabaini,
Fikiri bila kariri, nikaingia rahani,
Fikiri kanipa hari, Iddi ikawa tamuni,
Fikira kwa kufikiri, Utamu ndani kwa ndani.
 
Fikiri nimefikiri, utamu nikabaini,
Fikiri bila kariri, nikaingia rahani,
Fikiri kanipa hari, Iddi ikawa tamuni,
Fikira kwa kufikiri, Utamu ndani kwa ndani.

Na sasa nimefikiri, mbuzi nishamgundua
Na bado ninafikiri, wapi ulimpatia?
Ninazidi kufikiri , mwenyewe aliridhia?
Sitoacha kufikiri, sio wangu alikuwa?
 
Na sasa nimefikiri, mbuzi nishamgundua
Na bado ninafikiri, wapi ulimpatia?
Ninazidi kufikiri , mwenyewe aliridhia?
Sitoacha kufikiri, sio wangu alikuwa?
Mbuzi hakufikiri, Kisu 'kapita shingoni,
Kabla hajakariri, Damu katoka shingoni,
Kabla hajatayari, Nyamaye kenda jikoni,
Likuwa mbuzi wa Iddi, Zawadi nililetewa.
 
Mbuzi hakufikiri, Kisu 'kapita shingoni,
Kabla hajakariri, Damu katoka shingoni,
Kabla hajatayari, Nyamaye kenda jikoni,
Likuwa mbuzi wa Iddi, Zawadi nililetewa.

Wangu pia alifana, alinona kwa majani
Wakati namtafuna, nilikuwa hayawani
Paja lake lilonona, katikati na pembeni
Nilichakua bila hiana, mbuzi mtamu jamani!
 
hehehehehe hivi umefichwa na nani?acha nifikiri.

Duh, kloro wala sijafichwa,
Fikiria tu Ngeleja anatembelea mtaa wenu,
Kila siku saa 12 hadi saa tano usiku,

Fikiria pale Internet Cafe wamepandisha bei,Saa moja 3000/= ,
si anatumia Jenereta...
Fikiria mtaji wangu wa Ice cream umekatika wote

Duh, acha tu,
Vipi huko jamani,
wife hajajifungua,

Nije kufua nepi,
nipate walau ya Cafe tu?
Hebu nifikirie, Fikirie.
 
Duh, kloro wala sijafichwa,Fikiria tu Ngeleja anatembelea mtaa wenu,Kila siku saa 12 hadi saa tano usiku,Fikiria pale Internet Cafe wamepandisha bei,Saa moja 3000/= , si anatumia Jenereta...Fikiria mtaji wangu wa Ice cream umekatika woteDuh, acha tu, Vipi huko jamani, wife hajajifungua,Nije kufua nepi, nipate walau ya Cafe tu?Hebu nifikirie, Fikirie.
Dah! sasa nani alikwambia uludi bongo bana? au ile viza ya botswana iliisha? au hukufikiria?
Waifu kenda kusalimia wazazi wewe njoo tu wala usihofu, mimi ni katika wateule wanaume waaminifu wachache sana waliobakia kwenye hii sayari.
 
Dah! sasa nani alikwambia uludi bongo bana? au ile viza ya botswana iliisha? au hukufikiria?
Waifu kenda kusalimia wazazi wewe njoo tu wala usihofu, mimi ni katika wateule wanaume waaminifu wachache sana waliobakia kwenye hii sayari.

Eti eeh, nakuja Kloro, umesoma mail yangu.
Hebu nijibu basi, mengine nikiweka Asprin atalia......

Fikiria mjukuu anakuja nyumbani kwa kloro,
Anaingia kabisa nyumbani kwake, na waifu hayupo.
 
Back
Top Bottom