Fahari ya kiswahili katika tungo za mashairi

Singo Batan

JF-Expert Member
Apr 24, 2020
292
191
FIKIRI

1.
Fikiri zako fikira, ufikiri kila tendo,
Fikiri lilo na dhara, ufikiri na Ia pendo,
Fikiri lilo tohara, ufikiri na uvundo,
Fikiri fikiri tendo, Ia amani na busara.

2.
Fikiri sana dunia, ina mzuri mdundo,
Fikiri sana yalia, ina mzuri mshindo,
Fikiri mwisho sikia, unapasuka msondo,
Fikiri fikiri tendo, Ia amani na busara.

3.
Fikiri ndugu dahari, dunia ina mikondo,
Fikiri hizi habari, ni kushuka na mipando,
Fikiri dunia pori, chaka Ia uwi na kondo,
Fikiri fikiri tendo, la amani na busara.

4.
Fikiri dau muundi, muunda dau muundo,
Fikiri lende kilindi, daule likaze mwendo,
Fikiri dau halendi, nguvu za dau upondo,

5.
Fikiri ninakariri, usiwe mwenye mfundo,
Fikiri tena fikiri, kila ovu liwe kando,
Fikiri mno hatari, ukiwa na mbovu nyendo,
Fikiri fikiri tendo, Ia amani na busara.

Kutoka kwa Abdalla Kizere (Mtunzi)
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom